Nihurumieni mwenzenu nakufa

Nihurumieni mwenzenu nakufa

Mods fungeni huu uchafu unajaza nafasi. Huyu yawezekana anataka kuzamia nchi flani anatafuta pesa ya kuweka ili aonekane ana pesa kwenye account yake. Achana naye tapeli mkubwa. FUNGA UZI.
 
Zogo la dogo shobo, shombo la chombo
Boost la dust Congo, gesi la Songosongo toka dongo la Bongo
Hongo la gongo bila Mboto, Kulwa asiye Doto
Susa kushusha vyombo, muziki wa Kyanga Songo
Barafu yamoto isiyo band, rubber band inatafuta hela za wasela
Simela, mkopo haufungi jela
Pafu ya instagramu photo
Omba kitana kitwana kipara ngoto
Komba magutu magoto, uwe Mobutu wa lotto
Omba njuka msokoto, vunja kokoto kwa joto
Omba suka apate tongotongo, aendeshe longolongo
Omba shuka fyongo, Kigilagila chukua viroboto
Omba raha msoto, gomba Mrisho Mpoto kwa muziki wa Jerry Kotto
Ngoma ya mtoto haikeshi, muamala uwe cash keshkesh
Jaza hips Kihabeshi
Magu kabana reli mpaka msafara wa jeshi!
Kukopa harusi, kulipa matanga, labda cheki MATAGA itataga
Nishani ya amani iso kifani kwa waghani
Duniani zamani tulidhani tafrani ni kani ya ku run pwani hata pwani
Greece Ubatani, tukasepea wadogo mpaka leo ukubwani...
Ahhhh

Shall I coniinue....?
Uje nikupeleke studio msukuma
 
Habari zenu wanajf wenzangu nina shida jamani eee Mungu wangu nisaidie niweze kueleweka nahitaji watu wenye moyo wa kujitoa wanisaidie jamani nipo karibu na mauti mimi.

Wapendwa nadaiwa pesa nyingi sana na bank na sijui wapi nitaweka sura yangu maana watu hawa wamechachamaa kweli mfukoni nina elfu 6500 tu jamani mimi nitaenda wapi natamani nijitoe uhai ila nawaza huko niendako itakuwaje nikikutana na moto wa jehanamu milele?

Wanajf nyie ndio tegemeo langu la mwisho naombeni mnisaidie deni linatakiwa kulipwa kabla mwezi kuisha la sivyo mimi nitahukumiwa jamani ohhh

Sina pa kukimbilia yeyote anayeweza kunisaidia kwa masharti yoyote nipo tayari ili mradi mimi niachane na hili deni jamani niishi kwa amani. Nahitaji watu 25 wakujitolea kila mmoja milioni moja nipate milioni 25 nilipe hii bank niishi kama watu wengine. Yeyote atakayenipa nitakua namlipa taratibu au anipe kazi yoyote nimfanyie bure na nitaifanya kwa akili na uwezo wangu wote.

Nisaidien jamani nawaomba Mungu atawaridishia mlipotoa.

I declare my interest ID hii ni mpya kwa sababu zisizozuilika.

Yeyote atakaeweza kunisaidia nipo tayari kuongozana nae hadi bank ili ahakikishe kweli ninadaiwa.

Story ya deni ilivyo
Pesa hizo ziliingizwa kimakosa kwenye akaunti yangu na bank yenyewe na mimi kwa vile nilikua nategemea pesa nikajua ndio zangu nikafanya nazo biashara na biashara yenyewe watu wamenidhulumu nimebaki sina kitu nifanyeje mimi na biashara ilikua haijasajiliwa sina haki hata ya kuwapeleka mbele ya sheria ninaowadai jamani nitakufa mimi dunia itaniua mimi
Chochote ulichonacho naomba mchango wako jamani nitafanyaje mimi sina hela nipo nipo tu natamani nikitembea gari linipitie nife hapohapo dah
Dada eeh! Hao watu 25 tukikupa iyo hela utaweza kufanya kazi kwa watu wote ili ulipe deni? Tanzania ni kubwa panda gari nenda sitimbi tafuta makazi yasiojulikana jichimbie huko na uanze moja ,jela inakuhusu na uje ujibu comment za watu huku naona umekacha
 
Usipewe hata miaaaaa.. nawaona sana watu kama nyie mkipata vihera vidogo mbio kufanya starehee na kujaza magari full tenki ..hatudanganyikiiii!!!
 
