Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Jamani nyie semeni tu, si mmezoea kusema chochote, leteni vitu ila isije ikawa tayari mmeshanunuliwa na mafisadi, MUNGU ATAWALAAANI WOTE MLAO KWA KUTENGENEZA MAJUNGU!
 
Hivi kule kwa Samuel Sitta nako kuna ufisadi au kuko clean?

I mean kama kuna watu wanaiba mpaka vocha za bembejeo za wakulima wetu kweli ofisi ya Mheshimiwa 6 itakuwa safi?
 
GT

Badala ya kuandika ufisadi wa kwa bwana 6 unapiga dana dana vipi weka nondo basi tujue mbivu?
 
Mi nilifikiri umetuletea data kumbe unatuuliza sisi.GT nawe sometimes unavituko!
 
Mbatia amshambulia Spika Sitta
• Aorodhesha mlolongo wa tuhuma za ufisadi dhidi yake

na Betty Kangonga


amka2.gif

MWENYEKITI wa Chama cha NCCR- Mageuzi, James Mbatia, ameingia kwenye orodha ya viongozi wa kisiasa kutoka kambi ya upinzani walioamua kurusha mashambulizi dhidi ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta.
Mbatia aliwaeleza waandishi wa habari jana kuwa uamuzi wake wa kujitokeza sasa unasukumwa na kauli ya hivi karibuni ya Sitta ya kumshutumu Mwenyekiti wa Chama cha upinzani cha TLP, Augustine Mrema, kuwa miongoni mwa viongozi wa upinzani aliodai wamenunuliwa kwa kazi moja ya kukisafisha Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambacho spika huyo ni mwanachama wake.
Mwenyekiti huyo wa NCCR ambaye historia inaonyesha kuwa msimamo wake dhidi ya CCM umekuwa ukiibua maswali mengi, alieleza kushangazwa na hatua ya chama hicho tawala kukaa kimya hata baada ya Sitta kukituhumu kuwanunua viongozi wa upinzani.
Mbatia alisema hatua hiyo ya CCM kukaa kimya pasipo kukemea au kutoa kauli juu ya matamshi hayo ya spika wake ni ushahidi wa wazi kwamba kinakubaliana na kauli hizo.
Akimgeukia Sitta, kiongozi huyo wa juu wa NCCR- Mageuzi alieleza kushangazwa na hatua ya spika huyo kujipambanua kuwa mmoja wa wapambanaji dhidi ya vitendo vya ufisadi, wakati mwenendo wake wa sasa na wa kihistoria ukimtia katika kundi hilo hilo la viongozi wenye tuhuma za ufisadi ndani ya CCM.
“Sitta amejivika joho la kupambana na ufisadi, tunampongeza katika hili… lakini swali la kushangaza ambalo linakosesha majibu licha ya yeye mwenyewe kujenga imani kubwa kwa Watanzania kuwa ni mtu safi,” alisema Mbatia.
Pasipo kutoa ushahidi wowote wa wazi wa madai yake, Mbatia alimtuhumu Sitta kwa kile alichoeleza kuwa ni kuchota kiasi cha shilingi milioni 200 na kuzipeleka katika Jimbo lake la Urambo Mashariki.
Kama hiyo haitoshi, Mbatia alirejea tena kumtuhumu Sitta kwa kukubali kupangishiwa nyumba yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa mwezi, madai ambayo spika huyo na Ofisi ya Bunge kwa nyakati tofauti mwaka jana walipata kuyajibu.
Katika majibu yake mwaka jana, spika aliieleza Tanzania Daima kwamba uamuzi wa kupangishiwa nyumba hiyo ulikuwa ni wa Bunge na si wake, na kwamba ulitokana na maelekezo ya Rais Jakaya Kikwete.
Tangu Bunge na Sitta watoe majibu hayo ya kumhusisha Kikwete na uamuzi huo wa kupangishiwa nyumba ambayo spika huyo alisema inafanana na hadhi yake, aliyoilinganisha na ya waziri mkuu, hakuna mamlaka yoyote ya dola, ikiwamo Ikulu iliyopata kutoa matamshi ya kuyakana.
