Ni tuhuma tu Lowassa kumbe si Fisadi!!

Ni tuhuma tu Lowassa kumbe si Fisadi!!

Huwa nawasikia watu waliochafuliwa majina wakitoa muda wa majina yao kusafishwa.....la watawaburuta wanaowachafua mahakamani

Sijui kwa nini Lowassa hawapeleki mahakamani wanaomchafua
Tena aanze kuwapeleka Mahakamani hao CDM waliomchafua na kumuita fisadi papa asiyesafishika nk
 
Ni kweli mkuu CDM wamebomoka kisiasa baada ya kumpokea lowasa LAKINI CCM inaendelea kuporomoka kwa kasi ya ajabu baada ya kushindwa kuwawajibisha na kuwafikisha mahakamani mafisadi 10 ambao walitajwa na cdm na bado wapo ccm mpaka leo hii....fanya utafiti na utatambua hilo mkuu
Usisahau na Mgombea wa UKAWA alitajwa kwenye list of Shame!!
 
wewe ni mmoja wa wale waliofaidika na ujio wa lowasa chadema. unachojaribu kutetea hata kichaa hawezi kukuelewa. mafisadi wanasafishwa na vyombo vya dola lakini sio watu tu wanajihukulia jukumu la kuwasafisha watu kwa intetest zao na sio za nchi. ni hatari kwa chama kama hiki kupewa uongozi wa nchi.hizi ni zama mpya jamani. lakini najua mpaka leo hamjaelewa lengo la lowasa kuja chadema. in short ni kuua upinzani.... angalia ajenda zote zenye nguvu zimezikwa. na hizo ndio zenye nguvu popote duniani. fanya research. usiwe mvivu kufikiri. chama sasa hakina mwelekeo, wameshaona hawana ajenda sasa ndio wanazuka na vitu vya ajabu ajabu, eti shikilia UKUTA. ujinga mtupu. huwezi kupambana na Magufuli kwa staili hiyo. mngekuwa na akili mngefuata ushauri wa Dr Kitila Mkumbo. alisema siasa za uanaharakati kwa uongozi wa Magufuli hazina mashiko. kwa sababu ni mtendaji wa ukweli na anatumikia wananchi kama wanavyotaka. sssa unataka nini zaidi ya hapo. siasa uchwara hizi za UKUTA hazitatufikisha popote. sana sana tutakuja jilaumu tena baada ya miaka 100 kuwa tumefikaje wakati tukiwa bado maskini. ni kwa sababu tunapotezeana muda kwa mambo ambayo si ya msingi kwa ujenzi wa uchumi wetu kitaifa na mtu mmoja mmoja. wajameni tuwe waangalifu
na wewe ni mmoja wa team membe!....hasira yako kwa lowasa ni pale wafuasi wake walipokataa kumuunga mkono membe....jadili hoja na uache matusi yako.
 
wewe ni mmoja wa wale waliofaidika na ujio wa lowasa chadema. unachojaribu kutetea hata kichaa hawezi kukuelewa. mafisadi wanasafishwa na vyombo vya dola lakini sio watu tu wanajihukulia jukumu la kuwasafisha watu kwa intetest zao na sio za nchi. ni hatari kwa chama kama hiki kupewa uongozi wa nchi.hizi ni zama mpya jamani. lakini najua mpaka leo hamjaelewa lengo la lowasa kuja chadema. in short ni kuua upinzani.... angalia ajenda zote zenye nguvu zimezikwa. na hizo ndio zenye nguvu popote duniani. fanya research. usiwe mvivu kufikiri. chama sasa hakina mwelekeo, wameshaona hawana ajenda sasa ndio wanazuka na vitu vya ajabu ajabu, eti shikilia UKUTA. ujinga mtupu. huwezi kupambana na Magufuli kwa staili hiyo. mngekuwa na akili mngefuata ushauri wa Dr Kitila Mkumbo. alisema siasa za uanaharakati kwa uongozi wa Magufuli hazina mashiko. kwa sababu ni mtendaji wa ukweli na anatumikia wananchi kama wanavyotaka. sssa unataka nini zaidi ya hapo. siasa uchwara hizi za UKUTA hazitatufikisha popote. sana sana tutakuja jilaumu tena baada ya miaka 100 kuwa tumefikaje wakati tukiwa bado maskini. ni kwa sababu tunapotezeana muda kwa mambo ambayo si ya msingi kwa ujenzi wa uchumi wetu kitaifa na mtu mmoja mmoja. wajameni tuwe waangalifu
wewe ulifaidika na fedha za membe mkuu
 
