Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

Wa
Tatizo lilikuja kutokea siku moja kwenye Birthday Party ya Mchungaji wetu ilifanyika usiku nyumbani kwake. Tulifika waumini kama wote.Kulikuwa na Nyama choma kama zote. Sasa yule demu mrembo mwenye ndinga lake nae alikuwepo. Nikasema leo lazima nitumie nafasi vizuri. Party ilifanyika nje halafu kulikuwa na kigiza giza fulani hivi, Nikasema Leo natumia hii nafasi vzr, Nikawa napiga piga nae story pale, mara tunapiga piga picha pale, sikufanya makosa hadi tukabadilishana namba. Kosa nililolifanya ni kwamba baada ya kutoka pale zile Picha nakumbuka nilipost Facebook. Halafu Kanya sijawai hata siku moja kumpost. Ugomvi kati yangu na Kanya ulikuwa mzito. Ishu ya namna hii kwa Wanawake ni kubwa sana.

poor reasoning
Wabongo katika ubora wenu
 
Aliianzisha on 15 april naona ikabuma akaja na hii mpya ya akina Kanya hio ya kwanza anadai yule muuza ngada ni Ibra halafu anasema yeye ni Muisilamu na alienda kanisani kujifanya ni mkristo hata huwezi kujua kipi kipi Bs tu yaani.

Hamko makini, ila kwenye kelele mko vizuri. Story ya mwanzo kaitoa mwaka jana, mpaka hapo ni zaidi ya mwaka. Na ukisoma unaona correlation na hii ya mwaka huu.

Mleta mada piga kimya tu, waachie raia wataimaliza wenyewe.
 
Hii CHAI HII CHAAI AISE KONDA USITUONE WOTE MAZWAZWA Nmesoma kichwa na sehemu ya 1 nkarefer na ile stor ya khumbu ambapo ulisema bondeni umefika kwa ndugu zako na ulkua na ndugu zako na lengo la kushuka bondeni llkua ni kujiendeleza na elim na ulienda round ya kwanza ukarudi kumalizia Advance bongo then ukarudi tena bondeni LEO UNALETA UZI TENA AAFU UNASEMA HUKUA NA NDUGU??YALEYALE YA MOTIVATION SPIKA enewei hii ni chai kama chai nyngne zlizojaa uko kwenye kula tunda kimasihara
Duuh endelea kushika zamu shuleni kwasbb wewe ni KILAZA
 
Hivi mkuu unapajua mpyagula , unaweza kupitia igunga au nzega, haya sio maisha kule mama ntilie wanauza 500 unapata ugali na kambale mkubwa, kuna mabasi wa waraabu koko yanaenda kule basi mtu kule anakuhadithia huku ukituliza hela unatoboa unamchek kiaina unasema ni kweli Boss, funguo za chumba chako lodge anakaa nazo mwenye nyuma, ukitakA kutoka anaitwa kufunga mlango ukirudi kijana anaenda kumwita akufungulie Bongo nyoso acha tu
Mpyagula kwny mipunga huko hadi kutokea Loya.
 
konda msafi hebu andika Uzi mwengine mtamu kuhusu maisha kule Kaburu maana naamini kuna visa vingi unavyo mbali kile cha khumbu!
Konda Msafi ana wivu sana. Ameona huu uzi unamfunika kwenye ule uzi wake wa Khumbu anaanza majungu, mara amuulize jamaa maswali yasiyo na kichwa wala miguu.

Mfano, eti ukioverstay South Africa huwezi kupita kwenda Lesotho hata kwa rushwa...kkkk, rushwa (kitu kidogo) ipo kila mahali.

Kuna mwaka nilikuwa natoka SA na basi la Shalom kwenda Lusaka ili niunganishe kuja Nakonde/Tunduma, Kondakta wa basi anatangaza kabisa kama passport yako ina shida (umezidisha siku za kukaa SA)nione, anazikusanya hizo passport na Rand 300 kila moja anaenda kuwagongea nyie mnasubiri kwenye basi. Tena ilikuwa December kipindi kibaya Home Affairs wote huwa wanaweka kambi hapo Beit Bridge.

Rushwa ipo Afrika nzima.
 
