KIBURUDISHO
JF-Expert Member
- Mar 28, 2011
- 1,002
- 274
WanaJF wenzangu habari za mida nimekumbuka mbali sana mara tuu nilipomkumbuka marehemu mjombaangu aliyekimbilia jijini hapa tangu miaka ya 1987 baada ya kukorofishana na baba yake mzazi juu ya suala zima la kumshinikiza kuoa na kuishi kijijini mara baada ya kuhitimu elimu yake ya msingi ambayo hakuchaguliwa kuendelea na elimu ya sekondari.
Kwa hiyo hapa jijini kuna wengi ambao si wazaliwa wa hapa ambao kila mmoja alikuja kwa namna yake.Kuna aliyekuja kwa kheri kuna waliokuja kwa shari kama mjombaangu, kwa matumaini ya kutafuta maisha na kufanikiwa mara baada ya kufika Dar es salaam.Kuna waliofanikiwa na kuwa matajiri wakubwa na wengine hawajafanikiwa hadi hivi sasa lakini tumaini lao likiwa ni moja tuu kuwa ipo siku watajaaliwa na mwenyezi mungu.
Hivyo basi nikaona ni vyema wanaJF wenzangu tukakumbushana kila mmoja kwa mara yako ya kwanza ulifikafikaje Dar es salaam na ulikuja kutafuta nini na kwanini na jee umekwishafanikiwa?
Kwa hiyo hapa jijini kuna wengi ambao si wazaliwa wa hapa ambao kila mmoja alikuja kwa namna yake.Kuna aliyekuja kwa kheri kuna waliokuja kwa shari kama mjombaangu, kwa matumaini ya kutafuta maisha na kufanikiwa mara baada ya kufika Dar es salaam.Kuna waliofanikiwa na kuwa matajiri wakubwa na wengine hawajafanikiwa hadi hivi sasa lakini tumaini lao likiwa ni moja tuu kuwa ipo siku watajaaliwa na mwenyezi mungu.
Hivyo basi nikaona ni vyema wanaJF wenzangu tukakumbushana kila mmoja kwa mara yako ya kwanza ulifikafikaje Dar es salaam na ulikuja kutafuta nini na kwanini na jee umekwishafanikiwa?