Ni lini Rais Magufuli amerasimisha kazi za Halmashauri kwenda Serikali Kuu?

Mimi nikisoma BIBLIA naona manabii na mitume walifanya kazi ya kuwaonya na kuwashauri wafalme na watawala.Wachungaji kazi yao kulilisha ,kulitunza na kuliangalia kundi la Mungu lililo chini yao.Kwa kuwa wakati huu hakuna tena manabii na mitume(kwa mujibu wa Biblia);ni kazi ya wachungaji na wainjilisti kuwashauri na kuwaonya watawala pale wanapoonekana kwenda tofauti na maadili na miiko ya uongozi na kuvunja katiba.Chakushangaza wachungazi(maaskofu) ndio wamekuwa mawakala wa wanasiasa jambo ambalo linawafanya wapiteze sifa ya kuwa mdomo wa Mungu.Ni aibu kwa wakili wa Mungu kujidharau kiasi chakujifanya dalali wa siasa.Si vibaya kiongozu wa siasa kutembelea nyumba yoyote ya ibada,naye ji kondoo kama wengine,alishwe,afundishwe na kuelekezwa maadili mema.Kazi ya kila siku ni kuwaombea.(1timotheo2:1-3;
 
Cha muhimu barabara inajengwa TanZania, fedha inachukuliwa wapi haijalishi kuna wengi sana wanaochukuwa fedha zetu na kuzipeleka kwenye akaunti zao Uswisi hivyo ni bora mara milioni 10 kwa Raisi Magufuli anayechukuwa fedha na kuziwekeza kuwasaidia Wananchi kwani hiyo br. siyo ya Raisi Magufuli na familia yake bali ni ya WatanZania wote na hiyo ndiyo tofauti ya Magufuli na fisadi Lowasa, Yeye (fisadi Lowasa) alihamisha fedha zetu na kuzipeleka Ulaya kununua majumba london na kwingineko lkn Raisi Magufuli anachukuwa fedha zetu na kuwekeza kwenye Mundo mbinu kwa ajili yetu!

Hivyo hilo swali lako ulipaswa umuulize fisadi Lowasa ni nani alimpa Mamlaka ya kuchukuwa fedha zetu na kupeleka London kumnunulia nyumba takataka zake!
Kwa watu wasiofikiri sawa sawa wewe unaweza kuonekana mtu wa maana sana, lakini sidhani kama sisi watanzania, pamoja na mapungufu yetu, tunaweza kuwa watu wa kiwango hicho cha kufikiri! Kumbe kama unashauri au unaona ni halali rais aingilie kila mara matumizi ya fedha kwenye halmashauri kuna maana gani ya kuwa na mgawanyo wa madaraka? Madiwani ambao tunawachagua sawa na tunavyomchagua rais wawe na kazi gani sasa? Najua umechangia "kinazi" ndio maana umeweka katika andiko lako hata watu wasiohusika na hoja hii, lakini hebu jaribu kufikiri vizuri kama jambo hilo linakubalika!
 
Leo nimemsikia Rais Magufuli akitoa ahadi ya kutengeneza kipande cha barabara konachotoka maeneo ya river side kwenda kwa mzee wa upako. Kimsingi kabisa hiyo ni kazi ya manispaa ya Kinondoni.

Lakini leo nimemsikia Zitto akisema kuwa Rais Magufuli amekwapua mapato ya majiji kwenda serikali kuu. Huu hasa ndiyo udhaifu tena mkubwa.

Kama rais wa nchi atahangaika na vitu vidogo dogo kama hivyo ni lini atalielewa taifa? Eti nimekuja ili nijionee! Kweli?

