Nilipata ulemavu sababu ya Mapenzi

Nilipata ulemavu sababu ya Mapenzi

Nafahamu ni ngumu mno lakini ninakuomba jitahidi umsamehe.

Kwenye kumsamehe vitu vingi sana vitafunguka upande wako bila kutegemea.
Kilicho moyoni mwako kwa sasa ni uchungu.achilia uchungu kwa kumsamehe uambie moyo wako una nafasi ya kufurahia maisha kwa mara nyingine.amini kila kitu hutokea kwa sababu mshukuru Mungu kwa kila kilichotokea kwenye maisha yako ndugu yangu
Asante dada yangu niombee niweze kuzuia hii chuki na majuto.
 
Pole sana Chapati 2 amini Mungu yupo pamoja na yote hayo unayopitia. Mungu ametuficha mengi mno ila kwa yote yanayotokea yapo chini ya uweza wake

Pia usijione umefika mwisho wa maisha yako ila ona kwamba huu ndio mwanzo wa maisha yako na bado unaweza kuwa bora. Mungu akupe imani na ustahimilivu
Asante dada naomba neno lako likawe baraka kwangu
 
Mpokee YESU kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako, utapata faraja ambayo hatuwezi kukupa. Kingine piga moyo konde na maisha lazima yaendelee. Hayo yaliyokupata naamini ni mipango ya MUNGU na kama sio mipango ya MUNGU ni MUNGU ndio karuhusu yakupate angeweza pia kuzuia hayo yasitokee. Songa mbele kila kitu kinatokea kwasababu, usijilaumu, jikubali songa mbele
Amen nitaufanyia kazi ushauri wako ndugu
 
Pole sana kama ni kweli
Ifikie wakati sasa wanaume tujitambue, kwani wewe sio wa kwanza kupatwa na mkasa kama huo kwenye maisha, kabla ya kuangalia utamsaidiaje mwanamke umpendae ili kuweza kujikwamua kwenye lindi la umaskini, basi ni vyema kuanza kujipanga na kujiimarisha mwenyewe katika maisha yako kwa kuwa na mikakati na mipango imara.

Hii itatusaidia pale ambapo uliejitolea kumsidia hata asipokujali basi maisha yako hayatotetereka wala kuyumba.

Wanaume tunajiona tuna upendo kiasi kwamba tunajisahau kupenda maisha yetu na kuhamishia upendo wote na kutaka kuwajengea maisha bora tuwapendao, hii tabia mara nyingi huwa inatucost pale tunapopatwa na majanga kwani hao tunaowajengea upendo huwa hawana upendo wa dhati kwetu.

Tuachane na hawa viumbe, wajengewe upendo na familia zao tusiwe watu wa kutumika kama daraja na badala yake mwanamke baada ya kupata mafanikio kiasi wanatuona sisi kama takataka. Na endapo tukipatwa na matatizo ndio wanatuacha njiani kama hawatujui na badala yake ana move on kuelekea kwa mwengine.

Tujifunze kutokana na makosa ya watangu wetu, naamini hata wewe ulishawahi kusikia/kuona mwengine kupatwa na mkasa kama huo kabla yako lakini hukujifunza na kuhisi hautakuwa miongoni mwa watakaopatwa na mkasa kama huo.

Pole sana
Bonge la point
 
Kitu nilichojifunza in life, kila binadamu anabadilika na haijalishi utawapa nini ambacho unadhani kitawafunga in life lakini wakikutana na watu au mazingira mengine watabadilika tu.. so, usijilaumu kwa kuwa mwema au kuyalaani maisha yako maana ndio uhalisia wa dunia ilivyo

Pia Pole sana maana naelewa unachokipitia lakini usijilaumu kwa yaliyotokea au kwa ulivyopoteza maana mara nyingine maisha hutufundisha masomo tunayoyahitaji kwa njia ngumu sana kama yako. hivyo Jifunze kwa ulipokosea na uanze kuhesabu kila baraka iliyobakia katika maisha yako na utajifunza kuyapenda tena kama yalivyo.

Naamini utakaa poa brother
 
Asante mkuu natamani ningejua ya kesho nikakwepa kuonana nae ila haisaidii mwenzangu leo anafuraha mimi ninamajuto
Hakuna ajuae kesho yake na kupotea njia ndio kujua njia. Na wengi wetu huwa tunaamini yaliyotokea ni mipango ya Mungu, hivyo ni sehemu ya mitihani ya dunia. Msamehe kwa yaliyotokea, huwezi kujua pia Mungu amekupangia nini kurudisha furaha yako.
Mshukuru Mungu kwa kila jambo.
 
Asante ni kweli naumia sana ndugu yangu, na najutia sana kukutana nae namasikitiko mengi ila haisaidii kitu
Mkuu yameshatokea huwezi rudisha wakati nyuma.msahau,samehe move on na maisha yako
Jiweke karibu na Mungu atakulinda,atakubariki,atakuinua kwa viwango vingine.una ulemavu wa sikio na mguu sio wa akili.bado una uwezo wa kufanya mambo makubwa
Utafanikiwa,utapata mke mwema,utapata familia bora..yote yanawezekana ukiamini na kumtanguliza Mungu.
Samehe jifanye mjinga ili uruhusu baraka zitue katika maisha yako.
 
Mkuu napenda kusamehe ila hali yangu kila nikijiona naona nakuwa na moyo mzito kusamehe na kusahau

Kusahau haiwezekani ila kuweka kinyongo na chuki kwa mtu asiyejali maumivu yako ni sawa na kujiumiza mwenyewe kama unavyofanya sasa.
Yeye kashaendelea na maisha yake na wewe inakupasa kufanya hivyo pia yaani hakuna njia nyingine

naelewa Kitu kibaya kuhusu watu wema kama wewe ni kudhani kila binadamu ana utu na wema kiasi cha kutokuweza kuendelea na maisha yake akimuumiza mtu.. Si kweli kabsaa maana kuna watu hawajali maumivu ya watu wengine, Cha msingi usijiumize walq kujidhuru kwa ubaya wa mtu mwingine. Jitahidi uendelee na maisha yako na yeye atanyooshwa na maisha yake mwenyewe
 
Back
Top Bottom