Ni makosa makubwa kushinikiza Serikali - Dk Benson Bana

Dr bana badilika ndugu, Hivi wewe Udaktari wako ni wa nini, unatumia macho na masikio gani? Nani amekupa kazi ya kutetea serikali wewe? unalipwa shillingi ngapi? je Una ndungu maskini huko vijijini? Tafakari na chukua hatua
 
huyu Bana huenda ni "msomi" lakini siyo "mtaalamu" wa mambo ya siasa. Hajui kuwa chimbuko la demokrasi ni kushinikizana; shinikizo la wengi ndilo linalotekelezwa. Inawezekana anazungumzia siasa za Tanzania ambapo hakuna demokrasia, lakini katika nchi zenye demokrasi mambo ya siasa yanakwenda kwa kushikizana kila siku. Mdiyo maana kwa Marekani kuna interest groups zinazoshinikiza wabunge na serikali kuhusu sera wanazotaka wao hadi wanafanikiwa kuzipata.
 
Kwa kawaida huwa sitoi maoni yangu kwa kila anachokisema huyu "msomi dr" Bana kwa kuwa sijawahi kumsikia akitoa maoni yeyote yanayo-justify hata kidogo kuwa nae ni msomi. Lakini hii ya leo imenikumbusha thread ya mjumbe mmoja hapa ukumbini aliehoji elimu yetu na jinsi watu wanavyopanda vyeo nchini kwetu.

Kusema ukweli lazima kuna uwalakini na mfumo mzima wa maisha yetu kwa ujumla (elimu, namna ya kupata viongozi, kupandisha watu vyeo and all that), otherwise iweje Bana akawa na PhD halafu akawa anatoa utumbo kila siku? Sitarajii mtu awe anatoa maoni yanayokubalika na wote siku zote, lakini kutoa utumbo tu kila siku???


I can't even begin to understand this situation of ours!!!!!!
Mtoboasiri.

Ndugu Kiranga ndiye aliyezungumzia hilo suala


Kuhusu wasomi wa aina ya Bana, njaa mkuu wangu ndiyo inawafanya wawe hivyo. Yaani jamaa ana njaa kiasi kwamba elimu aliyoipata haijamwelimisha. Nakumbuka kuna profesa mmoja alikuwa anawaita wasomi kama Bana walamba miguu ya wakubwa.

Bana ni mfano wa wasomi wengi hapa Tanzania na nchi nyingi za Afrika; wasomi wanaojipendekeza kwenye utawala, hususani viongozi wa utawala huo ili nao wanufaike na tawala hizo. Wasomi hao wamejazana kuanzia kwenye vyuo vikuu, bungeni hadi kwenye taasisi na idara za serikali. Wasomi ambao hawana guts za kusema ukweli wa mambo, kisa wanaogopa vitumbua vyao visiingie mchanga. Mkuu kwani huwaoni maprofesa walivyojazana bungeni? Impact yao ni nini zaidi ya kupiga meza tu?! Kwenye wizara, watendaji wakuu wengi wa wizara ni wasomi wazuri tu, tena wengine ni maprofesa, lakini angalia madudu. Mfano, katibu mkuu wa wizara ya elimu ni profesa, lakini angalia elimu yetu inavyoshuka!!

Hivi unafikiri Bana akaanza kuongea ukweli wa mambo ulivyo, akanyimwa mkataba muda wake ukiisha, chuo gani kitamwajiri? Kwa namna alivyoaanza kujipendekeza kwa utawala wa CCM, pona yake ni kuendelea kujipendekeza mpaka pale siku zake zitakapofika. Namhurumia. Hamwoni mwenzake Baregu, toka awali alikuwa akisema mbivu ni mbivu na mbichi ni mbichi, walipomchinjia baharini, akapata chuo kingine haraka tu, kwa sababu alionekana ni msomi aliyeelimika kweli kweli.
 
Last edited by a moderator:
Dr bana badilika ndugu, Hivi wewe Udaktari wako ni wa nini, unatumia macho na masikio gani? Nani amekupa kazi ya kutetea serikali wewe? unalipwa shillingi ngapi? je Una ndungu maskini huko vijijini? Tafakari na chukua hatua

Nje ya mada kidogo. oche, wewe ni mkaree..yaani toka mwaka 2008, hiyo ndiyo post yako ya kwanza?!
 
Last edited by a moderator:
gamba at work!!!

Kama wewe unasoma uhuru na unamsikiliza huyo msomi mfu, kwetu sisi tulio na fikra hai tunaina kama unaongea kutoka kuzimu.
 
hata mie nadhani amechamsha, nchi nyingi zilizo endelea na zinazo endelea viongozi wake waadilifu hujiuzulu kwa mashinikizo!!
.......tuseme tuseme serekali yetu ni kama ya YEMEN, hata hata wa dai ulipie pumzi...., hutaweza kuwatoa walipo

aaaaaaaa DOCKTA
 
ni aibu kwa elimu ya tanzania, ni aibu kwa chuo kikuu kuwa na msomi of this kind. inawezekana watanzania kwa mifumo yetu ya elimu maswala yasiyo na madesa ndiyo majibu yetu. labda kuna kosa la mwandishi maana haya ni maneno mtu anaongea na mwandishi anachagua ya kuandika. kazi ya bunge ni nini?kama siyo kusimamia serikali
 
ni aibu kwa elimu ya tanzania, ni aibu kwa chuo kikuu kuwa na msomi of this kind. inawezekana watanzania kwa mifumo yetu ya elimu maswala yasiyo na madesa ndiyo majibu yetu. labda kuna kosa la mwandishi maana haya ni maneno mtu anaongea na mwandishi anachagua ya kuandika. kazi ya bunge ni nini?kama siyo kusimamia serikali



mwacheni mwana BANA ASEME KABLA YA HESHIMAYAKE KUFUTIKA KABISA KATIKA NYANJA ZA TANZANIA 2015, ATAONA AIBU PAMOJA NA WASOMI THE LIKES WENGI WAKO HAPO..........................
 
aisee huyu Bana ni MCCM au MTanzania?? anafikiria atakula wapi... amweleze hayo mambo Nape na wazee sisi vijana ni mwendo wa Jino kwa Jino ... kila siku tunalaumiwa watanzania hatuko aggressive sasa tumebadilika... tunao.. hakuna cha Bana wala legeza hapa...
 