Kila siku tunaambiwa ni kwa nini CHADEMA walikubali kumpokea Lowassa mtu waliyekuwa wanamtuhumu kwa ufisadi wakati akiwa CCM. Hoja hii ya kukera inayoshabikiwa na kundi la watu ya aina ya Mzee Mwanakijiji na Nyani Ngabu siyo tu ni dhaifu bali pia inakera.

Siasa si nasaba ya kiasili (Gene) kwamba ukizaliwa CCM basi ukoo wako milele utakuwa ni CCM ama CHADEMA, bali ni mchezo ambao kanuni yake kubwa ni kufanikisha Agenda inayokubaliwa na chama husika cha siasa. Lowassa alipokuwa CCM alikuwa ni kihimili cha mfumo wa chama hicho, kina Kikwete na wenzake walikuwa anamtumia Lowassa kuunganisha nguvu za wanaopingana ndani ya chama hicho.

Mtu mwenye nguvu kama hiyo ndani ya chama cha siasa unatarajia vipi wapinzani wake wasimshambulie. Halafu CHADEMA walikuwa wanatumia taarifa za Kamati ya Mwakyembe kumshambulia Lowassa na wala si nje ya taarifa hizo. Kusema kwamba kwa kuwa CHADEMA walisema Lowassa ni fisadi basi anakuwa fisadi ni jambo la kustaajabisha kabisa.

Hoja kubwa ya CHADEMA wakati ule na hata sasa ni kuwa kama kina Mwakyembe waliona Lowassa kaitia hasara nchi kwenye Kandarasi ya kufua umeme iliyohusisha Kampuni ya Richmond, kwa nini asifikishwe mahakamani? Kina Mnyika na Lema kwa kutumia mbinu za kisiasa walikuwa wanasema kuwa inakuwaje wezi wa kuku wako magerezani wakati Lowassa yupo mtaani anadunda?

Swali la Msingi kama ufisadi wa Lowassa ulitokana na CHADEMA kusema ni fisadi wao CCM kama chama msimamo wao wakati ule ulikuwaje, walikuwa wanaona kwamba Lowassa ni fisadi ama si fisadi? Ajabu kubwa kuliko yote ni ukiwauliza wana CCM ufisadi wa Lowassa ni upi wanaishia kusema waliosema Lowassa ni fisadi ni CHADEMA!!

Mpaka sasa Lowassa anatuhumiwa tu kwamba ni Fisadi lakini hakuna hoja au ushahidi mahsusi kuonesha kwamba yeye kweli ni Fisadi. Na inawezekana akawa "fisadi" kwa kutumia mbinu na sheria kama za Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki na kina siye ndiyo tutakuwa Fethulla Gulen wa zama hizo!!

Hoja kwamba CHADEMA ndiyo "walisema" kuwa Lowassa ni fisadi ni za uwezo wa chini sana katika kujenga hoja. Tunataka mtu aje atuambie yeye anaposema kuwa Lowassa ni fisadi basi na atuambie kuwa ufisadi wake ni upi. Tumechoka kuishi kwa uvumi!!
mkuu umekaa kimya vipi hoja zimeisha. hivi wewe mkuu unatoka mkoa gani
 
Mnaanzisha nyimbo na kuwaaminisha watu mpaka wanaanza kuziimba halafu baadaye mnaanza tena kuwauliza wamejifunzia wapi na kwa nini wanaziimba?

Kwa nini mnawafanya kama wajinga wale Watanzania wanaoimba nyimbo mlizozianzisha?

