valid statement
JF-Expert Member
- Sep 18, 2011
- 2,851
- 868
Nina rafiki yangu ambae tumetoka nae mbali sana, ni zaidi ya rafiki kwangu mana tunaishi kama ndugu kabisa. Jamaa yangu ana GF wake ambae amejiandaa atamvisha pete desemba hii, na wafunge ndoa april 2012. Jamaa anampenda sana huyu binti, tatizo ni nimekuja kugundua huyu binti si MWAMINIFU KABISA kwa jamaa yangu. Nimejua hili baada ya kumfuma live akiingizwa lodge kwenda kumegwa.Hapo lodge hawana bar kubwa ila kaunta ndogo ya vinywaji va wateja wanaolala na masofa pembeni ya wageni wa vinywaji tu. Siku moja mimi nkiwa nko mapokezi kaunta nateremsha lager akaja na mwanaume wakabuku chumba, ile anajeuka akakuta namwangalia. Akaja kunisalimia kwa kweli alitetemeka sana. Mpaka kajasho kakawa kanamtoka. Na alivo na bahati mbaya, mimi hupenda kunywa hapo, so nlishamwona 3times. Mara mbili hakuniona. Nikamuuliza kiujanja mtu wa pale mapokezi kuwa huyu dada kila nkija kunywa hapa nae huja kulalaga. Yule mtu wa mapokezi akanambia, huyu dada huwa anakujaga kulala hapo mara 2 au 3 kwa kila mwezi na huyo mwanaume.
Kwa kweli nimehuzunika sana. Jinsi ya kuanza kumwambia jamaa kuwa GF sio mwaminifu ndo inanishinda.
Mshkaji yani kapenda kama vile amewekewa dawa.
Wadau embu nipeni msaada wa jinsi ya kumweleza ukweli jamaa yangu huyu ajue afanyaje mapema.
Kwa kweli nimehuzunika sana. Jinsi ya kuanza kumwambia jamaa kuwa GF sio mwaminifu ndo inanishinda.
Mshkaji yani kapenda kama vile amewekewa dawa.
Wadau embu nipeni msaada wa jinsi ya kumweleza ukweli jamaa yangu huyu ajue afanyaje mapema.