Ni kweli bilioni 10 zimejenga flat 20? Au tuna woga kuhoji gharama halisi?

Hakuna kinachoshindikana.
Kujenga kwa billion kumi ni kitu kinachowezekana kabisa na chenji inaeza kubaki. Ni sawa na kumshangaa mtu anae-survive kwa mshahara wa laki tatu kwa mwezi na ana familia. Wakati wewe una mshahara wa milioni tatu uko bachelor na haukutoshi.
Kama TBA wana ma-engineer wao permanent kabla hata ya mradi, au labda tuseme waongeze wachache kukidhi mahitaji. Posho za vibarua wa Tanzania kila mtu anajua ilivokua aibu hata kuzitaja, japo ndo wanalipwa hivo. Design kuanzia architectural mpaka structural pamoja na usimamizi BICO ya CoET ipo (wasioijua BICO, ni engineering Consulting firm ya UDSM), wana wafanyakazi wanalipwa always wawe wamefanya kazi au lah, na kazi ni ya chuo chao wenyewe ni suala la kutoa maagizo tu hiyo kazi inafanyika. Ukija kwenye material, Serikali ina share 30% twiga cement, possibility ya kupata Cement kwa bei chee upo. Kokoto na nondo ndio pekee wanaweza kununua kwa bei ya soko. Furniture zote, kuanzia vitanda, makabati yote yametoka workshop za CoET. Kwanini pesa hio isitoshe.
Katika mfumo wa kawaida architect atatafutwa atafanya kazi na bado atasimamia. Structural engineer atafutwa na atasimamia kazi, Contractors watatafutwa kuanzia structure yenyewe mpaka services zote (maji, umeme n.k) hapo wote inapaswa wafanye kazi kwa faida na wahakikishe pia wanakuepo site muda wote wanaohitajika. Hapo bado misunderstanding kibao zinazosababisha mradi uchelewe.

Tatizo la nchi hii ni moja tu, haijulikani imeegemea mfumo gani kama ni ubepari au ujamaa. Na kamani vuguvugu basi ijulikane, ili kila mtu kuanzia raisi mpaka housegirl ajue hilo na wote tuishi na kuzoea aina hiyo ya maisha. Ili kusudi kiongozi akija kivingine tumshangae wote kwa Pamoja. Lakini saiv hatujui tuko upande gani, makampuni mengine yanafunga biashara kwasababu wakati wanakuja waliamini sisi tunaelekea kwenye ubepari, sasa raisi Mjamaa kaja hawana chao tena, sharti wafunge virago. JK aliendesha nchi kipebari na yale yote yaliyotokea katika utawala wake yalitokana na mfumo huo. Kaja JPM nchi inaenda kijamaa na matokeo yake ndo haya mambo yanafanyika kijamaa ile pesa iliyokua inatakiwa iingie kwenye mifuko ya watu inaenda kwenye real things. Hapo lazima watu walie tu.
 
Pesa hizo zinatosha sana endapo mambo haya yameingia humo.
1. Cheap Labour
Kama amepata wafanyakazi kuanzia engineer mpaka vibarua wa bei rahisi
Let's say badala ya kumlipa mchora ramani tu milioni 20 wanamlipa milioni 3

2. Cheap Materials
Let's say cement wanauziwa kwa bei ya kiwandani ambayo ina tax exemption badala ya 11,000 wanapata kwa bei ya chini
Mchanga wanaweka gari za jeshi mafuta zinaufuata huko pugu or anywhere badala ya kulipa 250,000 kwa trip ya mchanga wanalipia 50,000 ya mafuta.
Nondo na material nyingine wafanye hivyo pia
 
Injinia kwa kiswahili ni mhandisi, wapo wa umeme, majengo, barabara, maji, visima, mabwawa, magari, ndege, boti, mitumbwi, miti, na wengine wa kuogofya watu.

Sijui huyu wetu anafiti wapi, maana kila sehemu anautumia, Kule aepoti alileta ujuaji, yan anajua kila kitu huyu
He must have ABC in Engeneering. Huyu rais wetu alikuwa wazir wa ujenzi. Anauzoefu na hii Mirad .
 
Hata mimi nakuwa na doubt magorofa ishirini yenye floor nne bilioni 10? Basi kama ni kweli ujenzi ni rahisi sana hawa wajenzi ndio wanatuibia maana unaweza kuwa unajenga jengo dogo tu la kawaida unakuta shs mil. 100
Ujenzi ni rahisi sana hasa kwa dar es salama basi uwa tunapigwa sana ukisimamia vizur ukiwa Na mil20 unajenga nyumba kubwa tu tena ya kisasa mkuu
 
kwahiyo milioni 125 haijengi floor moja waungwana? ok anyway tufanye wamejenga majengo yote kwa Tsh elfu 80, au trillion mia au billion 10, so what?????????
Tatizo ni Rais kudanganya akidhani watu wote hawana akili kama baadhi yenu mlivyo!
 
People with great minds can not be comfortable in this country and have nothing to celebrate so far.
People with great minds post serious issues and not complaints, blames and the like.

You're supposed to discuss about the main issue (cost of IDSM Students' hostels) posted herein!
 
