Ni kweli ndoa ya Clouds Fm na CCM ishafungwa?

Ni kweli ndoa ya Clouds Fm na CCM ishafungwa?

Tujadilini mustakabali wa TAIFA tusianze kujadili watu maana tumefika hapa kwa sababu tuliruhusu akili na macho yetu kusoma na kusikiliza mijadala iliyokuwa inajadili watu kabla ya mwaka 2005.
Tuangalie ishus maana kuna mambo kibao ya kuweka sawa kabla hatujaingia ktk chumba cha KURA
 
Siku walipoishukia JF, pia niliwasikiliza, kusema ukweli pamoja na vipaji vyao vya hali ya juu, wanabwabwaja kupindukia, hali inayopelekea kuvuka mipaka na hata kutumia lugha isiyofaa( Kibonde), kwa sababu amesifiwa amevimba kichwa, hivyo amejiweka juu na kuwaunder estimate wasikilizaji wake, kuwa mtangazaji ndio zaidi. Hii inapelekea wenye akili zao kuwaona they are just fools fulani wanafurahisha genge. Kibonde ni MC, lugha zake nyingi za utani na uwezo wa kuigiza sauti za watu mbalimbali, unakipa kipindi hicho ladha ya pekee na vionjo adimu, Gadner alionekana kama modarator akimdhibiti Kibonde asipitilize, lakini sasa lao limekuwa moja ndio kwanza Gadner anamchochea Kibonde kuzidi kumwaga upupu. Mimi yangu macho na masikio, ngoma ikilia sana mwishowe hupasuka, nawathibitishia wana JF, hii ngoma ya Jahazi, sasa yalia sana, inakaribia kupasuka!.

Ndiyo tayari wamevuka peak wanaelekea kwishne. Kibonde hata kwenye mambo ya MC ameanza kuchemsha. Hajui nini aseme wapi kwa nini na kwa watu wa aina gani. Kumbuka siku ya Uzinduzi wa uchangiaji CCM pale alipoanza na kuzungumzia taratibu zote za uchangiaji utadhani yeye ndiye kaandaliwa, nilijiuliza hivi kupewa briefing ya event ndiyo umepewa nafasi ya kuwa msemaji?
 
Tujadilini mustakabali wa TAIFA tusianze kujadili watu maana tumefika hapa kwa sababu tuliruhusu akili na macho yetu kusoma na kusikiliza mijadala iliyokuwa inajadili watu kabla ya mwaka 2005. Tuangalie ishus maana kuna mambo kibao ya kuweka sawa kabla hatujaingia ktk chumba cha KURA

Mustakabali wa taifa ni upi? Kumbuka hawa watu wanasikilizwa na watu wengi sana tuwaache waendelee hivyo hivyo? Kwani uchaguzi huo si ndiyo hawa hawa mamluki wa kundi fulani la watu na mafisadi wakiwemo? tunapowajadili tunafanya kosa gani? Adui wa Taifa hili ni watu hatuna mchawi mwingine kama tunadhani tumerogwa haya, hivyo mustakabali wa taifa hili utakuwa mzuri kama tutabadili mentality ya watu wake. Period
 
Uweli ni kuwa hii redio ina wasikilizaji wengi,tatizo ni kuwa watangazaji wake wanajadili mambo kwa maoni yao tu siyo kulenga jamii,kwani mtangazaji kama kibonde ni wa siku nyingi hivyo ni mzooefu sasa kama umaarufu umemuaribia hjiyo ni lugha nyingine.

nadhani tufunge mjadala hapa juu ya redio hii,kwani pale redioni kuna wajanja kweli kwani baadhi yao ndiyo wanaanzisha hapa thread ili wajadiliwe ili ionekane redio yao iko juu kumbe ni upupu tu.Watangazaji wengi wa redio hiyo wamejaa humu JF
 
mnataka kunangwa tena kwenye JAHAZI......subirini ndo mida hii!!!
 
