Ni Muda muafaka sasa Tanzania tuwe na Senate "Bunge la mabwanyenye"

Huoni kama ni gharama? You can’t be serious!!

Hiyo tija unayoizungumzia inaweza kupatikana na muundo huu huu tulionao sasa!
Sio lazima iwe gharama. Kwani huwezi kupunguza idadi ya majimbo kwa zaidi ya nusu ili pia uwe na nusu nyingine ya wawakilishi ambao ni senators! Ni utashi tu na tamaduni! US wana House of representatives na Senate ambao kwa pamoja wanatengeneza Congress, na wameweza kubalance gharama. Hata kama sioni tija kwa sasa bado kuna uwezakano wa kutoka unicameral na kuwa bicameral kwa gharama zilezile.
 
Kenya wana senators, vipi unaweza kuwaita wale senators ni mabwanyenye?
Walianza kuwa elected 2013 baada ya mabadiliko ya katiba,

Kuna aina mbali mbali za useneta, wa kurithi, kuteuliwa ama kuchaguliwa,

Ila msingi wa neno senate umetoholewa ukimaanisha an assembly of the senior,

Being an upper chamber of the legislature members wake wanategemewa kuwa wiser than those from the lower house.

Vyovyote vile utavyowaita au itavyokua naona kuna umuhimu wakawepo.
 
Umeleta mjadala mzuri tu. Bunge la Tanzania libadilishwe sheria za namna ya kugombea.

1. Uwe na angalau accomplishments kadhaa kwenye jamii katika sekta yako. Sio unafyatuka uko kama Babu Tale unagombea.

2. Uwe na exposure na sekta flani walau moja na uwe expert uko. Musukuma anajua nini kwa mfano, muda mwingi anautumia kuchekesha sijawahi ona mchango wake mzito.

3. Uwe na uwezo wa kifedha kuanzia kiasi flani, yani usiwe na njaa. Sio unakuja kuwa kama Lijualikani mwanaume mzima na kende zako unalia mbele ya camera, alafu wewe ndio ulikuwa unatunga sheria bungeni.

Tukirekebisha mambo mengi na sheria bunge linajitosheleza. Senate kwa nchi za Kiafrika ni kutengeneza instability na kuzidisha usumbufu. Kama kule Congo DR kuna viongozi wa majimbo hawaguswi hata na serikali kuu.
Hahaha sasa hao wote umewataja wana sifa, Babu Tale yupo successful kwenye Music industry so atachangua Arts, Musukuma ni businessmam kwenye madini na usafirishaji, Juakali kasomea sheria (nadhani) which ndo field muhimu sana kwa mbunge kujua sheria
 
Kwa elimu yangu naona kabisa suala la unicameral na bicameral systems lipo kwenye mabadiliko makubwa ya kikatiba na sio hizi hadithi za sokoni! Ni suala la unitary system versus federalism, je tupo tayari kwa serikali zinazojitegemea za majimbo? Sio suala rahisi la kuwa na the so called 'bunge la mwabanyenye'. It is complicated.
 
Hahaha sasa hao wote umewataja wana sifa, Babu Tale yupo successful kwenye Music industry so atachangua Arts, Musukuma ni businessmam kwenye madini na usafirishaji, Juakali kasomea sheria (nadhani) which ndo field muhimu sana kwa mbunge kujua sheria
Sio hivyo! Jamaa hajui kuwa anacho suggest ni total system overhaul na sio hao individuals na ambitions zao. Mimi sio constitutional law expert lakini naona kabisa haya yatakuwa matakwa ya katiba nyingine kabisa.
 
We don’t need a bicameral legislature.

It’s wasteful spending.
How is that so? Just pick a couple of "seniors", knowledgable and the experienced amongst the incumbent MPs, and give them tools to be senators. It does not have to be like Kenyan or Nigerian style, let us have our own.

Kwa mfumo tulio nao sasa mtu yoyote anaweza kuingia bungeni kwa kigezo cha umri na elimu ya chini kwa kupigiwa kura na wanajimbo. Mtu huyo sio tu anakwenda kuwakilisha mambo ya wapiga kura wa jimbo lake, lakini pia anaenda kuwa sehemu ya maamuzi ya kisheria na hata mambo makubwa ya maswala yanayohusu taifa. Hii inatoa fursa ya mtu kupewa haki na nafasi ya kufanya maamuzi, lakini hajaandaliwa kielimu na kiujuzi kuwa na weledi ya kufanya hivyo. Baraza la mabwanyenye linaweza kuwa dawa.

