Ni nini sababu ya binadamu kuletwa Duniani?

Ni nini sababu ya binadamu kuletwa Duniani?

Mmanu

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2015
Posts
1,977
Reaction score
1,219
Habari wanaJf
Nimekuwa nikijiuliza swali moja la msingi sana lakini majibu thabiti nimekuwa nikikosa kabisa...

Kwa wale wanaoamini kuhusu uwepo wa Mungu naomba wanijuze kwanini tumeletwa hapa duniani ambako tunaishi maisha mafupi na kupita, je Mungu hakuona namna nyingine ya kutufanya tufike huko kwenye maisha ya milele kunakosemwa na vitabu vyake bila kupitia hapa duniani kwenye shida na karaha?
Kulikuwa na haja ipi kutupitisha kwenye mateso hali ya kuwa ipo sehemu salama tunaelekea? ( Kwanini alitupitisha duniani?)

Hata wale wasioamini uwepo wa Mungu nao naomba wanisaidie kujua juu ya hili swali langu...kama hakuna maisha baada ya haya kwanini tupitishwe hii sehemu yenye taabu na mateso mengi tena kwenye maisha mafupi..kwanini tumetolewa huko tulikokuwa na kuletwa hapa duniani ambako kuishi kwetu ni muda mfupi na tisingebaki huko huko kama tulikuwa na maisha kabla?

Nini sababu ya sisi binadamu kuletwa/kupitishwa hapa duniani?
 
Habari wanaJf
Nimekuwa nikijiuliza swali moja la msingi sana lakini majibu thabiti nimekuwa nikikosa kabisa...

Kwa wale wanaoamini kuhusu uwepo wa Mungu naomba wanijuze kwanini tumeletwa hapa duniani ambako tunaishi maisha mafupi na kupita, je Mungu hakuona namna nyingine ya kutufanya tufike huko kwenye maisha ya milele kunakosemwa na vitabu vyake bila kupitia hapa duniani kwenye shida na karaha?
Kulikuwa na haja ipi kutupitisha kwenye mateso hali ya kuwa ipo sehemu salama tunaelekea? ( Kwanini alitupitisha duniani?)

Hata wale wasioamini uwepo wa Mungu nao naomba wanisaidie kujua juu ya hili swali langu...kama hakuna maisha baada ya haya kwanini tupitishwe hii sehemu yenye taabu na mateso mengi tena kwenye maisha mafupi..kwanini tumetolewa huko tulikokuwa na kuletwa hapa duniani ambako kuishi kwetu ni muda mfupi na tisingebaki huko huko kama tulikuwa na maisha kabla?

Nini sababu ya sisi binadamu kuletwa/kupitishwa hapa duniani?
evolution.................................... hakuna cha Mungu hapa it is purely science..................
 
Maisha ni fumbo.
Maisha ya duniani yalikuwa ni zawadi na sio adhabu, changamoto ni binadamu kutaka kuishi against nature, hapo ndipo mateso yanapo anzia.

Swali: Unauhakika gani kwamba upo duniani?
Umeshawahi kuota ndoto na ukajiona upo huko ndotoni? What if na hapa upo ndotoni na pengine ukifa hapa ndo unaamka kutoka usingizi uliokuwapo?
 
Swali gumu sana kupata majibu yanayo kidhi haja .
Wenyewe wenye dini wanasema tupo hapa ili tumjue Mungu tumheshinu kumuabudu na kwenda kwake!
Acha tubaki na imani hio ila ukweli usio na shaka kuna namna nyingine ya ufafanuzi wa maisha nje ya hii ambayo ina mantiki kidogo ambayo wenye mamlaka fulani hawataki ijulikane.
 
Habari wanaJf
Nimekuwa nikijiuliza swali moja la msingi sana lakini majibu thabiti nimekuwa nikikosa kabisa...

Kwa wale wanaoamini kuhusu uwepo wa Mungu naomba wanijuze kwanini tumeletwa hapa duniani ambako tunaishi maisha mafupi na kupita, je Mungu hakuona namna nyingine ya kutufanya tufike huko kwenye maisha ya milele kunakosemwa na vitabu vyake bila kupitia hapa duniani kwenye shida na karaha?
Kulikuwa na haja ipi kutupitisha kwenye mateso hali ya kuwa ipo sehemu salama tunaelekea? ( Kwanini alitupitisha duniani?)

