Nilipata ulemavu sababu ya Mapenzi

Nilipata ulemavu sababu ya Mapenzi

Mkuu pole sana sana kwa tatizo la kutosikia hata mm nilipata ila miaka kama 4 nyuma kwa quinine izo izo ila na story ya mapenzi ilishanitokea kama ivyo

Kifupi kuna kitu mfano ulipomfuata ila mm demu alinipenda sana mpaka washkaji wakanshtua oya demu anakutaka tukiwa chuo mwaka wa kwanza basi nilikuwa sina ishu nae kabisa napambana na matatizo yangu niko mnyonge lecture siambulii kitu more than notes on a pamphlet basi bhana nikamtokea akakubali fasta sasa mm ndo nikampenda zaidi hajawa kuniomba hela sema mm boom likitoka namega kwa wazazi iliyobaki budget ya mihogo kuiifanya mgumu kumbr pesa sina

Kuna kipind mwaka wa tatu alianza kuomba pesa anapiga gharama mara anataka laki ya nguo tu mi mwenyewe sina namchana mi mweupe sina hela dharau zikaanza kaka hapokei simu ,anajibu kwa nyodo ,kuna siku anasema eti bora tuachane then anacheka nikaona poa tu nikamwambia goodbye sitokupigia simu hata siku moja

Laiti ningembembeleza yangenikuta kama hayo kaka yaliyokukuta but nilijikuta niko sahihi kwa kiasi fedha nilituma kwa wazazi baraka namaliza tu chuo naajriwa na salary ya pesa ndefu kidogo sina preshanangojea alijelete tu
hongera ndugu yangu kwa ajira na pole kwa tatizo la masikio, najua jinsi unavyoumia na unayopitia, yani tatizo la masikio ndo limefanya hata nje nisitake kutoka mtu anakwambia hujambo unasema salama inaumiza sana, mazungumzo unapata kwa asilimia 40 tu hizo nyingine unabaki kusema ndio hivyo au kucheka inaumiza sana,

nandio kikwazo kikubwa kwangu kuanza kujiajiri nawaza nitahudumiaje wateja wa hizo nguo au ndio nitaulizwa hii bei gani nitasema salama tena Mungu anihurumie tu.
 
mimi kama SALIMU nachukua fursa hii kukuomba samahani sana, na kiuhalisia NAIMA alinifata mwenyewe, halikua lengo langu kumtafuna,.

pole sana mkuu, yule dada ni mkatili sana.


MZUSHI FLANI was here.
 
hongera ndugu yangu kwa ajira na pole kwa tatizo la masikio, najua jinsi unavyoumia na unayopitia, yani tatizo la masikio ndo limefanya hata nje nisitake kutoka mtu anakwambia hujambo unasema salama inaumiza sana, mazungumzo unapata kwa asilimia 40 tu hizo nyingine unabaki kusema ndio hivyo au kucheka inaumiza sana,

nandio kikwazo kikubwa kwangu kuanza kujiajiri nawaza nitahudumiaje wateja wa hizo nguo au ndio nitaulizwa hii bei gani nitasema salama tena Mungu anihurumie tu.
mkuu, pole sana. . unaweza kua na mtu wa kukusaidia pembeni kama mdogo wako ambae hana ishu mtaani saivi itasaidia sana.. mimi pia nina tatizo la masikio, nmekosa michongo mingi sana ila nna imani bado mapambano yanaendelea..
 
Pole broo .....lakini mbona kila siku tunawaambia humu kuwa mwanaume ishi maisha yako kwanza mbona hamuelewi.....? Tatizo ni ubishi na kujiona nyie ndio romantiki sana kushinda babu zenu na baba zenu....! Inauma sana ila ndio ishakuwa tutafanyaje sasa ...
Hayanaga ushauri hayo hadi yamfike mtu ya kumfika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu, pole sana. . unaweza kua na mtu wa kukusaidia pembeni kama mdogo wako ambae hana ishu mtaani saivi itasaidia sana.. mimi pia nina tatizo la masikio, nmekosa michongo mingi sana ila nna imani bado mapambano yanaendelea..
asante iwa ushauri mkuu, Mungu aendelee kutupigania tupige hatua
 
