Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,175
- Thread starter
- #61
SEHEMUU YA 32
Irene: Mbona unavua shati! Unataka kufanya nini jamani?
Mimi: Kukupepea....
Irene: Kunipepea na wakati AC inafanya kazi.
Mimi: Sasa unaona kabisa navua shati, unaniuliza nataka kufanya nini tena jamani! Jamani, kwani haujui kwamba ukitaka kula lazima uandae sahani!
Irene: Hahaha!
Nikaona kwisha kazi yake, wakati namsogelea zaidi, nikashtuka baada ya kusikia kioo cha gari kikigongwa, kuangalia, alikuwa msela ambaye sikumuelewaelewa. Nikashusha kioo.
Mimi: Nikusaidie nini? (niliuliza kwa hasira)
Jamaa: Umepaki vibaya gari, si unasikia unapigiwa honi wewe tu!
Aliponiambia hivyo ndipo nikasikia honi nyingi nyuma yangu. Wakati nilipokuwa nikimwangalia Irene ndani ya gari lile, wala sikusikia hizo honi zote mpaka nilipoambiwa na kutuliza masikio yangu.
Sikuwa na neno, nikapiga gia na kuondoka mahali hapo mpaka katika kituo cha Magomeni Mapipa ambapo Irene akataka ateremke.
Mimi: Kwa hiyo?
Irene: Si una namba yangu! Utanicheki lovie....
Mimi: Poa.
Huyu Irene akaanza kunichanganya, safari nzima nilikuwa nikimuwaza yeye tu, kiukweli sikumpenda ila nilimtamani kutokana na mazingira niliyomkuta nayo na hata yale mapozi yake aliyokuwa akiniwekea.
Sikuchukua muda mrefu nikafika nyumbani, nikalipeleka gari katika sehemu ya maegesho na kuelekea ndani. Kama kawaida nikamkuta mke wangu Salama akiwa sebuleni akiangalia televisheni, sikumsalimia japokuwa nilimuona, nikapitiliza mpaka chumbani na kutulia kitandani.
Kichwa changu kilimpa nafasi kubwa msichana Irene, nikachukua simu yangu na kuangalia namba yake, hakika niliiona namba yake kuwa nzuri kweli, rahisi kukariri japokuwa ilikuwa 739284.
Wakati nikiwa kwenye feelings zangu, nikasikia mlango ukigongwa, nilijua alikuwa Salama, nikataka kujua alikuwa akitaka nini, nilipomkaribisha, akaingia huku akiwa amebeba sahani zilizokuwa na chakula na kunifuata kitandani.
Salama: Pole na kazi mume wangu!
Mimi: (Sikujibu)
Irene: Mbona unavua shati! Unataka kufanya nini jamani?
Mimi: Kukupepea....
Irene: Kunipepea na wakati AC inafanya kazi.
Mimi: Sasa unaona kabisa navua shati, unaniuliza nataka kufanya nini tena jamani! Jamani, kwani haujui kwamba ukitaka kula lazima uandae sahani!
Irene: Hahaha!
Nikaona kwisha kazi yake, wakati namsogelea zaidi, nikashtuka baada ya kusikia kioo cha gari kikigongwa, kuangalia, alikuwa msela ambaye sikumuelewaelewa. Nikashusha kioo.
Mimi: Nikusaidie nini? (niliuliza kwa hasira)
Jamaa: Umepaki vibaya gari, si unasikia unapigiwa honi wewe tu!
Aliponiambia hivyo ndipo nikasikia honi nyingi nyuma yangu. Wakati nilipokuwa nikimwangalia Irene ndani ya gari lile, wala sikusikia hizo honi zote mpaka nilipoambiwa na kutuliza masikio yangu.
Sikuwa na neno, nikapiga gia na kuondoka mahali hapo mpaka katika kituo cha Magomeni Mapipa ambapo Irene akataka ateremke.
Mimi: Kwa hiyo?
Irene: Si una namba yangu! Utanicheki lovie....
Mimi: Poa.
Huyu Irene akaanza kunichanganya, safari nzima nilikuwa nikimuwaza yeye tu, kiukweli sikumpenda ila nilimtamani kutokana na mazingira niliyomkuta nayo na hata yale mapozi yake aliyokuwa akiniwekea.
Sikuchukua muda mrefu nikafika nyumbani, nikalipeleka gari katika sehemu ya maegesho na kuelekea ndani. Kama kawaida nikamkuta mke wangu Salama akiwa sebuleni akiangalia televisheni, sikumsalimia japokuwa nilimuona, nikapitiliza mpaka chumbani na kutulia kitandani.
Kichwa changu kilimpa nafasi kubwa msichana Irene, nikachukua simu yangu na kuangalia namba yake, hakika niliiona namba yake kuwa nzuri kweli, rahisi kukariri japokuwa ilikuwa 739284.
Wakati nikiwa kwenye feelings zangu, nikasikia mlango ukigongwa, nilijua alikuwa Salama, nikataka kujua alikuwa akitaka nini, nilipomkaribisha, akaingia huku akiwa amebeba sahani zilizokuwa na chakula na kunifuata kitandani.
Salama: Pole na kazi mume wangu!
Mimi: (Sikujibu)