Nifanyaje juu ya hili jambo?

Nifanyaje juu ya hili jambo?

Hata mambo yakienda ndivyo sivyo, mnamrudisha kwake, lazima ana eneo lake mahali.

Ninachojua ana nyumba tu, sehemu alikuwa nayo huko Musoma alipozalia mtoto wake wa kwanza nae nasikia kapauzaga kabakiwa na kanyumba tu, sijui atakuwa wa kurudisha Dar dada yake apambane sijui itakuwaje sijui kabisa, kwanini haya majaribu lakini?
 
pole nyama yao kaza moyo msaidie huyo mzee kisasi mwachieni mungu atalipa kwa niaba yenu gangeni yajayo
 
wengi wetu tushauguza wazazi wetu,,,,hilo lisikuumize,,, hivi akirest in pis mtasusa? fanya kama wewe,,, usiangalie ndugu waliokuzunguka......inuka ukatende wema kwa babako.....

Hya ni majaribu jamani! sijui naanzia wapi mana nimebaki mwenyewe.
 
Mama yeye anasemaje? Yuko tayari kumpokea na kumsaidia kipindi hiki anaumwa?

Kama na mjomba na msukuma, ambao nilidhani watakupinga sana, na wao wanakubali kukupa sapoti, basi msaidie mzee.

Dada yako hata asemeje, hufanyi kwa ajili yake, unafanya kwa ajili yako. Labda kwa kufanya kwako hivyo hata dada yako ataingiwa na imani.

Kuna wakati mzazi anakuumiza sana, lakini ukimkuta ana shida moyo unarudi nyuma, ndio kinachokutokea wewe. Bora ufanye mapema usije kujilaumu. Siamini saana kwenye laana, lakini najua ukitenda wema, malipo huja hapa hapa duniani.

Kongosho, kwa hili limeniumiza kuliko mengine niliyowaza juu ya huyu Mzee, kwamba ni kama "nimesusiwa" ila natamani kusaidia, ingekuwa ni msaada wakifedha tu nisingekuwa na shida, hapa hana mtu wa kumuangalia kwa karibu,huku kwangu atateseka tu, kwa mama, dada ndio ananiambia namsumbulia/mtesa mama yake kwa mambo yaliyopitaga na kujifanya nina huruma sana.
 
Unadhani mwenyewe unashindwa? Utaweza sana, kama msukuma yuko nyuma yako kwa nini ushindwe? Hakuna gumu lisilo na suluhisho.


Usumbufu, ndio utaupata, lakini huwezi kushindwa kama una nia.

Hya ni majaribu jamani! sijui naanzia wapi mana nimebaki mwenyewe.
 
Labda kwa sababu una imani thabiti, Mungu anatafuta pa kumsimnagia shetani.

Hatujaribiwi wenye imani ndogo, maana dunia haitajua, wanajaribiwa wenye imani kubwa, maana matendo yao yatawafikia na kuwagusa makumi elfu na kuonesha utukufu wa unayemwamini.

Ninachojua ana nyumba tu, sehemu alikuwa nayo huko Musoma alipozalia mtoto wake wa kwanza nae nasikia kapauzaga kabakiwa na kanyumba tu, sijui atakuwa wa kurudisha Dar dada yake apambane sijui itakuwaje sijui kabisa, kwanini haya majaribu lakini?
 
Likitokea la kutokea, mnatafuta njia rahisi ya kumaliza tatizo, kama wanae wenyewe hawasemi lolote. Lakini wazee wengine husema kabisa.

Ni ngumu kumuuliza swali kama hili. Au basi muulize ndugu zake wengine kama dada au kaka, watajua tu.

Ninachojua ana nyumba tu, sehemu alikuwa nayo huko Musoma alipozalia mtoto wake wa kwanza nae nasikia kapauzaga kabakiwa na kanyumba tu, sijui atakuwa wa kurudisha Dar dada yake apambane sijui itakuwaje sijui kabisa, kwanini haya majaribu lakini?
 
Siku zote ukifanya kitu usifanye kwa shinikizo la mtu au kwasababu huyo mtu alikuwa mwema kwako,tenda wema nenda zako usingoje shukurani!Huyo ni mzazi wako na kama unajitolea kumsaidia msaidie tu amalizie siku za kwa amani...usimpe lawama kwa yaliyopita si ndwele tugange yajayo...Hakuna kitu kinachoitwa laana ila usipomsaidia mzazi wako nafsi yako itakusuta maisha yako yote kwasababu nimekusoma unataka kumsaidia lakini unajali sana watu watakufikiriaje na itawaathiri vipi...wewe ni mtu mwema usifanye makosa aliyofanya mzazi wako muoneshe kwamba ijapokuwa hakuwa baba mwema kwako lakini wewe umekuwa mtu mwema,mwenye busara,hekima na utu.. na unajali maslahi yake.Hakika mzazi wako atafurahia matunda ya mbegu zake na atajuta kwa aloyatenda.
 
True, nakubaliana na wewe, just for God's sake!

Well said, nami nimenote roho ya huruma aliyonayo ingawa anatamani angekuwa na moyo mgumu kama wale waliokataa.

She should take care of her dad for God's sake. Itamsaidia sana.
 
Leo, nimeulizwa hili swali na dada yake Mzee, nimeshindwa kulijibu!

Hukuweza kujibu coz ulikuwa unajaribu kudanganya nafsi lakin ukweli kuwa mtaenda na kama kuna michango yoyote mtatoa mpaka hao wanaomkataa sasa hv.Msaidie mzazi wako kulingana na uwezo wako.
 
Kongosho, kwa hili limeniumiza kuliko mengine niliyowaza juu ya huyu Mzee, kwamba ni kama "nimesusiwa" ila natamani kusaidia, ingekuwa ni msaada wakifedha tu nisingekuwa na shida, hapa hana mtu wa kumuangalia kwa karibu,huku kwangu atateseka tu, kwa mama, dada ndio ananiambia namsumbulia/mtesa mama yake kwa mambo yaliyopitaga na kujifanya nina huruma sana.

hayo mateso Mugu keshampa hapa hapa duniani tayari na meshajuta, we msidie tu sbb ni mzazi wako..mzazi halipiziwi kisasi my dear..we msaidie tu na utashangaa Mungu atakavyokubariki maisha yako hapo baadae...funga macho beba mzigo japo mzito
 
Mama yeye anasemaje?[/COLOR]Yuko tayari kumpokea na kumsaidia kipindi hiki anaumwa?

Kama na mjomba na msukuma, ambao nilidhani watakupinga sana, na wao wanakubali kukupa sapoti, basi msaidie mzee.

Dada yako hata asemeje, hufanyi kwa ajili yake, unafanya kwa ajili yako. Labda kwa kufanya kwako hivyo hata dada yako ataingiwa na imani.

Kuna wakati mzazi anakuumiza sana, lakini ukimkuta ana shida moyo unarudi nyuma, ndio kinachokutokea wewe. Bora ufanye mapema usije kujilaumu. Siamini saana kwenye laana, lakini najua ukitenda wema, malipo huja hapa hapa duniani.

Imebidi nisiongee nae tena juu ya hili mana juzi kati aliniambia hivi kwanini mimi nimuuguze wakati alikuwa na wake kila kona? wajipange wanisaidie kama walivyonisaidia mwanzoni, mwehh, ni kama dada kashampiga mkwara mkali.
 
vipi mama yako amekubali? kama amekubali basi we mchukue tu.....ujue Mungu alivyo wa ajabu yani wale aliowatupa ndio wanamsaidia sasa, wale aliowajali ndio wamemtelkeza.....hicho tu chatosha kuwa mateso ya moyo kwake dumu daima..
 
Labda kwa sababu una imani thabiti, Mungu anatafuta pa kumsimnagia shetani.

Hatujaribiwi wenye imani ndogo, maana dunia haitajua, wanajaribiwa wenye imani kubwa, maana matendo yao yatawafikia na kuwagusa makumi elfu na kuonesha utukufu wa unayemwamini.

Maneno yako leo, mhh mana unazidi kunitilisha huruma juu ya huyu Mzee.
 
Uliza watu wenye kuwa thamini babazo !! wewe na mali yako ni mamluki wa baba yako!! Tafadhali wahisha upate radhi zake. utakuwa na maisha mema na baraka kataik uhai wako.
 
Siku zote ukifanya kitu usifanye kwa shinikizo la mtu au kwasababu huyo mtu alikuwa mwema kwako,tenda wema nenda zako usingoje shukurani!Huyo ni mzazi wako na kama unajitolea kumsaidia msaidie tu amalizie siku za kwa amani...usimpe lawama kwa yaliyopita si ndwele tugange yajayo...Hakuna kitu kinachoitwa laana ila usipomsaidia mzazi wako nafsi yako itakusuta maisha yako yote kwasababu nimekusoma unataka kumsaidia lakini unajali sana watu watakufikiriaje na itawaathiri vipi...wewe ni mtu mwema usifanye makosa aliyofanya mzazi wako muoneshe kwamba ijapokuwa hakuwa baba mwema kwako lakini wewe umekuwa mtu mwema,mwenye busara,hekima na utu.. na unajali maslahi yake.Hakika mzazi wako atafurahia matunda ya mbegu zake na atajuta kwa aloyatenda.

Hapo sasa....hizi mbegu mbona hakutaka kuzirutubisha aje avune kinachostahili?
 
pole mwaya...dah sipati picha ulivosihi bila baba na kukua...mimi baba yangu pamoja na kuachana na mama yangu alivonipenda na kunijali ilipunguza gape kuubwa ya kumkosa mama japo sikuwa nae..baba yangu alikuwa ndio kila kitu kwenye maisha yangu....,yaani hadi nimeolewa ananipa hela ya matumizi hadi nikawa naona aibu..... i can feel unavyojisikia kwa aliyokufanyia bali just forgive and forget the past..pole sana dear
 
Ubaya haulipwi kwa ubaya ndugu yangu. Huyo ni mzazi wako hata ufanyeje,haibadiliki. Usiangalie alichokufanyieni wakati huo wala usisikilize maneno ya watu,Kisasi hakijengi. Tekeleza jukumu lako kama mtoto,Mwenyezi Mungu atakuwa radhi na wewe juu ya kila jambo utakalofanya hapa duniani na utapata "peace of mind" hadi mwisho wa uhai wako. Mchukue wala usifikirie mara mbili mbili ndugu yangu,..usidanganyike na ulimwengu kama alivyodangayika yeye. Pumzi zina mwisho hizi.
 
Sijui nisemeje ndugu,mie bado nina kinyongo nae, bado sijaachia moyo kivilee.

Nyama yao nimeelewa situation muliyonayo!

Ngoja nitiririke hivi:

Baba yenu si mtu mzuri! Alichokifanya yastahili yamkute yanayomkuta sasa!
Nadhani ile principle ya karma inafanya kazi yake!

Ule msemo "fainali uzeeni" ndio unafanya kazi!

Ningependa utoe wasi wasi kwamba kitendo cha kumuabonden huyo mzee hakuna laana itakayokukuta!
Walatin walisema 'Volenti non fit injuria!' waswahili wakatafsiri 'kusudi haiambiwi pole!'

Laana anatoa Mungu ikiwa nawe unaamini nguvu na uwepo wake (Mungu) Laana hutolewa kwa kulipa mabaya pale ulipokopeshwa mema!

Hiyo ni wazi kwamba hakuna laana itakayokukuta kwa kutompokea baba yako!

Huo ni upande mmoja! Na ufuatao ni upande wa pili:

Waswahili walisema "mama ni mama hata kama ni rikwama/mkokoteni" Ikimaanisha, hata awe chizi, muhuni, malaya, katili nk, bado atabaki kuwa mama kwa wewe aliekuzaa! Hiyo inamaana ya kwamba WAJIBU WAKO KWA MAMA UTABAKI PALE PALE!

Ningependa usikariri! Neno mama hapo halijawa limited kumuexclude baba! kwa lugha nyepesi neno 'mama' lina maana ya 'mzazi'

Kwa mantiki hiyo, wajibu wako kwa mzazi (baba yako) bado uko pale pale!

Ukiamua kutomsaidia baba yako mzazi ni sawa kutokana na aliyoyafanya! Kuna mtaalamu alisema wajibu huendana na haki, haki yako ikivunjwa wajibu huna! But itakuwa sawa zaidi pale utakapoamua kumsaidia baba yako! Ukumbuke! Ile principle ya karma haitaishia kwa baba yako tu!

Siku zote ishi wewe kama wewe! Kitendo cha dada yako kukataa kumsaidia mzee isiwe sababu ya wewe kufata uamuzi wake! imeandikwa kila mtu atabeba mzigo wake!

Kitendo cha wewe kumsaidia baba yako licha ya mabaya aliyokufanyia (aliyowafanyia) ni kupata baraka za Mungu (kama unamuamini) na ni njia moja wapo ya kukuza nguvu zako za asili (psychic power) alizokujalia Muumba wako! For sure psychic power hufunguka kwa upendo na huruma! Embu zingatia hilo! Au haujui faida za psychic power?

Vile vile ukimsaidia baba yako licha ya mambo aliyowafanyia, hufanyi hivyo bure! Kuna malipo mazuri kwa Muumba wako!

Laiti ungetambua psychological disorder anayosuffer baba yako kwa sasa, hata usingeanzisha huu uzi instead ungemruhusu mzee wako kuja ktk himaya yako!
...
Ni vipi utamsaidia mzee wakati mmeo ni mtu wa kusafiri na wewe ni mtu wa mihangaiko?

Kwanza mshukuru Mungu kwa kukupatia mme bora na mwenye upendo! Kitendo cha mmeo kukuahidi atakuwa nawe bega kwa bega kutokana na janga linalokukabili, unapaswa uitumie vyema hiyo chance kwa kumuhudumia baba yako as if hakuna ubaya wowote aliyokutendea!

Jaribu hata kuajiri mtu ili akusaidie kumhandle mzee!
Usiache neema ya kumuhudumia mzee ikupotee hivi hivi! Yule ni baba yako!
...

I hope umenielewa na nakutakia kila la heri na Mungu akusaidie!
 
Back
Top Bottom