Kama hii stori yako ni ya kweli basi ulimwengu ni katili sana kwa baadhi ya watu.
ndugu yangu bado sijafikia hatua ya kuilaumu dunia mimi naamini maamuzi yangu ndio chanzo cha haya yote
 
IMG_2357.jpg
 
dada yangu najitahidi kuwa na moyo wa kusamehe ila hali yangu ya ulemavu na majuto yananiumiza na kunitesa mimi siwezi sahau na kusamehe nimejitahidi nimeshindwa
Hili ndilo kosa lako kubwa mkuu, ukisamehe utapata uponyaji wa roho na amani. Msamehe kabisa, ondoa kinyongo, mwambie Mungu naomba uanze maisha mapya na mimi. Utapata amani moyoni na maisha mapya yatasonga mbele bila ya kumuwaza Naima.

Pole sana mkuu
 
Habarini,

Jana katika kupitia taarifa za group, la shule niliyosoma secondary, nakutana na ujumbe kuwa naima, anaolewa jumamosi ya leo, nimekosa raha ndugu zangu, kwani ni miaka takribani 13 imepita nikijitahidi kusahau, ila kila nikiangalia hali yangu ya ulemavu najikuta nakumbuka na kuyachukia mapenzi.

Mimi nilizaliwa mzima kabisa na sasa nina miaka 35, baada ya kumaliza chuo, nilikuwa na mahusiano na binti fulani ambaye tulisoma nae secondary hapa dar, nakumbuka kuonana nae ilikuwa ni kama bahati tu na kila muda naumia natamani nisingeonana nae labda leo hii ningekuwa mzima kabisa.

Mwanzo alikuwa ni mtu wa kipekee sana, nilijulikana kwao na kwetu walimjua, na kwakuwa nilikuwa na kazi private office moja hapa mjini(sitapenda kuitaja) nilijitahidi fanya uwekezaji mdogo kwake nilikopa kiasi fulani cha pesa mil 7 kwa dhamana ya kazi nikamfungulia duka kwa matumaini ya kuwa, kwakuwa sisi ni kitu kimoja mwenzangu nae asimame kwani alikuwa anashinda tu nyumbani kwao.

Nilipata misukosuko kazini na nikasimamishwa kazi na hapo ndipo nilipoanza kutoelewana na mwenzangu dharau ilikuwa kubwa, kejeli, unamuomba muonane anagoma au anakubali na hatokei kabisa na simu anazima, ndani ya miezi miwili, nilikuwa nimepata msongo mkubwa wa mawazo maana madeni na hali ngumu na mwenzangu haeleweki sikujua nifanye nini zaidi ya kunywa pombe.

Siku ya tukio jumatano ile niliamka mzima kabisa, jioni nilipanga kwenda alipopanga naima bila taarifa kwani kila nikimjulisha basi hatoi ushirikiano. Nilitaka tukubaliane tuuze duka nifund hela kidogo ya kiwanja nilichonacho nifungue biashara nyingine, inisaidie kufanya marejesho bank.

Sikuwahi fikiria kama ananisaliti nilijua tu ni kutingwa na kazi na kuwa na mood mbaya, saa 1 nilienda kwake kwakujua aliishafunga biashara nilivyofika kwake, niligonga mlango kukawa kimya, nilikuwa na funguo za kwake na yeye alikuwa nazo za kwangu nikafungua mlango.

Sikuamini macho yangu naima alikuwa na rafiki angu kipenzi salim wakifanya mepenzi pale sebuleni wakapigwa na mshangao kwani hawakunitarajia, nilirudi nyuma na kuanza kutoka pale nikiwa na maumivu zaidi na kujiona sifai nikiwa mita chache tu kutoka pale nikivuka barabara nilisikia honi ya gari mara 2 baada ya hapo sikukumbuka kitu tena.

Baada ya kuamka nilikuta ndugu zangu wakiwa hospital namimi wakiwa na huzuni, baada ya siku 2 ndiyo niligundua mguu wangu wa kushoto sina tena nilielezwa uliharibika kutokana na kusagwa na gari, nililia sana na bado nalia sana, nilijiuliza nimefanya dhambi gani kustahili adhabu hii, niliwaza nitalipaje deni la bank na nitawezaje kuanza maisha katika hali yangu ya ulemavu.

