Wageni wakaazi wanapokuja nchini hupata kibali (working permit) ya miezi sita tu, hivyo kwa vyovyote vile ni lazima wapewe vitambulisho vya Mgeni Mkaazi kabla ya muda huo wa kibali chake hakijakwisha muda wake. Lakini pia Kitambulisho cha Taifa anachpoewa raia huyo wa kigeni kina ukomo tofauti na raia mzawa ambaye Kitambulisho chake cha uraia hakina ukomo. Aidha, idadi ya wageni wanaoomba vitambulisho vya Taifa kwa category yao ni wachache sana si zaidi ya 50,000 ukulinganisha na mamilioni kwa mamilioni ya raia wazawa, na hawa wageni wana aina yao tofauti ya Vitambulisho. Hivyo si kweli kwamba kuna upendeleo kwa wageni hakuna kitu kama hicho.
Kuhusu rushwa, ni vema tukaelewa kuwa unapojisajili kwa mara ya kwanza huduma yote ya usajili mpaka kupata Kitambulisho ni BURE hakuna malipo yeyote. Kama mtumishi wa NIDA anakuomba rushwa na una uhakika kabisa kuwa ni Mtumishi wa NIDA na una ushahidi wa kuombwa hiyo rushwa naomba tutoe taarifa TAKUKURU au kwa uongozi wa NIDA ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya wahusika. Tusilalamike tu bila sisi wenyewe kuchukua hatua lakini pia na sisi tusikubali kutoa rushwa, na ni vema pia tufahamu wako matapeli wanaojifanya ni watumishi wa NIDA wakati siyo, tunawapa pesa sisi wenyewe wakitupiga tunaanza kuwalalamikia NIDA, hatutendi sawa, hebu sisi wenyewe tusaidie mapambano dhidi ya rushwa kwa kukataa kutoa na kutoa taarifa.
Tatizo la watu ambao hawajapata vitambulisho vyao tayari imekwisha tangazwa rasmi kwamba Vitambulisho vimeanza kuzalishwa kwa wingi, kusambazwa na kugawiwa kwa wingi kwa wananchi wenye namba za Utambulisho. Zoezi la ugawaji Vitambulisho kwa Umma limezinduliwa hivi karibuni Musoma mkoani Mara, hivi sasa Vitambulisho vinaendelea kugawiwa kwa watu wote wenye namba katik awilaya zote za mkoa wa Mara, Wilaya zote za mkoa wa Mtwara, Wilaya zote za mkoa wa LIndi, Kigoma na Kagera. Baada ya hapo itafuata mikoa mingine hatua kwa hatua na wamesema bayana kuwa mpaka kufikia Machi 2024 wote tuliosajiliwa na kupata Namba tutakuwa tumepata Vitambulisho vyetu.
Jambo muhimu sana kuelewa ni kwamba Kilicho muhimu sana ni mtu kuwa na Utambulisho wa Taifa yaani umesajiliwa na kupata Namba yako ya Utambulisho wa Taifa ambayo hiyo ndiyo inatumika kukutambulisha na kukuwezesha kupata huduma yeyote hata kama huna Kitambulisho (Kadi). Kitambulisho au Kadi kama wengine wanavyokiita ni end product lakini Utambulisho halisi ni namba yako.