Kimsingi kwa sisi tunaomwelewa mzee wa upako, rais Magufuli kaenda kulipa fadhila kwa aliyotendewa (kwenye mabano) Sisi tunataka rais aelewe ni kipi anapaswa kufanya kama rais! Bajeti ya kujenga barabara ya Kibangu ambayo anasema fedha zipo ilipitishwa na nani? (Kupoka madaraka ya mihimili kunaendelea) Hili jambo baadhi yetu linatukera kwelikweli!
Bora tu afanye hivyo maana hamna namna. Halmashauri zimelalia pesa hatuoni maendeleo, safi sana Mh. Magufukli wakati wanasiasa huko chini wanalumbana wewe twende kazi. Kwanza ushauri kama ile awamu ya Tatu ilopvinjilia mbali Halmashauri DSM Mh. Magufuli fanya hivyohiovyo tumechoka siasa tunataka maenmdeleo!
 
Kwa watu wasiofikiri sawa sawa wewe unaweza kuonekana mtu wa maana sana, lakini sidhani kama sisi watanzania, pamoja na mapungufu yetu, tunaweza kuwa watu wa kiwango hicho cha kufikiri! Kumbe kama unashauri au unaona ni halali rais aingilie kila mara matumizi ya fedha kwenye halmashauri kuna maana gani ya kuwa na mgawanyo wa madaraka? Madiwani ambao tunawachagua sawa na tunavyomchagua rais wawe na kazi gani sasa? Najua umechangia "kinazi" ndio maana umeweka katika andiko lako hata watu wasiohusika na hoja hii, lakini hebu jaribu kufikiri vizuri kama jambo hilo linakubalika!


Hiyo siyo ishu, ishu hapa ni Je, Raisi kavunja Katiba ya nchi kwa huwo uamuzi au la?
 
Kama rais mwenyewe ndio anafanya allocation ya pesa bunge lina kazi gani?
Kama walikuwa wababaishaji sisi tunachotaka maendeleoa. Wacha wanasiasa wapige kelele zao sisi tunasonmga mbele!
 
Leo nimemsikia Rais Magufuli akitoa ahadi ya kutengeneza kipande cha barabara konachotoka maeneo ya river side kwenda kwa mzee wa upako. Kimsingi kabisa hiyo ni kazi ya manispaa ya Kinondoni.

Lakini leo nimemsikia Zitto akisema kuwa Rais Magufuli amekwapua mapato ya majiji kwenda serikali kuu. Huu hasa ndiyo udhaifu tena mkubwa.

Kama rais wa nchi atahangaika na vitu vidogo dogo kama hivyo ni lini atalielewa taifa? Eti nimekuja ili nijionee! Kweli?

Kimsingi kwa sisi tunaomwelewa mzee wa upako, rais Magufuli kaenda kulipa fadhila kwa aliyotendewa (kwenye mabano) Sisi tunataka rais aelewe ni kipi anapaswa kufanya kama rais! Bajeti ya kujenga barabara ya Kibangu ambayo anasema fedha zipo ilipitishwa na nani? (Kupoka madaraka ya mihimili kunaendelea) Hili jambo baadhi yetu linatukera kwelikweli!

Rais ni Rais. Kachaguliwa na watu wote awaongoze kwa maslahi ya taifa siyo Zitto aliyechaguliwa kuwakilisha kikundi au kona au kabila watu wachache. Hawa wanaompa mipaka wamechanganyikiwa, wakasome Government Orders. Wanajitia watetezi wa wananchi lakini wananchi hawohawo wote ndiyo waliomchagua kuwatetea. WM
 
"... tunataka Rais wa Maamuzi magumu...",
"..Huyu Rais ndio mrithi sahihi wa Hayati Baba wa Taifa"
Rais mstaafu Kikwete anakumbukwa zaid na waliokuwa wapinzani wake kuliko Rafiki zake.
Mpaka sasa kafanya maamuzi yapi magumu ya kuletea taifa faida? Sukari? Lugumi? UDOM? naomba maelezo ya kina kutetea hoja yako.
 
