Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

Wakuu leo naomba kuleta Story yangu ya kweli ya jinsi nilivyokwenda South Africa bila kuwa na ndugu kule wala mtu wa kunipokea.

Ukweli kuna wakati ilifika nilichoka sana maisha ya hapa nyumbani, ilikuwa Mwaka 2014, nilikuwa napitia changamoto nyingi za maisha hasa katika familia. Ukweli akili ilikuwa imechoka sana ilisababishwa na kutokuwa na ajira muda mrefu.

Hata baadhi ya watu sikuwa napenda kukutana nao sana. Nikajiuliza kwani Maisha ni hapa tu nyumbani? kwani hakuna sehemu nyengine? Nikajisemea labda sikuandikiwa kutoboa hapa nyumbani ngoja nikajaribu bahati yangu sehemu nyengine.

Kabla ya kufanya maamuzi ya kwenda South Africa, Kwanza niliwaza kujaribu bahati yangu Marekani, nina ndugu kama watatu huko. Nikamcheki ndugu yangu mmoja akanitumia Invitation Letter. Nikaanza kupambana pale Ubalozini. Nilifika kwenye Usahili lakini nilikosa VISA.

Sehem ya kumi vp
 
Mkuu mie unafiki huwa siuwezi, wewe unge-clear tu doubts zetu then ukaendelea kuleta stori. Haya mambo ya watu kuogopa kuuliza maswali ndio sababu hata nchi yetu imefikia hapa ilipo. Watanzania tulio wengi hatujiamini ndio maana viongozi wetu wanatuendesha wanavyotaka, yaani tuna taifa la ndio mzee hata kama kunahitajika maelezo. Kitu kama hakijakaa sawa wewe kitolee ufafanuzi. Kuna vitu hatuwezi kukubishia kwa sababu kweli kila mtu ana experience yake ila mkuu kuna vitu very technical huwezi kusema kila mtu ana experience yake pia, kuna baadhi vitu lazima viwe common kwa kila mtu. Mfano ni hili la kuoverstay haliwezi kumalizwa kwa rushwa ya rand 300 na likaisha completely kwa sababu ni issue ya usalama wa nchi na system iko linked nchi nzima kuanzia makao makuu ya immigration hadi idara zote zinazohusika na maswala ya uhamiaji. So wakiscan tu passport yako hapo boarder au sehemu yoyote inayohusika na mfumo wa passport control taarifa zako zinaonekana hadi makao makuu ya immigration kuwa kuna mtu kaoverstay anahitajika kukamatwa au kulipa fine whatever the case may be. Sasa huyo immigration officer atakusaidiaje hapo? Hiyo fine atakulipia? maana hiyo fine ni zaidi ya rand 4,000. Na hiyo fine inakuwa registered kwenye system mpaka uilipe ndio iwe cleared la sivyo unakuwa black listed kukanyaga nchini kwao for the next five years. Kwa hiyo hoja kama hii unatakiwa uitolee maelezo ili twende sawa. Kuna watu humu wanafurahia tu stori na vitu kama hivi wanavioverlook kwa sababu either hawavijui kama vipo au wameamua kufunika kombe mwanaharamu apite. Halafu hata issue ya kupewa hifadhi na kanisa na yenyewe kuna utata kidogo kama hutajali pia itolee maelezo. South africa inajulikana kwa ujambazi na mauaji hivyo kwa mtazamo wangu sio rahisi viongozi wa dini wakupe hifadhi bila kujiridhisha kama wewe ni mtu salama au la. As a reasonable person nilikuwa nategemea wangekuhoji kwa kina kuhusu uhalali wako wa kuwepo nchini kabla ya kukupa hifadhi, lazima wangekuulizia documents zako kama upo nchini kihalali. Kumbuka hilo ni kanisa na linatakiwa kuheshimu sheria za nchi, hivyo hawawezi kurisk kumhifadhi mtu ambaye anavunja sheria maana ungekamatwa wangeonekana wanahifadhi wahalifu hivyo ingepelekea kanisa kuingia mgogoro na mamlaka za kiserikali na ingepelekea hatari ya kufutiwa usajili wa kanisa lao, mind you Mindrands ni makazi ya watu wenye hela kwa hiyo ni watu wenye uelewa mpana. Samahani wasomaji kama nawaharibia stori yenu ila nimeamua kutokuwa mnafiki kwa kuuliza haya maswali critical.
Kamalizie Uzi wako ndio ufafanue yote hayo
 
SEHEMU YA KUMI NA SITA

Ukweli niseme kitendo nilichokifanya cha kupost zile picha hata mimi nilikijutia sana. Unajua wakati mwengine ukimpenda mtu kuna vitu vingine unajikuta umefanya tu, hata ukiulizwa sababu kwa nini ulifanya hivyo huelewi. Malengo yangu yalikuwa yanamhitaji sana Yule demu mwengine kuliko Kanya. Siku iliyofuata nilienda mpaka alipokuwa anaishi Kanya, Nilijaribu kukaa nae kuzungumzia hii ishu, nilimuomba Msamaha mwishoe alinisamahe, maisha mengine yaliendelea.

