Ni muda gani, ambao ni sahihi, kwa mfiwa kuoa/kuolewa na mtu mwingine?

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,403
40,331
Aliyefiwa na mke au mume; ni baada ya muda gani ndio anaruhusiwa kuoa/kuolewa?

Maisha ya ndoa huwa ni matamu sana, hasa kwa wale wachache waliobahatisha kupata mtu sahihi.

Inafikia kipindi, wanakuwa na mfanano fulani; unaweza kuwa wa sura, kuongea, au tabia.

Inapotokea mmoja wapo anafariki, inakuwa ni pigo kubwa sana kwa aliyebaki. Inaweza kuchukua muda mrefu kuwa katika hali ya majonzi, huku akikumbukia namna walivyoishi na mwenzake.

Mnavyojua tena; kuwa na majonzi muda wote inakuwa haifai; kwa sababu aliyeondoka ameshaondoka, na hawezi kurudi tena; na maisha yanatakiwa yaendelee.

Ndipo pale, hitaji la kuziba pengo hutokea.

Sasa wakuu, nauliza; ni muda gani ambao ni sahihi, kwa mfiwa kuoa/kuolewa na mtu mwingine?
 
Aliyefiwa na mke au mume; ni baada ya muda gani ndio anaruhusiwa kuoa/kuolewa?

Maisha ya ndoa huwa ni matamu sana, hasa kwa wale wachache waliobahatisha kupata mtu sahihi.

Inafikia kipindi, wanakuwa na mfanano fulani; unaweza kuwa wa sura, kuongea, au tabia.

Inapotokea mmoja wapo anafariki, inakuwa ni pigo kubwa sana kwa aliyebaki. Inaweza kuchukua muda mrefu kuwa katika hali ya majonzi, huku akikumbukia namna walivyoishi na mwenzake.

Mnavyojua tena; kuwa na majonzi muda wote inakuwa haifai; kwa sababu aliyeondoka ameshaondoka, na hawezi kurudi tena; na maisha yanatakiwa yaendelee.

Ndipo pale, hitaji la kuziba pengo hutokea.

Sasa wakuu, nauliza; ni muda gani ambao ni sahihi, kwa mfiwa kuoa/kuolewa na mtu mwingine?
Hiiii nafikiri inatofautiana kulingana na mila na desturi ya kabila husika
 
Kwa wanamke baada ya eda kuisha ila kwa mwanaume watu wakishainua matanga unaweka mtoto mzuri ndani.

Kwa jinsi ulivyo malizia koment yako,Nadhani bado hujaoa .

Na kama umeshaoa basi una tatizo na ndoa yako.

Kuondokewa na mwenzi ni jambo zito sana hasa kwa yule mliyependana kwa dhati.

Haiwezi kuwa rahisi hivyo
 
Kwa jinsi ulivyo malizia koment yako,Nadhani bado hujaoa .Na kama umeshaoa basi una tatizo na ndoa yako.Kuondokewa na mwenzi ni jambo zito sana hasa kwa yule mliyependana kwa dhati.Haiwezi kuwa rahisi hivyo
Kweli mkuu, wapo wengine hawaoi wala kuolewa tena
 
Hili suala hua nahisi ni mapendeleo ya mtu. Lakini kifo cha mwenza sio jambo dogo kabisa.

Asilimia kubwa hua wanachukua muda kidogo mpaka wawe sawa kisaikolojia.

Na pia inategemeana kama kuna watoto hapo katikati. Maana kama wapo, hiyo transition hua sio ya muda mfupi kiasi hicho.

Mwisho wa siku inategemeana ntu na ntu lakini hua sio jambo la kukurupuka tu.
 
Inategemea saana na upendo uliokuwa nao na "mwendazake", kuna wanaoamua kutokuwa na mume/mke mpk mwsho wa maisha yao.

Na pia itategemea na umr alioachwa nao mgane/mjane, wengne wamefiwa baada tu ya kuingia ndoani.

Wengne wamekuwa wagane/wajane wakiwa wazee kabsa, sasa hapa anaweza aoe/aolewe am kinyume chake.


Lakn yote kwa yote inategemea na upendo uliyokuwa baina ya "mwendazake" na mfiwa......

Mfano:- Baba yangu alikaa miaka 6 ndyo akaja kuoa tena, yangu n hayo.
 
Kwa mtazamo wako, unafikiri ilitakiwa ichukuwe muda gani?
Pale ambapo muhusika ataona inafaaa baas,

Maana iii ishu imekaaa kibinafsi saana tuaeza sema mwaka ye akona mbali tuaeza sema miez miwilii kumbe ye ndan ya mwezi mmoja anataka kumiliki ya kwakeee peke yake akigeuka anaikutaaa,nafikiri imekaaa kibinafsi saaana
 
Back
Top Bottom