If we do a cost benefit analysis of the current arrangement, it is possible to see that we may be saving money but losing more that that.
 
Ulichowaza ni sahihi kabisa coz tushaona mara nyingi maamuzi ya bunge kwa kiasi kikubwa ni kupendelea serekali hata kama ni maamuzi ya kuumiza nchi.
 
Nimewaza tu kwamba tunahitaji kuwa na mawazo mbadala ya bunge lililopo sasa,

Hata hivyo kwakua nchi nzima hatuna mikoa zaidi ya 35 bajeti yake nayo haitakua kubwa kwani maseneta hawatazidi idadi ya mikoa.
Kwa kuwa ni dhahiri bunge letu halina faida yoyote, labda bunge lolilopo lifanyiwe marekibisho kwa kuwa na uwakilishi wa kimkoa badala ya majimbo na, pamoja na majukumu yake ya sasa, liongezewe hayo majukumu ya ki-senate uliyoainisha.

Hii itasaidia kupunguza gharama kwa kuwa na bunge dogo.
 
Ulichowaza ni sahihi kabisa coz tushaona mara nyingi maamuzi ya bunge kwa kiasi kikubwa ni kupendelea serekali hata kama ni maamuzi ya kuumiza nchi.
I have sometimes wondered if we even need this institution. Kama ni kutunga sheria, sheria zinaandikwa na serikali wao wanapelekewa kupitisha. Kama ni bajeti, bajeti inaandaliwa na serikali wao wanakutana zaidi ya miezi miwili kuipitisha.

Afadhali tuwe na bunge dogo sana lenye wawakilishi wawili toka kila mkoa watakaofanya haya kwa gharama ndogo.
 
Nimewaza tu kwamba tunahitaji kuwa na mawazo mbadala ya bunge lililopo sasa,

Hata hivyo kwakua nchi nzima hatuna mikoa zaidi ya 35 bajeti yake nayo haitakua kubwa kwani maseneta hawatazidi idadi ya mikoa.
Nakubali bungee la mabwenyenye ila nakubali wajumbe wake,kwani tatizo la wabunge walio ni umaskini wanaproject nyingi za kuwaingizia pesa halali na zisizo halali,wajumbe 35 watanunulia wote.wajumbe wawe watu wenye investment zinazo fikiabilion 50 na wastaafu Maris nawenyeviti wa chama vyenye wabunge kadhaa walio maliza muda wao
 
Npaka sasa tunao Wabunge Mabwanyenye kadhaa wakiwemo Bashiru na Polepole
 
Hahaha sasa hao wote umewataja wana sifa, Babu Tale yupo successful kwenye Music industry so atachangua Arts, Musukuma ni businessmam kwenye madini na usafirishaji, Juakali kasomea sheria (nadhani) which ndo field muhimu sana kwa mbunge kujua sheria
Babu Tale mafanikio ya kukaribiana na Diamond na kuwa janjajanja ndio yatumike kuleta mawazo chanya bungeni?

Musukuma hana elimu, hizo biashara za madini wapo wenye elimu ndogo kabisa wamefanikiwa uko kama Mzee Layzer hatuwezi kuwaleta bungeni. Hawawezi kutunga sheria wala kujadili hoja ya msingi. Ndio maana anachoweza Musukuma bungeni ni kuchekesha.

Lijualikali kasoma sheria ila hana career yeyote. Kadumu kuwa mwanasheria kwa muda gani, wapi na kashiriki kesi ngapi. Hana accomplishment muhimu ukiachana na degree yake.

Elimu, successful career, uwezo wa mtu binafsi na kipato lazima vizingatiwe. Sasa bunge likijaa vilaza, watu hoehae hata kodi hawajawahi lipa, ukiachana na degree hana kazi aliwahi fanya. Hapo mtegemee maajabu gani.
 
Mataga mnataka serikali za majimbo kama Marekani??
Nimewaza tu kwamba tunahitaji kuwa na mawazo mbadala ya bunge lililopo sasa,

Hata hivyo kwakua nchi nzima hatuna mikoa zaidi ya 35 bajeti yake nayo haitakua kubwa kwani maseneta hawatazidi idadi ya mikoa.
 
