NIDA, mbona wageni wana vitambulisho na sio namba?

BLACK MOVEMENT

JF-Expert Member
Mar 11, 2020
2,712
6,508
NIDA imejaaa uhuni mwingi sana, Ulaghai na ujanja ujanja na kwa sasa wamewekeza sana kwenye Media. Diily wako kwenye media kuelezea mafanikio yao ambayo kiuhalisia hayapo zaidi ya Hadaaa tupu.

Raia wazawa waliojiandilisha 2018 wana namba pekee hadi sasa na kadi wanapigwa danadana hazija printiwa.

Cha kushangaza wageni wote wawe wanapewa vitambulisho vya ukaazi au vya uraia vya magumashi au vya halali ila wote wana vitambulisho na sio number.

Wahindi wote wana vitambulisho na sio number, wahamiaji haramu wana vitambulisho vya uraia na sio number.

Kuna raia mmoja ni Mkenya sijui alifanya fanya vipi akajiandilisha NIDA wanajua utaratibu wao wanao tumia kuwapa watu wasio raia Vitambulisho vya Uraia,Sasa huyo Raia amejiandikisha mwezi wa 6 mwaka huu,na tiyali ana kadi ya kitambulisho.ELewa kwamba kajiandikisha mwaka huu mwezi wa 6 ila NIDA wameisha mpatia kitambulisho.

Raia wanasafa tangia mwaka 2018 kadi zao hazijawahi printiwa.ila kuna watu wao wanakuja nyuma tena kagumashi na wanapewa kadi.

Sasa je raia wote na wao wanyoeshe mkono kwa stafu wa NIDA ili wapate kadi?

Taasisi imejaaa hadaaa sana ila cha ajabu inasifiwa na watawala nashindwa kukua wanasifiwa kwa lipi hasa.
 
NIDA imejaaa uhuni mwingi sana, Ulaghai na ujanja ujanja na kwa sasa wamewekeza sana kwenye Media. Diily wako kwenye media kuelezea mafanikio yao ambayo kiuhalisia hayapo zaidi ya Hadaaa tupu.



Taasisi imejaaa hadaaa sana ila cha ajabu inasifiwa na watawala nashindwa kukua wanasifiwa kwa lipi hasa.
Hii ndio Tanzania bwana. Na haya mambo yanapatikana Tanzania tu
 
Tukiongea kuhusu intelligence ya nchi tunaonekana siyo wazalendo NIDA ni sehemu sensitive lakini cha kushangaza ukiwa na laki4 au 5 kesho yake unaletewa kitambulisho chako mpaka nyumbani yani ata foleni ukai kuna wasomali na wakenya kibao wamekuja juzi tu sasa ivi wao na familia zao wanavitambulisho OG vya NIDA ..mwenzangu na mie utaambulia namba tu tena ni ya kusubiri baada ya wiki 2 ..

Kuna Wilaya Moja apa dar mkijiorganize watu kumi mkitoa 15k kila mmoja yani ile kufika Home jioni tayari upo kwenye system namba yako ya NIDA tayari ..TISS wapo kazi yao sijui ni nini kama NIDA inachezewa ivyo vipi uko sehemu nyingine.
 
Waache wadharau waruhusu huu ujinga, itafika mahali Vitambulisho vya Nida vitakua vinakataliwa sehemu.

Na sishangai kuna sehemu ukienda hawataki wala hawaelewi kitambulisho cha NIDA yani ni ujaanza upya process.
 
Tukiongea kuhusu intelligence ya nchi tunaonekana siyo wazalendo NIDA ni sehemu sensitive lakini cha kushangaza ukiwa na laki4 au 5 kesho yake unaletewa kitambulisho chako mpaka nyumbani yani ata foleni ukai kuna wasomali na wakenya kibao wamekuja juzi tu sasa ivi wao na familia zao wanavitambulisho OG vya NIDA ..mwenzangu na mie utaambulia namba tu tena ni ya kusubiri baada ya wiki 2 .. kuna Wilaya Moja apa dar mkijiorganize watu kumi mkitoa 15k kila mmoja yani ile kufika Home jioni tayari upo kwenye system namba yako ya NIDA tayari ..TISS wapo kazi yao sijui ni nini kama NIDA inachezewa ivyo vipi uko sehemu nyingine.
Kua mtanzania sio kigezo au haitoshi kukupa kila kitu bila kusota, tuko kwenye capitalism ambapo pesa ni muhimu kuliko utu au uzalendo, ujimaa ilisha kufa na Nyerere kitambo.........

Eewe endelea kuimba nyimbo za kale utakufa masikini na uzalendo wako wa kijinga, tafuta pesa ukanunue huduma muhimu ili uendelee kuishi vizuri, au wa Kenya wa hindi wa China wana haki nchini humu kuliko wewe kwasbb wana pesa zao na biashara zao zinalipishwa kodi serikali haiwezi kuwafuatilia sana kama unapo fikieia.
 
Dp wold wapewe NIDA si tumekiri kuwa tutachelewe sana bila Dp world apewe na Rita
 
Kua mtanzania sio kigezo au haitoshi kukupa kila kitu bila kusota, tuko kwenye capitalism ambapo pesa ni muhimu kuliko utu au uzalendo, ujimaa ilisha kufa na Nyerere kitambo.........

Eewe endelea kuimba nyimbo za kale utakufa masikini na uzalendo wako wa kijinga, tafuta pesa ukanunue huduma muhimu ili uendelee kuishi vizuri, au wa Kenya wa hindi wa China wana haki nchini humu kuliko wewe kwasbb wana pesa zao na biashara zao zinalipishwa kodi serikali haiwezi kuwafuatilia sana kama unapo fikieia.
Kweli mkuu..hii nchi kila Mtu anakula ofisini kwake
 
Huwa najiuliza,

Kwanini kadi ni muhimu kuliko namba ilihali kinachoandikwa kwenye hiyo kadi ni namba?

Kwanini tusiwe na namba moja tu inayoleta taarifa zote za mtu kuanzia uhai wa leseni ya udereva mpaka kodi za mapato anazodaiwa.

Kwa matumizi ya nje ya nchi zitumike passport.
 
Back
Top Bottom