Nilichokiona mara ya kwanza baada ya kuagiza kitu ebay

Nilichokiona mara ya kwanza baada ya kuagiza kitu ebay

Mbona cost zao eBay zinataka kufanana na Tanzania Sasa maana shipping na mzigoo wenyewe inarudi Ile ile TU ya bongo🤣
Bado haujajua kutumia vizuri eBay.
Pitia michango ya watu ujifunze.
Hivi karibuni nimetoka kununua PS4 Slim 1TB ikiwa na game pamoja na pad kwa USD 100.
Hauwezi amini, lakini wazungu eBay wanauza vitu kwa bei za ajabu sana.
 
Okay so ni recommendable? Kuna bidhaa natamani kuagiza, ila sijapata app sahihi ya kutumia, kikuu walinicheleweshea bidhaa zangu nikakata tamaa kabisa ya kuagiza vitu online
Agiza kwa Ebay au Aliexpress hautojuta
Ila kabla ya kufanya malipo zingatia kusoma vizuri maelezo ya mzigo unaotaka kulipia kama ni kifaa cha electronic lazima ujue ni used, new, refurbished or spare parts wengi hukurupuka kulipia kwa kuona unafuu wa bei badae mzigo ukifika analalamika kwamba amepigwa
Mfano kuna mwamba aliagiza kifaa flani kilipofika hakifanyi kazi akadai amepigwa lakini alipotaka kufungua madai ili arudishiwe pesa(hii inawezekana iwapo mzigo haukufika au umefika ukiwa na changamoto kubwa kuna taratibu za kufuata pesa itarudi) sasa huyu jamaa kumbe hakusoma maelezo ya hicho kifaa yeye aliangalia bei tu akalipia kumbe kifaa hakitumiki ila kinauzwa kama spare parts!
 
Ukienda tawi lolote la nmb wanakuunga na kadi wanakupa
Hapana, NMB hawakuungi na PayPal, ili kutumia PayPal inakutaka ufungue Account kabisa na P'word yako binafsi...wanachofanya NMB ni kukupa kadi maalum kwaajili ya manunuzi ya mtandaoni
 
Bado haujajua kutumia vizuri eBay.
Pitia michango ya watu ujifunze.
Hivi karibuni nimetoka kununua PS4 Slim 1TB ikiwa na game pamoja na pad kwa USD 100.
Hauwezi amini, lakini wazungu eBay wanauza vitu kwa bei za ajabu sana.
Hiyo usd 100 ni hadi umeipokea getoni mkuu??
 
Ninachoona mimi mzigo ni afadhali upitie Posta ambayo iko nje ya mji wa Dar Es Salaam, nilipokuwa naagiza na mizigo ikipitia Dar Es Salaam ilikuwa ni lazima nilipie lakini tangu nimeanza kupitishia Posta ya huu mkoa ninaoishi sijawahi kulipia.
Mkuu upo mkoa gani kwani?
 
Niliwahi kuagiza speaker ndogo za ndani za Tv aisee wanikikata hela ndefu hadi nikashangaa, bei ya spika ilifika usd 25, lakini nilikatwa 5900 ya Posta, 18% ya kodi, clearing fee, jumla nilikatwa kama , 28/29000. Iliniuma sana. Then tudude twenyewe tudogo tu!!
Kwahiyo makato ni kama nusu ya bei ya ( kununulia + shipping )..
 
Back
Top Bottom