Sifa moja kuu ya tawala za kidikteta popote Ulimwenguni ni kudanganya na kupika data...namba ndogo huongezewa sifuri mbele iwe kubwa na kubwa hupunguziwa sifuri ili iwe ndogo...it is the case with Russia, Uganda, Rwanda nk. na sasa Tanzania...kama unafanya research katika nchi hizo inabidi uchanganye akili za kuambiwa na za kwako maana information is frightfully not reliable!
 
Kwaiyo ndege zilinunuliwa kwa zaidi ya trillion moja???!!
We kiboko asee duh!

Na Mh Zitto alisema ni mtumba hizo ndege, hadi leo hajaleta mrejesho. Kama hatoliongelea kwenye bajeti ya Wizara husika, atakuwa amejifedhehesha
 
Tunafurahia kupata hostel mpya za kulala wanafunzi pale Udsm. Ni sawa. Tumefahamishwa kuwa kuna flat 20 zenye floor 4 kila moja.

Mimi sio mtaalamu wa majengo. Lakini wataalamu wa majengo wanaweza kweli kututhibitishia kuwa hizi bilioni kumi ndio halisia? Ukiangalia kwa ukaribu unapata shaka. Naamini kuna hela imezidi Ila kwa vile mkuu alishatamka hicho kiasi basi TBA wamelazimika kuendelea kukariri bilioni kumi.

Jé wasimamizi wa mradi huo walikuwa hawalipwi? Bodi ya ukadiriaji majenzi ina standard zake katika kujenga Jengo lolote. Nina amini ipo siku tutapata uhalisia wa gharama hizo.

Kuna athari kubwa ya kutokuwa wakweli katika mradi huo. Athari yake ni kuwa kila jengo litakalojengwa nchini kama litapita gharama hizo basi wataambiwa wameweka chá juu. Tuliona hili kule Simiyu. Rais alikataa Jengo lenye kukadiriwa hela nyingi. Akatoa mfano wa bilioni kumi katika mradi huu wa mabweni ya udsm. Wataalamu watakuwa na woga kuleta gharama halisi zá majengo kwa hofu ya kuambiwa wameweka chá juu.

Tunahitaji kupata majengo haya kwa gharama nafuu lakini isiwe chini ya nafuu. Natoa wito wakadiriaji majenzi waje hapa kutupa standard zao zikoje kwa majengo kama haya. Wasiogope kusema ukweli.

Flat 20 ina maana kila flat iligharimu shilingi milioni 500. Jé flat moja lenye floor 4 gharama yake ni milioni 500? Na hapo hapo wakajenga na uzio. Sitaki kufurahia tu kupata majengo haya lakini lazima gharama halisi zionekane.
Mkuu Ngalikivembu swali lako ni la msingi sana ili pia tujue huko siku za nyuma tulikuwa TUNAIBIWA kiasi gani? Huu mradi una Architects, una Engineers na una Quantity Surveyors na ninaamini wako humu JF wathibitishe hili ili sisi ambao tuko kwenye ujenzi tuanze kuchkua hayua stahiki kurekebisha mambo.
 
Kila siku mnalalamika tu fact hamtoi, Kuna kipindi mlisema haitowezekana na ikiwezekana basi majengo sio imara.. Kelele nyingiiiii
 
Mimi hiyo ni taaluma yangu nakuthibitishia haiwezekani anayetaka kuaminisha watu kuwa bil 10 zimeyajenga naye atakua kujaza tu
Unathibitishaje? Kwa kusema hiyo ni taaluma yangu nathibitisha? Wooooi, ujinga mzigo. Yaani wewe mwenye jina feki jf muoga kama mimi sembuse hata hiyo fani unayooiita yako hujui inaitwaje eti unataka uaminike kuliko rais wa nchi? Ndugu yangu nenda Mombasa kufanya hiyo fani yako, huku hutapata wateja
 
Hatujakataa, nyinyi mnaojiita wataalam wa hiyo fani si mtupe mchanganuo ili tuwaelewe? Ukiishia kusema tu kwamba wewe ni mtaalam hivyo huamini, haitusaidii sisi.
 
Mimi hiyo ni taaluma yangu nakuthibitishia haiwezekani anayetaka kuaminisha watu kuwa bil 10 zimeyajenga naye atakua kujaza tu
Hebu tupe mchanganuo wa flat angalau moja tu yenye floor nne tukuelewe,hayo mambo ya sijui ni taaluma yako hatuwezi kukuelewa, tutajuaje pengine ni mjenzi wa mtaani tu.
 
Lakini Bilioni 10 kwa ajili ya Material na Vibarua tu inaweza kutosha.

Kumbuka pale Mchanga umechimbwa bila kulipiwa ushuru, Cement ya bila Ushuru, Material za Finishing bila Ushuru

Wahandisi ni wafanyakazi mishahara yao ni ile ile haijawekwa hapo lazima itoshe
 
Kwa mazoea ya kujenga kiwizi wizi lazima uone haitoshi...Mfano mdogo we na kijiwanja chako nenda kwa mshauri wa ujenzi akushauri jinsi ya kujenga hiyo gharama we mwenyewe utaanza kuona giza kujenga..Lakini sasa amua kuanza kujenga msingi wake utaanza kuona una deviate kutoka kwenye estimates zake.. Baadae akikuta jengo limesimama anaanza kusema chini ya kiwango,,,,Mfyuuuuuuuuuuuuuu kiwango kamwekee mkeo kitandani...SHUBAAAMIIIIT!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom