Nihurumieni mwenzenu nakufa

Nihurumieni mwenzenu nakufa

Habari zenu wanajf wenzangu nina shida jamani eee Mungu wangu nisaidie niweze kueleweka nahitaji watu wenye moyo wa kujitoa wanisaidie jamani nipo karibu na mauti mimi.

Wapendwa nadaiwa pesa nyingi sana na bank na sijui wapi nitaweka sura yangu maana watu hawa wamechachamaa kweli mfukoni nina elfu 6500 tu jamani mimi nitaenda wapi natamani nijitoe uhai ila nawaza huko niendako itakuwaje nikikutana na moto wa jehanamu milele?

Wanajf nyie ndio tegemeo langu la mwisho naombeni mnisaidie deni linatakiwa kulipwa kabla mwezi kuisha la sivyo mimi nitahukumiwa jamani ohhh

Sina pa kukimbilia yeyote anayeweza kunisaidia kwa masharti yoyote nipo tayari ili mradi mimi niachane na hili deni jamani niishi kwa amani. Nahitaji watu 25 wakujitolea kila mmoja milioni moja nipate milioni 25 nilipe hii bank niishi kama watu wengine. Yeyote atakayenipa nitakua namlipa taratibu au anipe kazi yoyote nimfanyie bure na nitaifanya kwa akili na uwezo wangu wote.

Nisaidien jamani nawaomba Mungu atawaridishia mlipotoa.

I declare my interest ID hii ni mpya kwa sababu zisizozuilika.

Yeyote atakaeweza kunisaidia nipo tayari kuongozana nae hadi bank ili ahakikishe kweli ninadaiwa.

Story ya deni ilivyo
Pesa hizo ziliingizwa kimakosa kwenye akaunti yangu na bank yenyewe na mimi kwa vile nilikua nategemea pesa nikajua ndio zangu nikafanya nazo biashara na biashara yenyewe watu wamenidhulumu nimebaki sina kitu nifanyeje mimi na biashara ilikua haijasajiliwa sina haki hata ya kuwapeleka mbele ya sheria ninaowadai jamani nitakufa mimi dunia itaniua mimi
Chochote ulichonacho naomba mchango wako jamani nitafanyaje mimi sina hela nipo nipo tu natamani nikitembea gari linipitie nife hapohapo dah
Mm nakupa pole
 
Mkuu kuna mzee alikuwa anadaiwa laki 6 kiboriloni hapa kajinyonga mpka kufa wew Million 25 unazubaa embu kuwa serious mkuu jilambe kitanzi mbio mbio kuokoa muda
 
Swali kwaza: Je, hivi bank kukuwekea pesa katika account yako then ukazitumia, sheria inasemaje hapa?! Maana cha kuokota si cha kuiba, wewe umeikuta katika account yako na hukuomba kuwekewa, shida mwanaharamu, umezitumia iwaje sasa wakuulize tena na haukuwaomba?!

Swali la pili: Wewe na bank mliingia mkataba gani juu ya hizo million 25?! Je walikukopesha, ulifanya overdraft, au ilikuwaje, ni mkataba gani ambao umevunja juu ya hizo 25 million hadi wakupeleke mahakani kuzidai....maana hii ni kama uokote bahasha ya mamilioni usijue ni ya nani kisha ukaamua kuitumia then atoke mtu aseme ni zake na atake kukushtaki ili kuzidai, sasa anakudai kwa makubaliano yapi, alikukopesha au alikuazima, kwa mkataba upi nauliza?!

Swali la tatu: Sheria za wafanyakazi wa bank zinasemaje juu ya negligence ya wafanyakazi wao pale wanapofanya uzembe kama huu wa kudeposit pesa kwenye account ya mtu ambaye hausiki na pesa?!

Swali la nne: Bank huwa zinaweka insurance cover kwenye pesa zake, je inapotokea tukio kama hili, bank wanapata hasara kweli, sio kwamba hapa insurance wanalipa hizi hasara

Swali la tano na la mwisho: Je, hawa watu 25, utawalipaje na wote wakitaka pesa zao kwapamoja?!
 
hiyo asset uliyotumia kupata mkopo iuze mwenyewe haraka maana benki watauza kwa hela mbovu
 
Pole sana!Lakini kwanini unataka kujiua?kwani bank wamesema watakupa adhabu gani kubwa kuliko kifo, nadhani hamkuelewana, watakudai lakini mwisho wa siku watafuata sheria, lakini sijui kama mahakama ina adhabu ya kifo ukishindwa kulipa hata senti moja . Sana sana watachukua ulichonacho, tunza uhai.
pole san wangu
 
Tatizo lako halina mashiko...something is wrong...Yaani upate million 25 kizembe hvo usawa huu wa Anko Magufuli..

hehehe kaibe unako ibaga
 
Mimi sio tapeli jamani ila kila mtu ana maoni yake na ninayaheshimu hii story ni ndefu sijui nianzie wapi na niishie wapi hiyo milioni 25 haikuingizwa yote iliingizwa 12m na mimi nilikua na deni na hiyo bank so wamepiga mahesabu natakiwa kurudisha 25m mimi naipata wapi mwenzenu sina hata pa kuanzia jamani sina mali zozote zaidi ya fridge na godoro langu uwiii mimi
Kama hii stori si chai,Inawezekana vipi Mamilion yapukutike mpaka 6500/= Ma mdogo??Duh!! Japo sishawishiki kuamini Lakn mchango wangu ni "POLE " mkuu
 
Habari zenu wanajf wenzangu nina shida jamani eee Mungu wangu nisaidie niweze kueleweka nahitaji watu wenye moyo wa kujitoa wanisaidie jamani nipo karibu na mauti mimi.

Wapendwa nadaiwa pesa nyingi sana na bank na sijui wapi nitaweka sura yangu maana watu hawa wamechachamaa kweli mfukoni nina elfu 6500 tu jamani mimi nitaenda wapi natamani nijitoe uhai ila nawaza huko niendako itakuwaje nikikutana na moto wa jehanamu milele?

Wanajf nyie ndio tegemeo langu la mwisho naombeni mnisaidie deni linatakiwa kulipwa kabla mwezi kuisha la sivyo mimi nitahukumiwa jamani ohhh

Sina pa kukimbilia yeyote anayeweza kunisaidia kwa masharti yoyote nipo tayari ili mradi mimi niachane na hili deni jamani niishi kwa amani. Nahitaji watu 25 wakujitolea kila mmoja milioni moja nipate milioni 25 nilipe hii bank niishi kama watu wengine. Yeyote atakayenipa nitakua namlipa taratibu au anipe kazi yoyote nimfanyie bure na nitaifanya kwa akili na uwezo wangu wote.

Nisaidien jamani nawaomba Mungu atawaridishia mlipotoa.

I declare my interest ID hii ni mpya kwa sababu zisizozuilika.

Yeyote atakaeweza kunisaidia nipo tayari kuongozana nae hadi bank ili ahakikishe kweli ninadaiwa.

Story ya deni ilivyo
Pesa hizo ziliingizwa kimakosa kwenye akaunti yangu na bank yenyewe na mimi kwa vile nilikua nategemea pesa nikajua ndio zangu nikafanya nazo biashara na biashara yenyewe watu wamenidhulumu nimebaki sina kitu nifanyeje mimi na biashara ilikua haijasajiliwa sina haki hata ya kuwapeleka mbele ya sheria ninaowadai jamani nitakufa mimi dunia itaniua mimi
Chochote ulichonacho naomba mchango wako jamani nitafanyaje mimi sina hela nipo nipo tu natamani nikitembea gari linipitie nife hapohapo dah
weka supporting evidence hapa (ushahidi) tuamini kama ni kweli kabla ya kutoa pesa. mimi ninaweza kukusaidia laki tano hata kesho kama utatoa vielelezo vya kuthibitisha unadaiwa kweli
 
weka supporting evidence hapa (ushahidi) tuamini kama ni kweli kabla ya kutoa pesa. mimi ninaweza kukusaidia laki tano hata kesho kama utatoa vielelezo vya kuthibitisha unadaiwa kweli
Sina hakika kama support evidence anayo maana wengi wametaka kujiridhisha lakini wamefeli
 
Back
Top Bottom