Kuna sheria inayomkataza rais kujenga barabara iliyo kwenye manispaa?
Kazi ya rais si kujenga barabara, rais Hana hela yake bianafsi ya kujengea barabar bali Kuna hela ya uma abayo matumizi yake hufanywa kilingana na bajeti iliyopitishwa na wawakilishi wa wananchi, yani wabunge na madiwani
 
Hiyo siyo ishu, ishu hapa ni Je, Raisi kavunja Katiba ya nchi kwa huwo uamuzi au la?
Rafiki yangu Barbarosa nani alikwambia katiba ni Biblia au Quran? Kuna kitu kinaitwa hekima ambacho kinazidi nguvu hicho unachokiita katiba. Lakini najua unakumbuka pia maneno ya Mwalimu JK Nyerere (mwenyezi Mungu amrehemu huko aliko) ambaye alitahadharisha kwamba kwa katiba yetu hii tukiwa na rais dikteta anaweza kuliangamiza taifa hili. Sasa ni vizuri kuelewa kwamba rais mwenye hekima hawezi kufanya kila jambo linalomruhusu kikatiba hata kama lina 'ladha' na matokeo yanayochefua wengi!

Najua (kwa andiko lako) wewe ni mfuasi mwaminifu wa chama chetu au siasa za mkuu wetu, lakini kusapoti mwenendo huu ni kuwa sehemu ya watu wasiolitakia mema taifa hili. Tukiacha leo kuheshimu mgawanyo wa madaraka kwa sababu tu sisi tumekalia kiti cha enzi, je tutaweza kuvumilia wengine wakitenda hivyo hivyo sisi tutakapokuwa hatuko tena kwenye kiti hicho cha enzi?
 
Mpaka sasa kafanya maamuzi yapi magumu ya kuletea taifa faida? Sukari? Lugumi? UDOM? naomba maelezo ya kina kutetea hoja yako.

1) Kafukuza vilaza UDOM
2) Kamchana Jk hadharani
3) Kazoa uchafu ferry kwa mikono yake Independent day
4) Kaapa kupambana na Waagizaji wa sukari now
5) Kaenda kuahidi ujenzi wa Barabara kanisani
6) No Bunge Live
7) Kipeperushi cha Mawio kimefutwa ( sio kufungiwa)
8) Kaamuru Polisi kuiba tairi za Magari kwa wenye trafick case za BRT.
9) Kapiga Marufuku kusema fedha hazitoshi Wizarani.
10) ......
Hayo ni Trailer picha kamili linakuja baada ya kupita Bajeti 2016/17
 
Wacha barabara itiwe lami wananchi wa eneo la Kibangu tumeteseka kwa muda mrefu sana,Mungu amesikia kilio chetu kupitia nabii Lusekelo.
 
Shida ya wanadamu wanaoishi Tanzania ni ushabiki wa kijinga. Kaondoka wa ziara za nje sasa kaja wa ziara za ndani, yeye za kwake za kushtukiza. Wasi wasi wangu ni lini na saa ngapi anapata nafasi ya kufikiri juu ya masuala mazito ya taifa letu. Mwanzoni kwa ujinga wangu nilidhani rais kazi yake ni mikakati ya kiuchumi kwanza, kumbe ni ziara za kushtukiza.
 
Rafiki yangu Barbarosa nani alikwambia katiba ni Biblia au Quran? Kuna kitu kinaitwa hekima ambacho kinazidi nguvu hicho unachokiita katiba. Lakini najua unakumbuka pia maneno ya Mwalimu JK Nyerere (mwenyezi Mungu amrehemu huko aliko) ambaye alitahadharisha kwamba kwa katiba yetu hii tukiwa na rais dikteta anaweza kuliangamiza taifa hili. Sasa ni vizuri kuelewa kwamba rais mwenye hekima hawezi kufanya kila jambo linalomruhusu kikatiba hata kama lina 'ladha' na matokeo yanayochefua wengi!

Najua (kwa andiko lako) wewe ni mfuasi mwaminifu wa chama chetu au siasa za mkuu wetu, lakini kusapoti mwenendo huu ni kuwa sehemu ya watu wasiolitakia mema taifa hili. Tukiacha leo kuheshimu mgawanyo wa madaraka kwa sababu tu sisi tumekalia kiti cha enzi, je tutaweza kuvumilia wengine wakitenda hivyo hivyo sisi tutakapokuwa hatuko tena kwenye kiti hicho cha enzi?


