Ni nani anayemdanganya Edward Lowassa?

Ni nani anayemdanganya Edward Lowassa?

Dunia inatambua Lowassa ana utajiri wa kifikra kuhusu njia ya kuwa fisadi nchini Tanzania. Kinachoendelea kwa sasa kinadhihirisha Lowassa anahitaji huruma za kisiasa kutokana na mwenendo wake kisiasa. Anahitaji sana ushauri usio wa kinafiki kuhusu hatima yake kisiasa nchini.

Nilivyomsikia kwa mara ya kwanza akitoa madai kuwa ukimya wake baada ya Uchaguzi Mkuu umesababisha kuwepo amani nchini, nilidhani kinachomsumbua ni mihemko ya kisiasa.

Nilipomsikia pia kwa mara ya pili akitamka maneno hayo Mkoani Arusha wakati akishiriki katika kampeni za Uchaguzi wa Jimbo la Arusha ambao uliahirishwa katika siku ya Uchaguzi Mkuu baada ya kifo cha mgombea wa ACT-wazalendo Estomih Mallah sikushangaa sana.

Kilichonishangaza zaidi ni pale nilipomuona tena kwa mara ya tatu ndani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Usharika wa Monduli akisema kunyamaza kwake baada ya wananchi kupiga kura kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 kumewafanya wananchi wasiuane. Eti anadai wananchi walikuwa wanasubiri neno lake ili waingie barabarani na kuanza kuuana.

Lowassa anataka kutuambia watanzania wengi ni kama nyumbu kwamba kila atakalolisema watalifuata au kulitenda. Anataka kutuambia watanzania wengi wanafanya mambo yao kwa kutegemea kauli zake. Anadhani yale aliyokuwa anayaita mahaba kwenye mikutano yake ni unyumbu.

Hawa watu wanaomshauri Lowassa waache kumdanganya. Kuna baadhi ya watu wanamjaza ujinga ili adhani ana hekima na busara zaidi ya Watanzania wengi.

Lowassa na wapambe wake hawafahamu kama watanzania wengi wana haiba ya kutopenda vurugu. Hafahamu kama kuna chaguzi kuu nne zimefanyika na Tanzania imeendelea kuwa nchi ya amani na kuheshimiana. Hafahamu utawala wa machifu uliokuwa na nguvu kubwa (powerful influence)katika jamii nchini ulipigwa marufuku na Tanzania ikaendelea kuwa na amani na kuheshimiana. Hafahamu tuna makabila zaidi ya 120 yenye imani za kidini tofauti lakini yanaishi katika msingi wa kuheshimiana na undugu.

Lowassa na wapambe wake wangetafuta kwanza uzoefu kuhusu haiba ya Watanzania kutoka wapinzani ambao wamekuwa katika uwanja wa upinzani kabla yeye hajawaza/kufikiria kama kuna siku atakuja kuwa mpinzani wa serikali ya CCM.

Kinachoonekana kwa sasa Lowassa yuko katika safari ya kisiasa ambayo Augustino Mrema amepitia! Lowassa has gone from hero to zero! As a politician, he is finished. There is no way back for him.

Ni nani anamshauri Edward Lowassa? Mwacheni akachunge ng'ombe wake Monduli!
Kwa akili yako ndogo unamlinganisha Lowasa na nani katika nchi hii!!! Acha u nyumbu. Eti akachunge ng'ombe!! And politically finished!! Acha upuuzi huu!! Usiandike kitu usichokijua. Acha kabisa.
 
Macheni mmasai wa watu...

(Kwa sauti ya mshenga)
 
"Uchaguzi wa Mwaka Jana , CCM tulishindana Wenyewe kwa Wenyewe , Kwa Maana Upinzani umekufa na tukabaki wenyewe tu , Waliokuwa Upande wa Pili woote Wazawa wa CCM "

Mbunge Msukuma
Star TV LIVE
 
Mpuuzi ni yule anayedhani amani ya Tanzania alikuwa ameishikilia kwenye mdomo wake!

