Nilipata ulemavu sababu ya Mapenzi

Nilipata ulemavu sababu ya Mapenzi

Nikupe pole tu ndugu yangu....Nakushauri ujikubali uanze upya hivyo ulivyo... Maisha lazima yasonge mbele...huyo hakuwa wako...alikutumia kwa malengo yake....wako wa shida na raha anakuja kama utakuwa tayari kuyaacha yalopita.

Tunaondokewa na wapendwa wetu wa damu kabisa ..tunazika na maisha yanaendelea sembuse huyo.....usikumbatie tatizo...hata ungefanikiwa kuwa nae ungechapiwa vile vile.
 
Daaah pole sana ndungu! Mapenzi haya jamani wanaume sijui tumelogwa na nani unamfunguliaje biashara demu tu tena kwa hela ya mkopo bank? fanya hivi kwa mkeo tu sio kimada madhara yake ni makubwa hawa viumbe ni wa kuishi nao kwa akiri sana otherwise ni mateso ya maisha kama haya, Kumsomesha mwanake kabala hujamuoa,kumfungulia biashara, acha huo upuuuzi utakuja kujuta, au kumpa mavitu ya dhamani kuliko uwezo wako kwa kutaka kujionyesha wewe mwanaume ni hatari kwa afya yako .
Labda sikio la kufa! Kama mwanaume umeamua kuwekeza kwa mwanamke ambaye si mkeo basi fanya hivyo kama msamaria mwema ili mambo yakigeuka mezea na songa mbele.
Pia tujifunze kufanya mambo yaliyo ndani ya uwezo wetu, sio kufurahisha wengine wakati unajiteketeza, tuwe na kiasi. Hao waliopo kwenye ndoa tu changamoto sembuse mpenzi?.
 
Daaahh mapenzi haya jaman.......nimuhimu Sanaa mtu kujifunza mapema namna ya kuruhusu mapenzi yasikutawale......na hii imenipa nguvu kuendelea kuwa hii tabia yako ya mim kuonekana sipo romantic na Wala sijui kujali...

Natamkiwa hii kauli karibu kwa kila mwanamke ninae kuwa nae kwnye mahusiano...!!
Haikua hivi mwanzo.....nilianza kuwa hivi baada ya kugundua mapenzi yanaweza kuniharibia maisha yangu Kama nikiendekeza kuyaabudu.

Hata mke wangu asije tegemea kwamba love yangu kwake itavuka beyond 70%......never....!!!

Mwanamke hata umpende vipi!! Umjali vipi!!! Kitandani umfanye kwa mastyl yote tena kwa rate ya 1hr/bao........bado itafika tu time atakuletea pigo za usaliti na dharau...

Na tangu niutrain ubongo na moyo wangu kuwa hivi,,,,,,imekuwa very easy to let it go......!!!
Yani nikishaona tu mwanamke kaanza kubadilika vitabia, majibu ya hivyo, misunderstanding, dharau, poor communication.....basi fasta sana napiga u-turn na kuendelea kula maisha katika njia zingine.
Na Cha ajabu ni kwamba hii imekua Kama dawa katika mahusiano yangu.....wengi wao wamekua wakijirudi baada ya kugundua wananiletea ujinga wakitegemea ntateseka kumbe holaahhhh.......

That is my principle!!!

Pole Sanaa ndugu yangu kwa yalio kukuta....Mungu akasimame na ww
Amen na asante ndugu kwa ushauri
 
Nikupe pole tu ndugu yangu....Nakushauri ujikubali uanze upya hivyo ulivyo... Maisha lazima yasonge mbele...huyo hakuwa wako...alikutumia kwa malengo yake....wako wa shida na raha anakuja kama utakuwa tayari kuyaacha yalopita.

Tunaondokewa na wapendwa wetu wa damu kabisa ..tunazika na maisha yanaendelea sembuse huyo.....usikumbatie tatizo...hata ungefanikiwa kuwa nae ungechapiwa vile vile.
Asante dada angu kwa ushauri.
 
Pole Sana mkuu

Ila kuhusu suala la deni naamini benk nyingi Zina kipengele cha disability kama security ya kutokuendelea ila lazima iwe permanent na iathiri ufanisi wako wa kazi

Ivo fuatilia mkataba maana uwa hatusomagi
 
Amen na asante ndugu kwa ushauri
Kwa kujazi nakushauri ifanye haya..