Hata wale wasioamini uwepo wa Mungu nao naomba wanisaidie kujua juu ya hili swali langu...kama hakuna maisha baada ya haya kwanini tupitishwe hii sehemu yenye taabu na mateso mengi tena kwenye maisha mafupi..kwanini tumetolewa huko tulikokuwa na kuletwa hapa duniani ambako kuishi kwetu ni muda mfupi na tisingebaki huko huko kama tulikuwa na maisha kabla?

Nini sababu ya sisi binadamu kuletwa/kupitishwa hapa duniani?
Kwakweli mimi binafsi sijui.

Kila jibu nililowahi kulipata hali make sense.

Infact, ukituondoa sisi binadamu wote humu duniani, dunia na viumbe vingine vyote vitaendelea kuishi na kuzaliana kama kawaida
 
Maisha ni fumbo. Maisha ya duniani yalikuwa ni zawadi na sio adhabu, changamoto ni binadamu kutaka kuishi against nature, hapo ndipo mateso yanapo anzia.

Swali: Unauhakika gani kwamba upo duniani?
Umeshawahi kuota ndoto na ukajiona upo huko ndotoni? What if na hapa upo ndotoni na pengine ukifa hapa ndo unaamka kutoka usingizi uliokuwapo?
Na inawezekana sisi ni virusi tupo ndani ya tumbo la mnyama mkubwa , na akimeza dawa tunakufa na kupungua kwetu ni nafuu kwake🤔🤔
 
Swali gumu sana kupata majibu yanayo kidhi haja .
Wenyewe wenye dini wanasema tupo hapa ili tumjue Mungu tumheshinu kumuabudu na kwenda kwake!
Acha tubaki na imani hio ila ukweli usio na shaka kuna namna nyingine ya ufafanuzi wa maisha nje ya hii ambayo ina mantiki kidogo ambayo wenye mamlaka fulani hawataki ijulikane.
Kwani mungu yeye angepata hasara gani kama asingetuumba? Na kwanini atuumbe viumbe dhaifu kiasi hiki halafu eti ndio tumeumbwa kwa "sura na mfano wake?". Hapana kwakweli, haiingii akilini hata kidogo.
 
Maisha ni fumbo. Maisha ya duniani yalikuwa ni zawadi na sio adhabu, changamoto ni binadamu kutaka kuishi against nature, hapo ndipo mateso yanapo anzia.

Swali: Unauhakika gani kwamba upo duniani?
Umeshawahi kuota ndoto na ukajiona upo huko ndotoni? What if na hapa upo ndotoni na pengine ukifa hapa ndo unaamka kutoka usingizi uliokuwapo?
Binadamu kutaka kutaste nature ndo ubinadamu wenyewe, ndivyo tulivyoumbwa.
Angetuumba tusiwe na mawazo ya kutaste nature naamini alikuwa na uwezo huo.

Yaani utengeneze kitu kina mapungufu halafu ukikasirikie na kukipa adhabu wakati ni makosa yako wewe mwenyewe. Doesn't make sense
 
Kwakweli mimi binafsi sijui.

Kila jibu nililowahi kulipata hali make sense.

Infact, ukituondoa sisi binadamu wote humu duniani, dunia na viumbe vingine vyote vitaendelea kuishi na kuzaliana kama kawaida
Tutafute jibu linaloweza kutupa majibu thabiti kwanini tumeletwa duniani..
Lakini pia kuna maandiko yanasema viumbe vyote vitaangamizwa duniani ndiyo wanasema itabaki tupu
 
Binadamu kutaka kutaste nature ndo ubinadamu wenyewe, ndivyo tulivyoumbwa.
Angetuumba tusiwe na mawazo ya kutaste nature naamini alikuwa na uwezo huo.

Yaani utengeneze kitu kinamapungufu halafu ukikasirikie na kukipa adhabu wakati ni makosa yako wewe mwenyewe. Doesn't make sense
Hukutengenezewa kama upungufu, ni zawadi, kwamba uwe na free will. changamoto tu ni kuwa will power haina mipaka, na unaweza ukafanya jambo hata kinyume na aliyekupa huo uwezo wa kuchagua. Hasa ndo kinachokutesa.

Hasira ya Mungu ipo kwasababu uliumbwa ukiwa mkamilifu. Kwa hiyo mapungufu uliyonayo ni ya kujitakia tu, ni kama unavyolea mtoto wako alaf afanye kitu tofauti na unavyo mwelekeza utakasirika
 
Back
Top Bottom