Ni wakati muafaka sasa Mifugo itozwe kodi. Msukuma au Mmasai anamiliki zaidi ya ng’ombe 1,000 na hachangii chochote! It is not fair

Kididimo

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
3,791
3,360
Hivi karibuni kumeibuka manung'uniko makubwa ya uonevu kwa wafanyabiashara kuhusu tozo kubwa za kodi.

Mishale na lawama wamekuwa wakitupiwa ndugu zetu wa TRA.

Lakini, ukichunguza kwa umakini utagundua tatizo la msingi haliko kwao.

Tatizo ni ubunifu usiotosheleza wa nchi yetu katika kubainisha vyanzo vya kodi.

Vyanzo vikubwa kama Mifugo, vimeachwa bila sababu.

Kwa hesabu ndogo tuu, mfano Wilaya kama Meatu ina takriban ya ngombe zaidi ya laki nne. Ukitoza kodi angalau 2,000/= kwa kichwa cha ngombe kwa mwaka utapata almost 800 million, bado mbuzi na wanyama wengine.

Hiki chanzo kingeweza kupunguza lengo la makusanyo ya Wilaya yaliyoelekezwa kwa wafanyabiashara tu.

Halikadhalika, Serikali hutumia gharama kubwa kutengeneza miundombinu ya mifugo. Ni kwa nini gharama hizo zisitokane na kodi ya mifugo,badala ya kutumia kodi za wafanyakazi na wafanyabiashara.


Ni maoni yangu kuwa sekta zote za kipato rasmi,zichangie kwa usawa maendeleo ya nchi yetu badala ya kuelekeza nguvu zote kwa kundi dogo.
 
Kelele za wangapi walipe Kodi zingepelekwa kwa Kodi zetu zinafanya nini, na je ni value for money..., makusanyo ya migodi, maliasili na watalii ? Itakuwa ni Fikra potofu / upeo mfupi iwapo tunashangilia mkulima aongezewe / apigwe kodi wakati huyo Bwana ndio anatulisha hivyo indirectly ni wewe, wewe pia utakayelipia..., Bidhaa kupanda bei....
 
Kodi ya mifugo isiyojuliana inapatikanaje?

Mifugo haina vaccines wala matibabu yoyote.

Serikali ingepata chanzo maridhawa cha kodi kama hawa wanyama kungekuwa na subsides kwenye pembejeo na chanjo za uhakika. Pia wawe na bima ndio kingekuwa chanzo maridhawa cha ilivyo kwenye kodi na bima za magari.

Usione vyaelea mkuu wamaasai mpaka wanaywesha gongo wanyama wao wanapougua, maana hata dawa ya magonjwa mengine wao hawazijui.

Lazima serikali ikitaka hiki kuwa chanzo cha mapato iwekeze. Imagine katika mipango miji (master plan) huwezi kuona mahali pametengwa kama mahali pa kufuga au malisho ya wanyama.

Sasa hawa wanyama wanakuwa attached na makazi ya binadamu ila serikali haiwatambui hata kwa makazi tu halafu ukiite chanzo cha mapato. Magonjwa, ukame na udhoofu unapowakumba wanaokufa mpaka unaogopa.
 
Kodi ya mifugo isiyojuliana inapatikanaje?

Mifugo haina vaccines wala matibabu yoyote....
Mkuu, unaweza kuwa sahihi pale utakapobainisha ni nini kitangulie kati ya kodi na chanjo. Tunatoza kodi ili tununue chanjo! Hiyo ni logical thinking na ambayo ndiyo hufuatwa na serikali kwa kodi zote. Ni sawa na kusema tunatoza kodi ili tujenge reli, barabara nk.
 
Hata walio na namakalio makubwa nao walipe kodi, yajayo yanafurahisha,na wa rangi nyeupe nawo walipe kodi.
Nilitegemea kwa jinsi uchumi unavyokuwa kwa kasi ya ajabu serikali itaanza kuwalipa wananchi wasio na kazi kwa mwezi.
 
Unataka kutuharibia wafugaji ? Tulikimbia kwenye maduka baada ya kuona kodi zimezidi na kuhamia kwenye kufuga ng'ombe wa kunenepesha kwa ajili ya kuuza! Na huku mnataka kutufuata tena?
 
Hivi karibuni kumeibuka manunguniko makubwa ya uonevu kwa wafanyabiashara kuhusu tozo kubwa za kodi.

Mishale na lawama wamekuwa wakitupiwa ndugu zetu wa TRA.
Lakini, ukichunguza kwa umakini utagundua tatizo la msingi haliko kwao.
Tatizo ni ubunifu usiotosheleza wa nchi yetu katika kubainisha vyanzo vya kodi.
Vyanzo vikubwa kama Mifugo, vimeachwa bila sababu.

Kwa hesabu ndogo tuu, mfano Wilaya kama Meatu ina takriban ya ngombe zaidi ya laki nne. Ukitoza kodi angalau 2,000/= kwa kichwa cha ngombe kwa mwaka utapata almost 800 million, bado mbuzi na wanyama wengine.

Hiki chanzo kingeweza kupunguza lengo la makusanyo ya Wilaya yaliyoelekezwa kwa wafanyabiashara tuu.

Halikadhalika, Serikali hutumia gharama kubwa kutengeneza miundombinu ya mifugo. Ni kwa nini gharama hizo zisitokane na kodi ya mifugo,badala ya kutumia kodi za wafanyakazi na wafanyabiashara.


Ni maoni yangu kuwa sekta zote za kipato rasmi,zichangie kwa usawa maendeleo ya nchi yetu badala ya kuelekeza nguvu zote kwa kundi dogo.
Mhesh Rais alikwishaelekeza TRA wawe wabunifu.
 
Back
Top Bottom