1. Kama unatumia pombe ili kuondoa mawazo acha!

2. Tafuta hobby ya kukukip busy! Nashauri anza kushabikia mpira! Tafuta timu ya kushabikia, nakushauri kama huna timu anza kushabikia man united na simba kwa bongo!

Yani ikifika weekend jichanganye kwenye kibanda umiza kama huna tv!

Ukitoka hapo akili itakua imetuliaaaa... rudi geto jipange kwa ajili ya kesho!!

3. Anza kuangalia namna ya kujiajiri. Tumia muda mwingi kuweka akili yako kwenye biashara yako.

4. Kaa mbali na mapenzi kwa sasa.

5. Futa kila kitu kinacho muhusu huyo mwanamke... kuanzia namba mpaka picha.. hii ndio hatua ya kwanza ya kumsahau (actually hii nlitaka kuiweka namba moja...)

6. Anza kuwa karibu na Mungu (Muhimu).

Pole sana na nikutakie kila heri.

Mshana Jr Divine... Heaven Sent et al.,
 
Pole Sana mkuu

Ila kuhusu suala la deni naamini benk nyingi Zina kipengele cha disability kama security ya kutokuendelea ila lazima iwe permanent na iathiri ufanisi wako wa kazi

Ivo fuatilia mkataba maana uwa hatusomagi
@Chapati 2 fwatilia huu ushauri..

Hata mimi nilisha sikia hii kitu na sio ulemavu tu mkopo lazima uwe na bima!!

Kwasababu mleta mada hana kazi na ana ulemavu basi aende benki na uthibitisho wa dokta.

Naiman anaweza samehewa deni.

Narudia tena mleta mada soma upya mkataba wa mkopo wako na uende benki ukawape facts juu ya ulemavu wako.
 
Habarini


Jana katika kupitia taarifa za group, la shule niliyosoma secondary, nakutana na ujumbe kuwa naima, anaolewa jumamosi ya leo, nimekosa raha ndugu zangu, kwani ni miaka takribani 13 imepita nikijitahidi kusahau, ila kila nikiangalia hali yangu ya ulemavu najikuta nakumbuka na kuyachukia mapenzi.


mimi nilizaliwa mzima kabisa na sasa nina miaka 35, baada ya kumaliza chuo, nilikuwa na mahusiano na binti fulani ambaye tulisoma nae secondary hapa dar, nakumbuka kuonana nae ilikuwa ni kama bahati tu na kila muda naumia natamani nisingeonana nae labda leo hii ningekuwa mzima kabisa.


Mwanzo alikuwa ni mtu wa kipekee sana, nilijulikana kwao na kwetu walimjua, na kwakuwa nilikuwa na kazi private office moja hapa mjini(sitapenda kuitaja) nilijitahidi fanya uwekezaji mdogo kwake nilikopa kiasi fulani cha pesa mil 7 kwa dhamana ya kazi nikamfungulia duka kwa matumaini ya kuwa, kwakuwa sisi ni kitu kimoja mwenzangu nae asimame kwani alikuwa anashinda tu nyumbani kwao.



Nilipata misukosuko kazini na nikasimamishwa kazi na hapo ndipo nilipoanza kutoelewana na mwenzangu dharau ilikuwa kubwa, kejeli, unamuomba muonane anagoma au anakubali na hatokei kabisa na simu anazima, ndani ya miezi miwili, nilikuwa nimepata msongo mkubwa wa mawazo maana madeni na hali ngumu na mwenzangu haeleweki sikujua nifanye nini zaidi ya kunywa pombe.


siku ya tukio jumatano ile niliamka mzima kabisa, jioni nilipanga kwenda alipopanga naima bila taarifa kwani kila nikimjulisha basi hatoi ushirikiano. Nilitaka tukubaliane tuuze duka nifund hela kidogo ya kiwanja nilichonacho nifungue biashara nyingine, inisaidie kufanya marejesho bank.


sikuwahi fikiria kama ananisaliti nilijua tu ni kutingwa na kazi na kuwa na mood mbaya, saa 1 nilienda kwake kwakujua aliishafunga biashara nilivyofika kwake, niligonga mlango kukawa kimya, nilikuwa na funguo za kwake na yeye alikuwa nazo za kwangu nikafungua mlango


Sikuamini macho yangu naima alikuwa na rafiki angu kipenzi salim wakifanya mepenzi pale sebuleni wakapigwa na mshangao kwani hawakunitarajia, nilirudi nyuma na kuanza kutoka pale nikiwa na maumivu zaidi na kujiona sifai nikiwa mita chache tu kutoka pale nikivuka barabara nilisikia honi ya gari mara 2 baada ya hapo sikukumbuka kitu tena.