Mbatia katika mashambulizi yake mengine dhidi ya Sitta, alimtuhumu kwa kutumia mamlaka yake ya kuwa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) wakati wa Serikali ya Awamu ya Tatu kuomba msamaha wa kodi kwa ajili ya makampuni hewa, ikiwamo ile ya Richmond.
“Wakati akiwa TIC kati ya mwaka 1996 mpaka 2005, alikuwa mstari wa mbele kuombea makampuni hewa ya nje msamaha wa kodi kutoka Hazina, ikiwemo Kampuni maarufu ya kufua na kuzalisha umeme ya Richmond na mchakato huo ulihusisha kampuni yake binafsi ya kisheria,” alisema Mbatia.
Ingawa Sitta hakupatikana jana kujibu tuhuma kuhusu utendaji wake akiwa TIC, hususan suala zima la kutoa misamaha ya kodi kwa kampuni hewa za uwekezaji, taratibu na sheria za uwekezaji zinaonyesha kuwa mwenye mamlaka hayo kisheria ni Waziri wa Fedha.
Kuhusu Richmond, mwaka jana Sitta mwenyewe alipata kulieleza gazeti hili kukumbuka kufanya mawasiliano na Mkurugenzi Mkuu wa Richmond wakati akiwa TIC, na akasisitiza kwamba maombi yao ya kutaka kuwekeza katika mradi mmoja yaligonga mwamba, baada ya serikali kuthibitisha kuwa kampuni hiyo haikuwa na uwezo.
Ukiacha tuhuma hizo, Mbatia katika mkutano wake wa waandishi jana alimwelekezea Sitta tuhuma za kuhusika na ufujaji ambao ulilifanya Bunge linunue samani za shilingi milioni 300 kwa ajili ya ofisi yake ndogo jijini Dar es Salaam.
“Kamati ya Hesabu za Serikali inayoongozwa na John Cheyo ililielezea taifa kuwa ofisi ya Sitta imefuja zaidi ya sh mil. 300 za kununulia samani kwa ajili ya Ofisi Ndogo za Bunge, huku akidaiwa masurufu ya sh milioni 100,” alisema Mbatia.
Katika majibu yake ya mwaka jana kuhusu tuhuma hizo pia, Sitta alipata kukaririwa akisema, yeye alikuwa hana mamlaka ya kuchagua aina ya samani anazopaswa kuwekewa na badala yake mwenye wajibu na jukumu hilo kisheria ni Katibu wa Bunge. Akihitimisha mashambulizi yake dhidi ya Sitta jana, Mbatia alisema mlolongo wa tuhuma hizo za kimaadili ni ushahidi kwamba hakuna kiongozi yeyote ndani ya CCM anayeweza kusimama na kutamba kwamba yeye ni safi. Kutokana na hali hiyo, Mbatia alimgeukia Rais Kikwete ambaye naye ni mwana CCM na kumuomba atenge muda wake wa kazi ili siku moja aweze kukaa meza moja na viongozi wa vyama vya upinzani ili kujadili kuhusu hali na mwenendo wa taifa.

mY COMMENTS: KAZI NI NZURI SANA , ILA CHAMA CHA MAFISADI HAKINA WA KUCHUKUWA HATUA. ALIKUWA NYERERE NA SOKOINE TU, MBAYA ZAIDI WAMETUTOKA.rip BOTH
 
Ninapenda sana tactics za rostam... amegundua wapinzani wana njaa sana na hiki ni kipindi cha mavuno na anawatumia vizuri sana siku hizi

bado yeye kupenyeza rupia CHADEMA sasa, and i am hopeful hiyo haitatokea
 
"RAIS ATENGE MUDA WA SIKU MOJA KUKUTANA NA VIONGOZI WA UPINZANi...."viongozi wenye mtazamo na fikira kama za mbatia ni upuuzi na kupoteza muda mchache alonao raisi wetu msafiri. Mbatia hana sera nilindani akutane na raisi ili wamulize nini utekeleziji wa maazimio ya bunge na kwanini mjadala wa richmond ulifungwa na bunge. Mbatia damu changa nilitegemea awe chachu ya mijadala mizito kwa ustawi wa nchi kumbe yee anataka huruma ya sisiem? Lini amekuwa mshauri wa ccm na nani alimpatia wadhifa KIJANA MZIMA HOVYOO......
 
