Niko dillema, naomba mawazo yako

Niko dillema, naomba mawazo yako

Ww ni mwanaume kuendelea kulelewa na mwanaume utakuja ujikute umeloa nyuma oooh namuamin anaweza kupitiwa yule ni binadamu nenda kijijin kafanye kazi
Hana hiyo dirty mind, ila wewe pekee yako
 
Nimesoma reply zako zinaonesha unataka kurudi kwa mshangazi ukalelewe, yani wale wanaokupa ushauri unaoambatana na kurudi ndio unawaona wanakushauri vizuri bila shaka unasumbuliwa na genye na upwiru wa kummiss huyo unaemuita mzazi mwenzio

Komaa town mzee wanawake sio wa kutegemea kabisa komaa ujenge kwako komaa upate kitu cha kufanya town mishe nyingi jichanganye acha kufungwa na mawazo ya kuajiriwa na elimu ulionayo

Usirudi kwa huyo mshangazi utakuta maumivu hakuna mwanamke anaemtafutia ugali mwanaume halafu akawa mwaminifu hakunaaa
Kwa nini mshangazi? Kwa hiyo unataka amwache ili tuongeze singo maza mtaani? Wacha hizo mkuu! Aende kwa mzazi mwenzake waendeleze gurudumu bwana!
 
Inaonekana wewe ni wale watu wanaopenda kulelewa.
Kuendelea kujitolea ni kupoteza muda halafu kukaa kwa mshikaji muda mrefu sio vizuri.
Mzazi mwenzako amekupa ramani nzuri kabisa sehemu ambayo utaenda kupambana kwa jasho na Damu upate chochote sio kwamba huko amekuita akakuhudumie kama ulivyozoea. kafanye kazi ndungu usichezee hiyo bahati Kuliko kukaa Dar kupoteza muda na kuongezea watu mzigo. Kafanye kazi.
 
Habari za w'end wakuu

Niende moja kwa moja tu bila chenga, akili imewaza ila sijapata mwafaka.
Thread zangu za nyuma zinaweza kuwa reference ya kile nachopitia, anyway:

Wakuu nipo mjini DSM na hadi Saivi nipo mahakama fulani nijitolea, kuna kipindi nilipitia wakati mgumu hadi nikatamani kurudi kwa mzazi mwenzangu, shida tu alikuwa likizo na bahati mbaya niliondoka baada ya ugomvi mkubwa sana - Saivi karudi na anataka niende nkafanye kilimo nikiwa nasubiri pengine kibarua, mwanzo nilishindwa kukubali moja kwa moja sababu nilikuwa nasubiri passport yangu, mpaka kuja kuipata tayari nilikuwa nimeshapata mahali pa kujitolea(mahakamani) niliona sawa kupata elfu tano tano mara moja moja kuliko kubaki iddle nyumbani.

Probability ya kuja kuajiriwa ni ndogo Sababu hasa wanahitaji watu wenye diploma (Rumors nilizosikia) kazi niliyopewa ni ukarani-kwa wiki mbili tu nlizoserve itoshe kusema wanaume tuwe makini sana na wanawake hasa hawa wanawake wa ndoa 🙌

Nistoke kwenye mzizi wa thread, nafanya with no hope kwamba pengine naweza kupata gape la kuja kuajiriwa, kiuhalisia sioni kama itakuwa kama navyotamani, kumbuka yote yanajiri nipo kwa mshikaji wangu-haonyeshi kunichoka kulingana na hali yangu ananisaport sana kwa kila namna. Kuna muda hadi nasikia aibu hapa ndipo mawazo yanapoanza kwamba nikiondoka ataona nimedharau jitihada zake, lakini pia fursa dar ni nyingi; je naondoka dar then What?? changamoto nyingine ni mimi nitabaki kwake hadi lini, jibu linakuja lazima nitafute kwangu kama kidume-kwa kazi ipi? Hili ni swali jingine.

Option yangu inabaki bora nirudi kwa mzazi mwenzangu ila changamoto kama mnavyojua jinsia upande wa pili hisia zikipungua plus yeye anahudumia dharau zinaanza, ijapo tayari tumeshapangilia nini cha kufanya, bad thing TAMISEMI wamemtupa KIJIJINI haswa Njombe ndani ndani uko so pow, mwaka huu kalima heka 1 kapata gunia 13 za mahindi.
Najua wengi humu mmepitia/kuona haya mna experience za kutosha, hivyo mawazo yako ni muhimu.
Nitachukua kile ambacho kitafaa ili nifanye maamuzi sahihi zaidi kwamba "nibaki Dar au niende Njombe"
Natanguliza shukrani, karibu nipate mawazo yenu🙏🙏
Rudi njombe kalime
 
b
She so Sweet kiasi kwamba mwenyewe sioni ugumu kwenda tatizo lipo kwenye malumbano, leo ananipigia akinieleza kuna pahali ananiombea kazi ili nisogee alipo (kuna watu watakuja kusema ataliwa na boss wako) nasubiri mrejesho wake.
In short yule ni mke wa kuoa ndugu na ikitokea nimefeli kufanya hivyo basi ni sababu zilizo nje ya uwezo wangu, we turn 8-9 years now, tulipoendana skuli tukaja kukutana kwa mara ya kwanza kimwili 2018❤️‍🩹
bro nenda njombe kwa mkeo then komaa na kilimo you never know MUNGU amekuandalia nini kaka amini kwamba
 