Uweli ni kuwa hii redio ina wasikilizaji wengi,tatizo ni kuwa watangazaji wake wanajadili mambo kwa maoni yao tu siyo kulenga jamii,kwani mtangazaji kama kibonde ni wa siku nyingi hivyo ni mzooefu sasa kama umaarufu umemuaribia hjiyo ni lugha nyingine.

nadhani tufunge mjadala hapa juu ya redio hii,kwani pale redioni kuna wajanja kweli kwani baadhi yao ndiyo wanaanzisha hapa thread ili wajadiliwe ili ionekane redio yao iko juu kumbe ni upupu tu.Watangazaji wengi wa redio hiyo wamejaa humu JF

rutunga M, sijui kama hapa ni kweli mm sio mtangazaji wala mwandishi wa habari mm ni Raia wa kawaida kama wengine, haya ni mawazo yangu mana nimekera na KIRADIO HIKI
 
Sijui kuhusu kiwango cha elimu cha watangazaji wa clouds lakini kama kweli hawana taaluma ya habari basi tukubaliane wana uwezo mwingine wa ziada ambao sio wa kuupuuza. Nani hajui kama clouds ni miongoni mwa radio station yenye wasikilizaji wengi popote inaposikika??? Ninachoweza kusema kwa sasa ni kwamba washikaji wamepoteza mwelekeo na huo ndo utakaowagharimu muda si mrefu wasipojishtukia na kujirekebisha. Ni kweli kwa baadhi ya vipindi ambavyo nabahatika kusikiliza (Jahazi na PBF) mara nyingi napata hisia za kwamba ama jamaa wanajipendekeza kwa chama na serikali kwa sababu wanazozijua au wanatumwa kufanya wanayofanya. Sitaki kuamini kwamba hawajui wanachofanya. NI nyakati kama hizi hata magenge ya mapusha hutundikwa bendera za chama??!!
 
Nadhani Kibonde ameshindwa kuelewa upepo unaendaje,sasa namshauri asome alama za nyakati,watanzania wanataka kutoka kwenye Udanganyika.Asifikiri kwa mawazo magando,he has to open up his mind vinginevyo akiloose populality hata pata deal nyingi.Kusema kweli wafanyakazi wengi wamemchukia sana kibonde in these three days.
 
Amini usiamini ujio wa clouds(achilia mbali mchango wa Shigongo) umechangia kwakiasi kikubwa uharibifu wa maadili katika taifa hili, na sio maadili pia clouds imechangia kiasi kikubwa kuharibu lugha yetu ya kiswahili kwa kuyapigia debe na kuyatumia maneno yasiyo sahihi ya kiswahili kama vili LISAA LIMOJA badala ya saa moja, NJUMBE badala ya ujumbe eti ujumbe wingi wake ni njumbe!!!!!!!!!!!!!!!!! wanaakili hawa kweli?? n.k
 
wanatafuta ajira ccm
kibonde ndo mc wa kampeni
ruge incharge no more malaria na studio ya kurekodia aliyowapa bongo fleva
 
Suluhisho ni kuacha kusikiliza radio zote zenye mwelekeo wa Chama Cha Majambazi. Mie nilikuwa nasikiliza Clouds enzi zile za kipindi cha 'Power Breakfast' kilichokuwa kinaendeshwa na Fina Mango na Masudi Kipanya. Hawa vijana walikuwa wanakosoa pale panapostahili bila kuegemea upande wowote. Walionyesha wanajua kazi yao na walikuwa na upeo mkubwa sana. Sijui wako wapi vijana hawa!
 
Ukitizama kwa uhakika na kwa umakini juu ya mambo yanayofanywa na Clouds/ Primetiem na watangazaji wao wa aina ya Kibonde utagundua mambo kadhaa yatakayokufanya ujiulize kama una akili timamu
1. Clouds waliaandaa tamasha la kukataa malaria rais akaalikwa na kiingilio kikatozwa ilhali tamasha lile lilidhamini kwa asilimia zote, sababu za malipo walizotoa ni kuwa ulinzi kwa rais. Hapa hatuongelei kuhusu suala la Mr II kudhulumiwa na kina Ruge
2 Asilimia kubwa ya watangazaji wa redio hii ni wasemaji wa maneno tu, ninawajua watangazaji ambao hawana elimu kubwa sana lakini ipindi vyao vina maana sana na vinavutia kusikiliza ama kutazama, tazama tbc na hasa asubuhi, pale pana vitu vizuri
Kibonde ni mganga njaa mkubwa anayetumika na kutumiwa kwa maana yake


AKILI SAFI HAIPIMWI NA TBS
 
Wanafanya ambacho wengi wanatamani lakini hawawezi... Dare showing openly!!!