Kwanza kama mngekuwa mna ubinadamu, mngemuomba msamaha huyo Lowassa badala ya kuanza kuwauliza maswali wale wanaimba nyimbo zenu.
Kwahiyo ccm wamepokea wimbo wa CDM bila kujiuliza nao wanaimba hivyo hivyo bila kuchanganya na akili zao ehh
1471703198884.jpg
1471703229062.jpg
hawa nao ni katika wimbo ule ule au mnapelekana chaka??? Au ndio kuiga bila mipaka kama hivi???
1471703400199.jpg
 
Allen Kilewella. Kama wewe ni verified user na hiyo picha ni yako basi hii ni aibu kubwa kwako na ukoo mzima wa akina Kilewellas. Mzee mzima unajishusha hadhi namna hii? Ulistaafu mapema na sasa unabangaiza kwenye siasa ama?

Anyway - nashauri kwanza uanze na Kubenea na Mwanahalisi yenu ambayo for more than ten years mlikuwa mkimshambulia Lowassa na kumwita fisadi Non stop. Ninyi mlikuwa na ushahidi?

Look, mtaruka ruka sana na Lowassa ambaye Kubenea alishasema hasafishiki lakini mwisho wa siku mtakiri tu kuwa kumkaribisha kuwa mgombea wenu wa uraisi ndilo lilikuwa kosa kubwa kabisa la kimkakati na ambalo upinzani utachukua miaka mingi sana ku-recover. Sasa mnapuyanga tu bila falsafa jumuishi ya kueleweka utafikiri walevi. Na kuna siku mtamkumbuka Slaa. Lowassa was/is na ataendelea kuwa liability hata mjitahidi kumsafisha namna gani!
 
Ulistaafu mapema na sasa unabangaiza kwenye siasa ama?

Anyway - nashauri kwanza uanze na Kubenea na Mwanahalisi yenu ambayo for more than ten years mlikuwa mkimshambulia Lowassa na kumwita fisadi Non stop. Ninyi mlikuwa na ushahidi?
Kwanza kwa kawaida taasisi ina tabia ya kukua. Nashangaa sasa nyie mnatufundisha ubora wa Slaa wakati ni sisi tuliyemchukua baada ya nyie kuona hafai hata kugombea ubunge, leo mnatufundisha kuamini kuwa ni yeye pekee aliyekuwa anafaa kugombea urais kupitia CHADEMA mwaka 2015. Lakini kufaa kwa Slaa kunakuja baada ya nyie kutuambia kwamba hafai kugombea Urais mwaka 2010 kwa kutokuwa na maadili hasa kwa suala la Kumwacha Rose Kamili na ndoa yake na Josephine Mushumbusi pamoja na kuacha Upadri? Walioshinikiza ile kesi mahakamani siyo nyie watu wa Lumbumba?

Pili mimi sipo hapa kuwakilisha ukoo wa kina Kilewela na wala sijawahi kuishi kwa kutegemea siasa na katika maisha yangu yote sijawahi kuwa mfia chama, viongozi wako wananijua vizuri zaidi kuliko wewe na tunaheshimiana. Hoja hapa kwa mawazo yako na kwa utashi ulio nao wewe binafasi jenga hoja kama Lowassa ni fisadi au siyo fisadi. Huo ujinga wa kusema kwamba Lowassa asafishiki kwa kuwa tu Kubenea alisema hivyo, ukome. Kwani Kubenea ni mungu wa akili zetu kwamba akiumbacho yeye ndiyo huwa hivyo milele? Mkamuulize yeye aliposema Lowassa asafishiki alikuwa anamaanisha nini na kwa kutumia vigezo gani?
 
