Nyani Ngabu, huwa naheshimu sana hoja zako nyingi. Ninaomba unitie moyo niendelee kuheshimu kwa kuonyesha ukweli.
CHADEMA, ni chama cha upinzani hakina dola wala hakiongozi serikali. Report ya Mwakyembe imebainisha kwamba Lowasa ni fisadi. Tena kwa taarifa zaidi kwamb kuna mengine yamehifadhiwa kwa usalama wa nchi. Wewe ulitaka CHADEMA waseme kwamba Lowasa ni safi, kabla hajasafishwa mahakama??
Watanzania wakategemea kwamba mafisadi hao waliotajwa Lowasa, na wenzake wengi tu watapelekwa mahakamani ili
wahukumiwe kwa mujibu wa sheria, lakini kimya kikaendelea. Siyo kwa Lowasa bali kwa watuhumiwa wote wa ufisadi hadi leo tunaona keusi na kekundu.
Huo ukweli mwingi unaoujua wewe, kama ndivyo ilivyo, kwa nini hapelekwi mahakamani? Akiwa ccm alikuwa ni ajali za kisiasa, lakini baada ya kuamua kuondoka kwa hiyari yake, sasa kawa fisadi? Nidyo tuseme ni fisadi, kwa nini hapelekwi mahakamani?
Vipi mafisadi wa ESCROW, Lugumi na wengine wengi wanaofugwa ccm na serikali yake. Mnasubiri waondoke ndipo muanze kuimba wimbo wa ufisadi wao? Adhabu ya fisadi ni kutokuondoka Ccm? Hukumu ya fisadi ni kuzomewa? Kwa sheria zipi Nyangi ngabu?
Unaposema walichemsha, nani aliyechemsha? CHDEMA waliosema ni fisadi kwa sababu ya taarifa ya tume ya Mwakyembe?
Kamati ya Mwakyembe iliyosema Lowasa ni fisadi? Ccm kumsafisha kwamba ilikuwa ni ajali ya kisiasa? Srikali kukosa ujasiri wa kumpeleka mahakani au ccm kuanz akuimba wimbo wa ufisadi kipumbavu bila kurejea taarifa ya Mwakyembe na kuaishi kusema CHDEMA walisema?
Naomba uwe serious.
Ok. Lowasa ni fisadi, kwa nini Serikali haimpeleki mahakani? Pengine tuanzie hapa!