inakuhusu nini sasa?kama alimaliza au hakumaliza shule inahusikaje hapa?off point
Kama shule ilimshinda ndio ataweza siasa? siajabu atashindwa hata kumalizia huo uenyekiti ahamie kwa rostam kutafuta pesa

Kigogo trust me, kutomaliza shule ni dalili tu ya kukosa reliability kwa chochote
 
"RAIS ATENGE MUDA WA SIKU MOJA KUKUTANA NA VIONGOZI WA UPINZANi...."viongozi wenye mtazamo na fikira kama za mbatia ni upuuzi na kupoteza muda mchache alonao raisi wetu msafiri. Mbatia hana sera nilindani akutane na raisi ili wamulize nini utekeleziji wa maazimio ya bunge na kwanini mjadala wa richmond ulifungwa na bunge. Mbatia damu changa nilitegemea awe chachu ya mijadala mizito kwa ustawi wa nchi kumbe yee anataka huruma ya sisiem? Lini amekuwa mshauri wa ccm na nani alimpatia wadhifa KIJANA MZIMA HOVYOO......

ukimsema mtu, umenunuliwa...ukiongea kitu umenunuliwa...hivi kwanini msiangalie mada alizosema instead mnamjadili mwenyewe, kama amemaliza shule hajamaliza swali ni kwamba ana point au hana..KAMA HANA POINT ELEZEA KWANINI HANA, sio mnajiandikia tu kwa kuwa you can,wana JF wengi humu ndani mnatuangusha......
 
Wakati tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu Octoba mwaka huu, tutashuhudia mengi na huu ni mwanzo tu.........Ooooh God Heaven
 
ukimsema mtu, umenunuliwa...ukiongea kitu umenunuliwa...hivi kwanini msiangalie mada alizosema instead mnamjadili mwenyewe, kama amemaliza shule hajamaliza swali ni kwamba ana point au hana..KAMA HANA POINT ELEZEA KWANINI HANA, sio mnajiandikia tu kwa kuwa you can,wana JF wengi humu ndani mnatuangusha......



Ndo maana wakti mwingene huwa napenda kuwaa mtazamaji.
Watu humu JF hawajdili maada wanajadili muhusika na jinsi gani anawakera.
Wanasema mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.
Jamaa ana hoja lakini watu wamemgeukia yeye badala ya alichoongea.
 
Siku za karibuni limeibuka kundi la watu ambao wako tayari kufa au kufanya lolote lile kumtetea Sita, wamevuka mipaka kiasi cha kutojadili maada au hoja bali kumtetea tu! ninachofahamu ni kuwa

Sita+Mwakyembe+Lowasa+Rostam+Kikwete+Warioba+Kilango+Makamba+Ngeleja+Masha+sofia Simba+Mkapa=CCM.

watu mtakaojitokeza kumtetea yoyote katika hao na kuponda wengine nadhani ni kutokutumia akili ya kawaida kabisa ya kuzaliwa!

However, inapendeza zaidi kuwatetea baadhi ya watu mliowapa majina ya wapiganaji kama wewe ni mwana CCM, yaani mmoja wao, ila inahuzunisha beyond words ukimkuta mtu mwenye akili timamu anatoka povu kumtetea Sita ana kina mwakyembe ambao ni wasaliti na wezi kabisa wa tafa hili ,jana leo, na hata kesho, never even mention akina EL na AR,

CCM lao moja! kipindi hiki cha uchaguzi ndio mtawaona kwa matendo yao! waoi Kilango? wapi Mwakyembe? kelele ziko wapi? wanaofadhili hizo chaguzi zenu ni akina nani?
 