Mpuuzi ni yule anayedhani Watanzania wengi ni kama manyumbu!

MsemajiUkweli a.k.a MsemajiUongo,
Weye ndiye mpuuzi na mjinga waheed. Ni mtu mpumbavu na mwehu tu kama weye ndo aweza kupingana na hoja ya kwamba utulivu ambao umetamalaki baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015 ni kutokana na Lowassa kutotoa tamko la kuruhusu wafuasi/Watanzania zaidi ya milioni 6 kuingia mtaani kupinga matokeo ya Uchaguzi yaliyotangazwa na NEC.

Kumbuka kuwa EL alikuwa na kura nyingi zaidi ya Magufuli kulingana na matokeo halisi kutoka vituo vyote vya uchaguzi kama yalivyokuwa yakipokelewa na kituo cha majumulisho UKAWA Tallying centre kilichovamiwa na Polisi/UWT ili kuficha ukweli huo!

Mpaka sasa Kompyuta za UKAWA za majumuisho ziko Polisi.Lakini pia kuna kompyuta zile za Jumuia za Haki za Binadamu waliokuwa waangalizi wa ndani nazo zilikamatwa kwa sababu zilezile za kuficha /kuchakachua MATOKEO HALALI NA HALISI YA UGHAGU MKUU 2015! Huu ni ukweli ambao NEC,CCM na MAGUFULI WANAJUA!

Swali kwako ewe nyumbu kichaa.Je, unajua kwamba kuna Taasisi za KIDINI zaidi ya 200 toka duniani kote zilikutana Desemba mwaka jana na kumtunuku LOWASSA ZAWADI YA AMANI sawa na NOBLE PEACE PRIZE kwa utulivu aliouonyesha Lowassa na wafuasi wake hata baada ya kuhujumiwa ushindi wake?

Kwa akili yako ya kinyumbu unafikiri hizi Taasisi walikuwa wapuuzi kufikia maamuzi hayo ili kumfurahisha EL?No way!Huo ni uhalisi wenyewe kama hujui!

Kumbuka Wamarekani wameinyima Tanzania kiasi cha zaidi ya Tshs.Trilioni 1 kutokana na madudu ya Uchaguzi Mkuu wa 2015!
 
"Uchaguzi wa Mwaka Jana , CCM tulishindana Wenyewe kwa Wenyewe , Kwa Maana Upinzani umekufa na tukabaki wenyewe tu , Waliokuwa Upande wa Pili woote Wazawa wa CCM "

Mbunge Msukuma
Star TV LIVE

Huyu Mbunge Msukuma anatokea jimbo la Geita kama sijakosea.Jimbo la Geita ndilo ambalo mgombea wa CHADEMA Marehemu Mawazo(rip) aligombea na baadae kuuawa kinyama!

Msukuma ashukru kuwa Serikali ya CCM inaongozwa kidikteta.Huyu jamaa alitakiwa kwa sasa awe ananyea ndoo pale gereza la Butimba! Hapana shaka nyuma ya mauaji ya Mawazo mbunge huyu fake anahusika kwa asilimia 100!
Msukuma anajua alishinda kwa hila na alijua kuwa pasi na kuondoa uhai wa Mawazo huo Ubunge wake usingedumu maana kitendo cha Mawazo kutinga Mahakamani ndiyo ungelikuwa mwisho wa ubunge wa Msukuma!

Huu ni ukweli mchungu ambao Msukuma,Magufuli na CCM wanalijua hilo!
 
Eti "watanzania wanahulka ya kupenda amani", aisee nimechoka kabisa na statement yako hii!!

Wewe unadhani wasomalia, wanaijeria, wanyarwanda, warundi, wakenya, wasyria, wamisri au wengine wote waliochoka na manyanyaso na ukandamizaji wa wenye madaraka hawana au hawakuwahi kuwa na hulka ya kuipenda amani!!??

Please, give me a break!!
Mimi ninaongelea Watanzania, wewe unaanza kuleta mifano ya mataifa mengine.