Moyo unasema niende akili inaniambia baki, moyo unasema baki akili inaniambia Nenda🙌
mkuu kachaa chini na mshkaji wako ongea nae kirafiki mpe mpango wako wa kupambana kwa kilimo ukiwa karibu na wife wako kwa masalahi mapana ya familia na yako binafsi jamaa ako ni muelewa atakuelewa na mahusiano yenu hayataharibika easy
 
Dar ni kama center ya michongo.

Haramu na halali yote ipo hapo.

Just make sure you listen, connect with the right people na uache kuongea sana.

Ukiwa unatoka nje ya Dar uwe na ramani kama siyo hivyo Dar ni best option.

Hata ukiamua kua mshona viatu, mshona viatu wa Dar hafanani na mshona viatu wa Kinyanambo C.
 
Mkuu asilimia kubwa ya hizi taasisi za serikali ukienda kujitolea bila barua rasmi ya mkataba, wataishia kukutumia tu kusafisha ma-file yao na kukimbizana na makaratasi yao ambayo wao wenyewe yamewachosha kuyafanyia kazi. Umeshasikia tetesi kabisa kwamba wanataka watu wenye Diploma, wewe huna, unategemea nini? You are literally wasting your youth energy on a dead end job kwa matumaini ya miujiza.

Serikali wakitaka kuajiri wanafuata taratibu na budget yao. Hiyo elfu tano unayoichukulia leo poa, itakufanya uwe stagnant kwa miezi mingine sita ijayo, halafu mwisho wa siku unaachwa hewani.

Huyo mshikaji wako hatokuonyesha tabia yoyote ya tofauti kwa sababu pengine ni mtu muungwana sana, lakini don't abuse his hospitality mzee. Kila mtu ana maisha yake na ana mambo yake ya siri anayotaka kufanya kwenye geto lake. Unazidi kujishusha thamani ukikaa hapo Dar bila ramani kuliko ukienda Njombe kupambana na mzazi mwenzako.

Mzazi mwenzako kavuna gunia 13 za mahindi kwenye heka moja tu! Huoni kuwa huo ni ushahidi tosha kwamba hiyo ardhi aliyopo ina baraka zake kiaina?. Huyo mwanamke ameshkutengenezea njia, wewe kama dume la familia nenda kamsaidie, kama msimu uliopita amepata gunia 13 peke yake, mkienda wawili mkaongeza nguvu na akili mkabarikiwa kuvuna gunia 50 au 100 si mtatoboa?

Huko Njombe ndiko kuna fursa yako ya haraka kwa sasa mzee, mchezo wa kilimo ukiujua vizuri unaleta hela ya haraka kuliko kuendelea kubaki bila ramani, matokeo yake unazidi kujilemaza tu.
Umemshauri vizuri, afikirie juu ya huu ushauri 📌📌📌
 
Kwa nini mshangazi? Kwa hiyo unataka amwache ili tuongeze singo maza mtaani? Wacha hizo mkuu! Aende kwa mzazi mwenzake waendeleze gurudumu bwana!
Mwanaume unamshauri mwanaume mwenzio "aende" kwa mwanamke hiyo yenyewe ina-sound kupoteza miliki na utawala, siku zote mwanamke ndio anatakiwa "kwenda" kwa mumewe

Singo maza sio kichaka cha kupoteza power ya kuwa mwanaume otherwise aende akalelewe tu
 
Mwanaume unamshauri mwanaume mwenzio "aende" kwa mwanamke hiyo yenyewe ina-sound kupoteza miliki na utawala, siku zote mwanamke ndio anatakiwa "kwenda" kwa mumewe

Singo maza sio kichaka cha kupoteza power ya kuwa mwanaume otherwise aende akalelewe tu
Sasa wewe mkuu unamshauri aendelee kufugwa hapo kwa jamaa?
 
Sasa wewe mkuu unamshauri aendelee kufugwa hapo kwa jamaa?
Kwa jamaa hafugwi wala kulelewa hapo anapambana wanaume huwaga hatuna masimango kama wanawake.

