hayo mateso Mugu keshampa hapa hapa duniani tayari na meshajuta, we msidie tu sbb ni mzazi wako..mzazi halipiziwi kisasi my dear..we msaidie tu na utashangaa Mungu atakavyokubariki maisha yako hapo baadae...funga macho beba mzigo japo mzito
Sijui nisemeje ndugu,mie bado nina kinyongo nae, bado sijaachia moyo kivilee.
King'asti, Kaunga, MwanajamiiOne,Preta,nyumba kubwa, Kongosho,The Boss, BAK, Asprin, Mbu, na wengineo hebu niambieni mwenzio nisipate "laana" mjue
Pagumu hapa Nyamayao, lakini msikilize sana dada yako na mama yako wote mfanye uamuzi wa pamoja, usithubutu kufanya uamuzi wa pekee yako bila kuwashirikisha. Kwa maoni yangu hapa hakuna laana, kutakuwaje na laana wakati yeye hakuwajali akawakimbia katika kipindi ambacho mlihitaji sana uwepo wake kama Baba/Mume!?
Kinachonistaajabisha ni kuona watoto aliowalea na kuwatunza vizuri nao wamemtelekeza. Ungekuwa na nafasi ya kumchukua kwako basi ningekushauri ufanye hivyo. Pole sana naona hili linakutafuna sana lakini huna kosa lolote lile na wala usijiumize kwa mawazo.
kama ni mimi ningekuwa namtumia hela ahudumiwe tu huko huko. nafikiri hata mungu angeona kama nimemsaidia mzee.
Hapo na mie ndio panaponishangaza, jana niliongea na dada yake mzee nikamuuliza hilo, akaniambia kila mtoto anakimbizana kumtengenezea maisha mama yake, kuna wanaomjengea mama yao mbweni huko nao wanasema hawana hela wapo kwenye ujenzi, wa mwanza huyo ndio wa kiume mkubwa ambae angeweza kupambana kwenye uuguzi ipasavyo nae kimya ni mama yake tu anaenda hapo kupika na mwanae nae anasema hana hela biashara zake hazipo vizuri kwasasa, jana hicho chakula nilichoambiwa amepikiwa nilichoka kabisaaaaa nikajuta kuuliza.
Kuna wakati hela si suluhisho. Hivi unakumbuka hata kwenye movie wakikasirika wanatukananaje? 'You will die alone'
Hakuna kitu kibaya kama kufa peke yako wakati familia yako haipo, mgonjwa anahitaji upendo, tane kama huyu anahitaji kujisamehe na kusamehewa. Hata kama akitangulia mbele, aende kwa amani.
Mtu baki, may be? Mzazi? Hapana kwa kweli.
Kuna wakati unaoga ugumu kumsaidia mtu sababu ya ugumu wa maisha unaokusonga. Mtu yule akifa, halafu na wewe ukawa umesha move step ahead, nafsi huwa inakosa raha kabisa ukikumbuka ulishindwa msaidia kitu kidogo kama kile. Usumbufu/gharama huwa ni vitu vya muda na hubadilika sometimes.
Be nice to people because you are nice to yourself
not because they are nice to you.....