Ni nani anayemdanganya Edward Lowassa?

Ni nani anayemdanganya Edward Lowassa?

Ni punguani peke yake ndiyo anaweza kukubaliana na hizo porojo za Lowassa, anadhani watanzania wote wana akili za nyumbu.
Nyumbu uko wewe na wenzako wa lumumba
 
Wingi wa kura alizopata una uhusiano gani na amani ya Tanzania?

Kwa fikra zako kwa sababu watu zaidi ya milioni sita walimpa kuwa kwa hiyo hata fikra zao amewashikia!
Zanzibar mlishindwa kuiba
 
Concerntrate na mambo yako
Wewe ndiye unatakiwa ukonsetileti na mambo yako!

Umeganda kwenye thread yangu badala ya kukonsetileti na mambo yako!

Inaonekana huelewi hata unachokifanya!
 
Kwa akili yako ndogo unamlinganisha Lowasa na nani katika nchi hii!!! Acha u nyumbu. Eti akachunge ng'ombe!! And politically finished!! Acha upuuzi huu!! Usiandike kitu usichokijua. Acha kabisa.
Simfananishi Lowassa na mtu yeyote lakini kilichowazi, Lowassa kwa sasa anapitia njia ya kisiasa aliyopitis Mrema
 
Mleta mada kitendo cha wewe kushindwa kumpuuza Lowasa na kumjadili kila Mara in dalili za kum admire
 
Kwa kuwa bado mdomo anao hebu awaambie basi wafuasi wake hata leo hii waingie barabarani tuone kama yaliyomo yamo.
 
Lowasa pesa zake ndo zinamdanganya mengine yoote ni hadithi kama angekua hana pesa hakuna ambae anagehangaika nae!!
 
Dunia inatambua Lowassa ana utajiri wa kifikra kuhusu njia ya kuwa fisadi nchini Tanzania. Kinachoendelea kwa sasa kinadhihirisha Lowassa anahitaji huruma za kisiasa kutokana na mwenendo wake kisiasa. Anahitaji sana ushauri usio wa kinafiki kuhusu hatima yake kisiasa nchini.

Nilivyomsikia kwa mara ya kwanza akitoa madai kuwa ukimya wake baada ya Uchaguzi Mkuu umesababisha kuwepo amani nchini, nilidhani kinachomsumbua ni mihemko ya kisiasa.

Nilipomsikia pia kwa mara ya pili akitamka maneno hayo Mkoani Arusha wakati akishiriki katika kampeni za Uchaguzi wa Jimbo la Arusha ambao uliahirishwa katika siku ya Uchaguzi Mkuu baada ya kifo cha mgombea wa ACT-wazalendo Estomih Mallah sikushangaa sana.

Kilichonishangaza zaidi ni pale nilipomuona tena kwa mara ya tatu ndani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Usharika wa Monduli akisema kunyamaza kwake baada ya wananchi kupiga kura kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 kumewafanya wananchi wasiuane. Eti anadai wananchi walikuwa wanasubiri neno lake ili waingie barabarani na kuanza kuuana.

Lowassa anataka kutuambia watanzania wengi ni kama nyumbu kwamba kila atakalolisema watalifuata au kulitenda. Anataka kutuambia watanzania wengi wanafanya mambo yao kwa kutegemea kauli zake. Anadhani yale aliyokuwa anayaita mahaba kwenye mikutano yake ni unyumbu.

Hawa watu wanaomshauri Lowassa waache kumdanganya. Kuna baadhi ya watu wanamjaza ujinga ili adhani ana hekima na busara zaidi ya Watanzania wengi.

Lowassa na wapambe wake hawafahamu kama watanzania wengi wana haiba ya kutopenda vurugu. Hafahamu kama kuna chaguzi kuu nne zimefanyika na Tanzania imeendelea kuwa nchi ya amani na kuheshimiana. Hafahamu utawala wa machifu uliokuwa na nguvu kubwa (powerful influence)katika jamii nchini ulipigwa marufuku na Tanzania ikaendelea kuwa na amani na kuheshimiana. Hafahamu tuna makabila zaidi ya 120 yenye imani za kidini tofauti lakini yanaishi katika msingi wa kuheshimiana na undugu.