Kwanza kwa kawaida taasisi ina tabia ya kukua. Nashangaa sasa nyie mnatufundisha ubora wa Slaa wakati ni sisi tuliyemchukua baada ya nyie kuona hafai hata kugombea ubunge, leo mnatufundisha kuamini kuwa ni yeye pekee aliyekuwa anafaa kugombea urais kupitia CHADEMA mwaka 2015. Lakini kufaa kwa Slaa kunakuja baada ya nyie kutuambia kwamba hafai kugombea Urais mwaka 2010 kwa kutokuwa na maadili hasa kwa suala la Kumwacha Rose Kamili na ndoa yake na Josephine Mushumbusi pamoja na kuacha Upadri? Walioshinikiza ile kesi mahakamani siyo nyie watu wa Lumbumba?

Pili mimi sipo hapa kuwakilisha ukoo wa kina Kilewela na wala sijawahi kuishi kwa kutegemea siasa na katika maisha yangu yote sijawahi kuwa mfia chama, viongozi wako wananijua vizuri zaidi kuliko wewe na tunaheshimiana. Hoja hapa kwa mawazo yako na kwa utashi ulio nao wewe binafasi jenga hoja kama Lowassa ni fisadi au siyo fisadi. Huo ujinga wa kusema kwamba Lowassa asafishiki kwa kuwa tu Kubenea alisema hivyo, ukome. Kwani Kubenea ni mungu wa akili zetu kwamba akiumbacho yeye ndiyo huwa hivyo milele? Mkamuulize yeye aliposema Lowassa asafishiki alikuwa anamaanisha nini na kwa kutumia vigezo gani?
Copy post yangu yote kisha uijibu usimege vipande na kupoteza mantiki yote.

Endeleeni kumsafisha Lowassa na pengine siku moja atasafishika na kuwa mweupe kama theluji. Kila la heri ndugu.

...Historia ya vyama vya upinzani itakapokuja kuandikwa kitendo cha CHADEMA kupiga about turn na kumsimamisha mtu ambaye alikuwa target ya mashambulizi yenu na MKAAMINI kuwa watu watawaamini kitakumbukwa kama kitendo pekee kilichojaa ubinafsi, ukengeufu wa dhamira, tamaa na mikakati potofu kilichowahi kufanyika na ambacho kiliudidimiza upinzani na kuurudisha nyuma kwa makumi ya miaka! Hii Kubenea Konstraktion daima itawaandama na mimi naomba iwaandame tu kwa sababu hakuna namna!

Kubenea Kostraktion...!!!
FB_IMG_1465258293203.jpg
 
Finally, Lowassa wins! Very interesting. Siku zote nimekuwa nikiamini kuwa Lowassa ni mmoja wa washirika wakuu wa ufisadi ndani ya CCM aliyegeukwa na wenzake, kutoswa na kubandikwa nembo ya "fisadi mkuu" ili kutuzuga wananchi kuwa "problem solved"; sasa chama kimebaki na watu safi pekee!

Kinachojitokeza sasa pia ni kuwa CCM iliwazuga CHADEMA kwanza kuhusu ufisadi wa Lowassa hivyo CHADEMA wakadaka chambo kwa papara zao na "kuangua kilio kikubwa kuliko mwenye msiba wake" kwamba Lowassa ni fisadi mkuu. Baadaye wakajikuta hawana ushahidi wowote wa maana bali wameingizwa chaka na watoto wa mjini kuwarahisishia kazi ya kumzima hasimu wao tishio.

Kibaya zaidi, CHADEMA wakagundua kuwa Lowassa ni mtaji mzito kisiasa; wakajikuta wakiuvutia upande wao. Sasa tumebakia kushuhudia timu pinzani zikiendelea Kupasiana mpira kila moja ikiepuka kufunga goli la kuthibitisha ufisadi wa Lowassa na kudai mwenzake ndiye mwenye data. Haya, sie tunaendelea kugeuka kulia, kushoto kushuhudia "ping-pong" isiyo na mwisho.

Sijui wenye serikali na vyombo vya dola pamoja na mahakama ya mafisadi wanajisikiaje kuishia kucheza ping-pong kuhusu "fisadi mkuu" na wenye mtaji wa kauli pekee. Ila Mh. Lowassa atakuwa anavuta tabasamu pana (from ear to ear) anapozidi kushuhudia mahasimu wake wa nyakati tofautitofauti wakijikanyagakanyaga mbele yake kama misukule. Sikutarajia kushuhudia kituko cha aina hii kwenye suala hili.
 
