Ni rekodi gani iliyompandisha chati Kikwete kiasi kile mwaka 2005?

Ni sifa zipi ambazo watanzania tuliziona kwa muheshimiwa Kikwete nakupelekea tukamchagua kwa kura lukuki wanaohijua historia yake kiuongozi ebu nisaidieni au tulimchagua kwa staili bendera ufata upepo.
 
Ni sifa zipi ambazo watanzania tuliziona kwa muheshimiwa kikwete nakupelekea tukamchagua kwa kura lukuki.wanaohijua historia yake kiuongozi ebu nisaidieni.au tulimchagua kwa staili bendera ufata upepo.
Labda wewe ulimchagua; ninachojua mimi alitangazwa na tume ya uchaguzi hizo kura kama alipata hutakuja kuziona mahali popote.

Kiuongozi hakuna kitu; maana Monduli walikataa kumpa kamisheni ya uafisa kwa saqbabu hakukidhi viwango labda ingekuwa sasa lukuvi afanye "standarsation".

Ila usisahau hii nchi ni ya amani na utulivu haturuhusiwi kuhoji cho chote.
 
Am happy sikumpigia kura, sababu sikuona chochote ndani yake.



Kama tu Membe na mvi.
 
Uongo mbaya nilimpa kura yangu 2005; najuta, natubu na nawaomba radhi waTz kwani kwa kushirikiana na mafala wenzangu tulimpa nchi Dhaifu (mwongo, mzururaji, muuza sura, mwizi, anaangukaanguka (mgonjwa?), hana maamuzi)
Naahidi sitadanganywa tena maishani mwangu na mafisadi waliompaisha mwanzo mwisho Dhaifu 2005 kwa hela za wizi (EPA) - EL, RA, Abdulrahman Kinena etc
Mbwa ukimjua jina hakusumbui..
 
Labda wewe ulimchagua; ninachojua mimi alitangazwa na tume ya uchaguzi hizo kura kama alipata hutakuja kuziona mahali popote.

Kiuongozi hakuna kitu; maana Monduli walikataa kumpa kamisheni ya uafisa kwa saqbabu hakukidhi viwango labda ingekuwa sasa lukuvi afanye "standarsation".

Ila usisahau hii nchi ni ya amani na utulivu haturuhusiwi kuhoji cho chote.
me nachojua uadilifu wake aliiba ubwabwa KAMBI YA RUVU,NA AFANDE UBWABWA ALIMUONA
 
Ni sifa zipi ambazo watanzania tuliziona kwa muheshimiwa Kikwete nakupelekea tukamchagua kwa kura lukuki wanaohijua historia yake kiuongozi ebu nisaidieni au tulimchagua kwa staili bendera ufata upepo.

Wengi walipiga kura kwa ushabiki tu bila kujua wanayemchagua ana sifa zipi na hasa za kiuongozi.
Na kwa mshangao mkubwa naona baadhi ya watanzania wanaelekea kurudia kosa hilo hilo la kuweka maisha yao rehani tena kwa miaka mingine mitano au kumi endapo Edward Lowassa atateuliwa na chama chake kugombea urais 2015. Hiyu jamaa amekua serikalini miaka nenda rudi lakini ni kitu gani ambacho amefanya ambayo inaweza kuwafanya watanzania wamuamini na kumchagua? Isije ikawa majuto kama wanavyojuta waliomchagua JK.

Naamini watanzania hawakotayari tena kupoteza muda kusubiri kuona wenzao wa mataifa mengine yakiendelea wao wakiendelea kuupa ufisadi nafasi ya kutamalaki.
 
Ninachomushukuru Mungu wangu nikuonyesha mapema kwamba huyu bwana hafai. sikuvutiwa tangu anatangaza nia. kama angepitishwa Mwandosya angepata kura yangu.

Kura yangu hakuipata na hatoipata.
 
[font=&quot]"aibu iwe juu ya viongozi na wafuasi wote wa ccm, wawe siku zote ni watu kupata aibu kwa kila jambo na wakose kibali machoni pa mungu na watz na watu wote waseme amen"[/font]
 
Nadhani swali alilouliza Kamanda hapo juu ni la msingi. Na tukiweza kulijibu ili swali basi hatutarudia kosa kama hilo huko mbeleni. Kamanda Mchapaji, viongozi wanaosifiwa na hawana accomplishment yeyote ya msingi, zaidi ya kufukuza wachawi - kina January Makamba, wako wengi na tusipokuwa makini tutapata Kikwete mwingine. Sasa nirudi kwenye swali lako, Kikwete alifanya kampeni kubwa ya kununua media yote na kuyazika maovu yake. Ila waliofanya naye kazi walijua ya kuwa tulikuwa tunauziwa mbuzi kwenye gunia. Leo hii tuna watu kama kina mama Migiro ambao wameshindwa kuongoza UN na mbays zaidi ameshindwa kusaidia hata wanawake wenzake hapa nyumbani alipokuwa keenye hiyo nafasi. Leo naye anataka kuwa rais?
 
Mimi sijawahi kumchagua JK na wala sijawahi hata kufikiria kumpa Jakaya kura yangu kwa sababu toka mwanzo nilimjua kuwa ni mnafiki na siyo mtu safi. Wakati akiwa waziri wa madini na nishati, aliwanyang'anya watanzania waliokuwa wanamiliki leseni za utafiti wa madini maeneo ya Nyakagwe, Geita na kisha akaipa kampuni ya kigeni. Baada ya muda mfupi, yeye akapewa hisa na ile kampuni bila ya kulipa chochote. Toka wakati huo nilijua kuwa huyu Bwana siyo mtu mwenye sifa za uongozi.

Watu hawafahamu, lakini ukweli ni kuwa mikataba ya mwanzo ya madini kati ya serikali ya Tanzania na makampuni yanayochimba dhahabu ilitiwa saini na huyu Bwana akiwa Waziri. Leo, kwa kujua kuwa watanzania siyo wafuatiliaji, na yeye anajifanya kutoridhishwa nayo.

Moyo wangu ni mweupe sana japo tunateseka wote, maana sikushiriki hata mara moja kumweka Jk madarakani. Niliwaeleza sana wafanyakazi wenzangu kuwa huyu Bwana hana uwezo, hana dhamira, siyo mtu safi;anachokitaka yeye ni prestige ya kuwa Rais, wenzangu hawakunielewa. Leo kila mmoja nikimkumbusha, kila mmoja anajutia.

Leo asubuhi alikuja nyumbani kwangu ustadhi mmoja, mzee wa hekima na mpole sana, na balozi wa nyumba kumi (CCM). Analalamika kweli. Kwa maneno yake alisema, 'huyu bwana (JK) ni balaa kubwa, hatujawahi kushuhudia ugumu wa maisha kama hiki kipindi chake. Kama tungejua aheri tusingeweka hata ukomo wa utawala wa miaka 10 kwa urais maana Mkapa angekuwa ametufikisha mahali pazuri. Huyu Bwana anaua watanzania wengi hasa huko vijijini. Watu hawana hata nauli ya kuweza kufika hospitalini wanapougua'. Akatolea mfano jinsi yeye ambavyo kuna wakati amewahi kuahirisha kwenda kupiga sindano wakati anaumwa kwa sababu siku nyingine alikosa nauli. Nilimwonea huruma sana maana amechoka vibaya kwa hali ngumu ya maisha.

nakupongeza kwa kufanya kitubio. Mwenzio mimi nilishtuka toka mapema. Kura yangu 2005 ilikwenda kwa freemana mbowe.

Yupo rafiki yake jk mmoja aitwaye remmy alikuwa mwandishi wa habari na mmoja wa watu wanaomtafutia viburudisho, remmy alipinga sana kitendo cha jk kugombea urais na alikuwa akisema siku zote kuwa jamaa hafai kuwa rais.

Sasa hivi ni marehemu, angelikuwepo nafikiri angekuwa ni mmoja wa watiu ambao wangekuwa na raha sana kuona alichokisema 2005 kimetimia
.
 
Mnaikumbuka sera ya;

HARI MPYA, NGUVU MPYA na KASI MPYA?

Na Je, Swala la Ajira Nyingi kwa Vijana?.​

Na ss, juzi tu serikali imeruhusu wananchi wa Afrika Mashariki kuja kufanya kazi ktk vyuo vya binafsi.... Kazi ipo.

Vipi, sera imekidhi haja ya Wa-Tz wengi?

mkuu, u handsome ulimfanya wamama na wadada wengi wampe kura.
 
Kwa sasa Watanzania hatuna haja tena ya kumfikiria mgombea yeyote wa CCM. Lazima tujiulize, kwa miaka yote hii ya utawala wa CCM, wametutendea nini hata kustahili kuendelea kupewa kura zetu. Tumekuwa na subira, tumewavumila, lakini ukweli ni kuwa hakuna walichotutendea zaidi ya wao kujiimarisha kama kikundi cha mafia ili kuendelea kufaida kwa kuwaibia watanzania.

Nadhani mahali pa kuanzia kufikiria kwa wagombea wa 2015, ni nani kutoka kundi la upinzani watastahili kuchaguliwa. Kuwa mwanaCCM iwe disqualification ya mwanzo kabisa kiasi cha kutofikiriwa kabisa.

Wengi walipiga kura kwa ushabiki tu bila kujua wanayemchagua ana sifa zipi na hasa za kiuongozi.
Na kwa mshangao mkubwa naona baadhi ya watanzania wanaelekea kurudia kosa hilo hilo la kuweka maisha yao rehani tena kwa miaka mingine mitano au kumi endapo Edward Lowassa atateuliwa na chama chake kugombea urais 2015. Hiyu jamaa amekua serikalini miaka nenda rudi lakini ni kitu gani ambacho amefanya ambayo inaweza kuwafanya watanzania wamuamini na kumchagua? Isije ikawa majuto kama wanavyojuta waliomchagua JK.

Naamini watanzania hawakotayari tena kupoteza muda kusubiri kuona wenzao wa mataifa mengine yakiendelea wao wakiendelea kuupa ufisadi nafasi ya kutamalaki.
 
Sikushiriki uchaguzi , ila akirugusiwa 2015 nashiriki ila simpi kura yangu.
 
Nadhani Kuna umuhimu kujua kuwa wapigakura wengi walikuwa wamekata tamaa ya maisha Hasa vijijini hawakuwa na mbadala wa kuwapa tumaini jipya na kikwete alijua Hilo akatangaza sana sura nzuri kama kigezo cha kuleta maisha bora kwa Kila mtanzania mnakumbuka Yale mabango nchi nzima pili kupungukiwa na uelewa kuhusu kiongozi bora imezoeleka Kuwa kiongozi akitangazwa na ccm hata kama hafai huitwa bora bila kujali ubora wake kitaifa ukoje kwangu Mimi rais kikwete alikuwa mzuri aliefaa kuongoza ccm kuvuta wanchama wapya lakini si kuongoza taifa sikuwahi kumpa kura yangu tangu 2005 sababu kwangu kiongozi wa taifa ni Yule tuu anayeheshimiwa na wote na sio anayependwa tutofautishe hapo na tupime kikwete alikuwa anapendwa Au anaheshimiwa? Ukimpenda kiongozi unamuondolea sifa kwa wasiompenda kiongozi bora ataheshimiwa na wote kama ilivyokuwa kwa salim kipindi kile akafanyiwa fitna. Hata Ukisikia sifa za kikwete toka kwa watetezi wake hapa wanasema alikuwa na mvuto kisiasa mshawishi wa watu msikivu hata serikali inaitwa sikivu mpanga makundi ya ushindi hizi zote hazitoshi kuwa kiongozi bora wa nchi kwa maoni yangu.
 
Back
Top Bottom