Kwanza ni vizuri kwamba umekiri ingawaje siyo moja kwa moja kwamba Raisi wa JMTZ hajavunja Katiba ya JMTZ kwa maamuzi yake hilo ndiyo muhimu klk yote, hivyo uamuzi wake uko ndani ya Mamlaka aliyo nayo Kikatiba kama raisi wa JMTZ!

Sasa baada ya hapo hayo mengine yote siyo muhimu, kwa maana kama unataka tuanze kusema ni Raisi yupi alitumia madaraka yake makubwa kwa maamuzi ambayo mengine yameligharimu Taifa basi Raisi Magufuli hajafikia hata 1/64 ya Mlm.Nyerere, kuanzia vita ya Biafra ambapo Mlm. Nyerere alituma watu wetu vitani na waliuliwa bila ya sababu yoyote ile ya msingi hatuna uhusiano wowote ule na Nigeria na uwepo wa Nigeria haukuhatarisha nchi yetu yoyote kwa chochote kile, mpaka vita ya Uganda, kuja kwenye vijiji vya ujamaa ambavyo ambapo Mlm.Nyerere kwa kutumia madaraka makubwa ya Uraisi alihamisha watu kwa nguvu hasa watu wa Kusini (Kusini mwa Mkoa wa Dar/Pwani) bila ya kufanya maandalizi yoyote yale kule alikokuwa anawahamishia watu hali iliyopeleka watu kuliwa na Simba, kuumwa na nyoka na matatizo mengine sana hivyo wewe kumnukuu hapa Mlm.Nyerere kwamba yeye ndiyo alikuwa mtumiaji mzuri wa Mamlaka makubwa ya Uraisi aliyopewa Kikatiba siyo kuwa fair kwa Raisi Magufuli kwa maana Raisi Magufuli mpaka sasa hivi maamuzi yake yote aliyoyatoa kwa kutumia madaraka yake makubwa aliyo nayo Kikatiba yamejikita kwenye kuboresha maisha ya Watanzania walio masikini na nitaorodhesha kuhamisha fedha za Bunge kununua Madawati, kuhamisha fedha za starehe kununua vitanda Hospitalini leo hii Wagonjwa hawalali chini kwa Muhimbili, kuhamisha Wafanyakzi ktk kwenye jengo la Muhimbili na kupisha wamama wazazi waliokuwa hawana vitanda na kuishi kwenye mazingira machafu, kuhamisha fedha za starehe ya Uhuru kujenga br. ya Moroko-Mwenge ili kumpunguzia mwananchi adha ya kukaa br. kwenye foleni, na mengineyo hivyo Magufuli anatumia madaraka yake makubwa aliyo nayo lkn kwa mazuri yetu!
 
Barbarossa MKUU acha tabia chafu ya kusema MTU una ushahidi gani kuwa Lowassa amefanya hivyo usemavyo? Usipende kujifanya unajua sana sasa hivi kuna sheria ya mitandaoni usije ukajikuta keko au segerea Na hao unaotaka wakusifu watakucheka
Mkuu mwembemdogo,wala huna haja ya kumkanya kiongozi wa team vilaza wa LB 7 huyo,kwani anafahamu vyema kuwa Lowassa ana hekima, busara, werevu na hofu ya Mungu,hivyo hawezi kuhangaishwa na vitu vidogo kama hivyo. Ndio maana kutwa kuchwa yeye ni kumtaja tu Lowassa.
 
1) Kafukuza vilaza UDOM
2) Kamchana Jk hadharani
3) Kazoa uchafu ferry kwa mikono yake Independent day
4) Kaapa kupambana na Waagizaji wa sukari now
5) Kaenda kuahidi ujenzi wa Barabara kanisani
6) No Bunge Live
7) Kipeperushi cha Mawio kimefutwa ( sio kufungiwa)
8) Kaamuru Polisi kuiba tairi za Magari kwa wenye trafick case za BRT.
9) Kapiga Marufuku kusema fedha hazitoshi Wizarani.
10) ......
Hayo ni Trailer picha kamili linakuja baada ya kupita Bajeti 2016/17
Nakuonea huruma ujui ulisemalo.
 