Una maanisha siku zote chadema wanaongopa wanapomtuhumu mtu? Mnajua hoja zenu mzitumie vizuri karne hii. We si kiongozi wa chama, unaleta yasiyokuhusu na huku unaharibu. Napata wasiwasi na sisi tunaojiita wapinzani kama hatujui tunachoandika.
Kila siku tunaambiwa ni kwa nini CHADEMA walikubali kumpokea Lowassa mtu waliyekuwa wanamtuhumu kwa ufisadi wakati akiwa CCM. Hoja hii ya kukera inayoshabikiwa na kundi la watu ya aina ya Mzee Mwanakijiji na Nyani Ngabu siyo tu ni dhaifu bali pia inakera.

Siasa si nasaba ya kiasili (Gene) kwamba ukizaliwa CCM basi ukoo wako milele utakuwa ni CCM ama CHADEMA, bali ni mchezo ambao kanuni yake kubwa ni kufanikisha Agenda inayokubaliwa na chama husika cha siasa. Lowassa alipokuwa CCM alikuwa ni kihimili cha mfumo wa chama hicho, kina Kikwete na wenzake walikuwa anamtumia Lowassa kuunganisha nguvu za wanaopingana ndani ya chama hicho.

Mtu mwenye nguvu kama hiyo ndani ya chama cha siasa unatarajia vipi wapinzani wake wasimshambulie. Halafu CHADEMA walikuwa wanatumia taarifa za Kamati ya Mwakyembe kumshambulia Lowassa na wala si nje ya taarifa hizo. Kusema kwamba kwa kuwa CHADEMA walisema Lowassa ni fisadi basi anakuwa fisadi ni jambo la kustaajabisha kabisa.

Hoja kubwa ya CHADEMA wakati ule na hata sasa ni kuwa kama kina Mwakyembe waliona Lowassa kaitia hasara nchi kwenye Kandarasi ya kufua umeme iliyohusisha Kampuni ya Richmond, kwa nini asifikishwe mahakamani? Kina Mnyika na Lema kwa kutumia mbinu za kisiasa walikuwa wanasema kuwa inakuwaje wezi wa kuku wako magerezani wakati Lowassa yupo mtaani anadunda?

Swali la Msingi kama ufisadi wa Lowassa ulitokana na CHADEMA kusema ni fisadi wao CCM kama chama msimamo wao wakati ule ulikuwaje, walikuwa wanaona kwamba Lowassa ni fisadi ama si fisadi? Ajabu kubwa kuliko yote ni ukiwauliza wana CCM ufisadi wa Lowassa ni upi wanaishia kusema waliosema Lowassa ni fisadi ni CHADEMA!!

Mpaka sasa Lowassa anatuhumiwa tu kwamba ni Fisadi lakini hakuna hoja au ushahidi mahsusi kuonesha kwamba yeye kweli ni Fisadi. Na inawezekana akawa "fisadi" kwa kutumia mbinu na sheria kama za Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki na kina siye ndiyo tutakuwa Fethulla Gulen wa zama hizo!!

Hoja kwamba CHADEMA ndiyo "walisema" kuwa Lowassa ni fisadi ni za uwezo wa chini sana katika kujenga hoja. Tunataka mtu aje atuambie yeye anaposema kuwa Lowassa ni fisadi basi na atuambie kuwa ufisadi wake ni upi. Tumechoka kuishi kwa uvumi!!
 
Una maanisha siku zote chadema wanaongopa wanapomtuhumu mtu? Mnajua hoja zenu mzitumie vizuri karne hii. We si kiongozi wa chama, unaleta yasiyokuhusu na huku unaharibu. Napata wasiwasi na sisi tunaojiita wapinzani kama hatujui tunachoandika.
Kwanza mimi si mpinzani bali ni mtanzania ninayeamini katika siasa za CHADEMA. Jambo la pili tuhuma kimantiki halitakiwi liwe ni jambo la kudumu. Lowassa katuhumiwa sana na sasa tunataka ifike mwisho kwa yeye kufikishwa mahakamani ijulikane kama kweli ni Fisadi au la!!
 