Lowassa na wapambe wake wangetafuta kwanza uzoefu kuhusu haiba ya Watanzania kutoka wapinzani ambao wamekuwa katika uwanja wa upinzani kabla yeye hajawaza/kufikiria kama kuna siku atakuja kuwa mpinzani wa serikali ya CCM.

Kinachoonekana kwa sasa Lowassa yuko katika safari ya kisiasa ambayo Augustino Mrema amepitia! Lowassa has gone from hero to zero! As a politician, he is finished. There is no way back for him.

Ni nani anamshauri Edward Lowassa? Mwacheni akachunge ng'ombe wake Monduli!
umenena vyema
 
Nadhani ifike mahali mtu ujipambanue mwenyewe umeachieve nini au umeacha legacy gani kwenye hii nchi kabla ya kumponda mtu kama Lowassa. Hata wale waliokua wanaongea vibaya juu yake ni kutokana na uchaguzi..pamoja na hayo yote walikua makini sana katika maneno yao
wengi ni wanasiasa mashuhuri nchini
leo hii anakurupuka mtu hajui hata kesho yake na elimu yake ya brn...Lowassa,lowassa...uchaguzi umeisha EL atabaki kua mtu mwenye influence kubwa sana nchini.(Hata ukipinga ukweli wa namba utakusuta,moyoni unaelewa) hivyo anasikilizwa na watu wengi na bado hekima zake zinahitajika.Tujenge nchi acheni uoga.
 
MsemajiUkweli a.k.a MsemajiUongo,
Weye ndiye mpuuzi na mjinga waheed. Ni mtu mpumbavu na mwehu tu kama weye ndo aweza kupingana na hoja ya kwamba utulivu ambao umetamalaki baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015 ni kutokana na Lowassa kutotoa tamko la kuruhusu wafuasi/Watanzania zaidi ya milioni 6 kuingia mtaani kupinga matokeo ya Uchaguzi yaliyotangazwa na NEC.

Kumbuka kuwa EL alikuwa na kura nyingi zaidi ya Magufuli kulingana na matokeo halisi kutoka vituo vyote vya uchaguzi kama yalivyokuwa yakipokelewa na kituo cha majumulisho UKAWA Tallying centre kilichovamiwa na Polisi/UWT ili kuficha ukweli huo!

Mpaka sasa Kompyuta za UKAWA za majumuisho ziko Polisi.Lakini pia kuna kompyuta zile za Jumuia za Haki za Binadamu waliokuwa waangalizi wa ndani nazo zilikamatwa kwa sababu zilezile za kuficha /kuchakachua MATOKEO HALALI NA HALISI YA UGHAGU MKUU 2015! Huu ni ukweli ambao NEC,CCM na MAGUFULI WANAJUA!

Swali kwako ewe nyumbu kichaa.Je, unajua kwamba kuna Taasisi za KIDINI zaidi ya 200 toka duniani kote zilikutana Desemba mwaka jana na kumtunuku LOWASSA ZAWADI YA AMANI sawa na NOBLE PEACE PRIZE kwa utulivu aliouonyesha Lowassa na wafuasi wake hata baada ya kuhujumiwa ushindi wake?

Kwa akili yako ya kinyumbu unafikiri hizi Taasisi walikuwa wapuuzi kufikia maamuzi hayo ili kumfurahisha EL?No way!Huo ni uhalisi wenyewe kama hujui!

Kumbuka Wamarekani wameinyima Tanzania kiasi cha zaidi ya Tshs.Trilioni 1 kutokana na madudu ya Uchaguzi Mkuu wa 2015!
Ikiwa wapo watanzania wengi wenye mawazo kama haya then nchi hii iko kwenye problem kubwa mno.
 
Back
Top Bottom