Sasa yeye alitegemea kwamba mkewe ampe mali anawajua wanawake vizuri au anawasikia?
Vitu alivyobugi:
Kaoa mwanamke mwenye watoto, kosa kubwa mwanaume hutakiwi kufanya.
Kajichanganya kumsapoti mwanamke kwenye utafutaji akiamini kitakuwa cha wote badala ya kukomaa na utafutaji wake ili mkewe ndie ajiegemeze kwake.
Watoto wa mwanaume mwingine sio watoto wake, hawawezi kumuona kama baba yao mzazi. Mke alipofariki tayari mkataba umeisha maana wale watoto sio damu yake so hawawezi elewana na ndio wameshaanza kuvutana na maswala ya mali hapo ndio imeisha watoto hawatataka tena kujuana nae.
Humu mitandaoni kila siku mnaelekezwa msipoyashika haya maelekezo msitegemee muujiza huko mbeleni yakiwakuta.
Acheni kujenga mazoea na wanawake wenye watoto, kama aliamua kuzaa na mtu na yupo waende wakapambane na hali zao huko huko kwann azae halafu atengane na huyo mtu na akuaminishe kuwa yeye na huyo mtu wamemalizana?
Wewe jichanganye sasa kujifanya Yesu una huruma na mizigo ya watu. Wanawake wamejaa tele tena vitoto vibichi wewe unakwenda chukua mwanamke kashazeeshwa kimajukumu ana mtoto na mtu we unakwenda kubeba uweke ndani tena na mtoto au watoto, kwann sasa asikunyooshe huko mbeleni?
Wanawake wenyewe huwa wanashangaa sana kuona mwanaume unataka mchukua huku ameshazaa ile kujifanya anakubali ni kukuachia tu ubebe mizigo ya bills zake sasa subiri apate kazi au mtu wake arudishe majeshi utajua haujui na mbaya zaidi atakugeuka kama hakujui wala hamkukubaliana.
Achana na wanawake wenye watoto katafute wa kwako. Uking'ang'ana na hawa waliozaa wale waliojitunza wataishi na nani na walijitunza wasizae hovyo?
Huo ni ukweli mchungu ila watoto wa kiume mkisimama nao mtaona masingle mother wanaanza kutoweka kwa kasi kwenye jamii.