Nilivyomliza mke wangu kwa siku 366

Nilivyomliza mke wangu kwa siku 366

SEHEMU YA 20

Kwa wiki ya kwanza sikutaka kula chakula chake chochote kile kwa kuogopa kulishwa limbwata, bado nililifikiria penzi la msichana aliyeniacha kwenye mataa, Isabela ambaye hakutaka hata kupokea simu zangu na hata nilipokuwa nikimtumia meseji, hakujibu hata moja.

Moyoni niliumia na ndivyo nikaongeza chuki kwa huyu mke wangu Salama. Sikumpenda kabisa, nilichoamua ni kumtesa, kumfanya akose raha ili aondoke kurudi kijijini lakini pamoja na kufanya hivyo kwa wiki nzima, bado siku iliyofuata alinionyeshea mapenzi utadhani jana nilimnunulia gari.

Siku ambayo ndiyo ilikuwa ya mwisho katika mwaka huo, nilitulia sebuleni, sikutaka kuzungumza kitu chochote kile, macho yangu yalikuwa kwenye simu, nilikuwa namtafuta Isabela kwenye simu ili usiku wa siku hiyo tuwe wote na mwaka 2014 ukiingia basi uingie tuwe wote.

Salama alikuwa kimya akiangalia televisheni, tayari alishachukua shuka lake na akawa ameifunika miguu yake pale kochini ambapo kila siku ndipo alipokuwa akilala, sikutaka alale chumbani kwangu kwani kila siku kazi yangu ilikuwa ni kumfungia mlango, asiingie, abaki palepale sebuleni, na alale hapohapo.

Salama: Usiku mwema mume wangu...( aliniambia huku akilivuta shuka pale kochini, wala sikumjibu, mimi nilikuwa bize kumtafuta Isabela kwenye simu)
Mpaka saa sita kamili inaingia, mafataki kuanza kusikika nje, bado Isabela hakutaka kupokea simu yangu, niliumia mno, maumivu niliyokuwa nayo kipindi hicho hayakuweza kuelezeka.

Ilipofika saa 6:30 usiku, simu yake haikuwa ikipatikana tena, ilikuwa imezimwa kitu kilichonifanya niwe na maumivu makali hata zaidi ya kipindi cha nyuma. Kinyonge sana nikasimama na kuanza kuelekea chumbani, nilipofika huko, nikajilaza kitandani huku nikiwa na mawazo lukuki.

Siku hiyo nilipitiwa na usingizi ilipofika saa tisa usiku wa manane kwani muda wote nyuma nilikuwa kwenye mawazo lukuki. Asubuhi ilipofika, niliamka na kitu nilichokikumbuka ni Isabela tu, nikanyong’onyea mno kwani kitu kilichotokea usiku uliopita kiliniumiza mno.

Nimejikuta tu naumonea huruma Salama...


Cc: mahondaw
 
SEHEMU YA 23

Jamaa 1: Nyumba hiyo hapo mbele! Kwani wewe ni nani? (aliniuliza, kilichojengeka akilini mwangu ni kwamba inaelekea msichana huyo hakuwa ametulia, hivyo na mimi nikajifanya waruwaru)

Mimi: Mimi bwana wake. Jana kanikimbia baa baada ya kunywa bia zangu....
Jamaa 2: Hahaha! Nilijua tu, huyu demu sijui atajirekebisha lini...kila siku kesi na ana bahati buzi lake halipo, lingekuwepo, angepigwa risasi (alisema jamaa huyo tena huku akiachia tabasamu lenye masikitiko, maneno yake yakaifanya damu yangu kuzunguka kwa kasi mwilini)
Mimi: Kwa hiyo mimi siyo wa kwanza?
Jamaa 1: Wewe kama wa nane hivi kuja kulalamika. Unajua hawa mademu zetu wa siku hizi wanapenda sana pesa, sasa mcheki mtu kama Isabela, anaishi na mzee mwenye pesa ndefu, mzee mwenye migodi na anapata anachokitaka, lakini hatulii.....

Kiukweli maneno yao yalinichanganya sana, nikabaki nikiwaangalia mara mbili-mbili, sikuamini kama kweli maneno hayo yalimhusu yule Isabela demu wangu au mwingine. Uso wangu ukajawa na tabasamu pana lakini moyo wangu ulikuwa kwenye maumivu makali, iweje yule Isabela, mwenye sura nzuri kama vile, mpole awe na mabwana lukuki, halafu eti aishi na bwana na wakati aliniambia anaishi kwao, tena na wazazi wake?

