Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

Ki ukwel wanasikitisha sana wanapeana na mbinu za kuwapata matajiri ili waolewe katikat ya Uzi wa mtu tena uzi unatufundisha watu mwingine anamatako makubwa wengine kukosoa hebu tupunguze ujuaji kidogo hata mleta Uzi nikituma hii episode sijui watanikosoa tena kuna mmoja alileta Uzi wake humu alikua akikosolewa anasusa na kutishia kuto kuendelea nashangaa kwenye Uzi huu kawa mkosoaji no 1 mkuu unaharb Uzi kama anakosea mwache hivyo hivyo (mgombea urais 2025) umejijua
Hahaha
 
SEHEMU YA KUMI NA TATU

Basi nilikaa pale Kanisani mpaka Asubuhi, wakati najiandaa kuondoka nikakutana tena na Yule Dada. Nakumbuka aliniuliza naishi wapi, nikamwambia Pretoria. Akasema mbona unaishi mbali sana, Gari za Kanisa lao halina rut za huko. Akaniambia kama sitojali, Kanisa kuna nyumba limewapangishia waumini wake wale ambao wanajitolea Kanisani. Akasema ataongea na Jamaa mmoja anaishi room peke yake, kama huyo jamaa atakubali basi atanipigia simu kuniambia.

Ukweli Yule Dada alionesha kunichangamkia sana. Basi nikaondoka zangu pale mpaka Pretoria kwa washkaji zangu wa Kibongo. Ukweli kama nilivyosema mwanzo, Mbongo yeyote ukianza kufanya harakati zako tofauti na wenzio wanaanza kukusema sema. Hili natoa kama angalizo kwa mtu ambae hajawai kufika South, lakini inabidi uwe na moyo mgumu kuweza kufuata ndoto zako.

Basi nikafika mpaka kwa Jamaa Y, akaniuliza kuhusu habari za Kanisani nikamjibu kwa ufupi tu kuwa ni safi tu. Sikutaka kumwambia kila kitu kilichoendelea kule kwa sababu ningewapa mada ya kunijadili zaidi. Kichwani niliwaza endapo Yule demu atanicheki kuniambia kuwa amepata chumba kule Midrand basi hawa jamaa nitawadanganya kuwa kule Midrand nilikutana na HomeBoy wangu Kabisa wa Mtaa mmoja hapa Temeke. Homeboy amesema nikaishi nae. Nilipanga kuwadanganya hivyo ili wasijue chochote kuhusu mpango wangu.

Basi siku zikaenda, kama kawaida asubuhi tunaenda kusimama kule Barabarani na Jamaa Y. Tayari nilishafikia hatua ya kupewa Kazi mbili tatu za kuwapelekea jamaa Fulani madawa, nilikuwa nafanya hivyo, lakini moyoni sikuwa comfortable, Nilikuwa najiuliza, ina maana mimi South nimekuja kuuza Madawa? Najisemea Hapana. Hapa lazima niendelee kutafuta Mchongo wa Halali. Jamaa Y alikuwa akikutuma kumkatalia unashindwa, kumbuka unaishi kwenye chumba ambacho yeye ndo analipia Kodi. Muda mwingi unakula chakula chake. Kwa hiyo akikutuma huwezi kumkatalia. Basi nikawa napiga michongo hiyo hapo ya hapa na pale, Siku nikipata nafasi ndo nilikuwa naenda kule Midrand Kanisani. Wale Vijana ambao Jamaa Y amewaleta South yan utawaonea huruma, wanapiga Kazi kama punda. Wao wanainjoi tu kuishi Ghorofani, Kuvaa vizuri na kula KFC.

Mpaka siku ambayo Yule demu wa Kanisani alinicheki kwa simu na kuniambia Jamaa amekubali nikaishi nae. Nilifurahi sana. Jamaa zangu ziliwadanganya kama nilivyopanga. Jamaa Y alikubali niondoke lakini sura yake ilionesha kutokupendezwa na mimi kuaondoka pale. Alikuwa ananiambia maneno Fulani hivi ya kunitaka niwe makini. Alisema majamaa wengine sio wazuri sana kuishi nao. Nikamwambia mimi naenda lakini nitakuwa narudi hapa mara kwa mara. Jamaa alikubali kishingo upande. Hata sikuchelewa zangu nikawaaga jamaa, nikabeba begi langu nikasepa.

