Ni rekodi gani iliyompandisha chati Kikwete kiasi kile mwaka 2005?

Naombeni tukumbushane sababu moja iliyofanya Kikwete kuaminiwa na kupewa ualali wa kuongoza Watanyania 2005.
Habari za kiintelijensia zilidokeza kuwa yeye na kundi lake wangehamia upinzani maana walijua hawapewi nchi. Na kwamba wangehakikisha wanatumia nguvu zote kuivuruga magamba. Wazee wa magamba kina Mwinyi, Mkapa, Kawawa, wakakesha usiku kucha mjini Dodoma wakijaribu kufanya maamuzi magumu zaidi. Tena yalikuwa maamuzi magumu mno kwa Mkapa. Ikalazimika huyu bo.gu.s apewe nchi japo kwa shingo upande
 
chaguo la mungu

Walio wengi tuliamini Mkuu huyu,angesimama na kuamua kuludisha heshima ya walio wengi ya kutokusikilizwa haswa kwenye ustawi wa Maisha bora kwa kila Mtanzania.

Tuliamini kuwa huyu uenda akawa msikivu na mwenye kutenda haraka kujibu majibu ya Watanzani walio wengi ambao maisha yao yalikuwa tayari mikononi mwa mafisaidi,ukizingatia kuwa alikuwa ni mtu aliyependa kujichanganya na watu wa rika na kada tofauti tofauti.

Watu waliamini kuwa angevaa viatu vya Nyerere,kama uwezo wa kumwambia rafiki yako aliyekosea kuwa HAPANA na IKAMAANISHA HIVYO HAPANA.NA UKAITETEA HAPANA HIYO MPAKA HATUA YA MWISHO KWA MANUFAA YA WENGI.

Tuliamini kuwa HATA KUWA NA LELEMAMA dhidi ya wale wanao hujumu Taifa dhidi ya rushwa na mikataba mibovu.Tuliamini atakuwa ndio tiba ya gonjwa baya la dhuluma dhidi ya watanzania kutoweka.HATA INGEMBIDI KUWA DIKTETA KAMA KAGAME KWA MASLAHI YA WENGI.WENGI TUNGEKUWA NYUMA YAKE DAIMA.Kama wananchi wa Rwanda walivyo nyuma ya Kagame pamoja na wanayoitakia Rwanda mabaya kusema ni Dikteta.

Tulijua Ataleta Neema kwa kila Mtanzania kufurahi kuwa kifua mbele kwa kuwa Mtanzania kwa kuzaliwa kwenye Nchi ya Maziwa na Asali [Madini na Maliasili za Ajabu Duniani].

Tulijua atatuvusha kutoka kwenye dalaja la umaskini wa Watanzania walio wengi,pasipo kujali vigezo vya Benki ya dunia bali kwa kuangalia Mazingira yetu wenyewe.Na hivyo kutufanya Taifa lililoendelea Kusini mwa Jangwa la Sahala kwa kipindi cha Miaka Kumi tu.

Tulijua Elimu,Afya na Uongozi ulio bora ungeimarika na kuwa na matazamio ya kusonga mbele kama Taifa la wamoja,na sio taifa lenye watu wenye fikra ya kutengana kama Tanzania bara na Tanzania visiwani.

Matumaini mengi sna,ambayo yangetimia tu,kama NIA ya dhati ndani ya mioyo ya TIMU ya tuliyemchagua INGEKUWA NA DHAMILA INAYO MWOGOPA MUNGU.

Sijui kama tumechelewa au la ?labda mnisaidie
 
nadhani ni ile dhana iliyoonekana jengeka ndani ya ccm ya kuchaguana maraisi wagombea kwa dhana ya UDINI badala ya SIFA za watu. kwamba zamu hii mkristo na zamu hii muislamu.
 
Sura ndo ilikua kigezo kikubwa,
+
lile tabasamu ndo kina mama na kina dada walibaki hoi.
 
Na kwa mwaka 2010 ni zile ahadi zake zisizo na idadi bila kujali kwamba zinatekelezeka ama vipi
 
Naombeni tukumbushane sababu moja iliyofanya Kikwete kuaminiwa na kupewa ualali wa kuongoza Watanyania 2005.
USANII maneno yaliyotoka mazuri yasiyo na uzingatiaji! kama vile: Ninafahamu matatizo ya watz, nitambana na UFISADI, nitairejelea mikataba ya madini upya! ili ilete faida kwa MTZ. Ninawafahamu wauza unga.
Tulinunuliwa kwa KAULI ZA KISANII PITY!!!!!!!
 
"If you want to conquer people, tell them what they want to hear." - Wahenga

Kikwete knew this...
 
Tuliamini atakua waziri mzuri sana wa mambo ya nje! Kama tunavyoona sasa hivi kila kukicha yuko nje ya nchi.
 
Tuliamini atakua waziri mzuri sana wa mambo ya nje! Kama tunavyoona sasa hivi kila kukicha yuko nje ya nchi.
Kwa hilo wala hajatuangusha kwa kweli. Na ile ndege iliyonunuliwa wakati tunakula nyasi inafanya kazi yake vilivyo!
 
Utabiri wa Marhemu Sheikh Yahya Hussein alishasema angekuwa rais tupende tuisipende. Si unajua hili taifa linaongozwa kwa kufuata mambo ya utabiri na upigaji ramli.
 
Hotuba ya kwanza ya JK bungeni 2005 ilikuwa ya mtu mwenye upeo mkubwa wa kuleta mabadiliko makubwa - tatizo aliitelekeza ile hotuba na kwenda kinyume na dhamira yake iliyokuwa imesheheni katika hotuba ile. Hakuwa bold kuiweka katika matendo - sababu Mungu anajua!!. Mwenye nakala aimwage hapa tafadhali.
 
Mkuu Paweda asalam aleykum! nataka bendera za CDM ndogo zile nikaning'inize kijijini kwangu kwenye kibanda changu nilichojenga, na vile kiko along the road basi kila anaepita awe anaona alama ya mabadiliko inapepea. vp ntapataje? next week naenda kupumzika kidogo mjini hali ya hewa imechafuliwa mno na moshi wa jeneretas. Tafadhali.
 
ilikuwani kumalizia ngwe za kukesha angani na ndege kama popo, huku mramba akitusifu kwa kula nyasi
 
Back
Top Bottom