Ni tuhuma tu Lowassa kumbe si Fisadi!!

Ni tuhuma tu Lowassa kumbe si Fisadi!!

Kila siku tunaambiwa ni kwa nini CHADEMA walikubali kumpokea Lowassa mtu waliyekuwa wanamtuhumu kwa ufisadi wakati akiwa CCM. Hoja hii ya kukera inayoshabikiwa na kundi la watu ya aina ya Mzee Mwanakijiji na Nyani Ngabu siyo tu ni dhaifu bali pia inakera.

Siasa si nasaba ya kiasili (Gene) kwamba ukizaliwa CCM basi ukoo wako milele utakuwa ni CCM ama CHADEMA, bali ni mchezo ambao kanuni yake kubwa ni kufanikisha Agenda inayokubaliwa na chama husika cha siasa. Lowassa alipokuwa CCM alikuwa ni kihimili cha mfumo wa chama hicho, kina Kikwete na wenzake walikuwa anamtumia Lowassa kuunganisha nguvu za wanaopingana ndani ya chama hicho.

Mtu mwenye nguvu kama hiyo ndani ya chama cha siasa unatarajia vipi wapinzani wake wasimshambulie. Halafu CHADEMA walikuwa wanatumia taarifa za Kamati ya Mwakyembe kumshambulia Lowassa na wala si nje ya taarifa hizo. Kusema kwamba kwa kuwa CHADEMA walisema Lowassa ni fisadi basi anakuwa fisadi ni jambo la kustaajabisha kabisa.

Hoja kubwa ya CHADEMA wakati ule na hata sasa ni kuwa kama kina Mwakyembe waliona Lowassa kaitia hasara nchi kwenye Kandarasi ya kufua umeme iliyohusisha Kampuni ya Richmond, kwa nini asifikishwe mahakamani? Kina Mnyika na Lema kwa kutumia mbinu za kisiasa walikuwa wanasema kuwa inakuwaje wezi wa kuku wako magerezani wakati Lowassa yupo mtaani anadunda?

Swali la Msingi kama ufisadi wa Lowassa ulitokana na CHADEMA kusema ni fisadi wao CCM kama chama msimamo wao wakati ule ulikuwaje, walikuwa wanaona kwamba Lowassa ni fisadi ama si fisadi? Ajabu kubwa kuliko yote ni ukiwauliza wana CCM ufisadi wa Lowassa ni upi wanaishia kusema waliosema Lowassa ni fisadi ni CHADEMA!!

Mpaka sasa Lowassa anatuhumiwa tu kwamba ni Fisadi lakini hakuna hoja au ushahidi mahsusi kuonesha kwamba yeye kweli ni Fisadi. Na inawezekana akawa "fisadi" kwa kutumia mbinu na sheria kama za Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki na kina siye ndiyo tutakuwa Fethulla Gulen wa zama hizo!!

Hoja kwamba CHADEMA ndiyo "walisema" kuwa Lowassa ni fisadi ni za uwezo wa chini sana katika kujenga hoja. Tunataka mtu aje atuambie yeye anaposema kuwa Lowassa ni fisadi basi na atuambie kuwa ufisadi wake ni upi. Tumechoka kuishi kwa uvumi!!
Hizi hoja hazijengi vyama vyenu mnabomoa. Tafuteni hoja nyingine na hizi zenye utata mziache kabisa maana mtu mwenye kuwaza kama jana wewe ulisema huyu mtu hafai na leo unabadilika unadhani unaweza kuaminika katika lipi ambalo ukisema sasa uonekane mkweli.

Hapo ni mawili ama yeye awe msafi na uonekane wewe uliyekuwa ukisema ulikuwa unadanganya na ndio siasa na ukiasema lolote watu wapuuze waseme ni siasa au ionekane wewe ni mkweli na ulilokuwa ukisema ni ukweli na wewe huwa husemi uongo na hivyo ukisema lolote leo uaminike.

Lakini yote hayo hakuna lenye unafuu maana kila utakalochagua utakumbana na swali la ziada.
 
Mahakama ndo yenye wajibu wa kuthibitisha?

Kanuni ya wapi hiyo?
Alaa! Kwani kama ni fisadi si anapelekwa mahakamani. CHADEMA hawakuwa kwenye nafasi ya kumpeleka Lowassa mahakamani wakati ule na wala hawana nafasi hiyo sasa!! Najua hoja yako ni kwamba mtoa tuhuma ndiye anayetakiwa kuthibitisha tuhuma zake pasiko shaka. Lakini waliokuwa madarakani wakati ule na ambao ndiyo wako madarakani sasa msimamo wao kuhusu Richmond ulikuwaje na ukoje?
 
"kusema kwamba kwa kuwa CHADEMA walisema lowasa ni fisadi na kweli amekuwa fisadi ni jambo linalostaajabisha sana" KUMBE CHADEMA HAMWAMINIKI NA TUSIWAAMINI KWA MATAMKO YENU?
 