Nakumbuka mwaka 2007 nilikua na ndoto za kwenda dzonga ila sikua na mpunga, kuna jamaa yangu alikua amerudi toka lebanon huko alikua deployed kwenye peace keeping alikua amerudi bongo na fedha za kigeni nikaona kupitia huyu mwamba nitapata nauli nitambae zangu ng'ambo.
Nikawa chawa wa mwamba full kumsaidia kusolve harakati za hapa na pale kutokana na uzoefu wangu wa mtaa
Sasa bhana mwamba alikua na binti mmoja wa kitanga ndio alikua anataka amfanye mkewe ili dingi yake ni mnoko kikuda mchumba ndio alituambia kipindi mwamba anampa idea ya kwenda bumbuli kujitambulisha ,mimi kama chawa nisie na maadili nikamshauri mwamba ampe binti ujauzito ndio tuende ili zoezi liwe rahisi mwana apate jiko na mimi niende zangu ng'ambo.
Mwamba akafanikiwa kurutubisha yai binti kitumbo kikaota ikapangwa safari ya kwenda usambaani kuonana na wazee.
Kufika Tanga tukapokelewa fresh na bimkubwa, na mashemeji kumbe kamanda walikua wanamjua wote kasoro mshua boy tu, na bahati mbaya au nzuri hakuwepo siku hio ikabidi mzee apigiwe simu alikua shambani kwake huko anakaaga hata mwezi bila kurudi home. Alitaarifiwa uwepo wetu akaombwa arudi fasta mzee akaomba aongee na muoaji, mshkaji akatoka nje kuongea na mkwewe, mzee akamwambia jamaa anarudi kesho jioni lakini asitukute nyumbani kwake na hataki kabisa kutusikia, mshkaji kwa tabia zake za kijeshi akamkazia mzee na mikwara ya hapa na pale kwamba hatuondoki tutakaa hata mwezi mpaka arudi tuondoke na mke wetu. Mshua akasema kesho jioni anarudi lakini hatotukuta maana tutaondoka bila kuaga kamanda akasema sawa ngoja tuoneshane umwamba.
Ilifika usiku tukapewa room ya wageni kuna bed mbili kila mtu na lake, tukaangusha na mwanangu ,tulienda na begi moja tu , mchumba aliliweka chumbani kwake kwa usalama zaidi maana chumba chetu kilikua nje,
Kufika mishale ya saa nane usiku niliota ndoto kwamba yule mzee kaihamishia mimba kwa mjeshi halafu tuko leba kamanda anajifungua, mimi na manesi tunamwambia mchizi push! push! Jamaa anapiga kelele kumbe mimi nivyoota hivyo napiga kelele kwanguvu na jamaa naye anaota ndoto hiohio na anapiga kelele za uchungu mara tukashtuka wote mshkaji ananiuliza mtoto wangu yuko wapi nikamjibu kua makini usimlalie kuinuka dah! Mwamba alikua kashusha bonge la kimba mazee halafu hawezi kulikataa yaani kafanana nalo copyright alafu mashuka yote kitanda kizima kilikua makimba tu , nikampa mashuka ya kitandani kwangu ajisafishe tutoroke kabla hakuja kucha maana asingeweza kubadili nguo zilikua chumbani na mama kijacho mjeshi akaniambia kukimbia ni mbinu ya kijesh kabisa wao wanaiita ku retreat.
Tulitoka chumbani mule kwa kucraw mpaka kwenye toyota porte yetu huku mchizi akiwa kajifunga shuka rubega tukatokomea
Tukiwa njiani mwamba ndio akakumbuka conversation yake na mkwe wetu kwamba tutaondoka bila kuaga kama PAUL KEAGAN
Tulifaka town hata mawazo ya kumpiga mzinga wa nauli ya kaisha maana analia tu kama kabinti muda wote
 
Konda Msafi ana wivu sana. Ameona huu uzi unamfunika kwenye ule uzi wake wa Khumbu anaanza majungu, mara amuulize jamaa maswali yasiyo na kichwa wala miguu.

Mfano, eti ukioverstay South Africa huwezi kupita kwenda Lesotho hata kwa rushwa...kkkk, rushwa (kitu kidogo) ipo kila mahali.

Kuna mwaka nilikuwa natoka SA na basi la Shalom kwenda Lusaka ili niunganishe kuja Nakonde/Tunduma, Kondakta wa basi anatangaza kabisa kama passport yako ina shida (umezidisha siku za kukaa SA)nione, anazikusanya hizo passport na Rand 300 kila moja anaenda kuwagongea nyie mnasubiri kwenye basi. Tena ilikuwa December kipindi kibaya Home Affairs wote huwa wanaweka kambi hapo Beit Bridge.

Rushwa ipo Afrika nzima.
Mkuu nilitaka nisikujibu ila nimeona nikikaa kimya watu wanaweza kuamini hiki ulichokiongea. Humu bhana hatujuani, hata wewe hunijui ila umeongea kama unanijua. Kama hatujuani huo wivu unaouongelea wa nini? Pili niwie radhi kukuambia kuwa kuna vitu huvijui na ni bora ukakaa kimya kuliko kujiaibisha. Kuhusu kuoverstay na kugongewa exit nina uhakika kuna kitu umekificha na kama hujakificha basi huyo kondakita alikuficha. Ukiover stay halafu ukawa unarudi kwenu immigration officer hawawezi kukuzuia kurudi kwenu japo wakikufanyia roho mbaya wanaweza kukukamata na kukufungulia mashitaka ila kwa sababu ulitoa rushwa ya rand 300 wanaweza kukuruhusu uondoke nchini mwao ila huwezi kukanyaga nchini kwao ndani ya miaka 5 kama hutalipa hiyo fine ya kuover stay. Ndio maana nimekuambia kuna kitu hujakiongea kuhusu kuoverstay au huyo konda wa basi hakukuambia. Ukioverstay ukiwa unarudi kwenu in most cases watakuruhusu upite ila utapigwa fine ambayo utaambiwa either uilipe hapo hapo au ukailipie ubalozini kwao nchini mwako. Usipoilipa huwezi kurudi tena nchini kwao kwa muda wa miaka 5 labda ubadirishe passport, na sasa hivi hata ukibadirisha passport ni kazi bure maana finger print zako zitasoma kwenye system yao. Kuna mengi ningekueleza ila acha niishie hapa.
 
Back
Top Bottom