Kwa kifupi nilikuja kujua kwamba Yule demu wa Kanisa anaitwa KANYA, Alikuwa ni mmoja wa waimba kwaya muhimu pale Kanisani. Waimbaji wote walikuwa wanaishi kwenye nyumba nzima ambayo walipangishiwa na Kanisa. Alivyonicheki aliniambia tukutane sehemu mmoja inaitwa KALFONTEEN, Sio mbali sana na Midrand. Aisee nakumbuka ile siku hadi kufika huko KALFONTEEN nilipotea sana. Yan kilichotokea ni kwamba mfano wewe hapa Dar unaishi Tegeta halafu mtu akwambie njoo tukutane Makumbusho, Halafu wewe upande daladala mpaka Kariakoo, ukifika Kariakoo ndo utafute Daladala za Makumbusho uende zako Makumbusho. Wenzetu miji yao mikubwa, barabara nyingi mpaka mtu unachanganyikiwa.

Hatimae nilifika mpaka aliponiambia Kanya tukutane, hapo nina begi langu Mgongoni. Hao mdogo mdogo kwa mwendo wa miguu akanipeleka kwa huyo jamaa ni raia wa Ghana anaitwa Thomas. Maisha yangu mapya yalianzia hapo Kalfonteen. Yan kwenye Chumba tulipokuwa tunaishi na Thomas na kule Wanapoishi Wadada waimbaji sio mbali sana. Tuliishi kwenye Chumba Kimoja kikubwa, Jiko na Choo. Hakukuwa na Sebure. Thomas alikuwa na visa vingi sana, kwa sababu kabla ya mimi kufika pale yeye na rafiki zake wengine wa Kanisani ndo walikuwa wana date na wale wadada waimba kwaya, nilivyofika mimi kibao kikageuka. Basi pale maisha yangu na Thomas yakawa magumu mno mpaka nikawachukia Waghana wote. Mpaka Nikatamani kurudi Pretoria kwa Jamaa Y.

Sehemu inayofuata nitaelezea maisha yangu na Thomas yalivyokuwa, Mapenzi yangu na Kanya yalivyoanza na Harakati zangu za kuanza kutafuta mchongo wa Halali.
Ntarudi badae
 
Uko sahihi kabisa mkuu. Mimi nimekaa capetown miaka mitano..bahati nilikua na permit ya kusoma. Ila niliona wabongo wengi sana wakipata shida hiyo ya kuishi na expired visa. Yaani huishi kwa amani na kila ukiona polisi presha inapanda.

Na mimi nataka nijue keagan alisafiri vipi kwenda lesotho visa yake ya SA ikiwa imeexpire...maana pale border wakiswap passport yake system hapo hapo inawashtua kwamba huyu mtu akamatwe kwa kuoverstay. Na kama hawajamkamata lazma wajieleze kwa wakubwa zao maana system inatuma taarifa. Na kama alitoka na kuingia lesotho alirudi vipi SA? Maana adhabu ya kuoverstay ni kwamba huruhusiwi kurudi SA kwa miaka mitano.

Na mimi nasubiri sana ufafanuzi
Na mm pia
 
Mimi ni mwanaume lakini niseme ukweli. Katika nchi zenye wanaume wa hovyo hovyo, wavivu na saa zote wanawaza ngono wanapoona mwanamke ni Tanzania. Tuko nyuma kweli kweli na hatujui dunia inakokwenda. Na hali imekolezwa zaidi na mitandao kuingia. Watu wana approach kila wanayedhani ni mwanamke kwenye mtandao. Comments zimejaa sexism za kijinga na zilizopitwa na wakati. Habari ya nzuri yenye mafundisho mazuri ikiambatana na picha ya mwanamke watu wanakimbilia ku-comment kuhusu yule mwanamke na kuacha habari. Hii ni sehemu nzuri sana ya kuingiza kipato kwa wale matapeli wanaijifanya ni wanawake wanaotafuta wanaume.
Si tu Tanzania hayo ni miongoni mwa madhara ya mitandao ya kijamii ukiachilia mbali faida zake lukuki.
 
