Ni wakati wenu huu tambeni

Ni wakati wenu huu tambeni

Anaweza kuwa ni huyu!
Wanabodi, kwenye bandiko hili Ndugu, Jamaa na Marafiki, Njooni Tumtetee Makonda Dhidi ya Mapapa Wauza Unga Wanaomzushia... nilishauri

Hata baada ya kuteuliwa kuwa Mwenezi wa CCM, Paul Makonda bado anapigwa vita na wasiomtakia mema, wasioitakia mema CCM na wasio itakia mema Tanzania.

Japo Tanzania ni nchi ya vyama vingi, na kwa mujibu wa katiba ya Tanzania, mamlaka kuu ya nchi ni wananchi, kupitia katiba, serikali ya CCM ilifanya mabadiliko ya katiba kinyume cha katiba na kupoka ukuu wa mamlaka kuu ya wananchi, na kuikakabidhi kwa chama cha siasa, ambapo sasa mamlaka Kuu ya nchi ni chama tawala, CCM ndio imeshika hatamu kuongoza serikali, hivyo katika ukuu wa chama, CCM ndio kila kitu, hivyo Makonda kama msemaji wa CCM, kikao cha CCM kinaweza kumwagiza Rais wa JMT atekeleze jambo lolote lililoelekezwa kwenye ilani ya CCM, Katibu Mwenezi ndie msimamizi wa ilani ya CCM, ana mamlaka yote ya kumuamrisha hadi Rais wa JMT, atekeleze ilani ya uchaguzi ya CCM, hivyo Makonda yuko very right kumuamrisha Waziri Mkuu na kumpa ultimatum ya miezi 6 kumaliza migogoro yote ya ardhi ya nchi hii.

Na baada ya miezi 6, kama Waziri Mkuu, Majaliwa Kasim Majaliwa atashindwa kuitatua migogoro yote ya ardhi, atakuwa ni ameshindwa kazi, Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi, itakutana na kumuagiza Rais wa JMT, kumuondoa Waziri Mkuu, kwa kushindwa kazi na kumteua Waziri Mkuu mwingine mwenye uwezo.

Hata ikitokea Rais Samia ameshindwa kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM, chama kinaweza kumfuta uanachama na hivyo kupoteza urais!, hivyo Mwenezi wa CCM ni mtu mkubwa sana, kuliko serikali yote ya Tanzania, na hii ndio maana halisi ya Party Supremacy, CCM ndio imeshika hatamu za kuiongoza serikali ya Tanzania .

Hongera sana Mwenezi mpya wa CCM, Paul Makonda, kuiheshimisha CCM, endelea kutoa maagizo na ultimatum kwa viongozi wote kuhusiana na utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM, wewe ndiye msimamizi wa ilani ya CCM!.

Angalia ilani ya CCM imeelekeza nini kuhusu Bunge la JMT, toa maelekezo kwa Spika with ultimatums, Spika akishindwa kutekeleza Spika anaondolewa!, enzi za Spika Sitta, aliponea chupu chupu kuondolewa, kuna mtu mmoja very powerful ndani ya CCM aitwae "The King Maker" ndie alimuokoa Spika Sitta kwa kumpa maelekezo Mwenyekiti wa CCM, JK, na hii ndio salama yake!.

Makonda angalia ilani ya uchaguzi ya CCM inasema nini kuhusu mhimili wa Mahakama, toa maagizo with ultimatum kwa Jaji Mkuu atekeleze.

Angalia ilani ya uchaguzi inasema nini kuhusu majeshi, ulinzi na usalama, toa maelekezo with ultimatum kwa Amiri jeshi Mkuu na kwa Mkuu wa majeshi, IGP , etc.

Ila kwa nafasi ambazo sio za kichama kama Jaji Mkuu, Mkuu wa Majeshi, CAG, Mwenyekiti wa NEC, Msajili wa Vyama vya Siasa, Wakuu wa vyombo vya Ulinzi, Mwenyekiti wa Tume ya Utawala Bora na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma ambao ni wateule wa rais, Paul Makonda anaweza kuwapa maelekezo bila ultimatums kwasababu hawa chama hakiwezi kuwafanya chochote, na badala yake, chama kitampa maelekezo mamlaka yake ya uteuzi ambaye ni Rais wa JMT, awaondoe!.

Kiukweli ninamkubali sana Paul Makonda!, Tangu nilipoanza kumkubali Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam
He has never let me down!. Tena niliwahi kushauri Baada ya Magufuli, 2025 Makonda atatufaa sana, kwasababu ana uthubutu kuliko hata JPM!. Apunguze... ushauri huu still stands, kwasababu miaka hii 4 ya Mama ni kumalizia awamu ya Magufuli, awamu ya baada ya Magufuli inaanza 2025, ila Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke hivyo you never know with politics, everything is possible!.

Paul Makonda kanyaga mwendo, chapa kazi, kazi iendelee!.
Paskali.
P
 
Yes only if aliyepo atakuwa amekamilisha
  1. SGR nchi nzima
  2. Umeme wa Stiggler
  3. Tanzania ya viwanda
  4. Nchi ya uchumi wa gesi
  5. Nchi ya uchumi wa Kati
  6. Tanzania Kuwa a donor country
Kama kuna lolote Kati ya hayo halijakamilika, wananchi wazalendo wa Kweli wa nchi hi, tutaandamana mabarabarani kushinikiza katiba ibadilishwe, kile kipengele cha ukomo kiondolewe, huyu bwana aongezwe as much time as it takes kuikamilisha.

Huu mtindo wa taifa to spend millions mfano kwenye katiba, na kuachia katikati kwa matumaini anayefuatia atamalizia, kisha huyo anayefuata anasema sio agenda yake, it's not good at all. This time huyu tusimwache hadi akamilishe miradi mikubwa yake yote!.

https://www.jamiiforums.com/threads...-haja-kufanya-uchaguzi-wa-rais-2020.980346/[/
P.
Chawa mnaoamini katika mfumo mtu. Leo hii hata hamjui mshike lipi!
 
Nimewahi kusikia maneno kutoka kinywani Kwa Mzee wangu (Mkemia mkuu mstaafu)
Anasema Nyerere alikuwa na Udhaifu mmoja Wa kupendelea majina yale yale Kwa Kila kazi
Unasikia Yuko wapi Jakaya, utasikia John (yaan Malecela sisemi Magufuli)
Utasikia Samweli , Mara utasikia Butiku, au Warioba, na kipenzi chake saana alikuwa SALIM AHMED SALIMU
ila pamoja na kwamba aliwapendelea hakusita kuwakemea wanapofanya upuuzi

Ukaja wakati Wa Mwinyi akawaweka wote chini akaanza na Wa kwake

Ni wakati wao walitesa sana,

Wakati Wa Mkapa kuna kina Masilingi, Kina Zimbihile kina Kinyondo, kina Zombe, Kina Yona na Balali,

Wakati Wa Kikwete Kina Makamba, Kina Sadik hata Lukuvi wametamba

Awamu ya 5 ndio maajaabu kabisa imezungukwa na washamba sana

Leo hii Kina Makonda wanadhani wako juu ya sheria au ndio wenye nchi mpaka wanasahau mipaka ya kazi zao, ngoja wale mambo ndio wakati wao

Wakae wanajua mwaka 2025 kutakuwa na mwingine ambaye atakuwa na utaratibu wake

View: https://www.facebook.com/share/v/1EoTRBT5Dz/
 

Oktoba tunaniki, Samia 5 tena
20250610_072519.jpg
 
Back
Top Bottom