Mke wangu wa zamani alikuwa pasua kichwa, nilimuacha nikaoa mwingine sasa nina furaha

kimsboy

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
8,992
17,892
Kusema kweli sikuwahi kuzungumzia maisha yangu humu JF hususani mambo ya ndoa ila naomba nishare nanyi hili jambo.

Niliwahi kuwa na ndoa ya kwanza lakini mke wangu wa kwanza alikuwa pasua kichwa balaa, ana gubu, kiburi, na mdomo sana, ilikuwa inafika mahali naona hata sio busara kurudi nyumbani mapema.

Nyumba niliiona kama kuzimu, sikuwahi kumdhania mwanzo kipindi najuana nae alikuwa kondoo kavaa ngozi ya chui. Baada ya kumuoa ndo nilianza kushuhudia rangi yake, muda wote ni kukasirika, gubu, kiburi kugombana muda wote na wivu wa kijinga.

Kitu kidogo tu atasusa wivu ya kijinga jinga tu jambo hata hana uhakika nalo au kuhisi unarudi unakuta ashavunjavunja vitu eti ni hasira na wivu. Hata kitu alikuwa anakosa kwa hili sijikwezi ila kiukweli hakuna kitu alkua anakosa nilikua najitahidi namtimizia kila kitu ili awe na furaha vitu na mahitaji ambayo hata wanawake wengine baadhi wanakosa nilikua nampa kila kitu lengo ni kuhakikisha aishi kama malkia lakini wapi!

Ni kama nilikuwa napambana kujaza maji kwenye gunia nilikuwa naishia kukonda tu na kuwa na hasira sometimes nakunywa pombe maana hakuna jema kwake zaidi ya makasiriko,kiburi,gubu na wivu wa kijingajinga tu jambo dogo atakua na hasira atatamani hata kujidhuru atajitupa kitandani kwa hasira yule mwanamke alikuwa kiboko alikuwa na kiburi sijapata kuona sio kwangu tu iwe ndugu zangu au wake walikua wanamuogopa balaa, hadi kwao kaka zake na wadogo zake walimfahamu na walimuogopa kwa jinsi alivyokua na kiburi kikali

Mwanamke alikuwa na kiburi muda wote ni gubu tu na maneno mabaya kubishana na ugomvi, alikua habadiliki sikua na furaha kabisa na yeye kiukweli naheshimu sana wanawake, huwa ni mwiko kwangu kunyanyua mkono na kumpiga mwanamke huwa ninapinga sana suala la kupiga wanawake na nalichukia sana lakini kwa huyu maji yalinifika shingoni.

Nilianza kumpiga kwasababu ya tabia zake za hovyo hovyo,siku moja alikuta namba ya dada mmoja ambaye nina ukaribu naye akaniuliza ni nani nikamjibu na nikampa maelezo kwamba huyo dada ni masuala ya kikazi tu wala sina mahusiano naye na wakuu sikuwahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na huyo dada na hata hizo chats zilikua sio za kimapenzi huwa tunapenda kutaniana sana na huyo dada.

Kulipokucha nikaenda kwenye kazi zangu narudi nakuta mtu keshavunjavunja laptop yangu kavunja vunja vitu ndani eti anadai ni hasira kwasababu nachepuka na huyo dada jambo ambalo sio kweli, nilisikia hasira sana hiyo siku nilimpiga sana.

Ikawa ndo desturi yangu nikawa nampa kipigo kila akifanya jambo la kijinga yaani ni mwanamke mwenye kiburi, jeuri mwenye fujo mwenye maneno ya karaha muda wote anakushutumu tu hadi kitandani hacheki ni kununa tu ilifika mahali nikaamua nioe mwanamke mwingine na yeye nikampiga talaka mbili

Nakumbuka nilileta uzi humu wa kuomba ushauri na kulalamika kujutia ndoa yangu

Nikaoa mwanamke mwingine huyu nikafanya navyojua nikahakikisha nimempa talaka mbili na japo nilipitia misukosuko maana alikua anangangania tuendelee na hataki aachike lakini niliamua kumuacha maana nilikua nishachoka, ndoa isiwe chombo cha kukutesa hata kidogo kuna watu wanafia ndoa ambazo zinawapa mawazo msongo na kila aina ya tabu.

Kumuacha ilimuuma sana na tena akasikia namuoa rafiki yangu ndo alizidi kuchanganyikiwa kabisa mambo ni mengi sana nikieleza hapa sitamaliza hadi mambo ya kishirikina ya huyu mwanamke eti nisioe na nisimwache vimbwanga kibao nitakuja kueleza nikipata muda.Ila nilifanikiwa kumpiga talaka mbili nikahakikisha nimemchomoa na nyumba nikapangisha na nikaachana nae.Nikaoa tena


Ukizingatia huyu mwanamke wangu wa kwanza hakua hata na akili ya maendeleo mama wa nyumbani tu ambaye hakua na akili hata umpe milioni ngapi afanye biashara itakufa tu, alikua hana akili ya biashara kabisa yaani in fact hakua na maajabu yoyote alikua mwanamke wa hovyo kuwahi kutokea japo nimezaa nae.

Na nilimuoa rafiki yangu mwanamke ambaye tulifahamiana miaka zaidi ya 13 tokea advance huko hadi chuo, mwanamke ambaye alikua rafiki yangu mkubwa, rafiki nikimchukulia kama mtu wa karibu yangu,mshauri nk nikaja kumuoa yeye.

Nina furaha sana tokea nimuoe huyu mwanamke kusema kweli ananipenda sana, kiukweli kuna wanawake wanajua thamani ya ndoa,kuna wanawake wanajua maana ya mume, maana ya familia, najiuliza nitampa zawadi gani mke wangu ambayo nitauridhisha moyo wangu,kusema kweli huyu mwanamke ni wa kipekee sana ananijali sana, ana akili ya maendeleo sijui nieleze vipi ananisapoti kila hali yule wa kwanza tokea niwe nae niliishia kumiliki Vitz new model iliyochoka vibaya mno, lakini huyu muda mchache tu biashara zimesimama vizuri na mpaka sasa nishamiliki gari mbili Nissan duals na harrier mpya.

Kusema kweli wakati mwingine mafanikio yako ya ndoa au maendeleo yanadetermine na factor ya aina ya mwenzi ambaye unayo.

Huyo wa zamani alishatafuta mbinu ili arudi lakini wapi?Kila njia alishafanya turudiane lakini wapi.

Ndoa ni tamu ukimpata mwenzi sahihi trust me hutojutia.
 

Attachments

  • 08932d4c33ae4acf96b0b1ece1704189.jpg
    08932d4c33ae4acf96b0b1ece1704189.jpg
    38 KB · Views: 14
Back
Top Bottom