Ushahidi mzuri upo humuhumu jf... wauwaji wakuu wa jk na timu yake mwaka jana sasa hivi wamekua kimya na wengine kubadili user names zao.... Clouds was conceived kwa njia ya pesa na watafanya chochote kupata pesa, haikuanzishwa kusaidia wananchi, ilianzishwa kama duka la mtu, profit first!!


 
Nimesikiliza kipindi cha jahazi leo jioni.Waendesha kipindi wametumwa,sijui na nani? lakini wametumwa.Baada ya Bla bla...! za mkuu juzi zilizochafua hali ya hewa mtaani,jamaa wametumwa kumsafisha.

Jamaa wanatulazimisha kumwelewa mkuu.Wanatufanya watanzania wote wajinga.mimi sikumwelewa,na bado sijamuelewa sijui ninyi wadau(mwaweza nisaidia).Kosa alilolifanya wanayemsafisha la Mgaya kuonekana ndiye anayewafungua macho na masikio wafanyakazi wa Kitanzania kujua wananyonywa,Clouds wanalirudia.

Wamemshambulia Mgaya kweli kweli.Kwa kila neno waliloona linafaa kumchafua mpiganaji,kisa! eti hakufika kwenye kipindi kwani walikuwa wamemualika,zaidi ya nusu saa jamaa(hasa huyu MC wa chama) yanawatoka tu kuhusu mgaya na TUCTA,very unfair and unethical.

Kwa ufahamu wangu mdogo nimeanza kuunganisha matukio.La kwanza ni hili,la pili ni lile la pale Mlimani city siku ya uzinduzi wa kukichangia chama,nadhani mshereheshaji mlimuona.Ambalo sina uhakika nalo ni kuwa,KWANI HII NDOA TAYARI IMEFUNGWA?
 
Yeah nimesikia hilo ngoja na wenyewe tuwaweke kwenye hiyo kona.. si wanialike na mimi tuzungumze!!! au ntajialika mwenyewe . Labda ndio sababu hawapokei simu!
 
jana walikuwa wanatetea hotuba feki ya JK ya wafanyakazi 350,000 wakipewa 315,000 kwa miezi 12 ni 6tr badala ya 1.5trillion.
kweli rais unamuambia mwananchi kama unataka nyongeza ya mshahara acha kazi kwa ajili kuna watu wengi tu wanatafuta kazi. Hao wakina Januari Makamba wenye akili sana ikulu wanashindwa kumshauri rais kwenye hili???

sana san huyu ephraim kibonde sijui wanadhani watu wendawazimu
 
Kwa kweli wamechemsha big time,na wao wemegeuka kuwa watu wa mipasho kama bwana mkubwa
 
jana walikuwa wanatetea hotuba feki ya JK ya wafanyakazi 350,000 wakipewa 315,000 kwa miezi 12 ni 6tr badala ya 1.5trillion.
kweli rais unamuambia mwananchi kama unataka nyongeza ya mshahara acha kazi kwa ajili kuna watu wengi tu wanatafuta kazi. Hao wakina Januari Makamba wenye akili sana ikulu wanashindwa kumshauri rais kwenye hili???

Hapo kwenye blue mkuu kachemka vibaya. Si ni mchumi yule? sasa hata hesabu za kuzidisha inakuwa shida! Msiwalaumu sana clouds jamani, wao Kikwete ni mtaji wao wa biashara, si mnakumbuka siku ya ukimwi walivyo mwalika na wao wakatengeneza pesa?
 
Hapo kwenye blue mkuu kachemka vibaya. Si ni mchumi yule? sasa hata hesabu za kuzidisha inakuwa shida! Msiwalaumu sana clouds jamani, wao Kikwete ni mtaji wao wa biashara, si mnakumbuka siku ya ukimwi walivyo mwalika na wao wakatengeneza pesa?
Mkuu wa Wahalifu,
Umesema ukweli mtupu.
 
Back
Top Bottom