Wanasema kwa kejeli ati najitia kuijua historia ya Uhuru wa Tanganyika

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,921
30,266
WANASEMA KWA KEJELI ATI NAJITIA KUJUA HISTORIA YA UHURU WA TANGANYIKA
Vitabu hivi vingekeuwa vimeandikwa miaka mingi sana na waandishi na kuwa sehemu ya historia ya uhuru wa Tanganyika.

Kwa nini haikuwa hivyo ni historia inayoanza mwaka wa 1962 mara tu baada ya kupatikana uhuru pale TANU ilipoamua kuandika historia yake.
Mradi huu haukukamilika.

Mwaka wa 1981 CCM ikaunda jopo la waandishi kuandika historia ya TANU.
Jopo hili lilikuwa chini ya Dr. Mayanja Kiwanuka.

Hiki hapo chini ndicho kilichotokea:

''Hassan Upeka, mmoja katika wasaidizi wa utafiti ule alipeleka katika jopo lile la utafiti na uandishi wa historia ya TANU, mahojiano aliyofanya na Abdulwahid Sykes miaka mingi iliyopita kuhusu historia ya TANU.

Hassan Upeka alifahamishwa kuwa historia inayoandikwa haimuhusu Abdulwahid Sykes.''
(Kutoka kitabu cha Abdul Sykes)

Historia ya TANU ikaandikwa bila ya kutajwa Abdul Sykes na wazalendo wengi walioshiriki katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Hii ilikuwa khiyana ya hali ya juu kabisa.

Matokeo yake ndiyo haya uwanja ukawa wazi na mtupu kwa kuandikwa historia hii wakati wake utakapofika.

Kama nisingenyanyua kalamu kuiandika hakika historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika isingekuwapo.

1697723444472.png

1697723496821.png

1697723527846.png

1697723649467.png




 
WANASEMA KWA KEJELI ATI NAJITIA KUJUA HISTORIA YA UHURU WA TANGANYIKA
Vitabu hivi vingekeuwa vimeandikwa miaka mingi sana na waandishi na kuwa sehemu ya historia ya uhuru wa Tanganyika
Mzew Mohamed Said

Kazania kuandika vitabu na makala kwa wingi. The time isnt our hands.

Kuna masuala tunayataka yawe bayana. Kuusimamia ukweli kuna gharama zake.

Usiogope, mahoka wapo nawe
 
Mzee wangu, heshima mbele.

Hoja kuu ya watu ni kwamba baadhi ya chambuzi zako ziko upande mmoja (biased) hasa mrengo wa dini yako.

Sote ni mashahidi historia imepindishwa kweli sio tu Tanganyika bali hata Zanzibar , mfano mwepesi mimi siamini na hadi kesho sitokuja kuamini Karume ni mwanamapinduzi sababu waliokuwepo siku hiyo wanamtaja mwanamapinduzi halisi ilhali Karume alikuwa amejifungia chumbani tu.

Je tunafanyaje huyu mwanamapinduzi halisi apewe heshima yake hata kama alikuwa ni mgeni na wa dini ya tofauti na ile jamii aliyofanya mapinduzi.

Nawasilisha.
 
Uje utuchambulie pia historia ya tanganyika kabla ya kuja wazungu na waarabu..
Maisha yalikuwaje,tuliishije,tulikuwa vp kiuchumi na kijamii,imani

Ova
 
Yuko sahihi wewe ndo unamkosea Tena

KUJITIA ,ni ile Hali ya kujifanya (unajua) au kujimwambafai juu ya jambo Fulani ,huyu

Baba yetu ,aheshimiwe ,ni mwandishi na ni mwingi wa misamiati na mjuzi wa lugha yetu ,anaitafuna atakavyo

Wewe umewaza kwingine ,pole
Umefikilia vibaya mkuu, nilihisi labda Typing error. Sema wewe ndo umefikilia tofauti kabisa...
 
Mzee wangu nilikuuliza kuhusu Chama Cha mapinduzi kuifanyia mapinduzi historia hiyo lakini ulikaa kimya.
 
Uje utuchambulie pia historia ya tanganyika kabla ya kuja wazungu na waarabu..
Maisha yalikuwaje,tuliishije,tulikuwa vp kiuchumi na kijamii,imani

Ova
Tanganyika haikuwepo kabla ya kuja mzungu.
 
A
Yuko sahihi wewe ndo unamkosea Tena

KUJITIA ,ni ile Hali ya kujifanya (unajua) au kujimwambafai juu ya jambo Fulani ,huyu

Baba yetu ,aheshimiwe ,ni mwandishi na ni mwingi wa misamiati na mjuzi wa lugha yetu ,anaitafuna atakavyo

Wewe umewaza kwingine ,pole
Anaelewa sana huyo, basi ni ufedhuli wake tu.
 
Mzee wangu , hukunijibu .nilikuuliza je, kitabu cha kwaheri ukoloni, kwa heri uhuru kimekuwa banned hapa tz?
 
Back
Top Bottom