Zogo la dogo shobo, shombo la chombo
Boost la dust Congo, gesi la Songosongo toka dongo la Bongo
Hongo la gongo bila Mboto, Kulwa asiye Doto
Susa kushusha vyombo, muziki wa Kyanga Songo
Barafu yamoto isiyo band, rubber band inatafuta hela za wasela
Simela, mkopo haufungi jela
Pafu ya instagramu photo
Omba kitana kitwana kipara ngoto
Komba magutu magoto, uwe Mobutu wa lotto
Omba njuka msokoto, vunja kokoto kwa joto
Omba suka apate tongotongo, aendeshe longolongo
Omba shuka fyongo, Kigilagila chukua viroboto
Omba raha msoto, gomba Mrisho Mpoto kwa muziki wa Jerry Kotto
Ngoma ya mtoto haikeshi, muamala uwe cash keshkesh
Jaza hips Kihabeshi
Magu kabana reli mpaka msafara wa jeshi!
Kukopa harusi, kulipa matanga, labda cheki MATAGA itataga
Nishani ya amani iso kifani kwa waghani
Duniani zamani tulidhani tafrani ni kani ya ku run pwani hata pwani
Greece Ubatani, tukasepea wadogo mpaka leo ukubwani...
Ahhhh

Shall I coniinue....?
Yes ndugu
 
Kama kweli pesa iliingizwa kwenye account yako kimakosa na wewe ulitegemea kupata hela katika siku kama hizo na unaweza kudhibitisha kuwa kweli ulikuwa unategema hela katika siku hizo, basi mtafute mwanasheria umueleze kila kitu atakusaidia sana. Sheria inakulinda sana. Nimesoma Laws related to Banking naelewa hii. Usipuuze pata msaada wa mwanasheria kabla hujaamua vingine
 
Fanya hivi, hiyo 6,500/- asubuhi nunua bundle la buku (data). Kisha 5,500/- tupia kwenye tigo pesa/m-pesa.

Download app ya 1xbet www.1xbet.com kisha fungua account humo kwa kufuata maelekezo. Kisha upload/deposit hiyo 5,000/-

Ukimaliza close app, fungua app ya Jamii Forums kisha ingia kwenye huu uzi


Wazee Wenzangu Wa Kuweka Mzigo (Kubet) - Karibuni Tubashiri Mechi Za Leo! - JamiiForums

Hapo utakutana na wataalamu wa mambo ya kuzalisha pesa kwa kucheza na intuition na lucky. Ukiwa na bahati mpaka jioni unaweza ukawa umepata pakuanzia.

 
Hii ni story ya uongo. Kwanza bank wakikosea wakaweka pesa kwenye acc yako haiwezi kufika zaid ya masaa 12 bila kujua ilo tatizo na kuzirudisha izo pesa au kukutafta kama umeshazitumia. Mimi ilishanitokea hata masaa 6 hayakufika wakawa wamenitafta na nkarudisha pesa yao.

Alafu pia kama hii story ni ya kweli, bank hawaweza kukupeleka popote yan wanakuwa wamekupa mkopo naa wewe unakubaliana nao kuwa uwalipe kidogo kidogo.

Acha itapeli.
 
umeshindwa kuilipa benk ndio uje utulipe wana uliotukuta jf!??
 