Kwa mfumo wa nchi nyingine huko wanaingia elites tu ambao watakua wanachuja maazimio ya Bunge la kawaida na kuyaboresha ili maamuzi yatayotoka yanakua bora zaidi.
Ndio mkuu huwezi kumkuta dogo graduate hana hata chumba cha kupanga eti anapewa mamlaka ya kutunga sheria za nchi.
Pale US mwanasheria akiwa mwanasiasa unakuta kawa Prosecutor wa jimbo kwa miaka kadhaa au kahudumu kampuni kubwa ya sheria na kuna kesi za kusisimua zilimfanya ajulikane uwezo wake. Mtu kama McCain alishiriki vitani Vietnam, ni veteran aliyekuwa anajua sana jeshi na alitumika mno kwenye Defense Budget. Bloomberg huyu billionaire na media tycoon atasaidia kujadili uwekezaji, kodi, regulations na mengine.

Mle ndani wote wana elimu na exposure, wako screened hakuna mkwepa kodi wala mwenye skendo. Sisi uku tuna wabunge wanakamatwa kwenye ujangili kesi hazisikilizwi mpaka leo.
 
Wingu la siasa za nchi yetu limechafuka kwa mijadala mbali mbali kuhusiana na maswala muhimu ya kitaifa yaliyoibuliwa na ripoti ya CAG pamoja na comments za wadau mbali mbali kuhusiana na ripoti hiyo.

Ripoti hiyo imegusia unaosemekana ni ufisadi uliotokana na mambo yanayohusiana na mikataba iliyopelekea ujenzi wa miradi ya maendeleo na ununuzi wa mali mbali mbali.

Kwa nyakati tofauti viongozi mbali mbali wa mihimili ya dola na vyama vya upinzani wametoa maoni yao kuhusiana na ripoti hiyo pamoja na maswala mengine ya kitaifa.

Maoni hayo yamepelekea kuibuka kwa mijadala mizito ambayo kwa ufupi nimeona suluhisho lake ni kuwa na Senate au Bunge la Mabwanyeye ambalo litasaidia kupunguza lawama lukuki inazotupiwa serikali na viongozi wakuu wa nchi.

Senate ni Bunge la juu ambalo wawakilishi wake hutokana na mikoa na sio majimbo ya uchaguzi.

Bunge hili huwa na majukumu yaliyogawanyika katika sehemu kuu tatu.

1. Kuidhinisha au kutoidhinisha mikataba iliyoingiwa na Rais kwa niaba ya Nchi.

2. Kuidhinisha au kutoidhinisha wateule wa Rais.

3. Kufanya uchunguzi na kutoa adhabu kwa viongozi wa serikali ambao wamefanya makosa mbali mbali dhidi ya nchi.

Mara nyingi senate hutumika kama mhuri kwa maamuzi yaliyofanyika na bunge la kawaida, na pia hupewa hadhi ya kikao cha bunge kinachochuja na kutolea maamuzi maazimio ya bunge kawaida.

Ukiangalia mambo yanayotajwa kama mapungufu katika ripoti ya CAG utaona kwamba kuna umuhimu wa kuwa na bunge hili ambalo litakua likichuja maazimio ya bunge la kawaida, kupitia tena miswada ya sheria, kupitia tena bajeti za wizara mbali mbali na kutoa ushauri kwa Rais.

Aidha lingekuwa jambo la heri kwa Taifa letu kama tungeweka sifa za kielimu ambazo zitawafanya maseneta kuwa na ubobevu katika maeneo flani ili kutoa michango na maamuzi yenye tija kwa Taifa.

Mfumo huu wa Bunge la Senate unatumika na nchi takriban 64 hapa Duniani na naimani kwamba kama tukiutumia utatusaidia sana na kupunguza lawama kwa serikali na viongozi wa kitaifa.
Walioshika mpini wa kisu hawatakubaliana nawe, kumbuka yule mstaafu aliyeshauri matokeo ya uchaguzi yahesabiwe hadharani baada ya kuonja joto ya jiwe ya aliyemwachia kiti
 
Walioshika mpini wa kisu hawatakubaliana nawe, kumbuka yule mstaafu aliyeshauri matokeo ya uchaguzi yahesabiwe hadharani baada ya kuonja joto ya jiwe ya aliyemwachia kiti
Tukiamua itawezekana.
 
Kwa kuwa ni dhahiri bunge letu halina faida yoyote, labda bunge lolilopo lifanyiwe marekibisho kwa kuwa na uwakilishi wa kimkoa badala ya majimbo na, pamoja na majukumu yake ya sasa, liongezewe hayo majukumu ya ki-senate uliyoainisha.

Hii itasaidia kupunguza gharama kwa kuwa na bunge dogo.
Kuwa na bunge effective ni muhimu.
 
Back
Top Bottom