1) Kafukuza vilaza UDOM
2) Kamchana Jk hadharani
3) Kazoa uchafu ferry kwa mikono yake Independent day
4) Kaapa kupambana na Waagizaji wa sukari now
5) Kaenda kuahidi ujenzi wa Barabara kanisani
6) No Bunge Live
7) Kipeperushi cha Mawio kimefutwa ( sio kufungiwa)
8) Kaamuru Polisi kuiba tairi za Magari kwa wenye trafick case za BRT.
9) Kapiga Marufuku kusema fedha hazitoshi Wizarani.
10) ......
Hayo ni Trailer picha kamili linakuja baada ya kupita Bajeti 2016/17
Familia ya Hifikepunye ingefahamu kiwango chako cha kutukuka cha ukilaza ulichonacho,wangekushitaki kwa kuchafua heshima ya jina lao.
 
Hicho kipande cha barabara angemtuma waziri wa ujenzi ingependeza zaidi.
Hata kitu kidogo anataka sifa yeye.
 
Kwanza ni vizuri kwamba umekiri ingawaje siyo moja kwa moja kwamba Raisi wa JMTZ hajavunja Katiba ya JMTZ kwa maamuzi yake hilo ndiyo muhimu klk yote, hivyo uamuzi wake uko ndani ya Mamlaka aliyo nayo Kikatiba kama raisi wa JMTZ!

Sasa baada ya hapo hayo mengine yote siyo muhimu, kwa maana kama unataka tuanze kusema ni Raisi yupi alitumia madaraka yake makubwa kwa maamuzi ambayo mengine yameligharimu Taifa basi Raisi Magufuli hajafikia hata 1/64 ya Mlm.Nyerere, kuanzia vita ya Biafra ambapo Mlm. Nyerere alituma watu wetu vitani na waliuliwa bila ya sababu yoyote ile ya msingi hatuna uhusiano wowote ule na Nigeria na uwepo wa Nigeria haukuhatarisha nchi yetu yoyote kwa chochote kile, mpaka vita ya Uganda, kuja kwenye vijiji vya ujamaa ambavyo ambapo Mlm.Nyerere kwa kutumia madaraka makubwa ya Uraisi alihamisha watu kwa nguvu hasa watu wa Kusini (Kusini mwa Mkoa wa Dar/Pwani) bila ya kufanya maandalizi yoyote yale kule alikokuwa anawahamishia watu hali iliyopeleka watu kuliwa na Simba, kuumwa na nyoka na matatizo mengine sana hivyo wewe kumnukuu hapa Mlm.Nyerere kwamba yeye ndiyo alikuwa mtumiaji mzuri wa Mamlaka makubwa ya Uraisi aliyopewa Kikatiba siyo kuwa fair kwa Raisi Magufuli kwa maana Raisi Magufuli mpaka sasa hivi maamuzi yake yote aliyoyatoa kwa kutumia madaraka yake makubwa aliyo nayo Kikatiba yamejikita kwenye kuboresha maisha ya Watanzania walio masikini na nitaorodhesha kuhamisha fedha za Bunge kununua Madawati, kuhamisha fedha za starehe kununua vitanda Hospitalini leo hii Wagonjwa hawalali chini kwa Muhimbili, kuhamisha Wafanyakzi ktk kwenye jengo la Muhimbili na kupisha wamama wazazi waliokuwa hawana vitanda na kuishi kwenye mazingira machafu, kuhamisha fedha za starehe ya Uhuru kujenga br. ya Moroko-Mwenge ili kumpunguzia mwananchi adha ya kukaa br. kwenye foleni, na mengineyo hivyo Magufuli anatumia madaraka yake makubwa aliyo nayo lkn kwa mazuri yetu!
Mazuri gani mpaka sasa?
 
Back
Top Bottom