Ni kipi kipindi bora cha asubuhi kwenye radio?

PB imejipambanua vizuri kabisa, kila mmoja ana role yake na anaimudu vizuri. Barbara ni Host mzuri kabisa, KP & Cza ni wachambuzi wanaochambua mambo kwa kina.

Sam anamudu vizuri usomaji wa magazeti kwa mtindo wa kipekee unaovutia masikio ya msikilizaji.

Bonge naye nafasi yake anaimudu vizuri jambo ambalo wanajikuta wanatengeneza timu moja hatari sana yaani akikosekana mmoja unaona kabisa kuna pengo.

Napenda sana pia segments zao zimepangiliwa vizuri sana ingawa huwa navutiwa zaidi na magazeti kutokana na namna Sam, KP na Cza wanavyoungana kuchambua mambo.

Huwa sifurahii kipindi Fredwaa akiwepo, sielewagi position yake pale CMG. Ila kwangu PB ya Clouds FM ipo juu sana na haina mpinzani kwenye shows za asubuhi kwenye redio za Tanzania.
umemaliza kila kitu mkuu.
 
Yani mtazamo wako Na wangu uko sawa kabisa kwa mm segment ya magazeti ndio huwa naikubali zaidi
Kama ni timu ya mpira basi imepata wachezaji waliozoeana, wenye muunganiko mzuri wenye kuathiriana, wanaoshirikiana na kupendana zaidi wanaojua wajibu wao.
 
Hizo redio ulizo zitaja ziko kwa ajili ya mihemeko kwanza makelele mengi yani hamnakitu hapoo mauthui ya na fanana na ujanja janja mwingi..
Hakuna redio zenye mpangilio mzuri kama hizi vipindi vya subuhi REDIO FREE AFRICA, TBC FM, REDIO ONE hawa ndio wanajua maana na maudhui ya kukupasha habari.
Well said
 
Hizo redio ulizo zitaja ziko kwa ajili ya mihemeko kwanza makelele mengi yani hamnakitu hapoo mauthui ya na fanana na ujanja janja mwingi..
Hakuna redio zenye mpangilio mzuri kama hizi vipindi vya subuhi REDIO FREE AFRICA, TBC FM, REDIO ONE hawa ndio wanajua maana na maudhui ya kukupasha habari.
Hizi ni redio za kishenzi
 
Nikimaliza bbc , pb inafata hasa segment ya magazeti akikosekana samm ndo bye bye
 
Hakuna
Mara kwa mara nikiamka asubuhi huwa napenda kusikiliza radio vipindi vya asubuhi. Asilimia kubwa ya vipindi vya asubuhi vinafanana kimaudhui hapa nitachukua sample ya vipindi vitatu. JOTO LA ASUBUHI ya EFM, POWER BREAKFAST ya CLOUDS na GOOD MORNING ya WASAFI FM.

Vipindi vyote vinaundwa na watangazaji wenye majina makubwa na uzoefu katika media. Binafsi baada ya kuvisikiliza sana hivi vipindi, nimeconclude kuwa PB ni bora kwa upande wangu na Kipanya ndio ananivutia zaidi.

Tukiweka ushabiki, chuki na mahaba pembeni na ukizingatia maudhui, hoja zinazowekwa mezani na critical reasoning ya watangazaji, kipi ni kipindi bora cha asubuhi kwa upande wako?
Hakuna Mtangazaji mkubwa hapo hao wote ni wapiga kelele,mfano Babra,kipanya kwenye hiyo PB ni kelele utafikiri watoto wadogo pia hawana weledi wowote!
 
Hiv wasaf kwenye magazet si ndo wale wanapigaga kelele na sifa za kijinga nyingi zisizo chekesha wala kueleweka?
 
Kabla Zembwela hajatoka East Africa Radio nilipenda sana kipindi chake cha asubuhi, saa saba ikifika nakamata Dw au Planet bongo hadi 10 kamili kama tu Dj Summer atakua mjengoni mana yule jamaa anapiga vitu vinakua kama live show yani unakua high mbaya, saa 10 wazee wa ndinga wako na utulivu sana kuanzia nyimbo na style yao yakuongea kama vile wako kwenye motion ya gari wanapiga stori, kama bado nipo saa mbili nawaacha na mipira yao labda nitatune Mawingu, saa tatu mzee tunakiwasha na Summer tena kwenye The Cruise
 
Radio nyingi zinaigana mfano kuanzia saa 1 na kuendelea utakuta radio kadhaa muda huu ni muda wa vipindi vya michezo
 
Ndaaah hapa umenikuna, nataka kujua kwann east redio , siku hizi wameacha vipindi vyao muhim sana ambavyo vilikuwa vinanifanya kila nikiamka lazima niwashe redio, kama kipind cha afya yako, kisha kipindi cha mind setting? Kwann siku hiz hivyo vipind havipo?
 
Back
Top Bottom