Tuliyamaliza lakini Kichwani nilibaki na dukuduku Fulani hivi, nilikuwa nawaza sasa nitafanyaje? Maana Kanya kwangu nilimuona kama mzigo wakati mimi nilipanga kutafuta demu ambae atanisaidia kufikia safari yangu. Namtema vipi Kanya? Yule demu mwengine tukawa tukikutana Kanisani tunasalimiana fresh, kwenye simu tunawasiliana. Ukaribu uliongezeka kiasi chake, Alikuwa hajui chochote kilichokuwa kinaendelea, Baadae nilikuja kujua kuwa huyu demu anaitwa Tshepiso na anafanya kazi Capitec Bank.

Sasa kuna wakati Kanisa lilitangaza kuna Safari ya kwenda kutoa Huduma za Kiroho kwenye Tawi lake lililopo Nchini LESOTHO. Kanisa lilikuwa na Matawi mpaka Marekani na Baadhi ya nchi za Ulaya. Walisema anayetaka kwenda na kama una Passport basi ruksa mtu yeyote kwenda, Usafiri, Chakula, Kulala vyote ni gharama za Kanisa. Nikasema hii ni fursa kwangu ya kuwa karibu zaidi na Mchungaji na Washua zaidi. Mpaka hapa kwa kweli nilianza kukubalika pale Kanisani si kama Mwanzo. Nilikuwa sio mgeni tena kwenye macho yao.

Lesotho ni nchi ndogo, Mfano ni kama Mkoa tu wa Morogoro au Morogoro inaweza kuwa Kubwa pia. Ni nchi ambayo ipo ndani ya nchi ya South Africa. Nchi yote imezungukwa na South Africa. Kama mtu hufahamu unaweza ku google ukaona.

Sasa kwa wasiofahamu, Vijana wengi wazawa wa South Africa hawana Passport za kusafiria, Wengi sio sana watu wa kusafiri safiri, kwa hiyo kigezo cha watu kuwa na Passport kilipunguza waumini wengi sana akiwemo Kanya. Alikuwa hana Passport. Kwenye Upande wa watu wa Camera, Mimi na Max tu ndo tulikuwa na Passport. Nilichofurahi Tshepiso alikuwa na Passport kwa hiyo alikuwepo kwenye hii safari.

Utaratibu wa siku ya Safari tulikuwa tunapewa gari Fulani zina muundo kama wa Toyota Alfad, rangi nyeupe, Mnakuwa mnachaguana wenyewe waumini kama sita, kati yenu anapatikana pia dereva, kisha mnaanza safari. Mimi na Tshepiso tulipanda gari tofauti. Siku ya safari ilikuwa ni jumamosi ila Muda wa safari mnapanga wenyewe wana Kikundi, Mchungaji alisema anachotaka watu wote Jumapili tuwe tumefika Lesotho. Kwa hiyo Kanisa lilitoa gari kama 10 hivi. Watu tukaanza safari. Sisi tulianza safari jumamosi jioni.

Kwenye gari yetu mwanaume nilikuwa peke yangu, wengine wote madem. Wote kati yetu hakuna hata mmoja anaijua njia ya kutufikisha Lesotho. Yan wenzetu wana barabara nyingi kiasi kwamba unaweza kuzaliwa palepale na Baadhi ya barabara za kuelekea baadhi ya nchi huzijui. Na ukikosea tu barabara unaweza kutumia muda mwingi sana kurudi kwenye barabara uliyoikusudia kupita. Nakumbuka tulipotea sana. Mpaka ikabidi tutumie Navigator kwenye simu zetu. Wote ndani ya gari tuliwasha Navigator tunamwelekeza dereva wetu wapi pa kupita.

Tulifika Boda kati ya South Africa na Lesotho usiku wa kama saa Saba hivi. Kwa kuwa nilikuwa na mademu wote, mimi ndo niliwaongoza mpaka mle ndani kwenye Ofisi za Uhamiaji. Kwa kuwa kwenye Passport yangu nilikuwa nimezidisha siku za kuishi mle South Africa, Nilisoma mazingira pale kwenye Passport yangu nikaweka Rand 300, nikagongewa bila shida. Japo Lesotho tulikuwa tunakwenda kukaa siku Tatu tu lakini Uhamiaji upande wa Lesotho walinipa siku Thelathini za kukaa Lesotho. Nilikuwa tayari mzoefu wa kupita kwenye Maboda.

