holy holm
JF-Expert Member
- May 6, 2017
- 4,671
- 8,671
- Thread starter
- #81
unasema uliruka kama ninja...Simu yangu ya kwanza kumiliki ilikuwa Alkatel, siku tatu za mwanzo sikuwahi kuiona iki vibrate.
The other day nilikuwa naendesha baiskeli simu nikatumbukiza kwenye back pack, sijui ilijibonyeza vipi ikaita kwa vibration, kitu ambacho nilikuwa sijakitegemea kabisa.
Nikajua ntakuwa nimebeba panya au snake kabisa. Niliruka kama ninja baiskeli ikadondokea chaka lingine mimi kwenye vumbi, begi nalo nimetupia mbali kabisa..
Nikatafuta bonge la fimbo nikaanza kutoa kichapo kwa lile begi hadi niliporidhika chochote kilichomo kitakuwa kimeshakufa.
Kuja kufungua begi duuh!! simu haifai. Nilitamani kwenda kujishtaki polisi mwenyewe