Smart911
Platinum Member
- Jan 3, 2014
- 175,967
- 194,043
SEHEMU YA 20
Kwa wiki ya kwanza sikutaka kula chakula chake chochote kile kwa kuogopa kulishwa limbwata, bado nililifikiria penzi la msichana aliyeniacha kwenye mataa, Isabela ambaye hakutaka hata kupokea simu zangu na hata nilipokuwa nikimtumia meseji, hakujibu hata moja.
Moyoni niliumia na ndivyo nikaongeza chuki kwa huyu mke wangu Salama. Sikumpenda kabisa, nilichoamua ni kumtesa, kumfanya akose raha ili aondoke kurudi kijijini lakini pamoja na kufanya hivyo kwa wiki nzima, bado siku iliyofuata alinionyeshea mapenzi utadhani jana nilimnunulia gari.
Siku ambayo ndiyo ilikuwa ya mwisho katika mwaka huo, nilitulia sebuleni, sikutaka kuzungumza kitu chochote kile, macho yangu yalikuwa kwenye simu, nilikuwa namtafuta Isabela kwenye simu ili usiku wa siku hiyo tuwe wote na mwaka 2014 ukiingia basi uingie tuwe wote.
Salama alikuwa kimya akiangalia televisheni, tayari alishachukua shuka lake na akawa ameifunika miguu yake pale kochini ambapo kila siku ndipo alipokuwa akilala, sikutaka alale chumbani kwangu kwani kila siku kazi yangu ilikuwa ni kumfungia mlango, asiingie, abaki palepale sebuleni, na alale hapohapo.
Salama: Usiku mwema mume wangu...( aliniambia huku akilivuta shuka pale kochini, wala sikumjibu, mimi nilikuwa bize kumtafuta Isabela kwenye simu)
Mpaka saa sita kamili inaingia, mafataki kuanza kusikika nje, bado Isabela hakutaka kupokea simu yangu, niliumia mno, maumivu niliyokuwa nayo kipindi hicho hayakuweza kuelezeka.
Ilipofika saa 6:30 usiku, simu yake haikuwa ikipatikana tena, ilikuwa imezimwa kitu kilichonifanya niwe na maumivu makali hata zaidi ya kipindi cha nyuma. Kinyonge sana nikasimama na kuanza kuelekea chumbani, nilipofika huko, nikajilaza kitandani huku nikiwa na mawazo lukuki.
Siku hiyo nilipitiwa na usingizi ilipofika saa tisa usiku wa manane kwani muda wote nyuma nilikuwa kwenye mawazo lukuki. Asubuhi ilipofika, niliamka na kitu nilichokikumbuka ni Isabela tu, nikanyong’onyea mno kwani kitu kilichotokea usiku uliopita kiliniumiza mno.
Nimejikuta tu naumonea huruma Salama...
Cc: mahondaw