Pole ila pambanua fedha ina muda gani tangu umeichukua kufanya biashara na kudhulumiwa,ikibidi wataje waliokudhulumu maana nao wameshiriki katika matumizi ya fedha za bank.Ni heri kudaiwa na Bank ila sio watu 25..Usiogope kufungwa kama ulitumia hiyo fedha ila ukadhulumiwa,kifungo chako hakitakuwa kikubwa cha msingi kuwa na nidhamu endapo utaeenda jela! Kujua ni nuksi hata kwa jamii yako
 
We binti umepotelea wapi?

Studio ya kurekodi au studio apartment?
We Kiranga tafadhari huu uzi wa matatizo hivyo msianze hayo mambo mwenzenu anahitaji 5000 toka kwenu. Hamuelewi????? Mi sitoi ng'o!!!
 
Pole sana sana. Ulipokuwa unatumia hizo fedha wakati unajua sio zako ulitegemea nini?
haya, wewe wa jinsia gani na umri miaka mingapi?
 
Hii ni story ya uongo. Kwanza bank wakikosea wakaweka pesa kwenye acc yako haiwezi kufika zaid ya masaa 12 bila kujua ilo tatizo na kuzirudisha izo pesa au kukutafta kama umeshazitumia. Mimi ilishanitokea hata masaa 6 hayakufika wakawa wamenitafta na nkarudisha pesa yao.

Alafu pia kama hii story ni ya kweli, bank hawaweza kukupeleka popote yan wanakuwa wamekupa mkopo naa wewe unakubaliana nao kuwa uwalipe kidogo kidogo.

Acha itapeli.
Wewe nani kakwambia haiwezi kuzidi masaa 12? Sisi bankers tunajua hii mambo. Hata siku 2 inawezekana. Especially kama ni weekend.

Tena inaweza hata kuchukua hata wiki mpaka mteja aliyetakiwa kuwekewa aulizie au lalamike. Maana suspense account zinakuwa zimebalance
 
We Kiranga tafadhari huu uzi wa matatizo hivyo msianze hayo mambo mwenzenu anahitaji 5000 toka kwenu. Hamuelewi????? Mi sitoi ng'o!!!
Dunia matatizo, fight tulizo kaa RIP Kizzo
Haya mengine maigizo ya ndizo sizo
We Igiza Ibiza, nakimbiza giza
Gabreselassie, uzuri wamhongela kuhasi
Common sense inatoweka kaa chura wa Kihansi
Toa ndugu toa ndugu, kimya ka sura ya bubu wa Bububu
Michango Sugu inaota kaa magugu
Chota maji Sahara kwa maneno ya kuhara
Toa kafara busara, zamisha meli Ukara
Kwa hadithi za ufala, omba sala na miamala
Ya kujenga barabara Salasala
Jishebedue ki Bedui, kimbia ka Nyambui
Sema kama hujui
Marathon Ikangaa, waache wanashangaa
Wakistikia umebugia damu mumia, wahangaaa
Piga kidachi, mpira one touch, ki Shakespeare
Usiache ushahidi kati, sitaki sikia
Jaza ujinga, hoja pinga kwa kinga inayolinda
Remba marinda kwa wanaodinda, toka kibingwa
Daresalama, kuishi karama ya kukabili gharama
Na wasanii wako wengi hawana alama
 

Ila we mzee wewe
Vyuma vya Baba J, buma ka Jei Kei
Huna kukaba bei, vuma la cheichei
Danga la Darislamu
Janga kabla salamu
Mpela mpela, shuta karamu, nanga haramu
Mnyonge Hanga, zubaa bila shufaa kaa sanamu
Moto boiling point ka Jehanamu, sina hamu
Kufa hatufi, maisha zigo la chuki
Mizinga na mikuki, kama nyuki
Kaiba haiba, swahiba kaimba
Faida sikawaida,kawinda kwa inda
Vumbua mavumba, zaa toa ugumba,
Uza nyumba weka heshima bar Zanzibar kindumba
Deni unalifuga, halifungi,halimbungi
Tamthiliya kubwa, "Weep Not, Child" wa Thiong'o Ngugi
 
Back
Top Bottom