Kuna kipindi jamaa angu aliona kwao wanamtumia tu anauza duka la kaka ake bila future yoyote, akaja magetoni tukawa tunachill wote tunapika na kula kipindi hicho mm napiga kitabu chuo, alikuwa akijishughulisha na mbaga za uwakala hadi akapata pa kushikia na akapanga geto lake mwanzoni nilikuwa nikimbust na boom langu lakin akajichanga akawa na kwake

Huyo jamaa aache mbaga za kuajiriwa na kujitolea, mtaani pesa ipo kuanza ni kugumu ila ukishazoea mwaka unaweza usifike unamiliki geto na mazaga mengine mjini hapa. Hapo sasa hata akimuita mzazi mwenzie atakuwa kifua mbele kuliko akaenda kutegemea mshahara wa uyo manzi ataletewa michepuko hadi usiku wa manane na asiweze kusema chochote
 
Nafurahi pale mtu anapotaka ushauri wa alime yaan afanye kilimo ama kazi.
Be a man bro rudi huko jishushe na umwambie mambo ya shamba akuachie na wewe upambane kweli. Coz nnavyojua hautakuwa ati wewe ndio wa kwenda kulima wewe ni kusimamia tu watu wakifanya kazi. Usiamini ke hawezi kukusaidia ndugu yangu she can na utaboa bora tu asiwe mshangazi. My friend kwanza huko kijijin ndo pazuri coz hujulikani. Utakuja kujulikana after kuwa umelima hata misimu (sio minokia na misamsung)miwili. Na mungu akakusaidia ukapata mazao na bei ikawa nzuri i swear hutakumbuka kuajiriwa ndugu yangu. Mwambie huyo unayeishi kwake akupe nauli kama hauna na uende huko bro na utanishukuru baadae.
 
Mkuu mbn adabu yako ni ndogo - jitahidi kuwa na busara si kila mahali ni pakutukana, haikupandishi ila inakushusha. Fanya hivyo itakusaidia 🙏
Wewe unachepuka na unataka kuheshimiwa tena.
Hata hujui uende wapi ukiitwa maraya si heshima hiyo
 
Kwa jamaa hafugwi wala kulelewa hapo anapambana wanaume huwaga hatuna masimango kama wanawake.

Kuna kipindi jamaa angu aliona kwao wanamtumia tu anauza duka la kaka ake bila future yoyote, akaja magetoni tukawa tunachill wote tunapika na kula kipindi hicho mm napiga kitabu chuo, alikuwa akijishughulisha na mbaga za uwakala hadi akapata pa kushikia na akapanga geto lake mwanzoni nilikuwa nikimbust na boom langu lakin akajichanga akawa na kwake

Huyo jamaa aache mbaga za kuajiriwa na kujitolea, mtaani pesa ipo kuanza ni kugumu ila ukishazoea mwaka unaweza usifike unamiliki geto na mazaga mengine mjini hapa. Hapo sasa hata akimuita mzazi mwenzie atakuwa kifua mbele kuliko akaenda kutegemea mshahara wa uyo manzi ataletewa michepuko hadi usiku wa manane na asiweze kusema chochote
Mimi nakwambia kama ana nguvu kule atateseka mwaka mmoja tu uchumi utarudi na atammiliki huyo mwanamke na ki mshahara chake cha ualimu! Kule Njombe kuna maneno mwaka mzima wanapiga kazi za shamba! Hivyo kwa mwaka anaweza kuvuna mara 2 au 3!
 
Mimi nakwambia kama ana nguvu kule atateseka mwaka mmoja tu uchumi utarudi na atammiliki huyo mwanamke na ki mshahara chake cha ualimu! Kule Njombe kuna maneno mwaka mzima wanapiga kazi za shamba! Hivyo kwa mwaka anaweza kuvuna mara 2 au 3!
Aje atupe mrejesho hapo baadae
 
Dar ni kama center ya michongo.

Haramu na halali yote ipo hapo.

Just make sure you listen, connect with the right people na uache kuongea sana.

Ukiwa unatoka nje ya Dar uwe na ramani kama siyo hivyo Dar ni best option.

Hata ukiamua kua mshona viatu, mshona viatu wa Dar hafanani na mshona viatu wa Kinyanambo C.
Huu ndo ukweli watu wengi hawajui kuhusu Dar, ukishindwa Dar seemu nyingine kutoboa si rahisi labda ufanye kilimo😇
 
Mimi nakwambia kama ana nguvu kule atateseka mwaka mmoja tu uchumi utarudi na atammiliki huyo mwanamke na ki mshahara chake cha ualimu! Kule Njombe kuna maneno mwaka mzima wanapiga kazi za shamba! Hivyo kwa mwaka anaweza kuvuna mara 2 au 3!
Nimepanga kujitoa sadaka 1/2 years kwenye kilimo na biashara
Biashara ya kununua bidhaa kwa jumla mjini nasambaza vijijini au mtaani kwenye maduka madogo madogo/ stationery ntafanya online application kama
TIN no.
Death & Birth certificate
Bima
Inshort Nina ujuzi wa kutumia kompyuta vizuri na mimi nina pc-mchawi hapa ni router
Nimplan hizi zitakuwa side hustle zangu kilimo ndo priority
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom