Nicas Mtei
JF-Expert Member
- Dec 21, 2010
- 11,556
- 7,085
Habar zenu great thinkers wote? Mimi ni kijana mfanya biashara, niliwah kupata rafik wa kike katika biashara zetu na ilitokea tukawa karibu zaidi kitu ambacho kilisababisha niwe na hisia za kimapenzi naye. Nilitokea kupenda awe mchumba wangu ili baadaye tufunge ndoa ila nilipo mueleza mwenzangu akasema yeye hayuko tayar kuwa na mahusiano nami hvyo haitawezekana.. Niliumia sana mwisho wa siku ilinibid niyaheshmu maamuz yake na ndipo nilipochukua ustaarabu wa kutafuta mchumba mwngne ambaye ndo natarajia kufunga naye ndoa.. Tangu nilipopata mchumba huyo yule rafiki yangu wa kike alianza kumchukia na kuanza kuwa na wivu. Na hata kwenye sherehe ya kumvisha pete huyu laaziz wangu mpya ye hakutokea bila sababu ya msingi.. Yani ananiweka kwenye wakat mgumu kwan amekuwa akimchunia na hata kuonesha chuki ya wazi kabisa... Naombeni msaada wenu waungwana. Ninateseka sana.