Wale mademu walikuwa wanazinguliwa pale, nikawaambia wekeni Rand 100 kwenye Passport zenu halafu nendeni tena, wakafanya hivyo kisha wakagongewa mihuri kasoro mmoja tu kati yetu ndo hakugongewa huyo demu alikuwa ni Mnaijeria, Kwanza Mnaijeria kuingia Lesotho inabidi alipie visa. Sio kama sisi wengine tunaingia free tu. Pili Yule demu kama mimi tu pale South Africa alikuwa amezidisha siku za kuishi (Ame Overstay). Kwa hiyo wale maafisa uhamiaji walikuwa wanataka pesa ndefu.

Nakumbuka alikuwa anasema “Mbona Mtanzania na yeye ametoka mbali lakini amegongewa bila shida”. Basi pale mmoja wetu akafanya mawasiliano na mchungaji, Mchungaji na baadhi ya waumini walikuwa wameshafika Lesotho tayari. Kwa kuwa sio mbali sana, ule ule usiku, mchungaji ikabidi aje mpaka pale boda. Akaongea nao wale Maafisa Uhamiaji, nadhani aliwapa pesa kidogo ila sina uhakika sana. Hatimae wakatuachia tukaendelea na safari yetu mpka Mji Mkuu wa Lesotho unaitwa Masseru. Masseru pa kawaida sana pengine hata Dodoma pazuri. Huwezi hata kulinganisha na Dar, Arusha au Mwanza. Basi tulienda moja kwa moja kwenye Hostel tulizopangiwa kufikia. Tulilala pale.

Asubuhi mapema sana tuliamka na kuanza kujiandaa kwa ajili ya kwenda kupanda Mlima kwa ajili ya Ibada, Ibada ya kwanza tulienda kufanyia milimani huko. Ibada ya Jioni ndo tulienda kwenye Kanisa lao. Kwa hiyo Hata kupanda huo Mlima nakumbuka ilikuwa ni tabu, Mlima ulikuwa mrefu kiasi chake. Wakati magari yetu yanakusanyika pale chini ya Mlima ndo nilikutana na Tshepiso.

Ukweli Lesotho tuliinjoi sana, kwanza tulikuwa wachache, kwa hiyo tulikuwa kama ndugu Fulani hivi, tulipiga picha kama zote mpka leo hii ninazo kwenye Email yangu. Nikiziangaliaga huwa zinanikumbusha matukio yote haya ninayoyaeleza. Kule Lesotho Mimi na Tshepiso tulikuwa marafiki kinoma yan, ile Camera ya Kanisa niliyokuwa natumia kupiga picha, Picha nyingi nilimpiga yeye. Wakuu zote hizo ni harakati za kutaka kutafuta Mchongo ndani ya nchi ya watu. Naomba nisieleweke kwamba mimi ni Marioo ila mazingira ndo yalikuwa yananilazimisha kufanya nilichokuwa nafanya. Nilijua hapa nikicheza tu Akiba yangu ya Pesa inaisha yote halafu kinachofuta ni maisha magumu na kurudi Bongo, halafu mpango wa Kurudi Bongo nilikuwa sina kabisa.Nilijua nikifanya uzembe nitarudi kuuza Dawa za Kulevya kwa Jamaa Y. Kwa hiyo nilikuwa najaribu kuuwahi muda. Na huyu mwanamke naona kabisa kwa maisha yake anaweza kunifikisha Mahali.
Kumi n saba vp
 
Kafara na jumba bovu ka angushiwa konda msafi kwa sasa ye ndio jambaz kuu pia kuna tu jambaz tu dogo dogo ila ata konda alipigwa maswali korofi lakin kumbu story iliisha labda ile nyingne pia holy holm nae alikutana na watu wavurugaji story sikuona kujali alendelea kushusha tu episodes up to end.
Changamoto zipo lazma watakuja watu watasema chai, ohoo ni porojo tu kam zngne piga chini endelea kushusha kama mtu anaona chai aongezee tangawiz anywe pumbavu uyu nae Analyse alipata wapinzani utafikir walikua wana mrecord maisha yake kumbe makanjanja tu by the way Keagan Paul rudi mkuu shusha episode wa lugha lugha achana nao ukweli unabaki kwako.
 