Nilichanganyikiwa, kama kupagawa, basi siku hiyo nilipagawa haswa. Nguvu zikaniisha, kwa kuwa kulikuwa na kibenchi pale nje, kwanza nikayakalisha makalio yangu.
Jamaa 2: Kama unataka kwenda anapoishi, nyumba hiyo hapo, ila muulizie kwanza kwa mlinzi, unaweza kuingia ukakutana na bwana wake mwingine ikawa msala. Bwana wake babu hayupo sasa hivi watu wanajilia vitu humohumo ndani....

Sikutaka kubaki mahali hapo, nilichokifanya ni kuondoka kuelekea kulekule waliposema anaishi. Nilipofika, nikakutana na mlinzi.

Nilihisi jambo tu huyu Isabela atakua hayupo sawa...

Cc: mahondaw
 
SEHEMU YA 28

Rafiki yangu, hayo ndiyo maisha niliyokuwa nikiishi na huyu mwanamke ambaye wazazi wangu waliamua kuniolea kijijini. Maisha hayakuwa mazuri hata kidogo, kila siku nilimtesa na kumpa maneno ya kejeli kisa tu alikuwa akiishi nyumbani kwangu.
Kichwa changu kiliendelea kumfikiria Isabela lakini sikutaka kwenda kule kwake tena kwani niliamini kuwa ningeuumiza moyo wangu. Nikajitahidi sana kufanya kazi zangu kama kawaida.
Kumbuka kwamba sikuwa na mapenzi kwa Salama na muda mwingi nilijiona kama mtu aliye singo hivyo nilikuwa na uhuru wa kufanya lolote nililotaka kufanya.
Wakati mwezi wa nne unaingia, nikaamua kutoka na kuelekea ufukweni kula bata kidogo. Nikiwa huko ndipo macho yangu yakatua kwa msichana fulani hivi, alikuwa mrembo, amejaajaa kwa nyuma, alivalia kinguo cha kuogelea, sikutaka kumuacha hivihivi, nikaamua kumfuata.
Wakati nikimfuata, kama kawaida watu wengine walikuwa wakimwangalia, alionekana kuwa mrembo hasa, alipendeza machoni kwa kila mwanaume aliyemwangalia, nilipomfikia tu, nikaachia tabasamu.
Mimi: Mambo mrembo.....
Irene: Safi tu.
Mimi: Naomba unifundishe kuogelea!
Irene: Nikufundishe kuogelea jamani?
Mimi: Ndiyo! Naogopa maji, nahitaji mwalimu kama wewe....(nilimwambia huku nikitoa tabasamu)
Irene: Hahaha! Mimi mwenyewe sijui kuogelea....
Mimi: Kweli?
Irene: Ndiyo!
Mimi: Basi naomba kampani yako, nataka tu niwe nawe kwa muda huu hapa ufukweni.
Irene: Weeee...unataka wifi anipige....
Mimi: Hahah! Wifi gani tena jamaniiii? Mbona unanitabiria hivyo? Au unaninyima kijanja kuungana nawe?
Irene: Mmmh! Wanaume nyie wala hamueleweki kabisa...
Mimi: Sawa! Hatueleweki, ila kwa leo naomba mimi nieleweke, pleasee...nielewe kidogo tu, yaani kidogo tu.
Irene: (Kimyaaa)
Wakati nazungumza hivyo, macho yangu yalikuwa yakitalii mwili wake vilivyo kabisa, alionekana kuwa mwanamke fulani hivi ambapo baada ya kumchukua mawazoni na kumpeleka chumbani, alikuwa balaa.


Sikio la kufa halisiki dawa...

Bado hajakoma huyo jamaa...