Ulisema hivyo wakati CHADEMA wanasema yeye ni fisadi?
Na pengine inakera kwa sababu ina ukweli mwingi ndani yake.
Ukweli mara nyingi hukera wale wasiopenda kuusikia.



Kwani wakati CHADEMA wanamtuhumu kuwa fisadi walitoa ithibati gani juu ya hayo madai yao?


Wakati CHADEMA wanasema kwamba Lowasa ni fisadi uliwakosoa na kuwaambia kwamba hoja zao ni za watu wenye uwezo wa chini sana katika kujenga hoja? Au ndo ulipaza sauti kuimba mapambio ya Lowasa ni fisadi?



Nyie wakati mnasema ni fisadi mlituambia ufisadi wake ni upi? Na kama mlituambia, ikawaje tena mwaka jana mkabadili gia angani?
Ni fisadi akiwa CCM lakini akiwa kwenu ni msafi?
Nyie kubalini tu kuwa mlichemsha.
Mtoa hoja anataka ww pimbi unapokuja kutuaminisha kuwa Lowassa ni fisadi basi Toa ushahidi halisi na siyo kwamba chadema walisema. Kama hauna ushahidi na takukuru juu ya tuhuma za Richmond ilisema hakukuwa na harufu yoyote ya wizi,basi wewe pimbi na mafisiemu yenzako ndo mafisadi ...... over
 
Ulisema hivyo wakati CHADEMA wanasema yeye ni fisadi?
Na pengine inakera kwa sababu ina ukweli mwingi ndani yake.
Ukweli mara nyingi hukera wale wasiopenda kuusikia.



Kwani wakati CHADEMA wanamtuhumu kuwa fisadi walitoa ithibati gani juu ya hayo madai yao?


Wakati CHADEMA wanasema kwamba Lowasa ni fisadi uliwakosoa na kuwaambia kwamba hoja zao ni za watu wenye uwezo wa chini sana katika kujenga hoja? Au ndo ulipaza sauti kuimba mapambio ya Lowasa ni fisadi?



Nyie wakati mnasema ni fisadi mlituambia ufisadi wake ni upi? Na kama mlituambia, ikawaje tena mwaka jana mkabadili gia angani?
Ni fisadi akiwa CCM lakini akiwa kwenu ni msafi?
Nyie kubalini tu kuwa mlichemsha.
Nauliza na mimi jee angeshinda kuwa mgombea wa uraisi kwa ccm je chadema wangesema unayoyasema leo?au mlikuwa mmepanga makabrasha kibao kuthibitisha ufisadi wake na mambo yalipobadilika akaja kwenu na kukinunua chama kwa mabilioni mmeyaficha maushaidi?leo hii lowassa nakuambia akirudi ccm yatatokea mengi sana ndani ya chadema maana sijui mtatoa ushaidi wa ufisad au mtakuwa mabubu,lakini nyie hmna aibu mnaweza kutoa ushaidi na kutudanganya tena kuwa mmeokota faili la ushaidi,nyie ni wanafik wakubwa hamjui mnavyovitaka,tena nashangaa kama mpaka leo mnaunga mkono swala hilo,ccm walisoma alama za nyakati kwa kutomchagua maana walijua sera yenu ni ufisad,hebu niambie unapanga una muoa jane awe mkeo na adui yako anapanga kumuoa susan na harusi yenu ni tarehe moja,mara kabla ya harusi suzan ameachwa kwa umalaya ambao wewe umekuwa ukisema na kutangaza kote susan hafai ni malaya wewe unamuacha mchumba wako jane unamchukua susan???grow up,reason and know what is best for you!!!!!only you,knows better what you deserve
 
