Nifuge Kuku au Sato?

Nifuge Kuku au Sato?

Habarini wadau.
Nimepata kamtaji hapa ka 10m, Nina eneo la ekari mbili mkuranga.
Enyi wajuvi.
Naombeni msaada kwenu.
Ufugaji upi unalipa kati ya samaki sato au kuku wa kisasa?
Naomba maoni yako hapa.
Fuga kuku mkuu andaa mabanda mazuri tu
Kufuga samaki sato ni ngumu kwanza utahitajika uchimbe mabwawa ya kufugia
Bado chakula ni bei sana
Uwe na source ya maji yakueleweka yasiwe ya chumvi
Utahitaji wataalamu wa aquaculture
 
Huo mtaji kwa samaki utakimbia mapambano. Hizo ekari mbili inafaa kwa kuku wawe wa kisasa au kienyeji utajua wewe ila kila kimoja kina mpangilio wake. Huo mtaji kuchimba bwawa la samaki tu haitoshi, maana huwezi chimba kibwawa cha samaki wachache economies of scale itakukatalia. Wakati kwa kuku unaweza fuga hata kama kucheza yaani huku shamba la mihogo hapa banda la kuku.
 
Huo mtaji kwa samaki utakimbia mapambano. Hizo ekari mbili inafaa kwa kuku wawe wa kisasa au kienyeji utajua wewe ila kila kimoja kina mpangilio wake. Huo mtaji kuchimba bwawa la samaki tu haitoshi, maana huwezi chimba kibwawa cha samaki wachache economies of scale itakukatalia. Wakati kwa kuku unaweza fuga hata kama kucheza yaani huku shamba la mihogo hapa banda la kuku.
Kufunga kuku uache kazi ufanye kazi
 
Back
Top Bottom