Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,175
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 25
Kwa kweli nilikasirika mno, sikutaka kukubali hata kidogo, niliamini kwamba Isabela alikuwa wangu na sikutakiwa kupokonywa na mtu yeyote yule. Nilipofika katika njia ile na kukata kona, cha kushangaza sikumuona mtu yeyote yule, yaani hawakuwepo wale wanaume wala lile gari, hakika ilinichanganya sana.
Nilibaki nikizunguka huku na kule, niliangalia kila kona, sikumuona mtu yeyote hivyo kuamua kuondoka zangu kurudi nyumbani huku nikiwa na mawazo tele. Nilipofika, kama kawaida ya Salama, alinipokea kwa mbwembwe, heshima kubwa na kunipelekea viatu chumbani.
Salama: Mbona upo hivyo? Kuna nini?
Mimi: Hakuna kitu...naomba uniache...(nilisema kwa hasira)
Salama: Jamani! Haupo sawa, sasa mimi nitakuachaje? Sipendi kukuona ukiwa hivyo, unanihuzunisha mume wangu.....
Mimi: Nani mumeo? Mimi mumeo? Nilikuoa lini? Una pete ya ndoa? Wewe mwanamke jichunge sana, yaani jichunge, usitake kuniletea za kuleta, kwanza nakurudisha kijijini, naona unanijazia nzi nyumbani kwangu (nilimwambia maneno yaliyoonekana kumuumiza mno)
Salama hakuzungumza kitu, maneno yale yalimuumiza mno, alibaki akiniangalia tu, niliyaona machozi yakijikusanya machoni mwake, yalijaa na hatimaye kutiririka mashavuni mwake.
Sikujali, sikuwahi kuishi naye, sikuwahi kumpenda, hivyo sikutaka kufuatilia sana. Mawazo yangu yalikuwa kwa Isabela tu. Kichwa changu kilivurugwa na penzi la Isabela, halafu huku nyumbani mtu anaanza kuniita mume wangu, ningemuelewaje?
Salama akainuka na kuelekea jikoni, kwa mbali nilisikia sauti yake, alikuwa akilia kwa kilio cha kwikwi, sikutaka kujali, kwani kulia kwake kulinihusu nini? Acha alie, akimaliza atanyamaza.
Zilipita dakika kumi, Salama akarudi sebuleni hapo, nilipouangalia uso wake, alionekana kuwa kwenye tabasamu pana. Akaenda mezani, akaweka chakula kisha kunifuata na kunikaribisha, tena kwa kupiga magoti.
Salama: Karibu mume wangu!
Kwa kweli nilikasirika mno, sikutaka kukubali hata kidogo, niliamini kwamba Isabela alikuwa wangu na sikutakiwa kupokonywa na mtu yeyote yule. Nilipofika katika njia ile na kukata kona, cha kushangaza sikumuona mtu yeyote yule, yaani hawakuwepo wale wanaume wala lile gari, hakika ilinichanganya sana.
Nilibaki nikizunguka huku na kule, niliangalia kila kona, sikumuona mtu yeyote hivyo kuamua kuondoka zangu kurudi nyumbani huku nikiwa na mawazo tele. Nilipofika, kama kawaida ya Salama, alinipokea kwa mbwembwe, heshima kubwa na kunipelekea viatu chumbani.
Salama: Mbona upo hivyo? Kuna nini?
Mimi: Hakuna kitu...naomba uniache...(nilisema kwa hasira)
Salama: Jamani! Haupo sawa, sasa mimi nitakuachaje? Sipendi kukuona ukiwa hivyo, unanihuzunisha mume wangu.....
Mimi: Nani mumeo? Mimi mumeo? Nilikuoa lini? Una pete ya ndoa? Wewe mwanamke jichunge sana, yaani jichunge, usitake kuniletea za kuleta, kwanza nakurudisha kijijini, naona unanijazia nzi nyumbani kwangu (nilimwambia maneno yaliyoonekana kumuumiza mno)
Salama hakuzungumza kitu, maneno yale yalimuumiza mno, alibaki akiniangalia tu, niliyaona machozi yakijikusanya machoni mwake, yalijaa na hatimaye kutiririka mashavuni mwake.
Sikujali, sikuwahi kuishi naye, sikuwahi kumpenda, hivyo sikutaka kufuatilia sana. Mawazo yangu yalikuwa kwa Isabela tu. Kichwa changu kilivurugwa na penzi la Isabela, halafu huku nyumbani mtu anaanza kuniita mume wangu, ningemuelewaje?
Salama akainuka na kuelekea jikoni, kwa mbali nilisikia sauti yake, alikuwa akilia kwa kilio cha kwikwi, sikutaka kujali, kwani kulia kwake kulinihusu nini? Acha alie, akimaliza atanyamaza.
Zilipita dakika kumi, Salama akarudi sebuleni hapo, nilipouangalia uso wake, alionekana kuwa kwenye tabasamu pana. Akaenda mezani, akaweka chakula kisha kunifuata na kunikaribisha, tena kwa kupiga magoti.
Salama: Karibu mume wangu!