Ritz,
Asante kwa maoni yako. Hata hivyo umetaja ahadi nyingine ambazo zijawahi kuzitoa wakati wowote kwenye kampeni zangu popote. Sijawahi kuahidi machinga complex mbili, kwa sababu naamini kwenye uzalishaji na huduma zaidi ya uchuuji. Tandale haipo katika jimbo la Ubungo, ipo Jimbo la Kinondoni; hivyo ahadi uliyoitaja sijawahi kuitoa. Kuhusu maji, barabara na ajira; ahadi zangu zilikuwa tofauti na ulivyozieleza; kwa kuwa naelewa vizuri kuwa kazi ya mbunge ni kuwakilisha, kuisimamia serikali na kutunga sheria. Ahadi zangu wakati wa kampeni niliziandika kwa ajili ya rejea kwa sababu niliamini ni mkataba baina yangu na wapiga kura. Mara baada ya kuchaguliwa nilizirudia hapa:
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/91961-ujumbe-wa-mbunge-shukrani-twende-kazi.html wakati wa kuwashukuru ili kuunganisha nguvu ya umma katika utekelezaji na pia upatikane msingi wa kupima utekelezaji wa ahadi husika katika kipindi cha miaka mitano. Kwa mwaka huu wa kwanza nimekuwa na utaratibu wa mara kwa mara kutoa mrejesho wa masuala mahususi, unaweza kufanya rejea tu humu. Lakini kwa kuwa tunaelekea mwisho wa mwaka nitatoa pia taarifa nyingine ya ujumla; na pia nitaelekeza zitolewe taarifa za kata kwa kata. Nakutakia heri ya Xmas na mwaka mpya na tuendelee kushirikiana katika utumishi wa umma.
JJ