Nyamayao
JF-Expert Member
- Jan 22, 2009
- 6,966
- 2,352
Habari zenu nyote, naomba niwashirikishe kwa hili linalonisumbua kwasasa,
Nilishawahi kusema humu kuhusu Baba yangu, Sasa huyu mzee kwasasa tunaambiwa ni mgonjwa sana, anahitaji watu wa karibu wa kumuangalia na misaada mingine ya matibabu, kwasasa hatupigii sisi simu bali anamtumia dada yake (Shangazi) aongee na Mama kwahiyo habari zote tunazipata kwa mama.
Anatakiwa mtu aende Dar ama mgonjwa aende mji wowote kwa maangalizi ya karibu, nikisema mji wowote namaanisha kwamba huyu Baba ana wanawake/watoto miji tofauti tofauti, labda Arusha, Musoma kuna Mtoto wake wa kwanza mkubwa tu ambae nilishawahi kumuona, Dar hiyo ana watoto/wake , Mwanza pia, tatizo langu ni kwamba hakuna anaetaka jukumu hili, hata wale watoto wake aliowalea vizuri wakakua wakaanza maisha yao na miji yao nao wapo kimya, Wanawake aliozaa nao tunaambiwa wanaenda tu hapo nyumbani kumpikia na kuondoka, hana mtu wa karibu wa kumpa uwangalizi mzuri.
Hili limegeuka shida kwetu, kwamba sasa mimi na dada yangu ndio tuchukue hili jukumu, dada yangu hataki hata kusikia hii habari, mie walimwengu wananiambia nibebe hili jukumu mana kuna "laana" Mzee asije kufariki tukapata "laana" kwamba nisichukulie maamuzi ya dada yangu bali niwe na maamuzi yangu kukwepa "laana" Najiuliza hivi "laana" zinaachwaje jamani, kwamba sisi kunung'unika koteee kipindi hiko baadhi ya walimwengu wananiambia ndio laana imemfika, kwamba maisha yake yamekuwa jinsi yalivyo kwasasa, siamini hili mana na sisi tuliyaacha hayo na kusonga na maisha yetu.
Sasa basi kama dada yangu mzazi hataki hili jukumu kwamba alikuwa wapi wakati tukitaabika na mama yetu yeye akila raha zake sasa hivi aje atusumbue? wanawake aliozaa/kula nao raha wako wapi, watoto wake rundo wengine wapo wapi, kwanini sisi?
Dada ameshajitoa, hapa ni mie niamua kufanya maamuzi ya kubeba huu mzigo, ni kwamba nimlete huku nilipo ana nilimpekele Njoro kwa mama, huku mimi sitaweza, sina mtu wa kunisaidia katika hili jukumu, mana kama naambiwa anaumwa sana basi sitaweza kumfanyia yote, Msukuma wangu ni mtu wa masafari sana hataweza, bali kaniambia yupo nyuma ya maamuzi yangu yoyote kwa msaada wowote, kilichopo ni kumpeleka kwa mama, MMh hapo kwa mama sasa, ni kwamba ni mashamba/maeneo ya urithi, Babu alivyoona mama anateseka wakati huo huyu Mzee alivyomtelekeza akamkatia mama Kiamba aanze maisha,alianza mdogo mdogo mpaka tumekuwa tumepatengeneza ipasavyo ndio mji wa mama akiwa amezungukwa na ndugu zake, Huyu mzee anaendaje kuanza maisha ya pale? Mama anasema hawezi kwenda Dar kukaa kwa "watu" akimaanisha hiyo nyumba ya Mzee ina wenyewe (wanawake aliozaa nao). Kaka yake na mama (mjomba) anasema haya ni maisha yanaweza kutokea kwa kila mtu kama ninaweza kumleta kwa mama nifanye hivyo, hapa dada yangu ananilalamikia kwanini nataka kumsumbua/kumtesa mama kwa mambo ambayo hayamuhusu tena? kwanini nakazania mambo na kujifanya nina huruma sana wakati Mzee hakuwa na huruma yoyote kwetu? "nina kiherehere sana"
Na mie kwa upande wangu najiuliza kwanini mie? kwanini nibebe hili jukumu la Mzee ambae hakujali maisha yetu kabisaaa, hii laana ninayoambiwa isinipate mbona haitendi haki jamani? kama ndio hivyo kwahiyo hii laana naikwepa mie mwenyewe tu lakini kwa watoto/wanawake/aliekuwa mke wake zitawafikia? na kama zitawafikia mbona hawana hofu wala hawaonekani kujali? Kwanini mie baadhi ya ndugu/jamaa/marafiki wananiambia nijiepushe na hii laana?
Kwa aliewahi kuuguza anajua mambo yanavyokuwa, na hali ikiwa ndivyo sivyo inabidi mie ndio niwe mchezaji mzima wa hilo game. kwanini nijitie kitanzini jamani?
Naomba muwe wapole, hatuhukumiani hapa bali nataka kusikia tu na wenzangu mngekuwa kwenye situation kama yangu mngeitatuaje?
