swahiba Senior
JF-Expert Member
- Nov 12, 2016
- 2,479
- 3,613
Aiseee uko vizuri nadhani una PHD ya mambo ya nyokaAnaconda akifutiwa na chatu wa Asia ya Kusini(ukubwa) (hawana sumu, wanaua kwa constriction)
Nyoka mkubwa mwenye sumu ni King Cobra
Nyoka hatari sana kama taipan(ana sumu yenye uwezo wa kuua mpaka watu 400)na Tiger snake wote toka Australia... Australia pekee ina top 10 ya nyoka wenye sumu kali zaidi duniani
Nyoka mwenye sumu kali Afrika ni Black Mamba(koboko) sumu yake inaitwa neurotoxin pamoja na cardiotoxin(inaathiri mfumo wa neva pamoja na moyo
ndo nyoka mwenye kasi zaidi pengine dunia anakwenda km 19 kwa saa(12mph)... Lakini kwa Afrika Boomslang na vine au twig wanaweza kuwa na sumu kali zaidi japo watu wengi wanachukuliwa poa kwa sababu sio wakorofi sana kama Mamba (silent killers (hawa wana sumu inayoitwa haemotoxin ambayo huathiri damu... ina chemical component ambayo huzuia damu kuganda (clotting) na chemical component nyingine husababisha kupasuka kwa mishipa ya damu hii husababisha damu kuvuja ndani na nje kupitia matundu ya mwili )
Puff adder (kifutu) ndo nyoka mwenye kuuwa watu wengi Afrika kuliko nyoka mwingine(sumu yake inaitwa cytotoxin hii huathiri tishu... Inasababisha kuungua au kuoza sehemu ilioumwa
Mozambican spitting Cobra ndo nyoka anaedhuru watu wengi Kusini mwa Afrika
NB:Angali nyoka wote kwa umakini japo asilimia 70 ya nyoka tz hawana sumu ya kudhuru binadamu... Nyoka mdogo ni hatari zaidi (concentration ya sumu kwa nyoka wadogo ni kubwa... Wanatumia kujilinda kutokana na udogo wao)
Nyoka wakubwa umbo lao laweza kuwasaidia kuogofya