Baada mwezi 1 nanusu nikatoka hospitalini, ila ikawa kama ninamkosi kwani baada ya mwezi nilikamatwa na malaria kali sana nikajua ndio mwisho wa maisha yangu, nilikuwa naweweseka sana, hospital wakaniwekea dripu ya Quinine, masikini ningejua naenda pata ulemavu mwingine ni bora ningejitibia nyumbani, ila nilipona vizuri baada ya week tu...

Baada ya miezi 7 nilianza poteza uwezo wa kusikia taratibu na kupoteza balance ya kutembea sikugundua mapema ila baada ya kufikisha mwaka na miezi 2, nilikuwa natatizo lingine la kutosikia vizuri.

Maisha yangu yalibadilika sikuwa na furaha tena na leo hii mwanamke alieniharibia maisha yangu ambaye naamini ni chanzo cha ulemavu wangu anaenda kuolewa najiuliza nimeikosea nini dunia, muda mwingine natamani kufariki kwani ninayopitia ni mazito kushinda uwezo wangu wa kustahili.

Ewe maisha, nilikukosea nini?
Kaka polee sanaa Sema nini mi nikifanyiwa hivyo naenda kigoma Kule kwa Yule mganga aliyempa mtu mimba ya Kuku yan mtu anarogwa Heavy .... Wache wacheze na Akili zetu
 
Pole sana kaka. Yaani pole nyingi nimeumia kweli utafikiri tumetoka tumbo moja... Naamini kwa muda wote huo ulikuwa umeshaanza kumsahau lakini baada ya kuskia hili tukio la yeye kuolewa ndio ikaamsha maumivu upya mpaka kufikia hatua ya kuandika huu uzi.

Nachelea kusema huu uzi utakupa ahueni kubwa sana na kama ulikuwa huna hamu ya kula basi leo utakula.

Nachokuomba usije ukathubutu kufuatilia tena habari zake tena, maana chochote kinachompa furaha upande wako wewe itakuwa ni maumivu. Hii ni kawaida kwa binadamu karibu wote tuko hivyo, kuwatakia mabaya waliotukosea na ikiwa tofauti basi tunaumia.

Huwa naamini binadamu yoyote ambaye bado hajakata punzi, Basi anaweza akaishi na furaha regardless his/her physicality.

Cha msingi tu tafuta mfumo mzuri wa maisha unaoendana na hali uliyonayo utakao ku-keep busy kiakili kiasi kwamba haitakuwa rahisi kwa wewe kufikiria mikasa mibaya iliyowahi kukukumba huko nyuma.

Halafu hii mikasa imekuwa mingi Sana siku hizi... Aisee Kuna haja ya sisi wanaume kupeana seminar namna ya kuishi na hawa viumbe nyakati hizi hili matukio kama haya yasiendelee kutokea.

Wanawake wa Leo sio Kama mama zetu.

Women are no longer the way they used to be back in old days.

Gone are the days when men give the huge sacrifices for women's interest and women reciprocate by being loyal and treat men like Kings.

Now days things are way different, you treat your woman like a queen, she treats you like trash in return.

Wanawake wana kitu kimoja kinaitwa natural state of hypergamy, na ndicho kilichoku-cost wewe na wenzako wengi sana.

Kuna siku nitakizungumzia kwa mapana jinsi gani ya kukitambua kwa haraka na kufanya maamuzi sahihi kabla hujawa muhanga.

Sent from my M100 using JamiiForums mobile app
Ukiandika usisaha 'kuni-tag' mkuu.

Mtoa mada pole sana.
 
Pole sana mtoa mada.
Matendo ya wanawake kama haya huwa yanawachukiza sana wanaume na wengine wanashindwa kuvumilia na kujikuta wanafanya mauaji na gunia la mkaa kuhusika.

Kuna haja ya kuzijua tabia za wanawake na kujifunza namna nzuri ya kuweza kuishi nao. Mfano, Kwa kubadilisha mitazamo yetu kwamba unaamini kuwa mpenzi ni mtulivu na hawezi kuwa na mahusiano na mtu mwingine. Pia tuache kujitoa kimwili na kiroho kwa wapenzi wetu, tuishi nao kwa staili ya kuwachukulia poa. Ukibaini haendani na itikadi zako achana nae kistaarabu kisha endelea na mishe zingine.
 
Back
Top Bottom