Tatizo la wadanganyika wengi ni kufuata mkumbo kwa kila mada itakayoanzishwa,humu jamvini wapo vilaza wengi sana kazi yao ni kuponda wenzao tuu bila ya kutumia brain.Wengine wamevuka mipaka hadi kufikia kuitwa 'dogma' kwa vile wanakubali kila wanachoambiwa kuwa ni kweli bila kuuliza maswali.Nani hasiyejua uchafu uliopo ndani ya CCM hadi mkamsifie 6 eti ni msafi!Usafi utatoka wapi wakati nguo aliyojifunga inanuka uchafu?Jamani kuweni wakweli tuu kwamba kinyesi kikitumbukia katika chakula japo kidogo tuu lazima hicho chakula kitaharamishwa,sasa uchafu uliopo CCM na huyo 6 akiwemo humo basi muelewe ni haramu tena mikosi vilevile ni nuksi kumsifia pia ujinga kumtetea katika mazingira kama hayo.
Narudia tena 6 ni mchafu wa kupindukia hawezi kukemea maovu wakati kwake ndio yanayotendeka.Ni upuuzi kusema eti rais ameamua apangishiwe hekaru na thamani za mamilioni wakati wapiga kura wake wanashinda kwa kula mafenesi na chikichi,aibu kubwa kabisa.Tena amevuka mipaka kwa kusema ALM amenunuliwa na CCM kuikampenia wakati yeye ni seneta wa hiyo CCM inamaana naye ametumia nafasi yake kumnunua huyo ALM kutekeleza uchafu huo,sasa usafi wake upo wapi?
Jamani tumieni akili kusifia watu na si kutumia yale yatokayo juu ya mdomo na chini ya macho!
Nasisitiza spika 6 ni fisadi,mbinasfi,mchonganishi na mlewa madaraka,ukitaka ndio hivyo usipotaka ndio hivyo,ukichukia chukia kwani sitashindwa kuendesha Shangingi langu kwa ajili yako!
 
Mwenyekiti huyo wa NCCR ambaye historia inaonyesha kuwa msimamo wake dhidi ya CCM umekuwa ukiibua maswali mengi,....

Pasipo kutoa ushahidi wowote wa wazi wa madai yake.............

Katika majibu yake mwaka jana, spika aliieleza Tanzania Daima kwamba uamuzi wa kupangishiwa nyumba hiyo ulikuwa ni wa Bunge na si wake, na kwamba ulitokana na maelekezo ya Rais Jakaya Kikwete

Tangu Bunge na Sitta watoe majibu hayo ya kumhusisha Kikwete na uamuzi huo wa kupangishiwa nyumba ambayo spika huyo alisema inafanana na hadhi yake, aliyoilinganisha na ya waziri mkuu, hakuna mamlaka yoyote ya dola, ikiwamo Ikulu iliyopata kutoa matamshi ya kuyakana

Kuhusu Richmond, mwaka jana Sitta mwenyewe alipata kulieleza gazeti hili kukumbuka kufanya mawasiliano na Mkurugenzi Mkuu wa Richmond wakati akiwa TIC, na akasisitiza kwamba maombi yao ya kutaka kuwekeza katika mradi mmoja yaligonga mwamba, baada ya serikali kuthibitisha kuwa kampuni hiyo haikuwa na uwezo.

Katika majibu yake ya mwaka jana kuhusu tuhuma hizo pia, Sitta alipata kukaririwa akisema, yeye alikuwa hana mamlaka ya kuchagua aina ya samani anazopaswa kuwekewa na badala yake mwenye wajibu na jukumu hilo kisheria ni Katibu wa Bunge


Kwa trend ya majadiliano inavyokwenda humu ndani ni rahisi kwa mwingine kuamini kuwa Tanzania Daima wamenunuliwa na Six, manake wamekuwa wakimjibia mwanzo mwisho...
 
Back
Top Bottom