Alaa! Kwani kama ni fisadi si anapelekwa mahakamani. CHADEMA hawakuwa kwenye nafasi ya kumpeleka Lowassa mahakamani wakati ule na wala hawana nafasi hiyo sasa!! Najua hoja yako ni kwamba mtoa tuhuma ndiye anayetakiwa kuthibitisha tuhuma zake pasiko shaka. Lakini waliokuwa madarakani wakati ule na ambao ndiyo wako madarakani sasa msimamo wao kuhusu Richmond ulikuwaje na ukoje?

Unataka kuhamisha magoli wewe.

CHADEMA waliposema Lowasa ni fisadi walitoa ithibati gani?

Na mwaka jana ikawaje akawa si fisadi tena ilhali miaka nenda rudi mmeimba kuwa yeye ni fisadi?
 
Hazitofautiani sana na wazee wa Ufipa.
1471549145810.jpg
1471549164685.jpg
1471549195207.jpg
1471549266133.jpg
1471549294218.jpg
 
Kwahiyo CHADEMA ikimuita mtu fisadi haipaswi kuchukuliwa siriaz???
Kwahiyo CHADEMA wakimshambulia kiongozi wa CCM maana yake ni wamempenda na wanataka ajiunge nao?
Hii inamaanisha nini kuhusu mashambulizi dhidi ya Tulia?
Inamaanisha nini kuhusu kumuita Magufuli dikteta?
 
Nasubir mahakama ya mafisadi watakao pelekwa mahakaman kwa tuhuma za ufisad na wakipata hukumu nitadirik kuwaita mafisad bt kwa sasa ss sote n watii
 
Mtoa mada hebu twende polepole..leo nikikwambia huyu mtu ni mwizi na uthibitisho ninao kisha kesho nikakuambia yule mwizi wa jana sio mwizi sababu hakuna uthibitisho wa wizi wake,utanichukuliaje!?..muda mwingine tuweke mahaba pembeni,huu mtindo wa kuamin kila unachoambiwa bila kufikiri kwa utashi wako ndio maana wengine wanatuita nyumbu.
 
Inakera wakilala wakiamka wanakuja na hoja kwamba CHADEMA "ilishindwa" mwaka jana kwa kuwa ilimsimamisha Lowassa. Chama kilichoongeza Madiwani, wabunge na kura za Rais kinakuwaje kimeshindwa. Malengo ya CHADEMA kwenye uchaguzi wa mwaka 2015 wao CCM waliyajua?
Kwahiyo unataka kuaminisha watu kwamba CDM walipoingia kwenye kinyang'anyiro hawakuwa na mpango wa kushinda??
Kuna ambaye hushindana pasi na lengo la kushinda??
Seriously??? [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Hizi hoja hazijengi vyama vyenu mnabomoa. Tafuteni hoja nyingine na hizi zenye utata mziache kabisa maana mtu mwenye kuwaza kama jana wewe ulisema huyu mtu hafai na leo unabadilika unadhani unaweza kuaminika katika lipi ambalo ukisema sasa uonekane mkweli.

Hapo ni mawili ama yeye awe msafi na uonekane wewe uliyekuwa ukisema ulikuwa unadanganya na ndio siasa na ukiasema lolote watu wapuuze waseme ni siasa au ionekane wewe ni mkweli na ulilokuwa ukisema ni ukweli na wewe huwa husemi uongo na hivyo ukisema lolote leo uaminike.

Lakini yote hayo hakuna lenye unafuu maana kila utakalochagua utakumbana na swali la ziada.
Kweli CCM ni viumbe wa ajabu!!! Nasikitika sana kutawaliwa na watu kama hawa
 
ndo tatizo la vijana kufuata mkumbo wa wanasiasa, leo hii wanasiasa wanamwita chenge ni fisadi kijana unafuata mkumbo unalibebelea bango "CHENGE NI FISAD" 2020 haohao wanampitisha chenge kugombea urais kupitia chama chao, kijana kwa kuwa umeshikiwa akiri na wewe unageuza bango na kusema "MWENYE USHAHID APELEKE MAHAKAMANI" tujitambue watz, wanasiasa si wakuaminika. tusiwekeze akiri na fikra zetu kwa wanasiasa.
 
Mnaanzisha nyimbo na kuwaaminisha watu mpaka wanaanza kuziimba halafu baadaye mnaanza tena kuwauliza wamejifunzia wapi na kwa nini wanaziimba?

Kwa nini mnawafanya kama wajinga wale Watanzania wanaoimba nyimbo mlizozianzisha?

Kwanza kama mngekuwa mna ubinadamu, mngemuomba msamaha huyo Lowassa badala ya kuanza kuwauliza maswali wale wanaimba nyimbo zenu.
 
Ulisema hivyo wakati CHADEMA wanasema yeye ni fisadi?

Na pengine inakera kwa sababu ina ukweli mwingi ndani yake.

Ukweli mara nyingi hukera wale wasiopenda kuusikia.



Kwani wakati CHADEMA wanamtuhumu kuwa fisadi walitoa ithibati gani juu ya hayo madai yao?



Wakati CHADEMA wanasema kwamba Lowasa ni fisadi uliwakosoa na kuwaambia kwamba hoja zao ni za watu wenye uwezo wa chini sana katika kujenga hoja? Au ndo ulipaza sauti kuimba mapambio ya Lowasa ni fisadi?



Nyie wakati mnasema ni fisadi mlituambia ufisadi wake ni upi? Na kama mlituambia, ikawaje tena mwaka jana mkabadili gia angani?

Ni fisadi akiwa CCM lakini akiwa kwenu ni msafi?

Nyie kubalini tu kuwa mlichemsha.
Mkuu nyani ngabu iko hivi,Ni kweli kabisa kuwa CDM walimsema lowasa kuwa ni fisadi akiwa ccm.Lakini cdm hawakumtaja lowasa peke yake kuwa ndiye fisadi.Walikuwa wengi tu,ambapo wengine bado ni viongozi wa ccm mpaka sasa.Lakini wakati cdm wanawataja mafisadi hao,CCM na vijana wao hawakutoa neno lolote lile,"walikaa kimya".
Swali liko hivi; Je,kama ccm wanafahamu na kuamini kuwa lowasa ni fisadi kwa mujibu wa maenezo yaliyofanywa cdm,Kwa nini ccm hawaamini na kuwatangaza wale wailiotajwa na cdm kuwa nao ni mafisadi kama wanavyo mtangaza lowasa?.Kwa nn ccm haisemi au kuwambia wananchi kuwa"'flani na flani walitajwa na cdm so hawa nao ni mafisadi kama lowasa.?.Kama ccm inaamini kuwa mafisadi waliotajwa na cdm ni sahihi,kwa nn isiwangaze hadharani kama wanavyo fanya kwa lowasa?
 
Mbona hii nchi kila mtu ni fisadi tu....Wengi hamjui maana ya UFISADI ni nini hasa wapinzani na chama tawala...siku mkijua mtakaa kimya...waacheni Kikwete na Lowassa wale bata kwakuwa wanajua Siasa...nyie mnaigiza.
 
Mkuu nyani ngabu iko hivi,Ni kweli kabisa kuwa CDM walimsema lowasa kuwa ni fisadi akiwa ccm.Lakini cdm hawakumtaja lowasa peke yake kuwa ndiye fisadi.Walikuwa wengi tu,ambapo wengine bado ni viongozi wa ccm mpaka sasa.Lakini wakati cdm wanawataja mafisadi hao,CCM na vijana wao hawakutoa neno lolote lile,"walikaa kimya".
Swali liko hivi; Je,kama ccm wanafahamu na kuamini kuwa lowasa ni fisadi kwa mujibu wa maenezo yaliyofanywa cdm,Kwa nini ccm hawaamini na kuwatangaza wale wailiotajwa na cdm kuwa nao ni mafisadi kama wanavyo mtangaza lowasa?.Kwa nn ccm haisemi au kuwambia wananchi kuwa"'flani na flani walitajwa na cdm so hawa nao ni mafisadi kama lowasa.?.Kama ccm inaamini kuwa mafisadi waliotajwa na cdm ni sahihi,kwa nn isiwangaze hadharani kama wanavyo fanya kwa lowasa?

Sasa kama na ni kweli kabisa kuwa CHADEMA walimsema Lowasa kuwa ni fisadi, iweje waje kubadili gia agani na kumteua mtu waliyesema ni fisadi kugombea urais kupitia chama chao?

Watu waamini lipi sasa? CHADEMA ile au CHADEMA hii?

Mbowe na wenzake walitenda kosa lisiloteteeka hata kidogo.
 
Unajua huo ndio ushaidi wa kiwango cha unafiki kilivyokuwa kikubwa kwa hao wajomba zetu. Kama kweli huyo mzee ni fisadi kwa nini asifikishwe kortini lama kina kitilya masamaki nk?
 
Sasa kama na ni kweli kabisa kuwa CHADEMA walimsema Lowasa kuwa ni fisadi, iweje waje kubadili gia agani na kumteua mtu waliyesema ni fisadi kugombea urais kupitia chama chao?

Watu waamini lipi sasa? CHADEMA ile au CHADEMA hii?

Mbowe na wenzake walitenda kosa lisiloteteeka hata kidogo.
Mkuu kumbuka kuwa cdm ile ndo iliwataja mafisadi hao lowasa akiwa miongoni mwa hao mafisadi na siyo cdm hii.Wakati huo ccm ilikaa kimya na hawakusema kuwa hao waliotajwa na cdm ni mafisadi kweli.CDM Hii ya sasa wamempokea lowasa na wanasema lowasa si fisadi huku ccm wakihubiri kuwa lowasa ni fisadi huku ccm ikitumia ushahidi wa cdm ile?!.SWALI langu ni hiv;"'Kwa nini ccm isitumie ushahidi wa ile cdm kuwatangaza wale mafisadi waliotangazwa na cdm ile?
 
Back
Top Bottom