Kitu kimoja tukubaliaane Keagan Paul ni muongo muongo.
Haiwezekani alienda SA kwa mara ya kwanza 2012(stori tofauti)
Halafu kwenye huu Uzi anasema alienda 2014.(stori tofauti tena).
Sijui why mnaikuza hivi mzee baba ishu hapa watu walitaman kujua mwisho wake ..lol..yaan let it be..iwe anafake au la...kuna watu wanapata motivation kupitia stry yake .waoga watajifunza wasiwe na woga😎
 
Nakumbuka mwaka 2007 nilikua na ndoto za kwenda dzonga ila sikua na mpunga, kuna jamaa yangu alikua amerudi toka lebanon huko alikua deployed kwenye peace keeping alikua amerudi bongo na fedha za kigeni nikaona kupitia huyu mwamba nitapata nauli nitambae zangu ng'ambo.
Nikawa chawa wa mwamba full kumsaidia kusolve harakati za hapa na pale kutokana na uzoefu wangu wa mtaa
Sasa bhana mwamba alikua na binti mmoja wa kitanga ndio alikua anataka amfanye mkewe ili dingi yake ni mnoko kikuda mchumba ndio alituambia kipindi mwamba anampa idea ya kwenda bumbuli kujitambulisha ,mimi kama chawa nisie na maadili nikamshauri mwamba ampe binti ujauzito ndio tuende ili zoezi liwe rahisi mwana apate jiko na mimi niende zangu ng'ambo.
Mwamba akafanikiwa kurutubisha yai binti kitumbo kikaota ikapangwa safari ya kwenda usambaani kuonana na wazee.
Kufika Tanga tukapokelewa fresh na bimkubwa, na mashemeji kumbe kamanda walikua wanamjua wote kasoro mshua boy tu, na bahati mbaya au nzuri hakuwepo siku hio ikabidi mzee apigiwe simu alikua shambani kwake huko anakaaga hata mwezi bila kurudi home. Alitaarifiwa uwepo wetu akaombwa arudi fasta mzee akaomba aongee na muoaji, mshkaji akatoka nje kuongea na mkwewe, mzee akamwambia jamaa anarudi kesho jioni lakini asitukute nyumbani kwake na hataki kabisa kutusikia, mshkaji kwa tabia zake za kijeshi akamkazia mzee na mikwara ya hapa na pale kwamba hatuondoki tutakaa hata mwezi mpaka arudi tuondoke na mke wetu. Mshua akasema kesho jioni anarudi lakini hatotukuta maana tutaondoka bila kuaga kamanda akasema sawa ngoja tuoneshane umwamba.
Ilifika usiku tukapewa room ya wageni kuna bed mbili kila mtu na lake, tukaangusha na mwanangu ,tulienda na begi moja tu , mchumba aliliweka chumbani kwake kwa usalama zaidi maana chumba chetu kilikua nje,
Kufika mishale ya saa nane usiku niliota ndoto kwamba yule mzee kaihamishia mimba kwa mjeshi halafu tuko leba kamanda anajifungua, mimi na manesi tunamwambia mchizi push! push! Jamaa anapiga kelele kumbe mimi nivyoota hivyo napiga kelele kwanguvu na jamaa naye anaota ndoto hiohio na anapiga kelele za uchungu mara tukashtuka wote mshkaji ananiuliza mtoto wangu yuko wapi nikamjibu kua makini usimlalie kuinuka dah! Mwamba alikua kashusha bonge la kimba mazee halafu hawezi kulikataa yaani kafanana nalo copyright alafu mashuka yote kitanda kizima kilikua makimba tu , nikampa mashuka ya kitandani kwangu ajisafishe tutoroke kabla hakuja kucha maana asingeweza kubadili nguo zilikua chumbani na mama kijacho mjeshi akaniambia kukimbia ni mbinu ya kijesh kabisa wao wanaiita ku retreat.
Tulitoka chumbani mule kwa kucraw mpaka kwenye toyota porte yetu huku mchizi akiwa kajifunga shuka rubega tukatokomea
Tukiwa njiani mwamba ndio akakumbuka conversation yake na mkwe wetu kwamba tutaondoka bila kuaga kama PAUL KEAGAN
Tulifaka town hata mawazo ya kumpiga mzinga wa nauli ya kaisha maana analia tu kama kabinti muda wote


Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Kitu kimoja tukubaliaane Keagan Paul ni muongo muongo.
Haiwezekani alienda SA kwa mara ya kwanza 2012(stori tofauti)
Halafu kwenye huu Uzi anasema alienda 2014.(stori tofauti tena).
konda msafi + Keagan Paul = Paul Makonda.

Baada ya kufanya utafiti na maesabu yasiyokua rasmi.

Multiple IDs, same person with different version of stories.

#JeifuIdumuMileleNaMilele
 
konda msafi + Keagan Paul = Paul Makonda.

Baada ya kufanya utafiti na maesabu yasiyokua rasmi.

Multiple IDs, same person with different version of stories.

#JeifuIdumuMileleNaMilele
@Melvine unahisi anafanya hivyo kwa faida gani?
 
Hao wanaigeria ujuaji wao unawacost kila sehemu hawakubaliki kutokana na tabia zao za kishenzi,utapeli,wizi etc
Kinachosababisha wakimbie kwao ni umasikini na kwa sasa nchi yao hali ya kisiasa sio nzuri muda wowote kitawaka
Soma hyo kwa makini
Screenshot_20210423-153058.jpg
 
Back
Top Bottom