Asanteni sana.
Nilishawahi kusema humu kuhusu Baba yangu, Sasa huyu mzee kwasasa tunaambiwa ni mgonjwa sana, anahitaji watu wa karibu wa kumuangalia na misaada mingine ya matibabu, kwasasa hatupigii sisi simu bali anamtumia dada yake (Shangazi) aongee na Mama kwahiyo habari zote tunazipata kwa mama.
Anatakiwa mtu aende Dar ama mgonjwa aende mji wowote kwa maangalizi ya karibu, nikisema mji wowote namaanisha kwamba huyu Baba ana wanawake/watoto miji tofauti tofauti, labda Arusha, Musoma kuna Mtoto wake wa kwanza mkubwa tu ambae nilishawahi kumuona, Dar hiyo ana watoto/wake , Mwanza pia, tatizo langu ni kwamba hakuna anaetaka jukumu hili, hata wale watoto wake aliowalea vizuri wakakua wakaanza maisha yao na miji yao nao wapo kimya, Wanawake aliozaa nao tunaambiwa wanaenda tu hapo nyumbani kumpikia na kuondoka, hana mtu wa karibu wa kumpa uwangalizi mzuri.
Hili limegeuka shida kwetu, kwamba sasa mimi na dada yangu ndio tuchukue hili jukumu, dada yangu hataki hata kusikia hii habari, mie walimwengu wananiambia nibebe hili jukumu mana kuna "laana" Mzee asije kufariki tukapata "laana" kwamba nisichukulie maamuzi ya dada yangu bali niwe na maamuzi yangu kukwepa "laana" Najiuliza hivi "laana" zinaachwaje jamani, kwamba sisi kunung'unika koteee kipindi hiko baadhi ya walimwengu wananiambia ndio laana imemfika, kwamba maisha yake yamekuwa jinsi yalivyo kwasasa, siamini hili mana na sisi tuliyaacha hayo na kusonga na maisha yetu.
Sasa basi kama dada yangu mzazi hataki hili jukumu kwamba alikuwa wapi wakati tukitaabika na mama yetu yeye akila raha zake sasa hivi aje atusumbue? wanawake aliozaa/kula nao raha wako wapi, watoto wake rundo wengine wapo wapi, kwanini sisi?
Dada ameshajitoa, hapa ni mie niamua kufanya maamuzi ya kubeba huu mzigo, ni kwamba nimlete huku nilipo ana nilimpekele Njoro kwa mama, huku mimi sitaweza, sina mtu wa kunisaidia katika hili jukumu, mana kama naambiwa anaumwa sana basi sitaweza kumfanyia yote, Msukuma wangu ni mtu wa masafari sana hataweza, bali kaniambia yupo nyuma ya maamuzi yangu yoyote kwa msaada wowote, kilichopo ni kumpeleka kwa mama, MMh hapo kwa mama sasa, ni kwamba ni mashamba/maeneo ya urithi, Babu alivyoona mama anateseka wakati huo huyu Mzee alivyomtelekeza akamkatia mama Kiamba aanze maisha,alianza mdogo mdogo mpaka tumekuwa tumepatengeneza ipasavyo ndio mji wa mama akiwa amezungukwa na ndugu zake, Huyu mzee anaendaje kuanza maisha ya pale? Mama anasema hawezi kwenda Dar kukaa kwa "watu" akimaanisha hiyo nyumba ya Mzee ina wenyewe (wanawake aliozaa nao). Kaka yake na mama (mjomba) anasema haya ni maisha yanaweza kutokea kwa kila mtu kama ninaweza kumleta kwa mama nifanye hivyo, hapa dada yangu ananilalamikia kwanini nataka kumsumbua/kumtesa mama kwa mambo ambayo hayamuhusu tena? kwanini nakazania mambo na kujifanya nina huruma sana wakati Mzee hakuwa na huruma yoyote kwetu? "nina kiherehere sana"
Na mie kwa upande wangu najiuliza kwanini mie? kwanini nibebe hili jukumu la Mzee ambae hakujali maisha yetu kabisaaa, hii laana ninayoambiwa isinipate mbona haitendi haki jamani? kama ndio hivyo kwahiyo hii laana naikwepa mie mwenyewe tu lakini kwa watoto/wanawake/aliekuwa mke wake zitawafikia? na kama zitawafikia mbona hawana hofu wala hawaonekani kujali? Kwanini mie baadhi ya ndugu/jamaa/marafiki wananiambia nijiepushe na hii laana?
Kwa aliewahi kuuguza anajua mambo yanavyokuwa, na hali ikiwa ndivyo sivyo inabidi mie ndio niwe mchezaji mzima wa hilo game. kwanini nijitie kitanzini jamani?
Naomba muwe wapole, hatuhukumiani hapa bali nataka kusikia tu na wenzangu mngekuwa kwenye situation kama yangu mngeitatuaje?
Asanteni sana.