Ni kwa kiasi gani tunaweza kupima ukweli wa historia inayofundishwa mashuleni?

Lidafo

JF-Expert Member
Sep 26, 2019
551
747
Wasalamu ndugu wana JF wote.

Historia ni somo muhimu na lenye tija sana kwa kuzingatia ukweli kwamba historia inatunza kumbukumbu muhimu kwa taifa, Kuanzia ngazi ya shule za msingi mpaka vyuo vikuu somo hili limekuwa linawajengea wanafunzi , walimu na wanahistoria kwa ujumla uwezo wa kutoa hoja na kuzitetea na historia inatumiwa na wanahistoria kama dira katika kuishauri jamii na serikali juu ya mambo ya mbeleni kwa kuzingatia athari na tabia za mambo ya nyuma.

Historia ni pana sana kuanzia historia ya dunia ambapo hapa sio wana historia tu bali hata wanasayansi wanaingia, Historia za mabara, Nchi mpaka vijiji juu ya maendeleo ya Kiuchumi, Mabadiliko ya tabia ya nchi, Maswala ya kisiasa kama ukoloni na harakati za uhuru, Historia za watu mashuhuri n.k

Sasa turudi upande wa pili, Mambo yote haya yanayohusu historia pamoja na tija zake bado kunabakia swali moja la msingi ambalo ni ..NI KWA KIASI GANI TUNAWEZA KUPIMA UKWELI WA HISTORIA TUNAYOFUNDISHWA?

Mfano katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika wapo watu wengi wanadai kuwa historia imepindishwa kidogo na inampendelea zaidi mwalimu Nyerere na kuwaacha baadhi ya watu ambao ndio walikuwa chachu ya uhuru wenyewe hasa kwa Tanganyika, Hili linatoa shaka juu ya ukweli wa historia zinazotolewa.

Mifano ni Mingi ambayo historia Imekuwa na utata katika kuelezea uhalisia wa jambo lililopita kwa uchache ni taje baadhi ya mambo kama Utata juu ya Maiti ya Farao wa Kipindi cha Musa, Ukweli kuhusu mapinduzi ya Zanzibar, Historia ya Mwenge wa uhuru n.k

Sasa kama mwanahistoria au mtu unayependa kujifunza mambo ya mada mtambukaa unafikiri ni kwa jinsi gani Tunaweza kupima ukweli wa historia?
 
Wasalamu ndugu wana JF wote.

Historia ni somo muhimu na lenye tija sana kwa kuzingatia ukweli kwamba historia inatunza kumbukumbu muhimu kwa taifa, Kuanzia ngazi ya shule za msingi mpaka vyuo vikuu somo hili limekuwa linawajengea wanafunzi , walimu na wanahistoria kwa ujumla uwezo wa kutoa hoja na kuzitetea na historia inatumiwa na wanahistoria kama dira katika kuishauri jamii na serikali juu ya mambo ya mbeleni kwa kuzingatia athari na tabia za mambo ya nyuma.

Historia ni pana sana kuanzia historia ya dunia ambapo hapa sio wana historia tu bali hata wanasayansi wanaingia, Historia za mabara, Nchi mpaka vijiji juu ya maendeleo ya Kiuchumi, Mabadiliko ya tabia ya nchi, Maswala ya kisiasa kama ukoloni na harakati za uhuru, Historia za watu mashuhuri n.k

Sasa turudi upande wa pili, Mambo yote haya yanayohusu historia pamoja na tija zake bado kunabakia swali moja la msingi ambalo ni ..NI KWA KIASI GANI TUNAWEZA KUPIMA UKWELI WA HISTORIA TUNAYOFUNDISHWA?

Mfano katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika wapo watu wengi wanadai kuwa historia imepindishwa kidogo na inampendelea zaidi mwalimu Nyerere na kuwaacha baadhi ya watu ambao ndio walikuwa chachu ya uhuru wenyewe hasa kwa Tanganyika, Hili linatoa shaka juu ya ukweli wa historia zinazotolewa.