Hizi ndizo fikra kama za Lowassa kudhani amani ya Tanzania ilikuwa ndani ya mdomo wake. Nani amekuambia Watanzania ni kama Wasomalia, Wanaijeria, Wakenya au Wamisri?
Ipo siku huu uhuni mnaofanya dhidi ya maamuzi halali ya wananchi kupitia sanduku la kura yatafikia mwisho kwa watu kusema enough is enough!!
Yeah, Siyo kosa kuota ndoto za alinacha.
Hebu angalia kinachoendelea Zanzibar ni uhuni mtupu. Kama sio busara za wapinzani wenu ktk chaguzi hizi, wananchi hawa mnaowaona kama wajinga vile ni sawa na nyasi kavu ktk nyika ambazo njiti moja tu ya kiberiti inaweza kuwasha moto ambao hakuna atakayeweza kuuzima!!
Zanzibar kuna amani kwa sababu wananchi wengi wameamua kuishi kwa amani. Hakuna kiongozi yoyote aliyeshikilia amani ya Zanzibar.
Mimi nakubali kabisa busara za opponents wa Magufuli kina Edward Lowassa na Seif Shariff Hamad na wengineo ndiyo maana leo unajitutumua kuandika upuuzi kama huu hapa
Mambo ya busara unayafahamu wewe lakini ninachosema, Lowassa kusema amani ya Tanzania alikuwa ameitunza kwenye mdomo wake ni kuwafanya watanzania wengi kama nyumbu.

Amani ya Tanzania iko mikononi mwa Watanzania wengi. Ni lini amani ya Tanzania ilimilikiswa kwa Lowassa?
 
Atakuwa Mbowe tu !!!
Mbowe anaendelea kumkamua huyu Mzee!

Kwenye biashara ya kisiasa nchini, Mbowe ni mmoja wa watu wanaoziweza biashara hizi!

Kwa sasa pesa ya ruzuku imeongezeka wakati huo huo, bado ni Mbunge na pia cheo cha KUB ataendelea nacho bila kusahamu Uenyekiti wa CHADEMA Taifa.
 
Na wale waliokua wanasema ccm imeleta amani msichague wapinzan wataleta vita nae ni mtu gani?
Wakina nani walikuwa wanasema maneno hayo?

Je, maneno yao yalikuwabaliwa na wale walikuwa wanawaambia waichague CCM?
 
Hata shetani ni shidaah. Shetani anajadiliwa sana kwenye makanisa na misikiti!

Hiyo nyota ya shetani ni hatari!

Yaweekana huyu ni Shetani kweli, katupotezea watu muhimu sana, Tumempoteza ,Kingunge Ngombale Mwiru, William Mngeja, Makongoro Mahanga, R Mwasha, Frola Mbasha, Woper, Kamtoa kwenye mstari Elikael Mbowe, Msigwa, Lissu, Mnyika, Kubenea na wengineo. Leo anakiri wapenzi wake wengi walikuwa ni wakwepa kodi, ati kubanwa kwao leo wanaonewa kwa sababu walimshabikia yeye!!! alitaka tumchague ili watu wake wake waendelee kutuliza!!!!
 
Kinachoonekana kwa sasa Lowassa yuko katika safari ya kisiasa ambayo Augustino Mrema amepitia! Lowassa has gone from hero to zero! As a politician, he is finished. There is no way back for him.

Ni nani anamshauri Edward Lowassa? Mwacheni akachunge ng'ombe wake Monduli!

Nadhani wanachomfanyia ni zaidi ya kumdanganya; ni kumtumia (take advantage of). Nina uhakika yeye na watu wote waliomshinikiza na kumuunga mkono kugombea Urais hawaamini kabisa kuwa wapo Watanzania wengi tu ambao hawakuwa tayari kumuona anachaguliwa kuwa Rais. Ukweli ni kuwa kama watu wangekuwa wanamtaka kweli na wangeamini hoja kuwa amedhulumiwa au ameibiwa kura watu hao wasingehitaji kusubiri neno lake. Tena tukiangalia tutaona tu kuwa tayari alishaanza kuwachochea ili wajitokeze mitaani pale alipojitangaza kuwa yeye ni mshindi na Tume imtangaze yeye kwani alikuwa tayari anaongoza. Ile ilikuwa ni namna ya kuwachochea watu waamini uongo na wajitoe mitaani kudai "atangazwe atangazwe".