baada ya kuamka nilikuta ndugu zangu wakiwa hospital namimi wakiwa na huzuni, baada ya siku 2 ndiyo niligundua mguu wangu wa kushoto sina tena nilielezwa uliharibika kutokana na kusagwa na gari, nililia sana na bado nalia sana, nilijiuliza nimefanya dhambi gani kustahili adhabu hii, niliwaza nitalipaje deni la bank na nitawezaje kuanza maisha katika hali yangu ya ulemavu.


baada mwezi 1 nanusu nikatoka hospitalini, ila ikawa kama ninamkosi kwani baada ya mwezi nilikamatwa na malaria kali sana nikajua ndio mwisho wa maisha yangu, nilikuwa naweweseka sana, hospital wakaniwekea dripu ya Quinine, masikini ningejua naenda pata ulemavu mwingine ni bora ningejitibia nyumbani, ila nilipona vizuri baada ya week tu


baada ya miezi 7 nilianza poteza uwezo wa kusikia taratibu na kupoteza balance ya kutembea sikugundua mapema ila baada ya kufikisha mwaka na miezi 2, nilikuwa natatizo lingine la kutosikia vizuri.


Maisha yangu yalibadilika sikuwa na furaha tena na leo hii mwanamke alieniharibia maisha yangu ambaye naamini ni chanzo cha ulemavu wangu anaenda kuolewa najiuliza nimeikosea nini dunia, muda mwingine natamani kufariki kwani ninayopitia ni mazito kushinda uwezo wangu wa kustahili.

ewe maisha nilikukosea nini?
Umeongea kwa hisia sana Kaka,Inaumiza sana,Lakini mtumainie Mungu bro atakushindia katika mengi haya maisha kuna wakati yanatugeuka na kutuumiza lakini tumtazame Mungu analo tumaini letu
Honestly nimeumia sana
 
Pole broo .....lakini mbona kila siku tunawaambia humu kuwa mwanaume ishi maisha yako kwanza mbona hamuelewi.....? Tatizo ni ubishi na kujiona nyie ndio romantiki sana kushinda babu zenu na baba zenu....! Inauma sana ila ndio ishakuwa tutafanyaje sasa ...
Ishamtokea mwenzetu so mda wa kumalalamikia, sasa nimda wa kumfariji maana hapo alipo anajuta.
Mpe maneno ya faraja so kumtonesha donda.
 
Hii
Habarini


Jana katika kupitia taarifa za group, la shule niliyosoma secondary, nakutana na ujumbe kuwa naima, anaolewa jumamosi ya leo, nimekosa raha ndugu zangu, kwani ni miaka takribani 13 imepita nikijitahidi kusahau, ila kila nikiangalia hali yangu ya ulemavu najikuta nakumbuka na kuyachukia mapenzi.


mimi nilizaliwa mzima kabisa na sasa nina miaka 35, baada ya kumaliza chuo, nilikuwa na mahusiano na binti fulani ambaye tulisoma nae secondary hapa dar, nakumbuka kuonana nae ilikuwa ni kama bahati tu na kila muda naumia natamani nisingeonana nae labda leo hii ningekuwa mzima kabisa.


Mwanzo alikuwa ni mtu wa kipekee sana, nilijulikana kwao na kwetu walimjua, na kwakuwa nilikuwa na kazi private office moja hapa mjini(sitapenda kuitaja) nilijitahidi fanya uwekezaji mdogo kwake nilikopa kiasi fulani cha pesa mil 7 kwa dhamana ya kazi nikamfungulia duka kwa matumaini ya kuwa, kwakuwa sisi ni kitu kimoja mwenzangu nae asimame kwani alikuwa anashinda tu nyumbani kwao.