Tatizo la watu humu JF wanapenda kusikia kile wanachotaka kusikia. Mtu ukiwa na mawazo kinzani kidogo japo ya kuwasaidia wanakuona kama umekuja kuharibu stori wakati hayo mawazo huenda yakawasaidia vijana ambao wengependa kujaribu bahati zao nje ya nchi. Story ya bwana Keagan Paul ni nzuri sana na inatoa darasa kwa vijana wenye ndoto za kutaka kusaka maisha nje.

Tatizo kuna details ambazo kuna watu humu huenda wakazichukua kama zilivyo bila kuchanganya na za kwao wakajikuta matatani. Naweza kusema bwana Keagan alikuwa na bahati sana tena sana, nadhani waliokaa South Africa watakubaliana na mimi kuwa alikuwa na bahati sana. Kitendo cha kuishi bila permit halafu unajiachia hivyo ni bahati sana kusurvive.

Kwa hiyo vijana wale mnaotaka kwenda huko muwe makini, bwana Keagan kama aliweza kujiachia bila permit msidhani maisha ndio yako hivyo, utadakwa dakika moja tu na kupelekwa sehemu inaitwa Lindela kusubiria kuwa deported. Kama nilivyosema kitendo cha kusafiri kwenda Lesotho wakati viza imeexpire ni bahati ya mtende na pia nampongeza sana kwa huo ujasiri.

Viza ikiexpire ukiwa ndani ya nchi ni kesi kubwa sana halafu akaamua kusafiri kwenda nchi nyingine wakati anajua hata kibali cha kuwemo nchi husika hana, huo ni ujasiri mkubwa sana na nachelea kumpa pongezi maana alikuwa kama anajiweka kwenye mazingira ya kurahisisha ukamatwaji wake.

Kwanza najiuliza walifikaje boarder ya Lesotho bila kukutana na roadblock hata moja na kukaguliwa ID zao? Pili yule immigration officer wa upande wa South Africa aligongaje exit stamp bila kumkamatisha kwa kosa la kuishi nchini illegally, najua amesema aliweka rand 300 kwenye passport.

Haya wakati wa kurudi aliwezaje kuingia tena SA wakati viza ilishaexpire? Bwana Keagan ukipata muda naomba uelezee kidogo kuhusu issue ya kutoka na kuingia tena South Africa wakati viza imeisha ili vijana wajifunze maana kuna wengine wanaweza kudhani kuishi bila vibali South Africa sio tatizo wakati ni tatizo kubwa sana linaloweza kuwapeleka jela.

Viza ikiexpire kisheria huwezi kurenew ukiwa ndani ya ardhi ya South africa hata kama unatoka SADC lazima utoke nje, na utapata misukosuko sana.
Rejea kitabu cha mbio za jasusi... Haahahhhahhh watu wana bahati zao lakini kuishi ughaibuni bila permit ni sawa na kulala chumba kimoja na chatu mwenye njaa.. Kama hapo Kenya tu inakuwaga msala cjui SA inakuaje.. Anyway tuendelee kunywa mchuzi nyama zipo chini
 
Tatizo la watu humu JF wanapenda kusikia kile wanachotaka kusikia. Mtu ukiwa na mawazo kinzani kidogo japo ya kuwasaidia wanakuona kama umekuja kuharibu stori wakati hayo mawazo huenda yakawasaidia vijana ambao wengependa kujaribu bahati zao nje ya nchi. Story ya bwana Keagan Paul ni nzuri sana na inatoa darasa kwa vijana wenye ndoto za kutaka kusaka maisha nje.

Tatizo kuna details ambazo kuna watu humu huenda wakazichukua kama zilivyo bila kuchanganya na za kwao wakajikuta matatani. Naweza kusema bwana Keagan alikuwa na bahati sana tena sana, nadhani waliokaa South Africa watakubaliana na mimi kuwa alikuwa na bahati sana. Kitendo cha kuishi bila permit halafu unajiachia hivyo ni bahati sana kusurvive.

