Ni Zanzibar ipi wanaitaka?

Ni Zanzibar ipi wanaitaka?

walau wao wanapinga hii kitu wazi wazi

sie tumekuwa waoga kama panya vile

CHADEMA toeni tamko kuhusu hili

swali la kizushi

hati za muungano kwa nini zinafichwa?

kwa niin sherehe za muungano hazifanywi zanzibar?
 
Naikumbuka picha hii ni kutoka moja ya mikutano ya CUF mwaka 2000 wewe unaileta hapa ?
Wewe hivo vikaratasi vilivo mikononi unajua vimeandikwa nini??? Hiyo picha ni ya jana jioni pale Lumumba iliopigwa na Polisi mmoja ninamsitiri jina lake, wacha Wazenji wadai chao.
 
walau wao wanapinga hii kitu wazi wazi

sie tumekuwa waoga kama panya vile

CHADEMA toeni tamko kuhusu hili

swali la kizushi

hati za muungano kwa nini zinafichwa?

kwa niin sherehe za muungano hazifanywi zanzibar?

arigold hapo kwenye red umeuliza swali hata mimi najiuliza sana sana
 
Last edited by a moderator:
una maana tsunami?

Juzi Juzi walikuwa wanaswali kuzuia Hurricane isiivamie kisiwa cha Zanzibar na kukizoa, leo wameamua kukutana kujitenga na Tanganyika. Nawaamini kweli wana Freedom Heart kupigania Uhuru wao uliosombwa na Tanganyika. Na Tanganyika walivyo Wezi kwanini Zanzibar wasiwakimbie? More Power to Zanzibari People.
 
Hata mimi naungana na hao walionyoosha mikono, kuwa muungano 'no'
 
Wakuu tumetoka mbali. Nikisoma mchakato wa Katiba ya Mwaka 1977 nashangaa.

  1. watu 20 waliteuliwa kutunga katiba mpya. Wakajifungia mahala na baada ya wiki moja wakaja na draft ya Katiba.
  2. Ikapelekwa kwenye chama. Chama kikajifungia kwa wiki mbili kikaja na mapendekezo ya Katiba.
  3. Mapendekezo ya Katiba yakapelekwa bungeni, wabunge 3 tu wakachangia na Katiba ikapitishwa! Ndiyo hii tunayoitumia hadi leo.

Leo hii inatungwa sheria, Tume inateuliwa na kupewa miezi 18 ili kutafuta maoni ya wananchi. Kisha ije na draft na kisha ipelekwe kwenye Bunge Maalum la Katiba. Tumepiga hatua.
 
Yule Mze alikuwa anajuwa kubaka tu waarab. English ilikuwa not reachable/no network.

Kumbe ndio maana hakuruhusiwa kwenda kusaini akiwa na washauri wake. Ila baadaye aling'amua akawa mkali lakini bahati mbaya mungu akampenda zaidi. Akaja Alhaji Abdu Jumbe Mwinyi naye akawa mjanja kidogo lakini akachafua hali ya hewa ya kisiasa akapewa makzi ya kudumu Mji mwema.
 
Muungano utadumu kwa vizazi na vizazi vingi vijavyo. Hao wanacheza makidamakida kwenye nyaya za umeme, kwisheni!!
Hivi! hawa wa TANGANIKA wanafaidika nini ktk Muungano? inaonekana wengi wanataka Muungano udumu, sio bure kunakitu hapa na wakotayari hata kutumia :laser::laser::laser:
 
arigold hapo kwenye red umeuliza swali hata mimi najiuliza sana sana

Kwani mwaka jana zilifanyika wapi ? Nijuavyo huwa sherehe hizi hufanywa kwa zamu,Labda sema lingine
 
Last edited by a moderator:
Ili tujue Nyerere alikuwa nabii au la, inabidi Muungano uvunjike.
Lakini jivu halijaribishwi kwa kidole ili kujua moto upo.
 


Jamaa wamechoka

kiukweli ogopa sana mwananchi wa kawaida akichoka,kama tutaendelea kuwalazimisha yaweza tokea ya YEMEN,LIBYA,TUNISIA maana hawa watu wanafanana kwa kila kitu

wazanzibar wamechoka,mtu akichoka huwezi mlazimisha hata iwe kwa bunduki
 
Last edited by a moderator:
Bado wanaukubali Muungano. Wanajadili chini ya Picha ya Rais wa Jamhuri ya Muungano. Muungano wa Tanz Bara na Zanzibar ukishavunjika unaofuatia ni ule wa Pemba na Unguja kwa sababu Zanzibar ni muungano wa Pemba na Unguja na ndio maana kule kuna Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar(SMZ) na hakuna Serikali ya Pemba.
 
546035_309801469087490_100001729176510_807237_1743018056_n.jpg

Walewale wamefanana na yule wa Guantanamo.
 
Naombeni kama kuna anaejua faida za muungano aniambie kama hakuna hauna tija!
 
Katika hali isiyo ya kawaida huko Zanzibar watu wengi wamefurika na wamehudhuria mhadhara ya kupinga muungano uliofanyika viwanja vya Lumuba mjini Zanzibar na hivyo kupelekea mpaka Polisi nao kushiriki katika uchukuaji picha za video katika mhadhara huo.

Kwa kweli Wazenji wamevunja ukimya na kuiweka SMZ katk hali ngumu ya mchakato wa katiba mpya licha ya kuwa kuna polisi wengi waliopelekwa kutoka Tanganyika kwa hofu ya kutokea fujo.

Kiswahili katika heading yako ni kibovu sana. Kwa mfano neno 'baadhi' umelitumia visivyo
 
Hata Nami wananichanganya sana wanaojiita wazanzibari. Hawajui kuwa visiwa vya mafia mpaka Kilwa Kisiwani vilikuwa chini ya Sultani wa Zanzabar toka 1802 na wakajenga jengo ambalo linaitwa Gereza Fort? Wazanzibari chini ya Masultani wameathiri sana maaneo mengi kuanzia Pwani mpaka Unyamwezi na mpaka Congo. Watumwa waliotoka usukumani kwenda Bara? na Viumbe vilivyotoka ikiwa pamoja na watu baada ya kugawanyika kwa mabara. Mzainzibari kwangu ni jina Pana sana, ama anayeishi Zanzibar ama anatokana na asili ya huko lakini hayuko Zanzibar
 
Walewale wamefanana na yule wa Guantanamo.

Hawa jamaa nawaminia walivyo na msimamo na umoja katika kudai haki, subirini si muda mrefu wataanza kuvaa mabomu. Wazenji wamechoshwa na ndoa isiyokuwa na manufaa kwao nyie mwawalazimisha, mtakula maneno yangu punde.
 
Back
Top Bottom