Mifano ni Mingi ambayo historia Imekuwa na utata katika kuelezea uhalisia wa jambo lililopita kwa uchache ni taje baadhi ya mambo kama Utata juu ya Maiti ya Farao wa Kipindi cha Musa, Ukweli kuhusu mapinduzi ya Zanzibar, Historia ya Mwenge wa uhuru n.k

Sasa kama mwanahistoria au mtu unayependa kujifunza mambo ya mada mtambukaa unafikiri ni kwa jinsi gani Tunaweza kupima ukweli wa historia?
Historia nyingi kwa wakati tulionao ni shida.Wale wenye mamlaka huingilia historia ili iwe upande wao.
Kwa hali hiyo historia halisi ya pahala hupatikana miaka 100 ijayo ama kwa njia za uchimbaji au baada ya wahafidhina wote kufa.
 
Historia nyingi kwa wakati tulionao ni shida.Wale wenye mamlaka huingilia historia ili iwe upande wao.
Kwa hali hiyo historia halisi ya pahala hupatikana miaka 100 ijayo ama kwa njia za uchimbaji au baada ya wahafidhina wote kufa.
Kwamaana hiyo Mwanahistoria anatakiwa kuwa makini juu ya vyanzo vyake vya historia asije akatumia vyanzo ambavyo vimeshaingiliwa.
Asante kwa mchango
 
Kwamaana hiyo Mwanahistoria anatakiwa kuwa makini juu ya vyanzo vyake vya historia asije akatumia vyanzo ambavyo vimeshaingiliwa.
Asante kwa mchango
Sawa kabisa.
Kwa mfano akitokea mtu akaandika historia ya taifa la Tanzania na nukuu zake ikawa ni vitabu hivi vinavyofundishwa sasa mashuleni.Historia hiyo itakuwa ni porojo tupu.
 
Kwamaana hiyo Mwanahistoria anatakiwa kuwa makini juu ya vyanzo vyake vya historia asije akatumia vyanzo ambavyo vimeshaingiliwa.

Sawa kabisa.
Kwa mfano akitokea mtu akaandika historia ya taifa la Tanzania na nukuu zake ikawa ni vitabu hivi vinavyofundishwa sasa mashuleni.Historia hiyo itakuwa ni porojo tupu.
Unafikri mtu akitaka kuandika historia ya Tanzania anatakiwa kutumia vyanzo gani ili aandike historia ya kweli?
 
Ungekuwa umefika chuo kikuu ukasomea angalau shahada moja ya history ungesoma kitabu kizima kinachoitwa what's is history usingekuja kuuuliza huu upuuzi umo ungepata adi mbinu za kuandika historia
 
Mbona rahisi sana hiyo,Kuna njia tofauti tofauti za kujiridhisha kama Anza na simulizi ,then Tafuta maandiko tofauti tofauti,hakikisha unatembelea wewe Binafsi eneo husika unalotaka historia yake,tembelea maeneo ya makumbusho kukusanya fact. Mbalimbali
 
pia watoto waelezwe ukweli Kuwa chimbuko labinadamu sio nyani Bora tuende navitabu vyadini au tusake historia mpya kuliko hii yauongo
 
Ungekuwa umefika chuo kikuu ukasomea angalau shahada moja ya history ungesoma kitabu kizima kinachoitwa what's is history usingekuja kuuuliza huu upuuzi umo ungepata adi mbinu za kuandika historia
Inawezekana kuna upuuzi nimeandika ndani ya andiko lakini haiwezekani andiko lote likawa upuuzi, Hata hivyo asante kwa mchango.
 
Nyerere si muasisi wa harakati za Uhuru bali alikuta tayari harakati za Uhuru zikiendelea sehemu mbalimbali nchini.
Alipewa heshima na nafasi ya kuwaunganisha wapigania Uhuru mbalimbali kwa sababu kwa nyakati hizo yeye ndie aliyeoneka amesoma na anafaa.
 
Mbona rahisi sana hiyo,Kuna njia tofauti tofauti za kujiridhisha kama Anza na simulizi ,then Tafuta maandiko tofauti tofauti,hakikisha unatembelea wewe Binafsi eneo husika unalotaka historia yake,tembelea maeneo ya makumbusho kukusanya fact. Mbalimbali
Asante kwa mchango.
Kwa maana hiyo ili upate usahihi wa historia ni lazima uunganishe mambo yote uliyoyataja na sio kutumia njia moja tu🙏🙏
 
Unataka kujua kuhusu Dr Livingston nenda ujiji,nenda bagamoyo nenda zambia,nenda nchi ya unyanyembe tabora
 
Back
Top Bottom