Nilipata misukosuko kazini na nikasimamishwa kazi na hapo ndipo nilipoanza kutoelewana na mwenzangu dharau ilikuwa kubwa, kejeli, unamuomba muonane anagoma au anakubali na hatokei kabisa na simu anazima, ndani ya miezi miwili, nilikuwa nimepata msongo mkubwa wa mawazo maana madeni na hali ngumu na mwenzangu haeleweki sikujua nifanye nini zaidi ya kunywa pombe.


siku ya tukio jumatano ile niliamka mzima kabisa, jioni nilipanga kwenda alipopanga naima bila taarifa kwani kila nikimjulisha basi hatoi ushirikiano. Nilitaka tukubaliane tuuze duka nifund hela kidogo ya kiwanja nilichonacho nifungue biashara nyingine, inisaidie kufanya marejesho bank.


sikuwahi fikiria kama ananisaliti nilijua tu ni kutingwa na kazi na kuwa na mood mbaya, saa 1 nilienda kwake kwakujua aliishafunga biashara nilivyofika kwake, niligonga mlango kukawa kimya, nilikuwa na funguo za kwake na yeye alikuwa nazo za kwangu nikafungua mlango


Sikuamini macho yangu naima alikuwa na rafiki angu kipenzi salim wakifanya mepenzi pale sebuleni wakapigwa na mshangao kwani hawakunitarajia, nilirudi nyuma na kuanza kutoka pale nikiwa na maumivu zaidi na kujiona sifai nikiwa mita chache tu kutoka pale nikivuka barabara nilisikia honi ya gari mara 2 baada ya hapo sikukumbuka kitu tena.



baada ya kuamka nilikuta ndugu zangu wakiwa hospital namimi wakiwa na huzuni, baada ya siku 2 ndiyo niligundua mguu wangu wa kushoto sina tena nilielezwa uliharibika kutokana na kusagwa na gari, nililia sana na bado nalia sana, nilijiuliza nimefanya dhambi gani kustahili adhabu hii, niliwaza nitalipaje deni la bank na nitawezaje kuanza maisha katika hali yangu ya ulemavu.


baada mwezi 1 nanusu nikatoka hospitalini, ila ikawa kama ninamkosi kwani baada ya mwezi nilikamatwa na malaria kali sana nikajua ndio mwisho wa maisha yangu, nilikuwa naweweseka sana, hospital wakaniwekea dripu ya Quinine, masikini ningejua naenda pata ulemavu mwingine ni bora ningejitibia nyumbani, ila nilipona vizuri baada ya week tu


baada ya miezi 7 nilianza poteza uwezo wa kusikia taratibu na kupoteza balance ya kutembea sikugundua mapema ila baada ya kufikisha mwaka na miezi 2, nilikuwa natatizo lingine la kutosikia vizuri.


Maisha yangu yalibadilika sikuwa na furaha tena na leo hii mwanamke alieniharibia maisha yangu ambaye naamini ni chanzo cha ulemavu wangu anaenda kuolewa najiuliza nimeikosea nini dunia, muda mwingine natamani kufariki kwani ninayopitia ni mazito kushinda uwezo wangu wa kustahili.

ewe maisha nilikukosea nini?
Testimony yako inahuzunisha sana. Imenisilitisha sana. Kiukweli umepitia mengi sana hadi leo. Nakushauri uangalie NGOs zinazotoa misaada kwa walemavu. Wasiliana nao wakusaidie. Wanatoa hata grants za mitaji nk. Sio kirahisi sana, lakini usikate tamaa ukiambiwa hapana hapa na pale. Mwishowe utafanikiwa.

Kiukweli watu wengi mapenzi yanawaharibia maisha. Kuna hata watu wanajiua sababu ya mapenzi. Naomba kuanzia sasa ugundue kwamba matatizo yanatokea katika maisha ili KUTUIMARISHA. Wazungu wanasema, whatever doesn't kill you, makes you stronger. Tatizo sasa ni kwamba kwa baadhi ya watu.. badala ya janga la maisha kukuimarisha linakudhoofisha.

Hapo ndio kosa ulilolifanya ulivyomkuta mpenzi yuko na best yako. Ujue ulemavu wako wala yeye hajali, na hata ungekufa, asingejali. Hakuna mtu wa kujali maisha yako, malengo yako, na mapambano yako zaidi yako ww binafsi. ULIRUHUSU AKAKUCHANGANYA AKILI, HADI UKASAHAU UNAVUKA BARABARA.

Binafsi, natumia changamoto kama hizo zinakuwa MOTO katika maisha yangu ya kuendelea mbele na kufanikiwa sana, na kuwaangamiza kabisa kimawazo wanaonitakia ubaya. T Woods alisema winning takes care of everything.

Inatakiwa mtu kama huyo anakufanya unakuwa IMARA, hata kama inaumaje.. usiruhusu malengo yake ya kukurudisha nyuma yakatimia. Kumbuka ukitetereka NDIO RAHA YAKE
 
Back
Top Bottom