Cc: mahondaw
 
SEHEMU YA 29

Basi nikakaa pale huku nikizungumza naye, lengo langu lilikuwa ni kumzoea tu kabla ya kumchombeza kwa vineno vya hapa na pale. Kwa nilichokigundua ni kwamba msichana yule hakuwa mgumu kivile japokuwa pale ufukweni kila mmoja alionekana kumuogopa. Kabla sijaanza kuishi na yule Salama, nilikuwa mkali kwa totozi hasa ‘loose ball’ kama zile, hivyo nilichokifanya ni kuonyesha umwamba wangu.
Mimi: Ningependa kupata muda wa kuzungumza na wewe...
Irene: Kuzungumza na mimi? Kuhusu nini?
Mimi: Mambo ya kawaida tu....
Irene: Sina muda....
Mimi: Najua muda unao ila hutaki tu.
Irene: Nitachelewa nyumbani...
Mimi: Usijali! Nina usafiri wangu, nitakurudisha.....tena nitakuwahisha....
Kitendo cha kumwambia nina usafiri wangu tu, mtoto akapagawa. Hapa ndiyo maana ninasema kwamba ukiona demu wako anachukuliwa na mtu mwenye gari, wewe kuwa mpole tu au tafuta lako uwachukulie washikaji wengine. Hawa wanawake wanapagawa sana na magari kana kwamba wamebatizwa kwa petroli.
Nilipomwambia hivyo tu Irene, akachanganyikiwa, uso ukawa na tabasamu pana, nikaona ni lazima nimchukue na kufanya mambo yangu! Basi akaogeleaogelea kwa muda, alipomaliza, akaenda sehemu ya kuvaa nguo zake, nikamchukua na kuelekea naye kwenye gari, ile kuingia tu, akajiachia, sketi yake ikapanda juu, mapaja yakawa wazi, nikabaki nayatolea macho, nikasahau kama nyumbani kulikuwa na Salama ambaye nilimnyima haki yake ya ndoa, mtoto akanikonyeza kisiri hivi, akanionyeshea bonge moja la tabasamu. LIKANIPAGAWISHA NA BABA JOHN KUAMKA.

Je, nini kitaendelea?


Inasikitisha sana hawa viumbe wanavyojirahisisha...


Cc: mahondaw
 
SEHEMU YA 30

Utulivu wangu ulikuwa sifuri kabisa ndani ya gari, macho yangu hayakutulia kuangalia mbele kule tulipokuwa tukiangalia, muda wote nilikuwa nikiyaangalia mapaja yake kwa macho ya kuibia. Huyu mtoto alikuwa balaa, kila nilipomwangalia, nilijua tu mambo yangeharibika.

Japokuwa kichwa changu kilikuwa kikimfikiria sana Isabela, huwezi amini muda huo mtu huyo hakuwepo kabisa kichwani mwangu, mawazo yangu yalikuwa na huyu mtoto, nifanye mikakati gani ili nimchukue kama ilivyokuwa kwa Isabela.

Sasa naye alivyokuwa na mapozi na miguu yake, mara aikunje kidogo, mara apandishe sketi, mara aitanue kidogo, yaani naye kama alijua vile kwamba ananipagawisha, nikawa naendelea kuyaangalia tu.

Mimi: Nimefanya kosa sana kutokujua jina lako, hivi unaitwa nani?
Irene: Naitwa Irene Godfrey.
Mimi: Waooh! Jina zuri! Mimi naitwa Denis, na unaishi wapi?
Irene: Naishi hapo Magomeni Mapipa.
Mimi: Sawa!

Wakati naendelea kupiga naye stori, akaipandisha miguu yake mpaka kwenye dashboard, hapo sketi ikaenda mpaka karibu na kiuno na kuifanya pichu kuonekana kwa kuibia.

Nikazidi kuwehuka, yaani ni kama nilizaliwa siku hiyo. Nikapagawa, tulipofika Mkwajuni Kinondoni, bado nusu nigonge basi la shule kutokana na muda mwingi kuwa bize katika miguu yake.
Irene: Jamani kuwa makini mpenzi....
Aliniambia bila soni. Hebu fikiria, mtoto nilimuweka kwenye tageti zangu, sikuwa nimemtokea mara mwisho wa siku anaanza kuniita mpenzi. Jamani jamani!

Haya magari kuna kitu Mzungu kaweka humu, haiwezekani eti from nowhere nishaanza kuwa bebi, basi nikaona siyo kesi, yeye si kajibebisha, na mimi nikakubaliana naye.
Mimi: Mpenzi una miguu mizuriiiii
Irene: Kweli?
Mimi: Ndiyo! Unantia hamu mwenzako (nilisema huku nikitoa kicheko cha chini, naye akakipokea)
Irene: Jamani! Yaani miguu tu ndiyo uwe hivyo?
Mimi: Ndiyo! Hebu subiri nipaki gari pembeni.

Muwindaji nae anawindwa...

Jino kwa jino....

Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom