karimu mtila mohamedi,
Nimemuona
NullPointer kupitia post #19 amekuka makavu kama Sospeter Muhongo fulani hivi but TRUST me, of all advices uliopata hadi sasa na ule utaoendelea kuupata, tumia ushauri wa NullPointer kama base ya vyote! Je, hivi hufahamu kwamba wanao-click hizo adsense ni watu kama mimi na wewe? I hope unafahamu hata kama watu wa IT watakuambia ya kwao! Sasa ikiwa wanao-click adsense ni watu kama mimi na wewe; ulishajiuliza ni watu wa ngapi kati ya sote ambao tumechangia mada hii hapo kabla walikuwa wanaifahamu blog yako? Mimi binafsi nilikuwa siifahamu my chance to click your adsense was 0%!
Hapo ndipo unapokuja umuhimu wa hoja ya kwanza ya NullPointer ya kutangaza blog yako purposely in order to drive traffic in! Haya mambo ya coding sijui nini na nini ni supportive tools tu and not otherwise! Google IT folks are too smart than many IT folks outside the ring kwahiyo huwezi kutumia maujanja yako ya IT kirahisirahisi tu halafu ukaanza kuzivuna za Google; no way! There's no easy money with Google Adsense!
Pili; hapa ni kama ndo umeitangaza blog yako ndio maana mtu kama mimi na probably wengine tumeweza kuifahamu kwa mara ya kwanza! Another questiom; hivi umeshawahi kujiuliza why should I visit your blog tomorrow and tomorrow or even few hours from now? I hate to say this, but if I wanna be honest to you; sina sababu ya kunifanya nitembelee tena blog yako; today or even after! Nakera enh? Inawezekana lakini huo ndio ukweli wenyewe... sina hiyo sababu!
Maudhi niliyokuletea hapo juu yanaleta hoja ya pili ya NullPointer... kwamba, andaa/tengeneza/tafuta original contents! Hakuna code yoyote ambayo ina-trick surfing yako na kujikuta umeingia JF bila kupenda... unakuja mwenyewe kwa mahaba yako tena bila kukulazimisha mtu! WHY? There's something in JF... contents! Good for JF because it's User's Based Content lakini kwa issue kama yako, ni Blogger's Based Content kwahiyo ni wajibu wako kutengeneza contents; ama wewe mwenyewe au kuwalipa watu! Remember; kuna watu wanaishi kwa kazi ya Contents Writing!
Endapo baada ya mimi kuingia kwenye blog yako ningekuta some contents of my interests, kesho ningerudi tu kama ambavyo narudi kila wakati JF kwa matarajio yale yale ya kukuta CONTENTS! Ukitanganza blog yako na watu wakatembelea na kukuta contents, based na preference ya mtu na ubora wa contents zako; asilimia fulani ya wale wanaotembelea kwa mara ya kwanza unaweza kuwa-retain coz' wamekuta kitu ambacho kesho tena watakuja kuangalia kama kuna pishi lingine! Asikudanganye mtu; traffic ndio msingi wa kila kitu na anayekuambia kinyume chake anakutengenezea short-cut which, in most cases doesn't work well!
Kwa bahati mbaya sana, Bloggers wengi wa Tanzania wame-fail ktk hili!
Tatu; hivi umeshawahi kuya-study vizuri matangazo ya Adsense yanacyojitokeza? Hili bado sijalithibitisha lakini bado nalifanyia kazi! At least for now, nimegundua kwamba endapo kwenye blog X umefungua content inayozungumzia masuala ya smartphones; basi more likely Adsense pop-ups of similar subjects zitaanza kujitokeza! The same for online education or else! Ni very rare kamba umefungua contents kuhusu smart tv halafu yakaja matangazo ya mitumba! If to some extent nipo right; hivi sasa ni MENU ipi kwenye blog yako naweza kufungua kisha adsense za issue husika zikaanza ku pop-up? Hii maana yake ni kwamba, hata ukiamua kuandika contents, ktk hali ya kawaida utaandika basing on your available categories and pages which are: HOME, KITAIFA, MAGAZETI, MICHEZO, AJIRA, KIMATAIFA, ENGLISH NEWS, WASILIANA NASI!!! Inawezekana am not well informed about this particular subject but, kwa ufahamu wangu, hakuna Google Adsense for those categories! Si kwamba hazitatokea kabisa lakini hazina sababu za kutokea! REMEMBER, Adsense zinachokonolewa toka huko ziliko kwa kutumia Keywords zilizopo kwenye contents zako! Sasa sijui ni habari gani ya kitaifa utakayoandika hata ikaiweza kuyachokonoa matangazo ya adsense ya Samsung Smart TV!
Hivyo basi, ikiwa umeupokea ushauri wa NullPointer kuhusu CONTENTS basi nami ningekushauri uongeze angalau CATEGORY moja zaidi kuhusu kile ambacho unaamini kina matangazo mengi ya adsense! Kama ningekuwa mimi, ningeongeza category Electronics or something like that ambayo itakuwa inabeba contents za hiyo category! Hapa ndipo inakuja hoja ya
Heri lee assuming anayosema yote kuhusu mapato yako ni kweli; kweli kabisa! Hapa anaweza kudhani ni maujanja yake ya ki-IT ndiyo yanamletea mapato kumbe blog yake ipo kwenye niche market ambayo kimsingi ni category yenye matangazo mengi online! Remember, blog ya mdau anasema ime-base kwenye masuala ya kompyuta na simu... hiyo ni niche market yenye matangazo mengi tu lakini ni ngumu sana uwe unasoma habari za magazeti halafu yatokee matangazo!
Anyway, nisije nikajaza page manake sie wengine kuandika sio issue!!!