Kwanza mimi si mpinzani bali ni mtanzania ninayeamini katika siasa za CHADEMA. Jambo la pili tuhuma kimantiki halitakiwi liwe ni jambo la kudumu. Lowassa katuhumiwa sana na sasa tunataka ifike mwisho kwa yeye kufikishwa mahakamani ijulikane kama kweli ni Fisadi au la!!
Hana haja ya kupelekwa mahakamani sisi tulikubali chadema walipotuambia maana tuna waamini sana hao chadema kwa kusema ukweli!!wao walimtuhumu je walimuomba msamaha hadharani?je walimpeleka mahakama ipi ikathibitika si fisadi?wao walimtuhumu na waowao wakamhukumu na waowao wakamsafisha hahahahahah
 
Drifter nashukuru kwa kuelezea kwa vizuri sana mazonge tuliyo nayo kuhusu Lowassa. Tatizo unaposema "Chama" unamaanisha viongozi, na kwa kweli Lowassa mahasimu wake ndani ya CCM ndiyo waliokuwa wanatoa "Siri" kwa viongozi wa CHADEMA wa wakati huo kuhusu Lowassa.Nao viongozi wa CHADEMA wakiongozwa na DK. Slaa ambaye bila ya shaka alikuwa anaona kabisa kama mwaka 2015 atashindana na Lowassa kwenye uchaguzi Mkuu wote wakiwa wagombea Urais, hali itakuwa ngumu kwake. Kwa ivo kiurahisi akaamua kumalizana naye mapema kwa kuanika hadharani "Siri" alizokuwa anapewa na watu wake ndani ya Serikali.

Kwa kina Slaa wakati ule waliamini kwamba Kikwete ni dhaifu bali nguvu yake inatokana na ushirika wake na Lowassa, hasa ikisemwa kwamba Lowassa ndiye alikuwa anaelekeza nini kifanyike ili "wanamtandao" waendelee kuwa madarakani. Kina Karamagi, Rostam Azizi, Samuel Sitta, Emmanuel Nchimbi, Sofia simba na wengineo wengi ilionekana wamegandamanishwa kwenye uhusiano wao na Lowassa.

Kosa kubwa walilolifanya CHADEMA ni kujiona wako salama kumshambulia watakavyo Lowassa kwa kuwa walikuwa nje ya mfumo wa CCM hivyo ilikuwa ni vigumu kwao kudhibitiwa na wanamtandao. Mwisho wa siku kuja kutaharuki kina Slaa ambao walikuwa hawaweki hakiba ya Maneno, wakakumbwa na mtihani mkubwa sana katika maisha yao ya kisiasa kwa yule waliyekuwa wanamshambuliwa kwa kutumia "Ushahidi" toka serikalini na CCM, alipokuwa anataka kujiunga nao!

Hata ingekuwa ni mimi Slaa nisingeweza kuwa na Ujasiri kukaa kwenye chama kimoja na mtu niliyekuwa namtuhumu kuwa ni fisadi na wananchi wakaamini. Slaa alioongoza mashambulizi dhidi ya Lowassa na hadi akaaminiwa na umma,lakini kiuhalisia mashambulizi hayo aliyokuwa anafanya kwa kauli mbiu ya "Vita haina macho" yamegharimu hadhi yake ya kisiasa na hatima ya maisha yake!!
 
kedekede Lowassa kanunua CHADEMA kwa bilioni ngapi, na hizo fedha zilikuwa Benki au zilikuwa wapi. Kwenye hiyo biashara serikali ilichukua kodi yake au ilikuwaje. Walioanzisha hiyo Propaganda ya Kijinga wenzio wameshaiacha kitambo!!
 
kedekede Lowassa kanunua CHADEMA kwa bilioni ngapi, na hizo fedha zilikuwa Benki au zilikuwa wapi. Kwenye hiyo biashara serikali ilichukua kodi yake au ilikuwaje. Walioanzisha hiyo Propaganda ya Kijinga wenzio wameshaiacha kitambo!!
Allen kwa nini uwe na mgombea wako wa miakamingi then all over a sudden uchukue mtuhumiwa wako mwenyewe utake kumpa madaraka makubwa kabisa ya nchi?ili iweje?
 
Back
Top Bottom