Kwa vile tayari anaamini yeye ni Rais wa mioyo ya Watanzania wakati umefika atengeneze Ikulu kwenye mioyo ya hao ili awatale.
 
Dunia inatambua Lowassa ana utajiri wa kifikra kuhusu njia ya kuwa fisadi nchini Tanzania. Kinachoendelea kwa sasa kinadhihirisha Lowassa anahitaji huruma za kisiasa kutokana na mwenendo wake kisiasa. Anahitaji sana ushauri usio wa kinafiki kuhusu hatima yake kisiasa nchini.

Nilivyomsikia kwa mara ya kwanza akitoa madai kuwa ukimya wake baada ya Uchaguzi Mkuu umesababisha kuwepo amani nchini, nilidhani kinachomsumbua ni mihemko ya kisiasa.

Nilipomsikia pia kwa mara ya pili akitamka maneno hayo Mkoani Arusha wakati akishiriki katika kampeni za Uchaguzi wa Jimbo la Arusha ambao uliahirishwa katika siku ya Uchaguzi Mkuu baada ya kifo cha mgombea wa ACT-wazalendo Estomih Mallah sikushangaa sana.

Kilichonishangaza zaidi ni pale nilipomuona tena kwa mara ya tatu ndani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Usharika wa Monduli akisema kunyamaza kwake baada ya wananchi kupiga kura kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 kumewafanya wananchi wasiuane. Eti anadai wananchi walikuwa wanasubiri neno lake ili waingie barabarani na kuanza kuuana.

Lowassa anataka kutuambia watanzania wengi ni kama nyumbu kwamba kila atakalolisema watalifuata au kulitenda. Anataka kutuambia watanzania wengi wanafanya mambo yao kwa kutegemea kauli zake. Anadhani yale aliyokuwa anayaita mahaba kwenye mikutano yake ni unyumbu.

Hawa watu wanaomshauri Lowassa waache kumdanganya. Kuna baadhi ya watu wanamjaza ujinga ili adhani ana hekima na busara zaidi ya Watanzania wengi.

Lowassa na wapambe wake hawafahamu kama watanzania wengi wana haiba ya kutopenda vurugu. Hafahamu kama kuna chaguzi kuu nne zimefanyika na Tanzania imeendelea kuwa nchi ya amani na kuheshimiana. Hafahamu utawala wa machifu uliokuwa na nguvu kubwa (powerful influence)katika jamii nchini ulipigwa marufuku na Tanzania ikaendelea kuwa na amani na kuheshimiana. Hafahamu tuna makabila zaidi ya 120 yenye imani za kidini tofauti lakini yanaishi katika msingi wa kuheshimiana na undugu.

Lowassa na wapambe wake wangetafuta kwanza uzoefu kuhusu haiba ya Watanzania kutoka wapinzani ambao wamekuwa katika uwanja wa upinzani kabla yeye hajawaza/kufikiria kama kuna siku atakuja kuwa mpinzani wa serikali ya CCM.

Kinachoonekana kwa sasa Lowassa yuko katika safari ya kisiasa ambayo Augustino Mrema amepitia! Lowassa has gone from hero to zero! As a politician, he is finished. There is no way back for him.

Ni nani anamshauri Edward Lowassa? Mwacheni akachunge ng'ombe wake Monduli!
Wewe ni zaidi ya nyumbu tena nyumbu kipofu
 
Uliza duniani kote nini maana ya wafuasi halafu ukipata jibu utagundua.Wafuasi siku zote huwa wanasikiliza kiongozi wao anasema nini na ukiangalia hata kwenye history uprising zote zilitokea hivyo
Mkuu huyo unaye mjibu ni nyumbu lipo hapo linafuata upepo tu
 
Back
Top Bottom