cold water
JF-Expert Member
- Oct 6, 2021
- 323
- 1,128
Aisee,nipo nyumba ya kupanga nimeweka dressing table Ina kioo, wadogo zangu wanapenda kunitembelea, wakifika tu kunitembelea lazima wazame chumbani niwepo nisiwepo,hata nisipokuepo lazima utakuta mabadiliko chumbani,nikasema isiwe kesi niweke kioo full sebureni hapa nilipoweka kochi na tv lakini bado lazima waende chumbani ni wadogo zangu wa damu mama mmoja baba mmoja,wa kiume lazima azame room shida ni kwamba chumba hakina mlango kina pazia tu ni ramani ya nyumba yenyewe mlango uko mmoja tu wa sebureni.huyu wa kike utakuta mimi nimekaa hapa sebureni utakuta anapitiliza moja Kwa moja chumbani vipi wakimkuta mwanaume wangu huko ndani amelala,ndio naishi peke angu lakini uwezi jua na mimi ni binadamu siku wakimkuta mtu huko room kwangu factly nakerekwa Sana na tabia Yao hii ya kuingia room bila utaratibu.leo Hadi nimeandika hivi nimekerekwa zaidi Kuna kipimo Cha mimba nilipima jana nilikiacha tu juu kwenye dressing table sikujua kama atafika dogo Leo home.