Msomi kutoka chuo kikuu cha DSM Dk Benson Bana amesema ni makosa makubwa serikali kuongozwa kwa mashinikizo.Dk Bana alikuwa akirejea shinikizo la kuwawajibisha mawaziri mafisadi na wazembe lililotolewa na bunge katika kikao kilichoisha jumatatu wiki hii.Dk Bana ameonyesha kukerwa na kitendo hicho kwani ni kutaka kuyumbisha serikali.

Source:Uhuru Jumatano
Huyu Mr. Benson Bana ataendelea kuishi kwa kujipendekeza kwa viongozi mpaka lini? Eti anajiita Doctor, doctor gani ambaye hawezi hata kutambua kuwa kama hutaki kuwajibika unawajibishwa? Ananitia kichefuchefu huyu doctor uchwara!!!!
 
Msomi kutoka chuo kikuu cha DSM Dk Benson Bana amesema ni makosa makubwa serikali kuongozwa kwa mashinikizo.Dk Bana alikuwa akirejea shinikizo la kuwawajibisha mawaziri mafisadi na wazembe lililotolewa na bunge katika kikao kilichoisha jumatatu wiki hii.Dk Bana ameonyesha kukerwa na kitendo hicho kwani ni kutaka kuyumbisha serikali. Source:Uhuru Jumatano
Huyu DR. BANA anasumbuliwa na matatizo ya kutokujua na kuamini kuwa MAFISADI hawatakiwi ktk nchi hii. Ila huyu Mzee ni KILAZA kweliiii; Kama SIO wananchi (pamoja na wananchi ambao ni viongozi wa kisiasa wazalendo) kuwabana viongozi wezi na mafisadi ni NANI HUYO ATAKAYEWEZA KUWASHUGHULIKIA HAO WEZI WALIOKUBUHU....?? BANA be serious, otherwise unaendelea kuleta tafrani mioyoni mwetu.
 
Msomi kutoka chuo kikuu cha DSM Dk Benson Bana amesema ni makosa makubwa serikali kuongozwa kwa mashinikizo.Dk Bana alikuwa akirejea shinikizo la kuwawajibisha mawaziri mafisadi na wazembe lililotolewa na bunge katika kikao kilichoisha jumatatu wiki hii.Dk Bana ameonyesha kukerwa na kitendo hicho kwani ni kutaka kuyumbisha serikali.

Source:Uhuru Jumatano
Kama kuna wasomi nchi hii nimewafuta kwenye data base yangu hata wakizungumza chochote sioni umuhimu wake kwangu na kwa taifa wakwanza ni huyu dr Bana, usomi wake utabaki kwenye vyeti lakini kiutendaji huyo ni zero hana maana kwenye taifa letu, sijui anatafauta uwaziri (vyeo vya kupewa) au?
 
Mzee huyu anafaidika sana na UFISADI na kama namuonea aje akanushe hapa. Ni Dr. Ambaye uwezo wake wa kufikiri umechuja.

Amekula sana hela ya mafisadi kupitia REDET na leo anaona serikali ikianguka naye atachunguzwa. Only that.

View attachment 52635

Naona hapo mhasibu mkuu aliamua kujilipa nyingi zaidi kuliko wengine wote serikalini. Madudu haya kama ingekuwa kwa wenzetu wazungu, mbona wahusika wangejuta kwa nini walizaliwa na kuwa watumishi wa umma. lakini kwetu bongo akhaaaaaaa, maisha yanaenda tu kama kawaida.

Hivi jamani tujiulize. Hivi kweli mkuu wa kaya hafaidiki kweli na huu wizi? Inawezekana kweli mtu aliyeapa kuitumikia nchi kwa uadilifu anakaa kimya kwa madudu kama haya?
 
njaa mbaya wakuu na njaa siku zote hudhalilisha.
bana kinachomsumbua ni njaa tena ya wazi.
 
Jamani huyu Dr Banna alipewa huu udokta kama kiongozi wa magamba au aliukeshea kabisa huo udokta wake....nway tutafika tu!

Hawa ndoi yanao ishauri CCM na kujenga hisia za woga kwa umma.Mtu kama huyu ni wa kumpuuza na kmbeza. by the way makada wa CCM pale political science dept UDSM wapo kibao! SHAME ON HIM!:shetani:
 
huyu Bana huenda ni "msomi" lakini siyo "mtaalamu" wa mambo ya siasa. Hajui kuwa chimbuko la demokrasi ni kushinikizana; shinikizo la wengi ndilo linalotekelezwa. Inawezekana anazungumzia siasa za Tanzania ambapo hakuna demokrasia, lakini katika nchi zenye demokrasi mambo ya siasa yanakwenda kwa kushikizana kila siku. Mdiyo maana kwa Marekani kuna interest groups zinazoshinikiza wabunge na serikali kuhusu sera wanazotaka wao hadi wanafanikiwa kuzipata.

anayajua yote hayo tena vizuri sana ila tatizo hapa si elimu ama ufahamu ni njaa na kutetea maslai
 
Back
Top Bottom