Kwa hiyo vijana wale mnaotaka kwenda huko muwe makini, bwana Keagan kama aliweza kujiachia bila permit msidhani maisha ndio yako hivyo, utadakwa dakika moja tu na kupelekwa sehemu inaitwa Lindela kusubiria kuwa deported. Kama nilivyosema kitendo cha kusafiri kwenda Lesotho wakati viza imeexpire ni bahati ya mtende na pia nampongeza sana kwa huo ujasiri.

Viza ikiexpire ukiwa ndani ya nchi ni kesi kubwa sana halafu akaamua kusafiri kwenda nchi nyingine wakati anajua hata kibali cha kuwemo nchi husika hana, huo ni ujasiri mkubwa sana na nachelea kumpa pongezi maana alikuwa kama anajiweka kwenye mazingira ya kurahisisha ukamatwaji wake.

Kwanza najiuliza walifikaje boarder ya Lesotho bila kukutana na roadblock hata moja na kukaguliwa ID zao? Pili yule migration officer wa upande wa South Africa aligongaje exit stamp bila kumkamatisha kwa kosa la kuishi nchini illegally, najua amesema aliweka rand 300 kwenye passport.

Haya wakati wa kurudi aliwezaje kuingia tena SA wakati viza ilishaexpire? Bwana Keagan ukipata muda naomba uelezee kidogo kuhusu issue ya kutoka na kuingia tena South Africa wakati viza imeisha ili vijana wajifunze maana kuna wengine wanaweza kudhani kuishi bila vibali South Africa sio tatizo wakati ni tatizo kubwa sana linaloweza kuwapeleka jela.

Viza ikiexpire kisheria huwezi kurenew ukiwa ndani ya ardhi ya South africa hata kama unatoka SADC lazima utoke nje, na utapata misukosuko sana.
Watu wengi yakishatukuta ndiyo tunaamini binafsi nimeelimika vyakutosha kuna vitu nimejifunza na kuna vitu si vya kujaribu labda itokee kama sina namna yakufanya ila tu ni njia ya kunifikisha kwenye safari yangu. Huwezi kuelezea kile mtu anachotaka kusikia isipokuwa eleza kile unachokijua.
 
Hiki kitu ndo kinanikwaza sana ...mwanamke ukijipeleka sehemu kama KFC kurefresh kwa hela yako watu wanadhani unadanga...ukinunua kagari kwa saving zako wanahisi umehongwa...ukianda cheo kazini kuna watu wapumbavu wanahisi unatembea na boss...watu wanawaza ngono ngono ngono muda wote
Mimi ni mwanamke sex ni part muhimu sana ya maisha lakini sio first priority katika maisha na sipendi initawale...napenda sana kuwa na marafiki wa kike na kiume ila sipendi kutongozwa...najikuta napata wakati mgumu kwa baadhi ya watu...ukimchekea tu kashawaza kukufunua nguo...come on maisha ni ziadi ya sex...watu hawawazi productive friendship bila ngono...and i hate that...ngono ngono ngono why?!
Nakukunda
 
Hiki kitu ndo kinanikwaza sana ...mwanamke ukijipeleka sehemu kama KFC kurefresh kwa hela yako watu wanadhani unadanga...ukinunua kagari kwa saving zako wanahisi umehongwa...ukianda cheo kazini kuna watu wapumbavu wanahisi unatembea na boss...watu wanawaza ngono ngono ngono muda wote
Mimi ni mwanamke sex ni part muhimu sana ya maisha lakini sio first priority katika maisha na sipendi initawale...napenda sana kuwa na marafiki wa kike na kiume ila sipendi kutongozwa...najikuta napata wakati mgumu kwa baadhi ya watu...ukimchekea tu kashawaza kukufunua nguo...come on maisha ni ziadi ya sex...watu hawawazi productive friendship bila ngono...and i hate that...ngono ngono ngono why?!
Pole hujapata mwanaume wa kukukunja vizuri pia hujapata mwenye tango nene pole sana dada ila ukipata mda njoo kwangu ili ukasimulie wenzio
 
Vailetii we ndo kekii mwngne fekii natamani uwe alizetiii nileee

Jamaa kashatekwa na Mr Y huko maana pale alipomtaja vaileti tayari kashamuuza
 
Back
Top Bottom